Posts

Showing posts from June, 2023

USIISHI TU ISHI KWA KUSUDI.

Image
  USIISHI TU ISHI KWA KUSUDI. Kuna watu wengi wanaamka kila siku, wanafanya kazi, wanatafuta pesa, wanapambana na maisha. Lakini ndani yao kuna swali ambalo bado halijajibiwa. Ambalo ni, “NIMEKUJA DUNIANI KUFANYA NINI?” Kwa sababu ukweli ni huu: sio kila mtu anayeishi anaelewa kusudi la maisha yake hapa duniani. Wengine wanafuata mkondo wa dunia. Wengine wanaiga maisha ya wengine. Wengine wanapoteza miaka mingi wakikimbiza vitu ambavyo havina maana ya kudumu. Lakini maisha hubadilika na kuwa na maana pale unapogundua kwa nini upo hapa duniani. Kusudi la maisha sio tu kupata pesa. Sio tu kuwa maarufu. Sio tu kumiliki vitu vingi. Wala si kuwa na kazi nyingi. Bali, Kusudi la maisha ni kugundua ZAWADI (uwezo, kipaji, karama, nguvu n.k) uliyopewa na Mungu. na kuitumia kuleta MWANGA(wepesi) katika maisha yako na maisha ya wengine. Ndiyo maana watu wanaoishi kwa kusudi huwa na nguvu tofauti. Changamoto zinakuja, lakini hawaachi kufanya. Wanakosolewa, lakini bado wanaende...

SIMULIZI YA KUSISIMUA KUHUSU “HATIMA YA KIMUNGU”. >>SEHEMU YA TATU.

Image
  SIMULIZI YA KUSISIMUA KUHUSU “HATIMA YA KIMUNGU”. >>SEHEMU YA TATU.   Ilipoishia....,.. Editrin baada ya kutulia alimsimulia kisa kizima mama yake tangu alipotoroka kwao, hadi kufikia hapa alipo na namna amba v yo El vine alivyopotea. Eliana alionesha kuumia sana kwani kwa namna nyingine tunaweza kusema yeye ndi y e aliyekuwa bibi wa mtoto yule. Wakiwa wanaendelea na mazung u mzo y ale Editrin akaanza kukumbuka kisa chote kilichomkuta kwenye maisha yake hata kupelekea yeye kutoroka kwao Dar es salaam na kuamua kuja kuishi Iringa.......   Kama hujasoma sehemu ya kwanza na ya pili bonyeza hapa. Sasa inaendelea...,.... Editrin alizaliwa Katika familia ya kitajiri sana. Baba yake alikuwa akiitwa Mr. Edward na mama yake aliitwa Eliana . Katika familia yao walizaliwa watoto wawili tu! ambao ni Editrin na Edger. T angu utoto wao walipendwa sana na wazazi wao wote wawili. Editrin na k aka yake Edger hawakuwahi kuyajua maisha ya shida ma an a baba yako ali...

JIFUNZE KUJIFUNZA (PART 1)

Image
JIFUNZE KUJIFUNZA (PART 1) Siku moja nikawa nimetulia natafakari   nikawaza na kuwazua kuhusu binadamu. Nikaona kuwa ni kawaida kabisa kwa binadamu yeyote kuzaliwa, kulelewa, kwenda shule au kutokwenda kabisa, kuoa/kuolewa wakati mwingine kutokuoa/kuolewa kabisa, kufanya kazi, kuzeeka na hata kufa. Lakini unaweza kufa hata kabla ya wakati wa kuzeeka kwako. Nikagundua kuwa katikati ya utoto na uzee/ kifo. Mwanadamu huyu atajikuta amefahamu vitu vingi sana. Aidha kwa kujifunza mwenyewe kwa kuona kusikia au kwa njia yeyote ile, au kwa kufundishwa na watu wengine nyumbani au kwa kwenda shule. Kwa kifupi   tumejifunza au tumefundishwa mambo kemkemu. Ukienda shule za St. Kayumba utafundishwa habari ya 3K   yaani, kusoma, kuandika, na kuhesabu. Na, ukibahatika ukapanda magari ya njano utafundishwa kuhusu, 3R s yaani, Reading, wRiting, and aRithmetic. Hata kwa wale hawakukanyaga kabisa umande wa asubuhi nao wamejikuta wamejifunza vitu vingi sana huko nyumbani na mtaani pia. ...

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.