Posts

Showing posts from June, 2023

SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI MISINGI.

Image
  SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI  MISINGI. Watu wengi wanapofikiria UWEKEZAJI, jambo la kwanza linalokuja akilini mwao ni pesa nyingi. Ndiyo maana wengine husema, “Nikishapata pesa nyingi ndipo nitaanza KUWEKEZA.”. Lakini ukweli ni tofauti kidogo. Uwekezaji wa kweli hauanzi na pesa nyingi. Unaanza na MISINGI sahihi ya KIFEDHA. Watu wengi hupata na kuzalisha pesa siyo tatizo kwao, lakini hawajengi utajiri. Kwa nini? Kwa sababu hawajajifunza misingi ya kuitunza na kuikuza. Kila kitu kina misingi na kanuni zake. Kabla ya kufikiria uwekezaji mkubwa, jifunze kwanza mambo machache ya msingi. Jifunze kuishi chini ya kipato chako. Jifunze kuokoa hata kama ni kidogo. Jifunze kupanga matumizi yako. Na jifunze kuwa na subira. Kwa sababu uwekezaji si mbio za haraka. Ni safari ya uvumilivu. Ni kama kupanda mti. Unapanda mbegu leo. Unaimwagilia kila siku. Unaipa muda ikue. Halafu baada ya muda, inaanza kutoa kivuli  na baadaye matunda. Tatizo la wen...

SIMULIZI YA KUSISIMUA KUHUSU “HATIMA YA KIMUNGU”. >>SEHEMU YA TATU.

Image
  SIMULIZI YA KUSISIMUA KUHUSU “HATIMA YA KIMUNGU”. >>SEHEMU YA TATU.   Ilipoishia....,.. Editrin baada ya kutulia alimsimulia kisa kizima mama yake tangu alipotoroka kwao, hadi kufikia hapa alipo na namna amba v yo El vine alivyopotea. Eliana alionesha kuumia sana kwani kwa namna nyingine tunaweza kusema yeye ndi y e aliyekuwa bibi wa mtoto yule. Wakiwa wanaendelea na mazung u mzo y ale Editrin akaanza kukumbuka kisa chote kilichomkuta kwenye maisha yake hata kupelekea yeye kutoroka kwao Dar es salaam na kuamua kuja kuishi Iringa.......   Kama hujasoma sehemu ya kwanza na ya pili bonyeza hapa. Sasa inaendelea...,.... Editrin alizaliwa Katika familia ya kitajiri sana. Baba yake alikuwa akiitwa Mr. Edward na mama yake aliitwa Eliana . Katika familia yao walizaliwa watoto wawili tu! ambao ni Editrin na Edger. T angu utoto wao walipendwa sana na wazazi wao wote wawili. Editrin na k aka yake Edger hawakuwahi kuyajua maisha ya shida ma an a baba yako ali...

JIFUNZE KUJIFUNZA (PART 1)

Image
JIFUNZE KUJIFUNZA (PART 1) Siku moja nikawa nimetulia natafakari   nikawaza na kuwazua kuhusu binadamu. Nikaona kuwa ni kawaida kabisa kwa binadamu yeyote kuzaliwa, kulelewa, kwenda shule au kutokwenda kabisa, kuoa/kuolewa wakati mwingine kutokuoa/kuolewa kabisa, kufanya kazi, kuzeeka na hata kufa. Lakini unaweza kufa hata kabla ya wakati wa kuzeeka kwako. Nikagundua kuwa katikati ya utoto na uzee/ kifo. Mwanadamu huyu atajikuta amefahamu vitu vingi sana. Aidha kwa kujifunza mwenyewe kwa kuona kusikia au kwa njia yeyote ile, au kwa kufundishwa na watu wengine nyumbani au kwa kwenda shule. Kwa kifupi   tumejifunza au tumefundishwa mambo kemkemu. Ukienda shule za St. Kayumba utafundishwa habari ya 3K   yaani, kusoma, kuandika, na kuhesabu. Na, ukibahatika ukapanda magari ya njano utafundishwa kuhusu, 3R s yaani, Reading, wRiting, and aRithmetic. Hata kwa wale hawakukanyaga kabisa umande wa asubuhi nao wamejikuta wamejifunza vitu vingi sana huko nyumbani na mtaani pia. ...

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.