Posts

Showing posts from September, 2025

SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI MISINGI.

Image
  SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI  MISINGI. Watu wengi wanapofikiria UWEKEZAJI, jambo la kwanza linalokuja akilini mwao ni pesa nyingi. Ndiyo maana wengine husema, “Nikishapata pesa nyingi ndipo nitaanza KUWEKEZA.”. Lakini ukweli ni tofauti kidogo. Uwekezaji wa kweli hauanzi na pesa nyingi. Unaanza na MISINGI sahihi ya KIFEDHA. Watu wengi hupata na kuzalisha pesa siyo tatizo kwao, lakini hawajengi utajiri. Kwa nini? Kwa sababu hawajajifunza misingi ya kuitunza na kuikuza. Kila kitu kina misingi na kanuni zake. Kabla ya kufikiria uwekezaji mkubwa, jifunze kwanza mambo machache ya msingi. Jifunze kuishi chini ya kipato chako. Jifunze kuokoa hata kama ni kidogo. Jifunze kupanga matumizi yako. Na jifunze kuwa na subira. Kwa sababu uwekezaji si mbio za haraka. Ni safari ya uvumilivu. Ni kama kupanda mti. Unapanda mbegu leo. Unaimwagilia kila siku. Unaipa muda ikue. Halafu baada ya muda, inaanza kutoa kivuli  na baadaye matunda. Tatizo la wen...

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31 Ilipoishia………. Elvine alipoteza amani kuliko hata mkewe maana kila alipomtazama mkewe basi moyo wake ni kama ulikuwa unachomwa na mwiba uliojishikiza huko kwenye mishipa ya moyo. Nafsi yake ilitaabika na ndipo alipoamua kutafuta muda mzuri, baada ya chakula cha jioni, azungumze na mkewe, maana ule ukimya wa siku mbili ulikuwa adhabu kubwa sana kwake. Kusoma sehemu ya 30 bonyeza hapa Sasa inaendelea………. Elimina mamy naomba kujua kwanini hutaki kuniuliza kuhusu sababu ya haya yote? Maana najua unajua kuwa kuna mahali mimi nilikosea, sasa unapokaa kimya hivyo… kiukweli unazidi kunichanganya maana ni kama hutaki kujua, sasa unadhani mimi roho yangu itatulia kweli?. Hata kama ungekuwa wewe lazima usingepata amani, ungekuwa hata unawaza hivi nakuwaziaje, nakuonaje na ninajisikiaje ninapokuona, sasa kwanini wewe umekaa kimya, sema neno tafadhali? (Elvine alikuwa akiongea bila kumtazama mkewe usoni maana moyo wake haukuwa katika hali ya utulivu). Pamoja na ...

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.