Posts

Showing posts from September, 2024

USIISHI TU ISHI KWA KUSUDI.

Image
  USIISHI TU ISHI KWA KUSUDI. Kuna watu wengi wanaamka kila siku, wanafanya kazi, wanatafuta pesa, wanapambana na maisha. Lakini ndani yao kuna swali ambalo bado halijajibiwa. Ambalo ni, “NIMEKUJA DUNIANI KUFANYA NINI?” Kwa sababu ukweli ni huu: sio kila mtu anayeishi anaelewa kusudi la maisha yake hapa duniani. Wengine wanafuata mkondo wa dunia. Wengine wanaiga maisha ya wengine. Wengine wanapoteza miaka mingi wakikimbiza vitu ambavyo havina maana ya kudumu. Lakini maisha hubadilika na kuwa na maana pale unapogundua kwa nini upo hapa duniani. Kusudi la maisha sio tu kupata pesa. Sio tu kuwa maarufu. Sio tu kumiliki vitu vingi. Wala si kuwa na kazi nyingi. Bali, Kusudi la maisha ni kugundua ZAWADI (uwezo, kipaji, karama, nguvu n.k) uliyopewa na Mungu. na kuitumia kuleta MWANGA(wepesi) katika maisha yako na maisha ya wengine. Ndiyo maana watu wanaoishi kwa kusudi huwa na nguvu tofauti. Changamoto zinakuja, lakini hawaachi kufanya. Wanakosolewa, lakini bado wanaende...

MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.