INUKA TENA
INUKA TENA Siku zote maisha siyo safari ya watu wasiopata changamoto. Ni safari ya watu wanaoanguka, wanajifunza, na kuinuka tena kwa nguvu zaidi boss. Watu wengi hudhani mafanikio ni safari ya moja kwa moja the straight line ambapo: unafanya vizuri kila wakati, hakuna kushindwa, hakuna maumivu. Lakini ukweli ni kwamba, kila mtu aliyefanikiwa amewahi kuanguka mara nyingi zaidi kuliko unavyofikiri boss. Tofauti yao na wengine si kwamba hawaanguki, noo, bali ni kwamba waliinuka tena baada ya kuanguka. BOSS, KUANGUKA SI MWISHO WA SAFARI. Kuanguka ni sehemu ndogo tu ya ukuaji. Kwasababu Unaposhindwa: unajifunza kitu kipya, unagundua makosa yako, unaelewa njia iliyo bora zaidi. na unapata uzoefu ambao hauwezi kufundishwa darasani ndugu yangu. Tatizo la watu wengi hufanya kosa moja kubwa: yaani, wanaona kuanguka kama mwisho wa safari yao, mara wao ni wakushindwa tu. Wao si lolote. Hapo ndipo ndoto nyingi hufa kabla hazijakomaa kabisa ndugu. Sikiliza boss, Kuanguka haku...