Posts

Showing posts from September, 2023

SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI MISINGI.

Image
  SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI  MISINGI. Watu wengi wanapofikiria UWEKEZAJI, jambo la kwanza linalokuja akilini mwao ni pesa nyingi. Ndiyo maana wengine husema, “Nikishapata pesa nyingi ndipo nitaanza KUWEKEZA.”. Lakini ukweli ni tofauti kidogo. Uwekezaji wa kweli hauanzi na pesa nyingi. Unaanza na MISINGI sahihi ya KIFEDHA. Watu wengi hupata na kuzalisha pesa siyo tatizo kwao, lakini hawajengi utajiri. Kwa nini? Kwa sababu hawajajifunza misingi ya kuitunza na kuikuza. Kila kitu kina misingi na kanuni zake. Kabla ya kufikiria uwekezaji mkubwa, jifunze kwanza mambo machache ya msingi. Jifunze kuishi chini ya kipato chako. Jifunze kuokoa hata kama ni kidogo. Jifunze kupanga matumizi yako. Na jifunze kuwa na subira. Kwa sababu uwekezaji si mbio za haraka. Ni safari ya uvumilivu. Ni kama kupanda mti. Unapanda mbegu leo. Unaimwagilia kila siku. Unaipa muda ikue. Halafu baada ya muda, inaanza kutoa kivuli  na baadaye matunda. Tatizo la wen...

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI NA TANO.

Image
SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”.   SEHEMU YA KUMI NA TANO.  Ilipoishia... Usisogee maana hapo unaposogea ndipo nataka kudondokea kwahiyo pishaaa!!" Kabla hajayatafakari yale maneno yule mtu alijiachia makusudi kabisa na kujitupa chini. Elvine alishangaa zaidi. Alitaka kusogea ili akatoe msaada lakini yule mtu ghafla alipotea.         Elvine alipata hofu zaidi. Akakimbia mpaka chumbani kwake na akajihisi kabisa hadi ile kiu imekata. Lakini alipofika chumbani kwake alipigwa na butwaa kwa kile alichokuwa anakiona mbele yake na wala hakuamini kwa haraka.... Kusoma sehemu ya 14 bonyeza hapa Inaendelea...     Alipotazama kitandani kwake alimuona kijana yule aliyekuwa kaanguka mchana na ndiye aliyemuona kajiangusha muda sio mrefu kutoka kwenye ngazi tena akiwa anacheka sana.       "Kumbe ni wewe? Unajua nilikuwa najiuliza sana kuwa ni kijana yupi ambaye anakaa hapa na anauwezo wa kufanya mambo makubwa. Kwakwel...

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI NA TATU.

Image
  SIMULIZI YA KUFURAHISHA,   “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI NA TATU.     Ilipoishia..   Aligundua kuwa kumbe Elimina anamachungu sana moyoni mwake. Aliacha kumfokea na kuanza kumwomba msamaha huku akitamani kujua tatizo ni nini hasa. Wakati akiwa anambembeleza alikaa pembeni ya Elimina kwenye sofa huku akisema samahani. Ghafla mama aliingia na kushangaa kwa kile alichokiona "Nyie watoto ni upuuzi gani mnafanya hapo?....." kusoma sehemu ya kumi na mbili bofya hapa   Sasa inaendelea....   Elvine hawakujua wamjibi nini maana walijua kabisa mama atakuwa kaelewa kwa tofauti sana.     "Samahani mama sio kama unavyofikiria. Ni kwamba Elimina hajisikii vizuri. Na alikuwa akilia na mimi sijui shida ni nini na ndio maana nilitaka aniambie" Elvine alijaribu kujitetea       "Jiandaeni kwaajili ya kikao cha familia akija baba yenu" mama aliongea kwa mkato kisha akaondoka na kuelekea chumbani. ...

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.