MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

JIFUNZE KUJIFUNZA PART VIII.

 

JIFUNZE KUJIFUNZA  PART VIII.

KANUNI ZINAZOENDESHA KUMBUKUMBU NDANI YA AKILI YAKO.

Ndugu msomaji u hali gani! Bila sha haujambo  na unaendelea vyema, na kama si hivyo Mungu akupe wepesi katika hilo. Kama utakuwa unafuatilia somo hili la jifunze kujifunza utakumbuka kuwa  tuliishia part vii huko tumejifunza mambo  kibao na kama hujasoma au kufuatilia sehemu zilizopita ni wazi kuwa kuna vitu umekosa. Lakini habari njema kwako ni kuwa kupitia hapa hapa addvaluenetwork unakwenda kuyapata masomo yaliyopita hivyo fuatilia kupitia linki hapo chini.

Kusoma part vii bonyeza hapa

Kama ilivyo kwa bank kuhifadhi pesa, ghala kuhifadhi chakula, tank kuhifadhi maji, mtungi kuhifadhi gasi, zizi kuhifadhi mifugo, nyumba kuhifadhi watu na mali zao, flash kuhifadhi taarifa, ndivyo ilivyo kwa akili kuwa na MEMORY ya kuhifadhi taarifa na michakato mingine  ndani ya ubongo wa mwanadamu. Niseme tu kuwa hii ndiyo sehemu ambayo inatunza na kuhifadhi kumbukumbu zako, watu hukumbuka matukio mbali mbali yaliyotokea muda mfupi au mrefu kutokana na kuwepo kwa sehemu hii.

Zipo sheria na kanunia ambazo zinaendesha na kuongoza memory  katika kukumbuka na kuhifadhi taarifa. Haijarishi ni kwa namna gani utakumbuka lakini, linapokuja suala la namna memory yako inavyofanya kazi huwa kuna sheria na kanuni kadhaa zinazoongoza memory yako katika kukumbuka. Hivyo hapa tunakwenda kuangalia kanuni hizo, fuatana nami;

..............................................................

Hukumbuka kwa haraka kitu cha kwanza na cha mwisho kuingia; Hiii wakati mwingine wazungu huiita primacy and recency effect. Ambapo mtu hukumbuka kwa haraka kitu cha kwanza na cha mwisho kuingia ndani yake, na ndiyo maana kama utakumbuka somo la pili tuliaangalia wakati gani mzuri wa kuiamru akili yako na tukaona kuwa ni wakati wa kwenda kulala au baada ya kuamka, kwasababu wakati huo subconscious mind huwa iko makini kupokea taarifa. Hali hii huchangiwa na namna memory yako inavyofanya kazi. Hata katika vikao ni rahisi  kumbuka namna mlivyoanza kikao na namna kikao kilivyo malizika, au namna muhubiri alivyoaanza kuhubiri na namna alivyomaliza ni rahisi sana kukumbuka nyakati hizi mbili kuliko zingine, hii ni kutokana na kanuni hii. Sijui kama unanipata.

..............................................................

Kama itapata mifumo (patterns) na miunganiko (connections)  ya vitu  ni rahisi kuvikumbuka; Kama utakumbuka katika sehemu ya tano tulizungumza kuhusu mifumo  na miunganiko hii katika ufanyaji kazi wa akili ya mwadamu, ambayo hufanya miunganiko na mifumo kama njia ya kupita hata unapojifunza  kitu kipya hutengeneza njia na hupita katika njia ziyo. Hivi ulisha wahi kukutana na mtu ambaye umemsahau jina lake? Hapo utashangaa utaanza kuvuta kumbukumbu na kujiuliza hivi ulikutana naye wapi kwa mara ya kwanza? Alikuwa na nani? Alikwambia anaitwa nani? Pengine ukikumbuka tu kuwa mlikutanaye kwenye tukio fulani, na alikuwa na mtu fulani pengine utajikuta umemkumbuka tayari hadi jina lake. Ipo mifano mingi sana kuitaja yote muda hautoshi lakini nadhani umepata picha.

..............................................................

Hukumbuka vitu ambavyo vilikushangaza au vipo tofauti na mifumo  au miunganiko ya akili;  katika kuvuta kumbukumbu akili yako hukumbuka kwa wepesi vitu ambavyo hutokea kwa kushangaza na venye utofauti kwenye kundi husika. Hebu jiulize kwamfano ukiwa katika kikao watu wanasimama kawaida tu na kutoa hija zao, lakini akatokea mmoja akasimama na kupita mbele huku akitoa hoja zake.  Au kwenye kundi utakuta kuna waafrika 50 na mzungu mmoja ni rahisi sana kukumbuka habari za mzungu huyo hata siku nyingi zikipita kwasababu ya utofauti wake. Au watu wote wanafanya biashara moja lakini akatokea mtu mmoja akaanzisha biashara yake tofauti na wengi, mtu huyu ni rahisi sana kufahamika kwa sababu ya utofauti wake. Hapa kunajambo la kujifunza kuwa ukitaka kuwa mtu wa tofauti lazima ukubali kufanya vitu vya tofauti.

..............................................................

Uwezo wako wa kukumbuka huimarika kutokana  na kujikumbusha vitu ulivyojifunza;  kama utakumbuka kwa habari ya REPEATITION  kama moja ya silaha za kupandikiza maneno ndani ya subconscious mind kama hujasoma rudi kapitie kufuata linki hapo juu. Nasema kwamba kadiri kitu unapokifanya kwa kurudia rudia kwa muda mrefu hugeuka na kuwa tabia. Hivyo hata katika kumbu kumbu memory yako hukumbuka kitu ambacho unakifanya mara kwa mara. Wakati mwingine kadiri unavyofanya mazoezi ndivyo unavyo zidi kuimarika na kuwa imara zaidi. Au hujasikia wahenga walivyosema kuwa “Practice makes improvement”, kujifunza pekee yake hakutoshi  bali inahitajika kufanyia kazi au mazoezi kwa kile ulichojifunza. kwani kadiri  unavyojifunza na kufanyia kazi kile ulichojifunza ndivyo utakavyokuwa nguli katika eneo husika. Si unajua kujifunza ni hitaji la chini sana katika mafanikio kwenye eneo lolote lile eeh! Hivyo iwe katika kazi yako yeyote ile ongeza maarifa hutabaki kama ulivyo.

..............................................................

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluenetwork. Karibu sana ujiongezee thamani yako.

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>> Migongoe.

Instagram>> migongo_elias.

Pinterest>> eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe.

 

Comments (4)

Loading... Logging you in...
  • Logged in as
Asanteh San mwl kwa SoMo zuri. Ubarikiwe
1 reply · active 88 weeks ago
Amen nashukuru sana ndugu
MARCO JINAYI's avatar

MARCO JINAYI · 88 weeks ago

Inasaidia sana
1 reply · active 88 weeks ago
Ahsante nashukuru ndugu

Post a new comment

Comments by

Popular posts from this blog

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

VITU 9 MUHIMU KWA MTU YEYOTE KUJIFUNZA KWENYE MAHAFALI.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.