P5. SABABU YA MAISHA YAKO KUBADILIKA AU KUHARIBIKA INAWEZA KUWA MAZINGIRA YAKO.

Image
  P5. SABABU YA MAISHA YAKO KUBADILIKA AU KUHARIBIKA INAWEZA KUWA MAZINGIRA YAKO. Self-awareness haiishi ndani yako  peke yako. Sehemu muhimu ya kujitambua ni kuelewa jinsi unavyoathiriwa na wengine na mazingira yanayokuzunguka, na pia jinsi unavyowaathiri wengine/ mazingira yako. Hii inaitwa Social & Environmental Awareness au Reciprocal Influence boss. 1. JINSI UNAVYOATHIRIWA NA WENGINE NA MAZINGIRA (Incoming Influence). Wewe ni kamq kisiwa,  ambapo kila siku, mazingira na watu  wengine wanaingiza: mawazo, mitazamo, hisia na tabia mbali mbali ndani yako. Wakati mwengine bila hata wewe kujua. Kwa mfano: Watu (Social Influence): Marafiki au jamaa wanaweza kukufanya uone shaka, hofu, au kuacha jambo muhimu sana maishani. Na Ukiwa na watu wenye nidhamu na maono, unachukua tabia zao mfano kuamka mapema, kupanga bajeti, au kufanya mazoezi. Unaishi Mazingira (Environmental Influence): Mazingira yenye kelele, vurugu, au tabia zisizo za tija huathiri mood na ...

USIISHI TU ISHI KWA KUSUDI.

 


USIISHI TU ISHI KWA KUSUDI.


Kuna watu wengi wanaamka kila siku, wanafanya kazi, wanatafuta pesa, wanapambana na maisha.

Lakini ndani yao kuna swali ambalo bado halijajibiwa. Ambalo ni,
“NIMEKUJA DUNIANI KUFANYA NINI?”

Kwa sababu ukweli ni huu:
sio kila mtu anayeishi anaelewa kusudi la maisha yake hapa duniani.

Wengine wanafuata mkondo wa dunia.
Wengine wanaiga maisha ya wengine.
Wengine wanapoteza miaka mingi wakikimbiza vitu ambavyo havina maana ya kudumu.

Lakini maisha hubadilika na kuwa na maana pale unapogundua kwa nini upo hapa duniani.

Kusudi la maisha sio tu kupata pesa.
Sio tu kuwa maarufu.
Sio tu kumiliki vitu vingi.
Wala si kuwa na kazi nyingi.
Bali,
Kusudi la maisha ni kugundua ZAWADI (uwezo, kipaji, karama, nguvu n.k) uliyopewa na Mungu.
na kuitumia kuleta MWANGA(wepesi) katika maisha yako na maisha ya wengine.

Ndiyo maana watu wanaoishi kwa kusudi huwa na nguvu tofauti.
Changamoto zinakuja, lakini hawaachi kufanya.
Wanakosolewa, lakini bado wanaendelea.
Kwa sababu wanajua wao ni akina nani, wametoka wapi, wapo wapi na wanaenda wapi?.

Labda leo unajiuliza maswali mengi kuhusu maisha yako.
Labda bado hujaona wazi KUSUDI la Mungu katika maisha yako.
Lakini kumbuka jambo moja muhimu:
Hakuna mtu aliyeumbwa bila sababu.
Hata kama wazazi wako hawakukutarajia, hata kama kama ulipatikana kwa njia isiyo sahihi. Elewa kuwa,
Hakuna maisha ya mtu yaliyoletwa duniani kwa bahati mbaya.

Na wewe pia haupo hapa kwa bahati mbaya.
Ndani yako kuna kitu ambacho dunia inakihitaji.
Utawezq kuipamba dunia na kuilemba kwacho.
Ndani yako kuna NURU ambayo inaweza kuwasaidia wengine kuona njia.
Usiishi tu kupita duniani.

Ishi ukigundua, ukikuza, na ukilitimiza kusudi la maisha yako.
Kwa sababu maisha yenye maana si yale unayoishi kwa mazoea.
bali yale unayoishi kwa kusudi ambalo Mungu amekuumba kwalo.


Self Awareness (Kujitambua).
Investment (Uwekezaji).
Personal Development (Maendeleo binafsi).
Migongo Elias.
+255767653697
Add Value Network.
Knowledge Is Power.

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29