SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI MISINGI.

Image
  SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI  MISINGI. Watu wengi wanapofikiria UWEKEZAJI, jambo la kwanza linalokuja akilini mwao ni pesa nyingi. Ndiyo maana wengine husema, “Nikishapata pesa nyingi ndipo nitaanza KUWEKEZA.”. Lakini ukweli ni tofauti kidogo. Uwekezaji wa kweli hauanzi na pesa nyingi. Unaanza na MISINGI sahihi ya KIFEDHA. Watu wengi hupata na kuzalisha pesa siyo tatizo kwao, lakini hawajengi utajiri. Kwa nini? Kwa sababu hawajajifunza misingi ya kuitunza na kuikuza. Kila kitu kina misingi na kanuni zake. Kabla ya kufikiria uwekezaji mkubwa, jifunze kwanza mambo machache ya msingi. Jifunze kuishi chini ya kipato chako. Jifunze kuokoa hata kama ni kidogo. Jifunze kupanga matumizi yako. Na jifunze kuwa na subira. Kwa sababu uwekezaji si mbio za haraka. Ni safari ya uvumilivu. Ni kama kupanda mti. Unapanda mbegu leo. Unaimwagilia kila siku. Unaipa muda ikue. Halafu baada ya muda, inaanza kutoa kivuli  na baadaye matunda. Tatizo la wen...

HUWEZI KUBADILIKA BILA KUJITAMBUA.


HUWEZI KUBADILIKA BILA KUJITAMBUA.

Watu wengi hutamani kubadilisha maisha ya tabia, kipato, mahusiano, au jinsi wanavyojiona. Wengine husoma vitabu, huhudhuria semina, na kuweka malengo mapya kila mwaka. Lakini, pamoja na juhudi zote hizo, hujikuta wakirudia hali ileile.

Sababu si kukosa bidii, no. Mara nyingi ni kukosa #KUJIJUA wao kama wao.

Kujiboresha bila kujitambua ni kama kujenga bila ramani.

Unapojaribu kubadilika bila kuelewa wewe ni nani, unaishia kuiga maisha ya wengine tu. Utaweka malengo yasiyoendana na hali yako, uwezo wako, au hali yako ya ndani.

Ndiyo maana baadhi ya malengo huonekana mazuri kwa macho ya watu, lakini moyoni hayana uzito wowote. Unapoanza kuchoka haraka, si uvivu tu, wakati mwingine ni ishara kwamba njia uliyopo siyo yako.

Kujitambua kunahitaji ujasiri wa kukubali ukweli kuhusu wewe.

#Kujitambua siyo kujipongeza kila wakati. Ni kukubali ukweli wote mtamu na mchungu.

Ni kuona #NGUVU zako bila kiburi, na #UDHAIFU wako bila kujilaumu. 

Ni kujiuliza maswali magumu kama: Mimi ni nani? Ninakwenda wapi? Kwa nini narudia makosa yaleyale? au Ni hofu gani inaniongoza bila kujua?

Huwezi kurekebisha kile ambacho hujakikubali.

Kujitambua huzaa mabadiliko ya kudumu

Unapojifahamu, maamuzi yako yanabadilika. Unaacha kuishi kwa mazoea na kuanza kuishi kwa #MAKUSUDI.

Unaacha kuhiuliza, “Watu watasemaje?” na kuanza kuuliza, “Hili linaendana na mimi?”

Mabadiliko yanayotokana na #SAUTI na #UELEWAwa ndani hudumu kwa sababu yanajengwa juu ya #UKWELI, si msukumo wa muda mfupi tu!.

Namaliza kwa kusema,

Kama kweli unataka kubadilika na kubadilisha chochote kwenye maisha yako, anza kwa kujifahamu wewe kwanza. Kaa kimya mara kwa mara tafakari, jisikilize kitokea ndani yako, na ukubali ukweli wako bila #KUHOFIA WALA #KUKIMBIA.


Kujitambua si mwisho wa #SAFARI—ni mwanzo wa #MABADILIKO ya #KWELI. Chukua muda mchache ujiulize swali hili:

Ni eneo gani la maisha yangu najidanganya

 mwenyewee na ninahitaji mabadiliko gani?


Add Value Network 

Migongo Elias 

#SeeYouNextLevel

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.