P5. SABABU YA MAISHA YAKO KUBADILIKA AU KUHARIBIKA INAWEZA KUWA MAZINGIRA YAKO.

Image
  P5. SABABU YA MAISHA YAKO KUBADILIKA AU KUHARIBIKA INAWEZA KUWA MAZINGIRA YAKO. Self-awareness haiishi ndani yako  peke yako. Sehemu muhimu ya kujitambua ni kuelewa jinsi unavyoathiriwa na wengine na mazingira yanayokuzunguka, na pia jinsi unavyowaathiri wengine/ mazingira yako. Hii inaitwa Social & Environmental Awareness au Reciprocal Influence boss. 1. JINSI UNAVYOATHIRIWA NA WENGINE NA MAZINGIRA (Incoming Influence). Wewe ni kamq kisiwa,  ambapo kila siku, mazingira na watu  wengine wanaingiza: mawazo, mitazamo, hisia na tabia mbali mbali ndani yako. Wakati mwengine bila hata wewe kujua. Kwa mfano: Watu (Social Influence): Marafiki au jamaa wanaweza kukufanya uone shaka, hofu, au kuacha jambo muhimu sana maishani. Na Ukiwa na watu wenye nidhamu na maono, unachukua tabia zao mfano kuamka mapema, kupanga bajeti, au kufanya mazoezi. Unaishi Mazingira (Environmental Influence): Mazingira yenye kelele, vurugu, au tabia zisizo za tija huathiri mood na ...

KUACHA URITHI.

 


#KUACHA #URITHI.

Watu wengi wanaishi wakifikiria leo tu.

Lakini wachache wanaishi wakijenga urithi wa kesho.

Ukweli ni huu ;

Maisha ya mtu hayapimwi tu kwa muda aliokaa duniani,

bali kwa athari na alama  aliyoiacha katika maisha ya wengine.


Wengine wanaacha majumba.

Wengine wanaacha mali.

Wengine wanacha mashamba.

Wengine wanaacha Magari.

Na hilo ni jambo jema, na ni urithi mzuri.


Lakini kuna urithi mkubwa zaidi kuliko mali.

Urithi wa maadili.

Urithi wa maneno ya kutia moyo.

Urithi wa mfano wa maisha uliouonyesha.

Urithi wa mifumo na mienendo ya maisha.


Kuna mtu leo anapigana vita za maisha kwa ujasiri kwa sababu kuna mtu aliwahi kumwambia, “USIKATE TAMAA.”

Kuna mtoto anajua KUHESHIMU kwa sababu kuna mtu aliwahi kumfundisha heshima. kuna mtu anajali #thamani na #utu wa watu sababu kuna mtu amewahi kumfundisha hivyo.


Maneno madogo yanaweza kujenga maisha na HATIMA ya mtu.

Na vitendo vidogo vinaweza kubadilisha #KIZAZI kizima.

Ndiyo maana maisha hayapaswi kuishi ishi tu.

yanapaswa kuishi kwa KUSUDI.


Jiulize kwa utulivu mkubwa:

Kama siku moja nitaondoka duniani, nitakuwa nimeacha nini nyuma yangu?


Kwa sababu mwisho wa siku,

mali inaweza kuisha. Vile vile pesa, majumba, magari vinaweza kuhàribika.


Lakini MOYO ULIOGUSA maisha ya watu,

MAADILI uliyopanda ndani ya wengine,

na MWANGA uliowasha katika maisha yao.

NJIA NA UJASIRI ulio upanda katikati yao.


vinaweza kuendelea kuishi hata baada yako.

Usiishi tu kupita duniani.

Ishi ukiacha kitu kitakachoendelea kuzungumza hata baada yako.


Hebu wajengee urithi wa kudumu watoto wako,  wafundishe nidhamu, wafundishe mifumo ya maisha, wafundishe kujitegemea, wafundishe nidhamu ya pesa, kutatua matatito, kufikiria, kujiamini, kujali kazi na utu,  wafundishe uongozi na mambo mengine kama hayo.

Wakumbuke hata watu, kama akina Mwl. Nyerere,  Mandela, mahathima, Magufuli n.k

Bado wanaishi wangali hawapo.

Huo ndiyo urithi wa kweli. 🔥

Kama umejifunza kitu tuambie kisha share ujumbe huu kwa uwapendao.

Migongo Elias 

Add Value Network 

#seeyounextlevel 

#knowledgeispower

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29