SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI MISINGI.

Image
  SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI  MISINGI. Watu wengi wanapofikiria UWEKEZAJI, jambo la kwanza linalokuja akilini mwao ni pesa nyingi. Ndiyo maana wengine husema, “Nikishapata pesa nyingi ndipo nitaanza KUWEKEZA.”. Lakini ukweli ni tofauti kidogo. Uwekezaji wa kweli hauanzi na pesa nyingi. Unaanza na MISINGI sahihi ya KIFEDHA. Watu wengi hupata na kuzalisha pesa siyo tatizo kwao, lakini hawajengi utajiri. Kwa nini? Kwa sababu hawajajifunza misingi ya kuitunza na kuikuza. Kila kitu kina misingi na kanuni zake. Kabla ya kufikiria uwekezaji mkubwa, jifunze kwanza mambo machache ya msingi. Jifunze kuishi chini ya kipato chako. Jifunze kuokoa hata kama ni kidogo. Jifunze kupanga matumizi yako. Na jifunze kuwa na subira. Kwa sababu uwekezaji si mbio za haraka. Ni safari ya uvumilivu. Ni kama kupanda mti. Unapanda mbegu leo. Unaimwagilia kila siku. Unaipa muda ikue. Halafu baada ya muda, inaanza kutoa kivuli  na baadaye matunda. Tatizo la wen...

KUJILINGANISHA NI SUMU HATARI.


 KUJILINGANISHA NI SUMU HATARI.

Tatizo kubwa la kizazi hiki si kukosa UWEZO binafsi.

Bali ni KUJILINGANISHA kupita kiasi.

Hebu tazama kwa mfano, nafungua simu yako, unaona maisha ya wengine, yanaonekana yamepangwa.

Wamefanikiwa.

Wanasafiri.

Wanaonekana kuwa na furaha sana.

Wanavaa na kula vizuri.

Halafu unaanza kujiuliza:

“Mimi niko wapi?” mara unasema mimi si chochote.

Mdogo mdogo, unajikuta unapima thamani yako kwa vipimo vya watu wengine. Hapo ndipo tatizo linapo anzia.

Lakini ukweli ni huu; 

๐Ÿ‘‰ kila mtu ana safari yake, kila mtu anasababu yake. Ambayo yaweza kuwa nitofauti kabisa na wengine.

Kuna anayekimbia haraka kwa sababu alianza mapema.

Kuna anayepanda polepole kwa sababu anajenga msingi imara.

Kuna anayeficha mapambano yake nyuma ya picha nzuri.

Usilinganishe mwanzo wako na mwisho wa mtu mwingine.

Si unajua maisha ni kama kitabu, ukurasa wako wa kwanza una weza kuwa ni wa mwisho kwa mwingine. Kila mtu anakitabu chake na kurasa zake.

Maisha yako hayakuitwa KUIGA watu wengine, bali kuishi KUSUDI lako.

Vipaji vyako ni vya kipekee.

Uwezo wako ni wakipekee.

Wakati wako ni wa kipekee.

Safari yako ina maana yake.

Badala ya kuangalia wengine wamefika wapi, jiulize:

๐Ÿ‘‰ Leo nimekua kiasi gani kuliko jana?

๐Ÿ‘‰ Nimejifunza nini leo?

๐Ÿ‘‰ Ninakaribia kiasi gani ndoto yangu?

Kumbuka;

Wakati unajilinganisha, unapoteza amani.

Kujlinganisha ni mwizi wa muda.

Mara tu unapojilinganisha unapoteza NGUVU, THAMANI YAKO NA UWEZO WAKO WA KUFIKRI.

Lakini ukiacha kujilinganisha, kimya kimya utaanzq  kujithamini, unapata nguvu, furaha, amani, kujiamini, kutumia uwezo wako na mengine kibao yafananayo na hayo.


Hivyo basi;

Tambua wewe ni nani, UDHAIFU na UIMARA  wako ni upi. Wekeza sana kwenye UIMARA wako.

Kisha pambana mdogo mdogo #MAISHA yanajengwa na kuandaliwa siku moja na wee utafika huko.

Baini, uko wapi unataka nini na unaenda wapi?. Heshimu hatua zako unazopiga kidogo kidogo.

Heshimu mwendo wako.

Heshimu historia yako.

Kwa sababu wewe sio wao.

Na wewe haukuitwa kuwa wao.

Wewe uliitwa kuwa wewe halisi. Yes wewe Orginal.๐Ÿ’™๐Ÿ”ฅ

Kama umejifunza kitu tuandikie kwa comment.

Kujifunza zaidi bonyeza hapa

Migongo Elias 

Add Value Network 

#knowledgeispower 

#seeyounextlevel

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.