NGUVU YA TATHMINI KATIKA KUBORESHA MAISHA YAKO.

Image
  NGUVU YA TATHMINI KATIKA KUBORESHA MAISHA YAKO. Kuna jambo moja muhimu sana katika safari ya mafanikio ambalo watu wengi hulipuuzia, lakini lina uwezo mkubwa wa kubadilisha kabisa mwelekeo wa maisha ya mtu yeyote. Jambo hilo si lingine bali ni TATHMINI. Ndiyo tathmini boss. Boss in short tathmini ni uwezo wa kusimama kwa muda, kuangalia ulipotoka, ulipo sasa hivi, na kule unakoelekea. Yaani ni sawa na kujiuliza hivi; Je, njia ninayotumia inanifikisha ninapotaka kwenda? Nimefanikiwa kwa kiwango gani? Nimekosea wapi? Nini kimefanya mambo yasiende kama nilivyopanga? Nifanye nini tofauti ili kupata matokeo bora zaidi? Kwa sababu huwezi kuboresha kitu ambacho hukijui wala hujakipima boss. Ndugu, TATHMINI SI KUSHINDWA HII NI HEKIMA Watu wengi wakiona mipango yao haijafanikiwa haraka huamua kuiacha na kuibwaga ghafla tu. Kibaya zaidi wengine huanza kulaumu: mazingira, watu wengine, bahati, hali ya maisha au kujilaumu wao wenyewe. Lakini mtu mwenye hekima hufanya kitu cha to...

SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI MISINGI.

 


SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI  MISINGI.


Watu wengi wanapofikiria UWEKEZAJI, jambo la kwanza linalokuja akilini mwao ni pesa nyingi.
Ndiyo maana wengine husema, “Nikishapata pesa nyingi ndipo nitaanza KUWEKEZA.”.

Lakini ukweli ni tofauti kidogo.
Uwekezaji wa kweli hauanzi na pesa nyingi.
Unaanza na MISINGI sahihi ya KIFEDHA.
Watu wengi hupata na kuzalisha pesa siyo tatizo kwao, lakini hawajengi utajiri.

Kwa nini?
Kwa sababu hawajajifunza misingi ya kuitunza na kuikuza. Kila kitu kina misingi na kanuni zake.
Kabla ya kufikiria uwekezaji mkubwa, jifunze kwanza mambo machache ya msingi.

Jifunze kuishi chini ya kipato chako.
Jifunze kuokoa hata kama ni kidogo.
Jifunze kupanga matumizi yako.
Na jifunze kuwa na subira.
Kwa sababu uwekezaji si mbio za haraka.

Ni safari ya uvumilivu.
Ni kama kupanda mti.
Unapanda mbegu leo.
Unaimwagilia kila siku.
Unaipa muda ikue.
Halafu baada ya muda, inaanza kutoa kivuli  na baadaye matunda.

Tatizo la wengi ni kutaka matunda kabla ya kupanda mbegu na kuimwagilia
Lakini ukweli unabaki kuwa huu:

👉 utajiri wa kudumu hujengwa kwa uwekezaji na uwekezaji hujengwa juu ya misingi imara.
Hata kama unaanza kidogo leo, usidharau hatua hiyo.
Kila akiba ndogo ni mbegu.
Kila uamuzi mzuri wa kifedha ni maji ya kumwagilia mbegu hiyo.
Na kadri muda unavyopita, mbegu hiyo inaweza kukua na kuwa mti mkubwa.
Anza pale ulipo.
Anza na kile ulichonacho.
Lakini hakikisha unajenga misingi sahihi ya uwekezaji.
Kwa sababu mwisho wa siku,
sio pesa nyingi zinazounda utajiri…
bali ni nidhamu ya kifedha inayojengwa taratibu.

Je, unachangamoto katika uwekezaji na unahitaji usaidizi?

Naamini umejifunza kitu kujifunza zaidi tembelea
https://addvaluetz.blogspot.com

Self Awareness (Kujitambua).
Investment (Uwekezaji).
Personal Development (Maendeleo binafsi).
Migongo Elias.
+255767653697
Add Value Network.
Knowledge Is Power.

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29