MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

SIMULIZI YA KUSISIMUA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. MFAHAMU KIJANA ELVINE, >>> SEHEMU YA KWANZA.


SIMULIZI YA KUSISIMUA, KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU.

>>SEHEMU YA KWANZA<<

 Moto mkubwa ulikua unawaka juu ya maji, Elvine alizidi kusogea pale huku akistaajabu sana, na aliogopa sana "haaa! hivi inawezekanaje Moto uwake ndani ya maji? au ndiyo ile muvi ya jana inajirudia ila huu ni mwendelezo wake?" 

  "Hapana, sioti Mimi jamani... au..... naota?". Ghafla alishituka kutoka usingizini. Kumbe ilikuwa ni ndoto tu!, alijiuliza sana lakini, kwakuwa alikua ni mtoto aliipotezea na asubuhi alikua ameisahau ndoto ile.

     Elvine alikuwa mtoto mdogo mwenye miaka 10. Na alikuwa akiishi na mama yake tu na hakuwahi kumfahamu  baba yake, wala ndugu yeyote toka aanze kujitambua. Maisha yao hayakuwa ya shida sana bali yalikuwa ya kawaida tu.

      Asubuhi aliamka akamsalimu mama yake ambaye alikuta kamuandalia chai ya maziwa mezani.

  " Shikamoo mama! "

   "Marhabaaaa El umeamkaje?"

   " Kama kawaida yangu ni upande wa kulia ndiyo nimeamkia" mama yake alicheka sana akasema,

 "sawa nishakuzoea kasumbufu kangu"

    Mama yake aliitwa Editrin alikuwa akimpenda sana mtoto wake. Licha ya kuwa na mtoto, Editrin alionekana ni binti mrembo sana, lakini hakutaka chochote ila mtoto wake awe salama muda wote. Alikua akifanya kazi Kama secretary Katika kampuni moja ya kuuza maziwa ya unga. Lakini, mara muda wa kazi ulipoisha tu, aliwahi shule kwenda kumchukua mwanaye ili arudi nae nyumbani. Hakutaka mwanaye aguswe bila kosa, na pia alibahatika sana. Maana, Elvine alipendwa na watu wengi sana. Alionekana kuwa mtii na mwenye adabu kwa kila mtu. Hivyo, alipata kibali kwa watu wa mtaa wa Tosa jijini Iringa.

     Elvine hakwenda shule Siku hiyo kwakuwa ilikua ni jumamosi. Editrin akamuuliza mtoto wake "hivi Elvine unataka nini ukiwa mkubwa?

    "Mimii... sitaki kitu! (akafikiria kidogo huku anaangalia ukutani ambako kulikuwa na tv ambayo imezimwa) enheee!!! Mama unakumbuka katuni ya jana? "

     "Imefanyaje sasa"

     "Anhaaaa! basi sawa kama hukumbuki "

     "Hivi unajielewa Elvine?"

     "Naisi tu ila nishapata jibu"

     "Enhee jibu gani sema nisikie"  

     "Nataka nikulinde wewe tu mama yangu". Baada ya jibu lile Editrin alicheka sana na akakumbuka kua katuni ya jana kuna mtoto aliulizwa na baba yake kuwa anataka nini akiwa mkubwa? Na akajibu kama alivyojibu Elvine.

     "Sawa sasa unahisi unaweza basi? "  

     "Naweza ndiyo"

     "Kweli? "

      Yeaaaaa!!!, Elvine alijibu kwa kelele huku akimkumbatia mama yake.

 Walikua na maisha ya furaha sana siku zote. Editrin alimlea mtoto wake vizuri sana tena katika malezi ya  kidini na mara nyingi alikuwa akimuita mwanae Mtumishi wa Mungu.

     Siku moja Elvine alienda kucheza kwa rafiki yake aliyeitwa Efraimu huko alikutana na wenzake wengi sana. Michezo iliendelea hadi usiku. Mama yake hakuwa na wasiwasi kwakuwa alijua kuwa mwanaye yupo salama. Ilipofika saa 2:15 usiku Elvine alianza safari ya kurudi nyumbani hakuwa na wasiwasi wowote maana watu walikuwa wengi sana njiani.

   Alipokaribia nyumbani, alimuona baba mmoja akitoka nyumbani kwao...

   ''Mmmmh huyu nani tena kwetu au mwizi? Ngoja nimwoneshe. Huyu jamaa hawezi kuiba na mimi nipo namtazama. Yaani, alichoiba lazima arudishe maana hii sura sijawai kuiona hapa mtaani wala haonekani kama mtu mwema. Kwanza sura yake inatisha. Ngoja...ngoja...ngoja"

       Elvine alijibanza ukutani karibu na nyumba moja ya jirani, kisha akaokota jiwe kubwa mithili ya kichwa chake. Kisha akatabasamu na kujisemea,

     "Leo na Mimi nitakuwa Daudi, namkamata Goriathi hapa siyo muda.."

      Akajiweka tayari kwa mashambulizi. Yule mtu pasipo kujua lolote alizidi kukaribia mahali alipojificha Elvine.

    'Paaaaah!!!!.' mlio ulisikika.

     "Mwiziiiiii,,. jamani mwizi kanishambulia ..... nakufaaaa..."Alitimua mbio yule baba kwenda kusiko julikana na hata Kama angeulizwa asingejua anaenda wapi na wala hakujua aliyempiga jiwe lile la kichwa ni nani?

      Huku nyuma Elvine alicheka hadi akakaa chini.

     "Haaaa!! kumbe na wababa wakubwa wanaliaga. Hahahaha! Sitaki kuamini hili. Hahahaaha!"

   Ghafla wababa wawili na vijana wanne walikuja pale wakamkuta Elvine ndiyo anasimama kutoka chini alipokua kakaa akicheka.

      "Mtoto mzuri umemuona mwizi maeneo haya akikimbia?" Aliulizwa Elvine na kijana mmoja, Elvine alitaka kucheka akajizuia.

" Mwi? " Akawaza kidogo,

 "anhaaaa ee ndiyo nimemuona"

Wakauliza kwa jazba zaidi wale vijana wakiwa wameshikilia mawe na malungu

" Kapita wapi?"

" Kapita..... Ilaaa hapana mi nadhani sio mwizi yule maana yeye ndiyo kaita mwizi. Kwahiyo nadhanii sijamuona."

"Aaaa tuondoke hapa huyu mtoto hajui kitu hebu twende mbele" walisemezana wale watu na kuondoka zao

     Elvine alizidi kucheka hadi nyumbani kwao. Akamkuta mama yake sebuleni

"Elvine ulikua wapi?"

"Si kwakina Efraimu" Elvine alijibu huku alicheka.

"Mpaka saizi? Alafu Mimi naongea wewe unacheka.!?"

"Hapana mama nisamehe. Ni kwamba nimefurahishwa huko nilikotoka"

"Na nini?"

"Kwanza upo salama mama?"

"Mimi mzima tu"

"Njiani nilimuona Daudi na Goliath wakiwa katika vita kali wakati huo Daudi alikuwa akitetea Israel iwe salama pamoja na waliomo"

"Mmmh!! umeanza hadithi za vikatuni"

"Lakini wewe si ulisema ni hadithi za kweli na ipo kwenye biblia au?"

"Sawa basi. Ndiyo ni ya kweli. Sasa wewe umewaona wapi? Na unamaana gani?"

     Akacheka huku akielekea chumbani kwake " Ni maono mama usijali"

" We mtoto hebu rudi hapa ule"

" Mweee samahani nishakula kwa watu maana, niliona chakula kinanukia vile nilishindwa kukataa. Ila kwakua ni wewe umepika na unajua kupika zaidi ya mama Efraimu ntakuja kula kidogo tena"

"Duuuh hapa mtoto Sina kwa kweli"alijisemea mama Elvine huku akitabasamu.

   Baada ya muda walikula chakula kisha, wakasoma biblia kama ilivyo ada yao. mama Elvine akamsomea biblia mwanaye Kisha wakaomba kwa pamoja na kila mmoja akaelekea kulala.

    Wakati Elvine akienda chumbani kwake kulala aligeuka na kumwita mama yake halafu akamuuliza kama kuna mgeni yoyote aliekuja kwao jioni ile

 " Mgeni? nani kakwambia mbona hakuna aliekuja?" Mama alijibu kwa jazba kidogo

     "Anhaa sawa mama usiku mwema" Elvine akaingia kulala lakini alishangaa kwanini mama yake alijibu Kama hakupenda lile swali. Lakini kwakuwa ni mtoto aliipotezea na kuona kawaida tu. Akaingia kulala....

   Siku iliyofuata ilikuwa siku ya jumapili. Hivyo, waliamka na kujiandaa kuelekea kanisani. Asubuhi hiyo ilikuwa ni njema sana kwa Elvine maana kati ya siku alizokuwa anazipenda sana ni siku ya jumapili.

    Walipofika kanisani aliowaona wageni wengi sana siku hiyo. Japo kanisani hapo kulikuwa na watu wengi lakini Elvine aliweza kufahamiana na watu wote wa pale kanisani hii ni kutokana na ujanja wake. Alishangaa sana hivyo akamuuliza mama yake kabla hawajatengana kuelekea kwenye madarasa yao ya jumapili.

"Mama mbona watu wengi wanaoingia kanisani ni wageni au tumepotea kanisa ninii.....?". Wote wakacheka hadi waliokuwa jirani yao walisikia na kucheka pia. Elvine alipendwa sana na watu wengi kutokana na ucheshi wake na maneno ya mzaha, hivyo alikuwa na kibali sana kila alipokwenda.

     Alipoingia kwenye darasa lao la Sunday school (shule ya jumapili kwa watoto). Alishangaa pia maana, kulikuwa na watoto wakike watatu ambao wailikuwa wageni. Alistaajabu kimoyomoyo akajisemea "mmmmh! leo siku ya ajabu sana,". Alipo watazama wale wageni mmoja aligeuka na kumtazama kisha nae akatabasamu. Elvine alishangaa kidogo nae akatabasamu tena.

      Alishangaa sana maana wageni wale walionekana kama wenyeji kuliko hata yeye. Maana kila sekta walikua wepesi kufanya jambo. Mwalimu aliposema nani anawimbo wa sifa mmoja wao aliiongoza sifa. Maswali yote ya siku hiyo wale watoto waliyajibu kwa wepesi sana, neno la siku hiyo mtoto mmoja kati yao ndiye Aliyetoa neno. Na neno hilo lilihusu "IMANI" Katika yote Elvine alibeba sentensi moja ya binti yule ambayo ilisema

    "ukiwa na imani unaweza kubadili dunia yako"

     Mwisho wa ibada watoto wale walijitambulisha nao walikua ni Elimina, Ester na Elvila.

   Baada ya ibada ile watoto wote walitakiwa kuingia kwenye ibada ya pamoja na watu wazima. Kabla ya kuingia Elvine alimfuata Mwalimu akamuhoji kidogo kuhusu hawa wageni  imekuwaje wametoa hadi neno ilihali ni wageni? Mwalimu alimwambia kuwa watoto hawa ni wageni wenyeji, na Elimina ni mtoto wa mchungaji wao 'Moses' ambaye anasoma nje ya nchi (ndie aliyetoa neno)

"Anasoma?.."alihoji kama hajasikia kilichosemwa na mwalimu.

"Anasoma nje huko"

"Wapi huko?"

"Nasikia ni China"

"Mmmmmh sawa"

     Elvine aliingia kanisani na akajikuta kaumia sana kwa kupata wivu moyoni mwake.

 Ndani ya kanisa ibada ya sifa ilikuwa ikiendelea na Elvine alipoingia kanisani alienda kukaa ukutani kabisa na akawa amejibanza kwa huzuni. Siku hiyo hakucheza wala kusimama wakati sifa ilikuwa imepamba moto, jambo ambalo halijawahi tokea. Alimfikiria na kumtamania mtoto wa mchungaji na alipata wivu sana. Muda wote wa ibada macho yake yalikuwa kwa mabinti wale watatu kwani aliwaona Kama watoto wa matajiri na akapata wivu mkubwa juu yao.

      Watoto wale walikuwa bize na sifa na hata hawakujua kama wanatazamwa na Elvine. Na isitoshe Ester na Elimina walikuwa pamoja lakini, hawakuwa wanafahamiana na Elvila. Hivyo, kila mmoja alikuwa bize na sifa japo walikaa viti vinavyofuatana. Wakati Elvine akiwa kazama katika wimbi la mawazo huku akiwa anawatafakari wale watoto.

     Ghafla alishtuka baada ya kuona ukimya wa ajabu mle kanisani. Akili ilirudi haraka na akageuka kutazama madhabahu. Lakini cha ajabu, mle kanisani alishangaa kuona hakuna mtu yeyote isipokuwa yeye na wale watoto watatu wageni. Alipata hofu zaidi maana aliona kana kwamba Kuna mwanga uliongezeka mle kanisani ambao haukutokana tu na taa zilizokuwa zinawaka. Bali, kulikuwa ni mwanga mkali na ukungu kwa mbali. Alipotazama nje kupitia dirisha aliona giza ambalo liliashiria usiku ulikuwa umeingia, tena sio mawio bali usiku wa manane.

   "Mamaaaaaaa" alipiga kelele na hakuna anaesikia  na cha ajabu zaidi ni kwamba, hata wale watoto watatu walioonekana kuwa bize na kucheza kwa staili za midundo ambayo haikuwa inasikika.

Sehemu ya pili itaendelea juma tano>>>>>usikose kufuatilia

  Bonyeza hapa kupata mwendelezo wake

 Hadithi hii imeandaliwa na kuandikwa na JACQUELINE JOHN. Mwimbaji na mtunzi wa nyimbo, mashairi, Hadithi (simulizi) na ngonjera.

 Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255789523850. Normal >>>>>+255747313148.

Imehaririwa na MIGONGO ELIAS. Mhariri.

Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255767653697. Normal >>>>>+255783327456.

GeT tO tHe NeXt LeVeL!.

 Kama umejifunza kitu shiriki nasi katika comment hapo chini, ili kujifunza na kuboresha zaidi. 

  


Popular posts from this blog

PANDE ZA MAFANIKIO

MAAJABU YA AKIBA

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.