MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

SIMULIZI YA KUSISIMUA KUHUSU “HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA PILI.

 

SIMULIZI YA KUSISIMUA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”.

>>SEHEMU YA PILI.

   Alipotazama nje kupitia dirisha aliona giza ambalo liliashiria kuwa ilikuwa ni usiku umeingia tena sio mawio bali usiku wa manane.

   "Mamaaaaaaa!" alipiga kelele na hakuna anayesikia  na cha ajabu zaidi ni kwamba hata wale watoto watatu walionekana kuwa bize na kucheza kwa staili za midundo ambayo haikuwa inasikika.

Kama hujasoma sehemu ya kwanza bonyeza hapa.

Sasa inaendelea......

   Elvine alizidi kuchanganyikiwa maana hakujua kama ni kweli anaona, anaota ama anaona maono. Alizidi kulia lakini hakuna aliyesikia kilio chake. Mlango aliuona upo mbali sana na nje pia aliogopa kutoka kwa lile giza nene. Aliamua kukimbilia mlangoni lakini hata nguvu za kufungua mlango hakuwa nazo akajikuta amekaa chini huku akitetemeka na kuwashangaa wale mabinti wageni.

   "Eee Mungu nisaidie... eeh Mungu nisaidie mwanao" alijikuta akitamka maneno hayo kwa woga na mtetemeko wa hofu kubwa.

     Wakati hajui cha kufanya, alishangaa kumuona Elvila akimgeukia na kutabasamu. Hili lilimshangaza zaidi maana Elvila alifanya hivi kila alipogongana nae macho, tangu wakiwa Sunday school hadi kanisani.

     "Huyu binti ananijua mimi? ananiona eeeh!" alijiuliza mwenyewe pasipo kuwa na majibu maana alikwisha tambua kuwa watu wengine hawamuoni yaani, Elimina na Ester.

     Elvila alitoka pale alipokuwa amekaa na kuanza kusogea pale mlangoni ambapo Elvine alikuwa amekaa chini akilia, tena alikuwa na tabasamu lisilo hata na hofu.

    "Elvine alijikuta anaanza kumuogopa hadi yule mtoto mwenzake, na isitoshe alishangaa zaidi namna binti yule alivyokuwa akimtazama na kutabasamu kana kwamba anamfahamu vizuri.

    "Elvine!!!" binti yule alimwita. Mapigo ya moyo wa mbio zaidi na akahisi kufa kufa hivi,

"We....we....wewe ni nani? Aliuliza kwa hofu sana huku machozi yanatiririka kama maji yaliokosa leso.

"Usiogope, upo salama, wewe ni mtoto wa Mungu uliyeugusa moyo wake, maana wewe ni mtu mkubwa sana. Usijifananishe na wengine hata kidogo maana thamani yako sio sawa na unayejifananisha naye. Mungu analo kusudi juu yako. We si, Mtumishi wa Mungu eeh!!" binti yule alieleza na kumalizia na swali.

"Eee....ndi.. ndio" alijibu Elvine kwa woga sana.

Alipotazama mbele alishangaa kuona kila kitu kimerudi kama mwanzo. Na Sasa ilikuwwa ni wakati wa neno. Mchungaji Moses yupo madhabahuni anatoa neno na nje pia kulionesha kuwa ni saa saba mchana.

Akageuka kumtazama Elvila ambaye bado alikuwa pembeni yake anatabasamu. Elvine alipiga kelele "mchungajiiiiii!!!!!" Lakini cha ajabu hakuna aliyekuwa anamsikia na watu walikuwa wametulia sana.

Alitaka kusimama lakini akagundua kuwa hata kusimama hawezi.

"Unataka nini?" alijikuta akimuuliza Elvila swali hili.

"Acha woga na ukafanye yalio mapenzi ya Mungu, na huu ndio ujumbe niliotumwa kwako. Maana wewe ulikwisha ahidiwa kuwa mtoto wa nadhiri kwa Mungu na hatima yako ni ya KIMUNGU."

"We ni nani?"

"Mtumwa tu wa ujumbe kuufikisha"

"Kwanini uje kwangu?"

"Ndiye uliyekusudiwa"

"Na wale wageni wengine ni wewe ndiyo umekuja nao?"

"Hapana wale ni watu wa kawaida tu, ila leo kwakuwa Mungu kamtuma mjumbe wake kwako, ilitakiwa wageni waletwe wengi ili, malaika wake aingie miongoni mwao. Kwahiyo, usiogope. Elvine hii ni habari njema ya hatima yako, Mungu anakupenda sana. Utasimama kuwakomboa wanyonge na wenye shida utawapa mahitaji yao". Maneno hayo halisemwa na Elvila huku akitabasamu. Elvila alimtazama kwa muda Elvine kisha akaendelea,

"Najua hunielewi kwakuwa wewe bado mdogo. Lakini, kuna wakati utaelewa, usiogope hata kidogo maana Mungu kaweka kitu ndani yako ambacho kitakupa nguvu ya kutumika". Elvila alimaliza kuongea na kumgusa Elvine kwenye paji la uso kwa mkono wake wa kuume, na baada ya kufanya vile mwanga mkali ulitoka katikati ya mkono wa paji la uso. Elvine akajikuta akisema..

"Yesu nisaidie mimi nipo tayari kukutumikia ila naomba unisaidie.." wakati anasema hivyo kwa mbali alimsikia Elvila akisema "sasa umekili na ndicho kilichonileta kwako, na Bwana kakuapisha leo na kukukubali wewe Elvine......"

Ghafla alishitushwa na mchungaji aliesema tusimame tufunge ibada.

"Heee! nilikua naota ama? Alitazama alipo na akagundua kuwa ni palepele alipokuwa kakaa mwanzoni mwa ibada baada ya kutoka Sunday school, na alikuwa kainamisha kichwa kama aliekuwa kasinzia.

Hapana hii sio kweli. Alijikuta kasema kwa sauti neno hilo hadi watoto wenzie wakamshangaa.

Mwalimu hakuwa mbali akamsogelea na kumwambia "hivi unanini wewe leo?. Maana umelala toka sifa hadi saizi na tumekuamsha hadi tumeshindwa. Halafu saizi unaanza kelele tena?"

Elvine alishangaa zaidi na akawa haewi hata cha kusema au kujibu, alikaa kwa kutulia hadi ibada ilipoisha kabisa na watu wakaanza kutawanyika. Alipotoka nje alikwenda kumfuata Elvila na akamuuliza kama kuna kitu kimetokea ibadani.

"Kitu! Kitu gani?"

"Aaaa.... Ni... Au basi samahani"

Elvila hakujibu kitu bali alitabasamu tena kama anaejua kitu. Elvine alitaka kumuuliza swali zaidi lakini kabla hajatamka neno alikuja mama mmoja na kumwita Elvila na kuondoka naye jambo ambalo moja kwa moja lilionesha kuwa wale walikuwa ni mama na binti yake au mtu wake wa karibu ambaye anakaa nae.

Elvine alikosa majibu ya maswali yake, na akabaki na maswali mengi kichwa. Baada ya mda Editrin alikuja na kumwita Elvine hivyo safari ya kurudi nyumbani ilianza.

Wakati wapo njiani Elvine aligeuka nyuma na akavutiwa na namna mchungaji na mkewe walivyokuwa wanafurahi na mtoto wao Elimina huku wakiingia kwenye gari lao aina ya 'prado' aliwatamani kidogo lakini moyoni akasikia ile sauti ya Elvila ikimwambia usijifananishe na mtu, wewe ni mtu mkubwa.

Alitamani kumwambia mama yake lakini akaogopa, maana mama yake alisha mkataza kulala kanisani hivyo hakujua namna ambavyo mama yake atalipokea jambo lile, na tangu siku hiyo wale wageni wote hawakuja tena hata yule mtoto wa mchungaji na rafiki yake nao walirudi china ambako ndiko walikokuwa wanasoma maana walikuwa 'family friend' yaani Ester  pia alikuwa ni mtoto wa mchungaji Joseph wa mkoa wa mbeya sehemu iliyoitwa uyole ya kati. Lakini, taarifa za Elvila hazikusikika tena tangu siku hiyo.

 Hii ilimpa tabu sana Elvine lakini akaamua kupotezea kwahiyo, hakumwambia mtu yeyote mpaka akaja kulisahau kabisa jambo lile.

  Elvine alifikisha miaka kumi na 15 na akawa darasa la Saba. Tangu utoto wake hata sasa alikuwa anakaa na mama yake tu.

   Siku moja akiwa anacheza na wenzake mtoto mwenziye alimtania na kumwambia yeye ni mtoto asiye na baba. Neno lile lilimuuma sana na akalitunza moyoni mwake mpaka aliporudi nyumbani.

 Tofauti na siku nyingine mama yake alimshangaa sana Elvine kwani hakuwa na raha kabisa siku hiyo. Jambo ambalo lilimshangaza sana Editrin aliyekuwa kakaa sebuleni akitazama runinga.        

   Editrin alishitushwa na mlio wa mlango uliobamizwa kiasi cha kulipuka moyo.

 "We Elvine nini shida mbona unabamiza mlango hivyo?." Editrin alihoji kwa kufoka kidogo. Ilikuwa rahisi sana kwa Editrin kujua kuwa Elvine hayuko sawa maana ndiyo ilikuwa tabia yake kubamiza milango pindi anapokuwa na hasira au huzuni.

 " Hamna kitu mama ila ninausingizi sana naomba niende kulala kwanza" alijibu Elvine kwa huzuni sana, kisha akaondoka kuelekea chumbani kwake ambako alijifungia na kulia sana. Mwanzo hakuwahi kujali kuhusu baba lakini siku hii ilikuwa ya huzuni sana kwake maana ndiyo siku ya kwanza kujiona tofauti na wenziye na akajikuta akitamani sana kama angekua na baba pia, lakini aliwaza anaanzaje kumweleza mama yake kuhusu hili? hapo ndio alichanganyikiwa sana.

  Aliogopa kumuhoji mama yake maana katika kusoma kwake alishawahi kusoma na kusikia taarifa na hadithi mbalimbali zilizoelezea namna ambavyo wanawake wengi wanavyotelekezwa na waume zao. Kwahiyo, alihisi yamkini ndicho kilichotokea kwa mama yake. Pia, aliwaza pengine angemfanya mama yake ahuzunike zaidi.

    Usiku alitoka chumbani na kwenda hadi nje kabisa na nyumba ambako alipofika huko alitazama juu na akaanza kujisemea mwenyewe

"Mungu, baba yangu yuko wapi? Nimuulize mama au....? Aaaa mi sijui cha kufanya kwa kweli. Lakini natamani na mimi kumjua baba japo jina. Maana mimi naitwa Elvine Editrin, kwanini na mimi nisiwe kama wengine, kwani mama yangu alifanya kosa gani hadi ukaruhusu afanyiwe hivi Mungu?" Aliendelea kijihoji huku akilia. Ghafla radi ikapiga na mvua ikaanza kunyesha alipotaka kurudi ndani haraka akajikuta anaona kizunguzungu na akaanguka chini, akapoteza fahamu.

  Editrin alishtuka saa 7 usiku akiwa na wimbi la usingizi na akajikuta anawiwa kwenda kumwangalia mwanaye maana alikuwa kaota ndoto mbaya juu ya mwanaye lakini aliposhituka kutoka usingizini hakuwa anaikumbuka ile ndoto, ila akakumbuka kuwa Elvine hakuwa sawa wakati anarudi shule.

" Hivi huyu mtoto anashida gani? Atakuwa aliamka kuja kula kweli? " Alijihoji bila kuwa na jibu.

 Alijivutavuta mpaka chumbani kwa Eliasi ambako hakumkuta mwanae kitandani. Alishituka sana na usingizi wote ulikata ghafla na akatoka mbio hadi sebuleni lakina bado hakumkuta Elvine, akakimbia zaidi hadi bafuni, chooni, na jikoni lakini Elvine hakuwepo. Aliogopa sana akatoka nje huku katahamaki na machozi yakiwa yameanza kumlenga machoni mwake.

    Alishangaa kuona alichokuwa amekiona. Alikuta kuna maua mekundu na viatu vya Elvine, lakini Elvine hakuwepo.

"Elvine mwananguuu!!! Alijikuta kapiga yowe iliyowaamsha majirani zake wote.

     Kufikia saa 11 alfajiri watu wengi walikuwa wamejaa pale nyumbani kwa Editrin. Taarifa zile zilisisimua watu wengi mjini pale ambapo kila mmoja alitamani kujua ni nini kimetokea kwa Elvine, hii ni kwa namna mtoto yule alivyokuwa akipendwa na watu.

      Editrin alikuwa hana ndugu mjini pale lakini, alikua na marafiki wengi sana ambao ndio waliokuwa wafariji wake na majirani zake walijitahidi kutafuta huku na huko kama wanaweza kumwona Elvine lakini jitihada zote hazigonga mwamba.

    Siku zilipita, wiki , miezi na hatimaye mwaka Elvine hakuonekana. Hali hii ilikuwa ngumu sana kwa Editrin na akawa kama kichaa maana mda wote alikumbatia viatu vya mtoto wake na hakutaka viguswe na mtu yeyote.

Stori ya Editrin na kupotea kwa Elvine ilienea kila mahali.

Siku moja Kuna mama mmoja alikuja kwa mama Efraimu ambako ndiyo Editrin alikokuwa kahifadhiwa huku akiwa kama hayuko sawa. Mama yule alikuwa wa makamo sana na kwa muonekano tu alionekana kuwa  ni mtu mwenye pesa sana. Alijitambulisha kuwa yeye ni mama wa Editrin. Na akaeleza kuwa Editrin alitoweka nyumbani kwa miaka mingi baada ya mgogoro uliowahi kutokea kati ya baba yake na Editrin, hivyo yeye kaweza kufika pale kwa msaada wa taarifa za habari.

Mama Efraimu alimruhusu yule mama kuingia kumwona Editrin. Yule mama baada ya kumwona Editrin alianza kulia na akaanza kuimba wimbo..

"Editrin for editing the world... Mama for all mothers in the world but Eliana mama is only one for you kids....oooh for you kids..."

Mama yule aliuimba ule wimbo huku akilia na kumsogelea Editrin ambaye alionesha kurudisha ufahamu baada ya kumtazama yule mama kwa mda mrefu.

''Mama!!" Editrin aliita na kumkumbatia mama yule aliyeitwa Eliana. 

   "My daughter" mama yule alilia zaidi.

Walikumbatiana kwa nguvu kama ruba kwenye ngozi ya binadamu. Walilia kwa mda mrefu sana na baadae walianza kuuimba ule wimbo wote huku bado wamekumbatiana

"Editrin for editing the world... Mama for all mothers in the world but Eliana mama is only one for you kids....oooh for you kids..."

Editrin alikumbuka wakati akiwa mdogo namna mama yao alivyokuwa akiwaimbia yeye na Edgar kaka yake. Na palepele aligeuza wimbo na akaimba tena,

      "Edgar for changing the world... Mama for all mothers in the world but Eliana mama is only one for you kids....oooh for you kids..." Wote walirudia wimbo na kulia sana.

Baadae Editrin akajikuta sasa anajitambua tena maana ni kama alikuwa amechanganyikiwa.

"Mama mwanangu wamemuiba"

"Don't cry (usilie)"

"How mama how.....(Kivipi mama kivipi?)"

"Mama kwanini huyu mtoto hana bahati jamani?. Aaaa mama. Editrin alilia kwa uchungu zaidi,"

(Tangu kupotea kwa Elvine ilikua ni mwaka mmoja na miezi miwili sasa. Hivyo watu walikwisha kata tamaa kuhusu Elvine.)

Mimi mwanangu najua atarudi tu japo sijui yupo kwenye hali gani. Alisema Editrin huku akizidi kulia.

Editrin baada ya kutulia alimsimulia kisa kizima tangu alipotoroka kwao hadi kufikia hapa alipo na namna ambavyo Elvine kapotea. Eliana alionesha kuumia sana kwani kwa namna nyingine tunaweza kusema yeye ndiye aliekuwa bibi wa mtoto yule. Wakiwa wanaendelea na mazungumzo yale Editrin akaanza kukumbuka kisa chote kilichomkuta kwenye maisha yake hata kupelekea yeye kutoroka kwao Dar es salaam na kuamua kwenda kuishi Iringa.......

Sehemu ya tatu>>>>>Itaendelea ijumaa. Usikose kufuatilia

Bonyeza hapa kupata mwendelezo wake.


 Hadithi hii imeandaliwa na kuandikwa na JACQUELINE JOHN.

Mwimbaji na mtunzi wa nyimbo, mashairi, Hadithi (simulizi) na ngonjera.

 Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255789523850. Normal >>>>>+255747313148.

 Na kuhaririwa na MIGONGO ELIAS. Mhariri.

Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255767653697. Normal >>>>>+255783327456.

           GeT tO tHe NeXt LeVeL!

 Kama umejifunza kitu shiriki nasi katika comment hapo chini, ili kujifunza na kuboresha zaidi.

Comments (8)

Loading... Logging you in...
  • Logged in as
Abel Banene's avatar

Abel Banene · 95 weeks ago

Mmmh 🙆🙆 ngoja tusubiri mwendelezoo
3 replies · active 95 weeks ago
Elias Migongo's avatar

Elias Migongo · 95 weeks ago

Unakuja soon
Elvine ameenda wap tena jaman ila so mbaya ngoja nisubir mwendelezo mkuu ahsant kwa simulizi nzur
Migongo Elias's avatar

Migongo Elias · 95 weeks ago

😁😄 yajayo yanafurahisha stay tuned
Sema Nini baba mbona kama mnatutapeli feelings zetu kutukatisha hivi kwelii 😔
1 reply · active 94 weeks ago
Elias Migongo's avatar

Elias Migongo · 95 weeks ago

Hahahahaha. Tuwe wapole
Judith ndumbaro's avatar

Judith ndumbaro · 94 weeks ago

Nimeipenda ngoja nisubir muendelezo
1 reply · active 93 weeks ago
Sawasawa Judith

Post a new comment

Comments by

Popular posts from this blog

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

VITU 9 MUHIMU KWA MTU YEYOTE KUJIFUNZA KWENYE MAHAFALI.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.