MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA NNE.

 

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU.

SEHEMU YA NNE. 

 Elvine alishituka na akajikuta hospitali. Alishangaa kuona kazungukwa na watu asiowajua kabisa, na cha ajabu zaidi walikuwa ni wachina wanne na mwafrika mmoja. Aliogopa sana kisha akauliza "hapa ni wapi?". Watu wale walionyesha tabasamu lililoashiria furaha ya yeye kuamka, lakini walionesha kuwa hawakuwa wanamuelewa kabisa anachoongea....

Kupata sehemu iliyopita bonyeza hapa

 Sasa inaendelea.....

 Elvine alizidi kuogopa baada ya kuchomwa sindano ambayo ilimfanya ahisi kuishiwa nguvu, kisha macho yake yakalegea na mwisho yakafumba kabisa. Alishituka badae na kujikuta kitandani, tena kwenye nyumba ya kifahari mno. Hakuwa anajielewa vizuri, aliamua kutoka nje. Alipofika sebuleni, alikutana na sebule nzuri mno ambayo hakuwahi kuona kwa macho toka azaliwe zaidi ya kwenye sinema tu.

"Mmmh! hapa ni ulaya nini?" Alijihoji huku akiwa haamini. Alisogea mbele kidogo, ghafla alikuja mama mmoja ambaye ni chotara wa kizungu na kichina na alikuwa akiitwa Exhao Mke wa Mr. Ezhu yang , yule mama na akasema "ooh! my son. How do you feel now?. Am proud you are good now."(ooh! Kijana wangu unajisikiaje sasa?. Najivunia upo vizuri Sasa)". Elvine alimkodolea macho tu yule mama pasipo kujibu neno, maana hakuwa anaelewa kitu, zaidi alichoelewa ni "my son" tu! Lenye maana ya kijana wangu, kitu kilichomfanya asielewe zaidi ni rafudhi na uongeaji wa haraka wa yule mama.

     Elvine alizidi kupata hofu maana hakujua yuko wapi, na yule mama ni nani. Yule mama na Elvine hawakuwa wanaelewana kabisa maana kila mmoja alitumia lugha anayoielewa yeye. Yule mama  akaamua kumshika mkono Elvine hadi mezani ambako kulikuwa na vyakula vingi mno kana kwamba kuna sherehe pale ndani. Dakika chache baadaye wakiwa pale mezani, alikuja baba mmoja wa kichina na kukaa kitako mezani huku akiwa na furaha mno,

  "unakwendeleaje?"

  "Vizuri" alijibu Elvine maana alimuelewa japo hakuwa anajua kiswahili vizuri baba yule.

   "Unajionaje afya jako sasa?, Moyo jangu ulipasuka pasuka baada ya kukuta  hali yakyo ni mbaya" alihoji mchina yule huku akiwa na kiswahili cha kipekee kidogo, lakini haikumpa shida sana Elvine kumuelewa. Kwahiyo akamjibu kuwa yeye hali yake ni njema.

    Elvine moyoni mwake alikuwa na shauku kubwa sana ya kumwona mama yake hivyo aliamua kuuliza kuwa ni nini kimetokea na yuko wapi mama yake Editrin, lakini yule baba alisema wale kwanza halafu atamwambia siku nyingine kuhusu hilo.

    Elvine alipewa uma na kisu, na mezani kulikuwa na nyama za kila aina, tambi, wali na vingine vingi ambavyo yeye hakuvijua.

   Alipeleka mkono kwenye tambi na akajichotea na kuanza kula, lakini sasa, loo! Radha aliyoitegemea haikuwa yenyewe kabisa lakini alijikaza na akala vijiko viwili tu, aliitamani nyama lakini staili ya ulaji wa wale watu ilimtisha maana kwao hawajawahi kula na kisu wala uma  nyama, bali ni mikono tu ndiyo ilikuwa ikifanya kazi yake.

    Aliamua kuugeukia wali lakini pia hapakuwa na kijiko pale mezani, lakini akajipa moyo mkuu, maana njaa ilkuwa kali sana. Alijitahidi kuula wali ule kwa uma na akaweza. Mwishoni mwa chakula akaona haina haja ya kujitesa wakati yeye ni mpenzi wa nyama, aliamua kutumia mkono wake, na akala pande moja la kitimoto lililonona haswaa!. Wale watu walimtazama tu na wakaonekana kufurahia hata alichokifanya.

    "Ooh dear, poye kwakua hatukuchua kuwa hujajua kuitumiya hiyi kishu na umaa"

    Elvine alitabasamu tu na hakujibu neno lakini alitamani kucheka, ila heshima tu ndiyo ilimzuia. Baada ya kula aliondoka mezani na kurudi chumbani alikokuwa kalala mwanzo. Kichwani alikuwa na maswali mengi sana ambayo yalihitaji ufafanuzi lakini hakujua aanze kumuuliza nani pale ndani.

   Akiwa chumbani alijikuta anaanza kulia huku akitaja 'mama', maana alihisi woga kidogo hasa kukutana na watu ambao hawajui kabisa.

      Ghafla mlango ulifunguliwa na wakaingia mabinti wawili na kijana mmoja wenye umri wake pamoja na yule baba wa kichina. Walipoingia Elvine kwa woga alishituka sana, akakurupuka pale kitandani na kusimama karibu nao. Yule baba akasema kuwa yeye anaitwa Mr. Ezhu yang na ni mchina lakini anafahamu kiswahili kidogo maana aliwahi kukaa Tanzania kama mwaka na miezi minne akiwa katika "research" ya kisayansi kabla hajafungua hospitali yake, na kuhusu mama yake asijali yupo tu.

    Lakini pia alimwambia pale ni Shanghai nchini China hivyo asihofu kabisa. Na wale watoto aliokuja nao ni marafiki zake kwanzia sasa maana ni watanzania ambao watamsaidia sana yeye kujua kiingereza vizuri na kuyazoea mazingira . Yule baba baada ya kuongea hayo aliondoka na kuwaacha wale mabinti wawili na kijana mmoja.

    Binti mmoja alimsogelea Elvine na kumsalimia.

  "Habari yako!"

   "Njema"

   "Sisi ni watanzania kama wewe, hapa tupo kimasomo tu, lakini pia sisi tunajua kiingereza na kichina kidogo, maana toka tukiwa wadogo tumesoma huku. Kwani kule unakaa sehemu gani?. Kabla Elvine hajajibu na yeye akamuuliza yule binti swali.

   "Hivi tumeshawahi kuonana mahali? Maana sura yako sio ngeni kwangu"

   "Sina uhakika, ila mimi sizani". Kabla hawajaendelea kuulizana maswali yule binti simu yake iliita na alipoipokea aliongea kiingereza kama mzungu wa marekani. Elvine alipata kawivu kidogo na akatamani sana angekuwa yeye. Yule binti baada ya kumaliza kuongea na simu aliondoka na akasema kaitwa nyumbani ila atakuja tena kesho kumuona. Baada ya yule binti kuaga na wale wenzake pia wakasema wanaondoka

Elvine alibaki pale akiwa hajui hatima yake.

   Rafiki zake wale, wakiafrika walizidi kuja siku baada ya siku hivyo akawazoea sana, lakini hakuruhusiwa kutoka pale ndani kwaajili ya matembezi wakidai bado ni mgeni. Baada ya miezi minne kupita alianza kujua vizuri kiingereza maana kila mtu alikuwa anaongea kiingereza na kichina tu mule ndani na hata Mr. Ezhu hakuwa mtaalamu wa kiswahili. Baada ya kuanza kuelewa kiingereza alipelekwa shule ya kimataifa iliyopo pale Shanghai. Hakuwa anaelewa chochote maana yeye aliishi kwa maelekezo tu kutoka kwa Mr. Ezhu yang. Alikaa kwa muda na akaanza kufurahia maisha ya pale, hasa baada ya kujua kiingereza.

   Siku moja usiku aliota mama yake anamuita huku analia sana. Baada ya ndoto ile alianza kuona kuna umuhimu wa yeye kujua kwanini mama yake hayupo pamoja naye. Alianza kuwasumbua walezi wake yaani, Mr Ezhu yang na mkewe madam Exhao.

    Siku moja akiwa chumbani kwake, alikuja daktari ambaye alijitambulisha kwa jina la dokta Exqu xhiao na alikuja na nesi wa kizungu aliyeitwa nesi Emma. Walimchoma sindano mkononi huku wakisema kuwa ni kwaajili ya afya yake maana bado hajapona vizuri.

    Baada ya ile sindano kuingia mwilini na kusambaa vizuri alianza kuhisi maumivu ya kichwa. Ghafla aliingia yule mama wa kizungu ambaye ndiye alikuwa wakwanza kumuona baada ya kuingia kwenye nyumba ile. Na alionekana kuwa na hasira sana

   "This is not ok! (Hii sio sawa)". Yule mama alifoka kwa jaziba sana. Kisha alianza kugombana na wale watu kwa kichina, kwahiyo hakuna ambacho Elvine alielewa baada ya lile jambo. Wakati ugomvi unaendelea aliingia Mr. Ezhu yang na akimshika mkewe kwa nguvu na kutoka nae nje.

    "It's ok baby" (usijali mtoto). Alisema yule daktari huku akimshika kichwa Elvine na kuchezea nywele zake. Elvine hakuwa anaelewa chochote, alichomwa sindano nyingine na hapo ndipo alipoishiwa nguvu kabisa na kulala.

     Huku nje Mr. Ezhu yang alikuwa katika mgogoro mkubwa na mkewe. Mgogoro wao ulikuwa katika uamuzi wa Mr. Ezhu kuamua kumfuta yule mtoto kumbukumbu jambo ambalo Exhao hakuridhia kabisa.

    Mr. Ezhu aliondoka kwa hasira pale ndani. Wakati Exhao akiwa hajui cha kufanya alienda chumbani kwao na akawa anakumbuka namna walivyompata Elvine.

   Alikumbuka kuwa miezi michache iliyopita yeye na mumewe walikuwa Tanzania katika matembezi. Exhao hakubahatika kuwa na mtoto toka aolewe na Mr. Ezhu yang hivyo alitamani hata kulea mtoto yeyote kutoka katika kituo cha watoto yatima.

     Siku moja usiku  alikuwa kwenye gari yeye na mumewe, wakiwa wanatoka kufanya utalii wao katika hifadhi ya kituro baada ya kuchelewa sana kutokana na mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha jambo ambalo liliwalazimu kuendesha gari taratibu sana. Walikuwa wanaelekea hoteli walikokuwa wanakaa kwa kipindi chote cha utalii wao, njiani walimuona mtoto kalala nje ya nyumba na mvua ilikuwa ikinyesha sana. Walishangaa sana hivyo walichukua mwamvuli na kuisogelea ile nyumba. Walipofika pale waligundua kuwa mtoto kazimia, lakini Exhao alijikuta kampenda yule mtoto hivyo akamwambia mumewe kuwa; yaweza kuwa bahati yao kupata mtoto kwa njia ile, alisema vile baada ya kuhisi yule mtoto atakuwa yatima, na pale atakuwa hakuwa na pakulala wakati mvua ilipoanza ndiyo maana kazimia.

    waliamua kumchukua yule mtoto, wakati wanambeba, viatu vilimtoka yule mtoto, lakini hawakujali. Walipoingia na yule mtoto kwenye gari, Exhao alitoka na maua na akaenda kuyaweka pale mwenye viatu akiwa na maana kuwa, anafuraha na mahali pale maana ndipo pamemsaidia yeye kupata mtoto.

    Waliondoka na Elvine mpaka kwenye hoteli waliyokuwa wamefikia. Kwakuwa walikuwa wanaondoka siku inayofuata waliona inaweza kuwapa shida kuondoka na yule mtoto hivyo asubuhi walimchoma sindano ya 'nusu kaputi' na wakamuweka kwenye boksi na kuondoka naye hadi China ambako walimpeleka kwenye hospitali yao ambayo wao ndio walikuwa wamiliki wa Hospitali hiyo. Na baada ya Elvine kutibiwa na kupona walijitahidi kutafuta uhalalisho wa mtoto yule kuishi pale nchini na wakafanikiwa. Tatizo lilikuwa ni moja tu, Elvine hakuwa yatima kama walivyojua na baada ya kujua hili Mr. Ezhu yang aliamua kumfuta kumbukumbu Elvine ili aweze kummiliki kama mwanaye halisi.

   Exhao hakutaka wamfute kumbukumbu maana alimuwaza mama wa mtoto Elvine atakavyochanganyikiwa. Alitamani amrudishe lakini yeye pia alishampenda Elvine.

    Baada ya Exhao kuwaza sana akaona hana jinsi zaidi ya kukubaliana na kilichotokea.

   Elvine alipelekwa hospitali baada ya kuchomwa ile sindano lakini walishangaa kuona Elvine haamki. Wote hawakujua sababu ya Elvine kutokuamka maana kila kitu kilifanyika vizuri kabisa. Siku tatu zilipita lakini Elvine bado hakuamka, hili liliwachanganya sana madaktari pamoja na familia ya Mr. Ezhu yang

    Usiku wakati Exhao kalala aliota ndoto kuwa Elvine anamuita, tena kwa jina lake la Exhao Ebrow. Aliposhituka kutoka usingizini ilikuwa ni saa 6:00 usiku. Exhao aliamka usiku ule pasipo kuaga aliondoka na kuelekea hospitali.

   Alipofika hospitali aliingia moja kwa moja mpaka kwenye chumba cha Elvine: kwakuwa haikuwa shida kuingia maana hospitali ile yeye na mumewe ndiyo walikuwa wamiliki, yaani ilikuwa hospitali yao binafsi.

   Alipofika chumbani alimkuta Elvine bado kalala hajitambui kabisa. Alianza kusogea pale kitandani kwa Elvine huku akimsemesha Elvine ambaye alijua kabisa kuwa Elvine hasikii.

  "Am sorry Elvine my son, it's our fault"(samahani Elvine, ni makosa yetu). Alipofika karibu na kitanda alicholalia Elvine ghafla taa ilizima. Yule mama alijikuta kapata woga sana maana kulikuwa giza ambalo lilimfanya asione hata hatua moja mbele. Aliingiza mkono kwa pupa kwenye mkoba wake ili atoe simu kwaajili ya kuwasha tochi, lakini kabla hajatoa simu alishangaa kuona mwanga ndani ya chumba kile. Alitazama taa juu lakini ilikuwa haiwaki.

   Aligeuka na kumtazama Elvine. Alishituka na akaogopa sana kwa kile alichokiona, maana Elvine alikuwa anawaka mwili mzima kana kwamba yeye ndiyo taa.

  Yule mama alirudi nyuma na kwa woga alipiga kelele lakini kulikuwa kimya sana. Wakati kasimama hajui afanyenini alibaki kajishika mdomo kama anayejizuia kuongea zaidi au anayeshangaa kupitiliza.

  Ghafla Elvine aliamka pale kitandani na akawa anatabasamu. Alipomtazama Exhao aliona kama tumboni kwa Exhao kuna mtoto mdogo wa kama miezi mitatu hivi toka kuzaliwa, akatabasamu na yule mtoto akatabasamu pia, Elvine akaanza kusogea pale Exhao aliposimama, na wakati huo Exhao naye akawa anarudi nyuma.

   Wakati Elvine anamsogelea Exhao alishangaa kuona yule mtoto aliyekuwa tumboni kwa Exhao amekabwa na mnyororo wa moto na palepele yule mtoto alikufa. Elvine alianza kulia kwa uchungu sana lakini akasikia sauti ikimwambia "why can't you save that woman? Save her with her child" (kwanini huwezi kumsaidia huyo mwanamke, msaidie yeye na binti yake).

  Elvine alifuta machozi na akasogea mpaka alipokuwepo Exhao, kisha akamshika yule mama tumbo na akasema "Elvila you can't die" (Elvila huwezi kufa) mara akaona yule mtoto kaamka na ile minyororo ikateketea. Elvine alitabasamu na akasema huyu ni mdogo wangu mimi kwahiyo apewe jina la rafiki yangu Elvila. Baada ya kusema vile mlango ulifunguliwa na madaktari ambao kumbe waliisikia ile sauti ya Exhao ya kupiga kelele. Walipoingia tu, taa iliwaka. Ghafla Elvine alianguka pale chini na kupoteza fahamu tena.

   Exhao hakuwa anaona kama kuna mtoto tumboni mwake wala hakujua chochote kilichoendelea pale ndani zaidi alichojua yeye ni kwamba Elvine aliamka na kushika tumbo lake.

  Kwa yale aliyoyaona mule chumbani Exhao hakuwa na hamu ya kubaki mule ndani, mlango ulipofunguliwa tu, aliona kama amefunguliwa kutoka kwenye gereza lenye wadudu na wanyama wa kila namna duniani, maana alikimbia kama kichaa. Kila mtu alimshangaa.

Alikimbia mpaka nyumbani, na alisahau kabisa kuwa alikuja na gari pale hospitali, hivyo 'miguu niokoe' hadi alifika nyumbani. Alipofika nyumbani alimkuta mume wake kalala. Kwa woga aliokuwa nao alijirusha kitandani kama muogeleaji aliye kwenye mashindano ya kupiga mbizi. Mr. Ezhu yang alishituka na akamuuliza nini kilichotokea, lakini hakuwa na uwezo hata wa kuongea na zaidi alitaja tu jina la Elvine.

Mr. Ezhu yang alishangaa sana lakini alimtuliza mkewe mpaka Exhao alipolala na yeye ndipo akalala.

Asubuhi walipewa taarifa kuwa Elvine kaamka. Exhao aliposikia zile habari alichanganyikiwa maana tayari alianza kumuogopa Elvine kwasababu alikuwa anajiuliza maswali mengi sana kuhusu yule mtoto Elvine na akaanza kujuta kwanini alichukua mtoto wa watu asiyemjua. Lakini hakumwambia mtu kilichotokea na hata alipotaka kusema alijiona mzito sana kuzungumza, kwahiyo ilibaki kuwa siri yake.

Jioni Elvine alirudi nyumbani, na vipimo vilionesha kuwa ni kweli Elvine hakumbuki chochote.

Elvine alikaa nyumbani wiki moja na alishangaa sana kuona namna Exhao anavyomuogopa na kumnyenyekea, kiukweli hata yeye hakuwa anakumbuka chochote kilichotokea ule usiku wa maajabu kwa Exhao. Elvine anianza kufundishwa kila kitu na akaambiwa kuwa yeye ni mtoto wa palepela China ila ni mwafrika kwakuwa wazazi wake walikuwa waafrika japo walikufa yeye akiwa mdogo.

 Elvine alianza shule, lakini tofauti kabisa na kwao, huku hakuweza tena kufundishwa mambo ya Mungu. Alipoanza shule wale rafiki zake wa mwanzo walishangaa sana kuona Elvine hawakumbuki, kwahiyo waliamua kujitambulisha upya kwa Elvine, nao walikuwa ni Elimina, Ester na Emmanuel, wote hawa walikuwa watanzania. Baada ya Elvine kupoteza kumbukumbu hakuweza kupata taarifa zozote kutoka kwa rafiki zake maana hakuwahi kuwaambia historia yake kamili.

Kila likizo rafiki zake walikuwa wakirudi Tanzania kwenye familia zao lakini Elvine hakuwa anajua kama kwao ni Tanzania, japo rafiki zake walimuambia, lakini hakuwa anaamini maana hata kiswahili kilianza kumpotea kichwani, jambo ambalo liliwafanya rafiki zake waanze kumfundisha tena kiswahili.

Baada ya miezi mitatu kupita Exhao aliaanza kujihisi tofauti sana. Na baada ya kupima aligundua kuwa anaujauzito wa miezi mitatu. Hakuamini kabisa maana alishawahi kuambiwa kuwa hatopata mtoto kabisa. Exhao alifurahi sana lakini hata mume wake alifurahi zaidi. Baada ya Exhao kujua kuwa kabeba mtoto wa kike tumboni mwake ndipo alipokumbuka ile siku ambayo Elvine alipokuwa akiwaka moto pale hospitali, na akakumbuka maneno ya Elvine kuwa "huyu ni mdogo wangu Elvila" kwahiyo mtoto alipewa jina la Elvila kama Elvine alivyosema ile siku, na baada ya hayo Exhao ndipo alipomsimulia Mr. Ezhu yang kilichotokea kule hospitali ule usiku. Wote walianza kumpenda sana Elvine na wakaona kama ni mtoto wa baraka na miuzija kwenye familia yao.

Elvine alisoma hadi akafika chuo kikuu na akawa hajui kabisa asili yake kuwa ni Tanzania. Rafiki zake walikuwa wakimwambia lakini hakuamini kabisa na yeye alikuwa akiwapenda sana wazazi wake na mdogo wake Elvila pasipo kujua ukweli.

Akiwa chuo yeye alikuwa hasali kabisa maana hata familia yake hawakuwa wanasali. Lakini Elimina na Ester walikuwa wanamwambia sana habari za yesu lakini hakuwa anaelewa. Emmanuel na Elvine walipofika chuo wakawa wasumbufu sana, maana walipenda kwenda 'clab' na Elvine akaanza kunywa pombe.

Elimina na Ester waliwaonya sana rafiki zao lakini hawakusikia. Taarifa za kunywa pombe kwa Elvine ziliwachukiza hata wazazi wake maana walikuwa wanamuona kama mtoto mtakatifu baada ya wao kupata mtoto. Lakini hali haikuwa kama walivyodhani, maana Elvine alikuwa ni shida pale nyumbani. Ilifika wakati anaweza akakaa nje wiki bila kurudi nyumbani.

Hali ilizidi kuwa mbaya na baadaye akaanza kuvuta bangi, makundi ya chuo yaliwaharibu kabisa, lakini "Mungu anawajua walio wake!". Siku moja akiwa amelala baa baada ya kulewa sana aliota ndoto.

"Moto mkubwa ulikua unawaka katika maji, Elvine alizidi kusogea pale huku akistaajabu sana, na aliogopa sana "haaa! hivi inawezekanaje moto uwake ndani ya maji? au ndio ile muvi ya jana inajirudia ila huu nii muendelezo wake? Akiwa anashangaa alimuona Eliana, Ester na Elvila pembeni na ilikuwa ni kanisani. Elvila akamwambia, 'Elvine wewe si mtumishi wa mungu eeh?'"(zilikuwa ni kumbukumbu za utotoni)

Elvine alishituka sana na akajikuta baa, aligundua kuwa kaibiwa hela zote alizokuja nazo siku hiyo baa. Moyo ulianza kuuma na akawa anasikia sauti kichwani mwake ya mtu ambaye alikuwa akipiga kelele akimwambia " wewe ni naniiiii!? Wewe ni naniiiii? Wewe sio Elvine" alianza kuona kizunguzungu, alilia sana pasipo kupata msaada na ndipo akamkumbuka Editrin mama yake. Akasema "mama yangu ni Editrin!!!...

 Sehemu ya tano itaendelea jumatano >>>>>. Usikose kufuatilia.

Bonyeza hapa kupata mwendelezo wake

Hadithi hii imendaliwa na kuandikwa na JACQUELINE JOHN.

Mwimbaji na mtunzi wa nyimbo, mashairi, Hadithi (simulizi) na ngonjera.

 Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255789523850. Normal >>>>>+255747313148.

                            Na, 

Imehaririwa na MIGONGO ELIAS. Mhariri.

Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255767653697. Normal >>>>>+255783327456.

 

GeT tO tHe NeXt LeVeL!

Kama umejifunza kitu shiriki nasi katika comment hapo chini, ili kujifunza na kuboresha zaidi.

 

 

 

 

 

 

 

 


Comments (4)

Loading... Logging you in...
  • Logged in as
Story nzu ri saana
1 reply · active 94 weeks ago
Ahsante nashukuru Ndugu
Simulizi nzuri yenye kusisimua na mafundisho ndani yake. Nasubilia kwa hamu sehemu ya Tano.
1 reply · active 94 weeks ago
Inakuja soon

Post a new comment

Comments by

Popular posts from this blog

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

VITU 9 MUHIMU KWA MTU YEYOTE KUJIFUNZA KWENYE MAHAFALI.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.