HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31
.jpeg)
SIMULIZI
YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”.
SEHEMU
YA TANO.
Ilipoishia..........
Kama hujasoma sehemu iliyopita bonyeza hapa
Kwa hasira aliyokuwa nayo alipanga kurudi
nyumbani na kuleta fujo kwa Mr. Ezhu yang lakini akakumbuka asili yake ya kweli
kuwa yeye ni mtoto wa kikristo na hakufundishwa tabia mbaya wala ugomvi na mama
yake Editrin.
Aliwaza cha kufanya akakosa majibu. Mwisho
aliamua kurudi nyumbani ili akapate taarifa kamili kutoka kwa walezi wake wale.
Akiwa njiani kurudi nyumbani alikutana na
Elimina.
"Elvine!"
"Yes"
"Are you ok?"(upo sawa)
"I don't know Elimina, I don't
know."(sijui Elimina, sijui). Elvine alipomtazama Elimina alishindwa
kujizuia kabisa na machozi yalianza kumdondoka. Elimina alishangaa maana
hakuwahi kumwona Elvine kwenye hali ile toka amfahamu. Mwisho Elimina alimshika
mkono na kutafuta hotel nzuri ili waweze kuzungumza. Elvine alimsimulia
historia yake kwa urefu sana hasa maisha yake alipokuwa mdogo, namna
alivyojikuta China, na namna alivyojikuta kapoteza kumbukumbu.
Elimina alionyesha kuguswa sana na stori ya
Elvine na yeye akawa anatamani sana kujua sababu ya Elvine kuletwa China na
kuhusu mama yake Editrin. Kama ilivyo kwa Elvine na ndivyo ilivyokuwa kwa Elimina
maana Elimina alionekana kuwa na tabia nzuri sana na moyo wa huruma sana, hivyo
wakakubaliana kuwa watakwenda wote kufuatilia kuhusu sababu ya Elvine
kutenganishwa na mama yake maana walihisi itakuwepo sababu.
Elimina naye alimueleza Elvine kuwa yeye ni
mtoto wa mchungaji anayeitwa 'Moses'. Na hapo ndipo Elvine alipomtambua Elimina
kuwa ni yule mtoto aliyewahi kumuona akiwa mdogo, Elvine Alishangaa sana na
mwisho akajikuta kasema
"kumbe ni wewe?"
"Mimi nini?"
Baba yako niii... Elvine alisita kidogo na
akajikuta katabasamu, halafu hakuendelea kuzungumza. Elimina hakujua kama
walishawahi onana wakiwa Tanzania.
Wakati huo Elvine alikuwa kasha pata wazo na
namna anavyoweza kumtumia Elimina kufika kwao, kwahiyo aliamua kukaa kimya
kwanza.
*
* * *
* * *
* *
Huku
Tanzania baada ya Elvine kupotea Editrin aliamua kukubali kuambatana na mama
yake, hivyo alirejea tena Dar es salaam kwa baba yake na mama yake. Alipofika
nyumbani baba yake alionyesha kufurahia sana binti yake kurudi nyumbani.
Mr. Edward hakumsumbua tena binti yake na
aliomba msamaha lakini hakukili kosa la kumuua Edwin. Editrin alishindwa
kumsamehe baba yake kabisa kwasababu ya Edwin, na alikuwa akimchukia sana baba
yake maana alimuona kama shetani kwake maana kwake yeye aliona baba yake ndiye
chanzo cha kusambalatika kwa familia yake.
Editrin akiwa kwa baba yake alishangaa
sana namna baba yake alivyobadilika na kuwa mpole sana. Mr. Edward alibadilika
na akawa ni mtu mwenye mawazo sana na mara nyingi alikuwa akichelewa nyumbani
jambo ambalo lilimfanya mama yake Editrin kuwa na mgogoro na mumewe kila siku
kwa kuhisi mumewe kaanza uhuni.
Mr. Edward alizidi kuonekana kama mtu
asiye na amani kabisa, na mwisho alianza ulevi na uchelewaji ukazidi.
Siku moja Editrin aliamua kumfuatilia baba
yake ili ajue baba yake huwa anakwenda wapi baada ya kutoka kazini maana
alimhurumia sana mama yake kwa namna alivyokuwa hana amani, lakini pia alifanya
hivyo kwakuwa mama yake ndiye aliyemuomba afanye kazi hiyo.
Alifika nje ya ofisi ya baba yake na
gari lake ambalo alipewa baada tu ya kurudi kutoka Iringa. Hakushuka haraka
kutoka garini bali alisubiri baba yake amalize kazi, na alijua kuwa akiwa pale
ataweza kuona kila mtu atakaye kuja pale ofisini siku hiyo.
Alikaa pale nje hadi jioni; alihisi njaa sana. Hivyo akashuka kwenye gari
na kuenda kununua chakula kwenye hoteli iliyokuwepo jirani na ofisi ya baba
yake. Alinunua chakula na kurudi tena kwenye gari lake.
Alikaa garini kwa mda mrefu hadi giza
likaingia lakini hakuona baba yake akitoka ofisini, alipotazama kwa makini
aligundua kuwa kuna gari lipo pembeni ya gari lake ambalo hakuliacha wakati
anaenda kununua chakula. Hivyo aligundua kuwa kuna mtu kaingia ndani ya ofisi.
Alikaa hadi saa 2:50 usiku na akaona
kachoka kusubiri, hivyo aliwasha gari na kuondoka.
Alipofika nyumbani alimwambia mama yake kuwa baba yake hajatembelewa na mtu
yeyote leo na wala hajatoka ofisini.
Kiukweli alidanganya lakini hakuwa na uthibitisho ambao ungemfanya aseme ni
nani aliyekuja ofisini siku hiyo.
Ulipofika Usiku muda kama wa saa
5:20 hivi alisikia kelele za baba yake kutoka sebuleni, kelele zile ziliashiria
kabisa kuwa baba yake kalewa. Na alipiga kelele za
kumuita yeye.
Zile kelele ziliwashitua hata wafanyakazi wa mule ndani hivyo wote walikuja
sebuleni kuona ni nini kinachoendelea. Editrin na mama yake pia
waliwasili sebuleni.
Mr. Edward baada ya kumuona
Editrin amekuja sebuleni alimfuata na kumpiga vibao viwili vya mfululizo ambavyo vilikuwa ni vizito
mno kwa Editrin. Jambo lile liliwashitua watu wote
pale ndani. Mr. Edward akaanza kufoka kilevi huku akitoa akonyesha kuongea kwa uchungu kama anayetaka kulia.
" Hivi we mtoto mbona unabalaa? Mimi
mbona nimekuacha na maisha yako, lakini wewe hutaki nikuache?. Haya niambie sasa,
ofisini kwangu ulikuja saa ngapi? Na nani alikuita kule?
Mimi ningekua nataka uje kazini si ningekuita?. Wewe mtoto huna akili. Na mimi
sikutaki tena."
Editrin alilia sana na kwauchungu
na yeye akajibu kwa hasira sana
"Kwani nani kasema mimi wewe ni baba
yangu, kwakweli nazidi kujua namna ambavyo unanichukia. Sawa nitaondoka na
sitaki mnitafute, niacheni na maisha yangu basi. Yaani umeharibu familia yangu
bado huridhiki tu? Au unataka nife na mimi?" Editrin aliongea kwa hasira
sana na baada ya kuongea vile aliondoka mpaka
chumbani kwake ambako alijifungia na kulia sana. Haikuwa hivyo kwake tu
hata Mr. Edward aliingia chumbani na akawa analia sana huku akisema kwanini
imekuwa hivi.
Mkewe hakujua ni nani amfariji kati ha
binti yake au mume wake Edward. Lakini hakuwa anajua kwanini Edward
analia kiasi kile. Edward alionekana ni kama anayejutia jambo,
lakini hakuweza tu kueleza. Eliana alihisi labda
pombe ndizo zilizomchanganya mumewe.
Asubuhi Mr. Edward aliondoka mapema sana
na kwenda kazini. Editrin alipoamka alikuwa kashajiandaa kuondoka pale nyumbani pasipo kujua hata anakwenda wapi, lakini mama yake aliomba
msamaha mwa niaba ya mume wake na akamsihi binti yake asiondoke.
Usiku ulipofika Editrin alikuwa nje ameketi
kwenye amua anawaza kuhusu maisha yake. Akiwa pale aliona gari la baba yake
linaingia, wakati anaendelea kuwaza alimwona baba yake akipokea simu na
alionekana kugombana na mtu.
"Hivi wewe shida yako ni nini?, Wewe
umeshaoa? ...... Huwezi kusema makubaliano hayajavunjika wakati wewe
tayari una familia. .... Nimesema hapana Editrin siwezi kumtumia kama bidhaa
tena. ... . Sawa lakini ..... Haiwezekani unifanyie hivyo .... Hivi lazima awe
Editrin tu?. Hapana... Hapana.... Sina maana hiyo". Simu ikakatwa, Mr
Edward alichukia sana na akaingia ndani
kwa hasira sana na leo hakuwa kalewa Kama siku nyingine na pia aliwahi kurudi
nyumbani.
Yale mazungumzo yalimfanya Editrin apate
maswali mengi sana, na ndipo akaanza kuhisi kuwa kuna jambo nyuma ya pazia
ambalo yeye anaweza kuwa halijui.
Alisubiri baba yake aingie ndani na yeye
ndipo alipoingia ndani na kwenda kulala. Usiku aliwaza sana. Akiwa katika
mawazo mengi sana alipitiwa na usingizini na ndipo alipoota ndoto ambayo
ilimfanya aone Edwin hakuuwawa na baba yake bali ni mtu
mwingine ambaye ndotoni hakumtambua kabisa lakini sio baba yake.
Alishituka sana lakini akajisemea mwenyewe kuwa ile ni ndoto tu.
Asubuhi alipoamka alikosa amani kabisa na
kile alichokiota kikawa kinazidi kuitesa akili yake. Alimsimulia mama yake
ambaye alimwambia aendelee kuomba Mungu wake tu maana hata haelewi chochote.
Editrin aliamua kumfuatilia baba yake tena
na wakati huu hakuishia nje ya ofisi bali aliingia
hadi ndani ya ofisi ili apate ukweli kamili
wa yeye kuzuiliwa kwenda ofisini kwa baba yake. Ofisini alimkuta baba yake
anaendelea na kazi zake za kila siku.
Kitendo cha Edward kumwona binti yake
ofisini kilimshitua sana, jambo ambalo hata Editrin aliligundua, yule baba
alisogea kwa Editrin na akamwambia hatakiwi kuwepo pale muda ule labda wakati
mwingine. Editrin hakuwa tayari kuondoka. Mr
Edward alijishusha na akaanza kama kumbembeleza kwa upole Editrin aondoke.
Editrin alishangaa sana, alipomuuliza sababu alimwambia atakuja kumwambia pindi
atakaporudi nyumbani. Wakati wanaendelea kubishana, ghafla aliingia Esau ambaye naye alionyesha
kutotarajia kumwona Editrin pale.
"Haa Editrin? Ni wewe kweli? Oooh
dear ni muda sana hatujaonana, hivi umerudi lini? Maana kuna siku nilikuona kwa
mbali lakini sikuwa na uhakika kuwa ni wewe" baada ya kusema vile Editrin
aligundua sababu ya baba yake kurudi ule usiku akiwa na hasira,
"Inamaana lile gari lilikuwa la Esau na
Esau ndiye aliyeniona mimi na kwenda kumwambia baba japo mimi sikumuona. Sasa
kwanini Esau anaonekana kama anajambo
la siri na
baba yangu?" Editrin alijiuliza kimoyo moyo.
Mr. Edward alimwambia Editrin akakae nje
mara moja. Editrin alikubali kuwapisha kidogo. Lakini hakwenda mbali bali
alijibanza ukutani na kuanza kuwasikiliza.
"Sikiliza Esau Mimi siwezi kuruhusu
umuoe Editrin, maana nimegundua wote ni ujinga, halafu mbona baba yako katulia
tu hana shida, tatizo lako ni nini wewe? Halafu isitoshe wewe tayari
unamke."
"Ooh, hilo lisikutishe
Mr. Edward. Mimi bado nampenda binti yako sana tu, na hata sijali kuhusu hilo.
Nachotaka ni kuwa lazima wewe unipe Editrin"
"Kwani kunaulazima gani wa
wewe kufanya hivyo?"
"Sikiliza mzee, hii pia ni biashara, na sitaki kubishana maana malikia wangu mtarajiwa asije
akasikia hapo nje halafu ikawa balaa. Kama nilivyokwambia mwanzo wewe fanya
maamuzi kati ya mimi kuivuruga hii kampuni yako ya "A quality" au
kunipa binti yako. Na Kama unavyojua mimi nikisema nimeshasema.
Uamuzi ni wako mzee"
Editrin alisikia yale yote na ndipo
alipogundua kuwa baba yake hakuwa anamuozesha yeye kwakupenda lakini alikuwa
akilazimishwa na Esau na familia yake kwasababu za
kibiashara maana, Esau na familia yao walikuwa matajiri kuliko wao. Sasa Editrin akawa
na swali moja kichwani "kwanini baba yake ahusike kwenye kifo cha mumewe? Na kama hahusiki basi kuna kitu anajua, sasa kwanini akae kimya?"
Editrin
aliamua kuondoka kwenda kanisani; maana ilikuwa jumatano siku ya ibada ya
jioni.
Alipofika kanisani ibada ilikua haipandi kabisa maana alikuwa na vitu
vingi sana kichwani. Siku hiyo alimuona mtoto mdogo pale kanisani ambaye umri
wake ulifafa sana na Elvine kabla hajapotea. Editrin alijikuta akimkumbuka sana
kijana wake, na hapo ndipo aliposhindwa kujizuia baada ya kuikumbuka familia
yake na kuanza kulia, moyoni mwake alikua na neno moja tu "walionidhurumu
familia yangu lazima walipe hata Kama ni baba yangu. Sitomsamehe".
Kanisani somo
la msamaha lilihubiriwa sana, lakini hayakuwahi kupata nafasi kwake. Somo la
msamaha lilipohubiriwa alikuwa akilia sana jambo ambalo wengine wangeweza
kuhisi labda kashukiwa na roho wa Bwana au amesamehe mtu aliyemuumiza sana. Lakini
ukweli ni kuwa alikuwa akilia kuomba msamaha kwa Mungu kwa kusema Mungu
amsamehe tu lakini hawezi kusamehe mpaka adui zake walipe ubaya wao. Neno la
muachie Mungu lilimkera japo alikuwa wa kwanza kusema Amina! Lakini haikuwa ya
kweli maana moyoni mwake ulijaa uchungu usiopimika.
Akiwa kanisani baada ya ibada kuisha, aliamua kufanya maamuzi magumu
sana ili tu aweze kumpata adui wa familia yake, hivyo alisogea mbele ya
madhabahu na akasema maneno machache tu lakini yalibeba uchungu na kiapo hatari
sana.
"Mungu nisamehe kwa huu uamuzi lakini no matter what, lazima nimjue
aliye na mtoto wangu na aliyemuua mume wangu. Mungu ni rehemu Kwahaya maamuzi lakini
naomba baraka zako maana siwezi kukaa kimya tena. Mpaka hapa nilipofikia basi
inatosha Mimi kuumia, maana nahisi hata mtoto wangu hawa watu ndio wanajua
aliko. Huu ndiyo mwanzo, nipo tayari kufa, maana Sina cha kupoteza. nisamehe sana ila niruhusu tu mimi nifanye
hivi please..."
Sehemu ya tano itaendelea ijumaa
>>>>>. Usikose kufuatilia.
Bonyeza hapa kupata mwedelezo wake
Hadithi
hii imendaliwa na kuandikwa na JACQUELINE JOHN.
Mwimbaji
na mtunzi wa nyimbo, mashairi, Hadithi (simulizi) na ngonjera.
Mawasiliano:
Whatsapno.
>>>>> +255789523850. Normal >>>>>+255747313148.
Na,
Imehaririwa
na MIGONGO ELIAS. Mhariri.
Mawasiliano:
Whatsapno.
>>>>> +255767653697. Normal >>>>>+255783327456.
GeT tO tHe NeXt LeVeL!
Kama
umejifunza kitu shiriki nasi katika comment hapo chini, ili kujifunza na
kuboresha zaidi.