Posts

Showing posts from August, 2023

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23. Ilipoishia...... Alipofika nje, alimkuta Elimina katahamaki sana tena anahasira sana.  "Umefanya nini Elvine? Elimina aliuliza kwa ukali sana tena hadi macho yalikuwa mekundu kama damu kwaajili ya kujaa hasira.... Swali; kwanini Elimina anahasira? Na Elimina huyu anasiri gani na nyumba iliyoungua moto? Kusoma sehemu ya 22 bonyeza hapa   Sasa inaendelea...... Elvine alikuwa anatetemeka  kwa hofu ya yale anayoyaona lakini alistaajabu kuona ni kama mkewe hajali sana kuhusu yeye. Alimtazama kwa makini sana mkewe akiwa anajaribu kutafakari kwanini anaonekana kuwa na hasira juu yake. Elimina akajishitukia "Hey, wewe! Nini sasa unanitazama hivyo?" "Nakutafakari sipati majibu!' "Nimefanyaje kwani?" "Hamna ila sijajua kama umenihofia mimi au hilo swali lako linamaana gani? "Elvine baba sina maana hiyo uliyoelewa wewe kabisa. Shida yangu mimi umefanya nini mpaka unataka kuhatarisha maisha Yako namna hii. Hujui namna ga

TIBA YA KUKATA TAMAA.

Image
    TIBA YA KUKATA TAMAA. Uhali gani ndugu msomaji! Bila shaka hujambo   na kama si hivyo basi Mungu akusaidie sana . Karibu katika mtandao wa addvaluenetwork tujifunze kwa pamoja, ambapo leo tunakwenda kuangali moja kati ya njia muhimu na makini katika kuondosha hali ya kukata tamaa. Kipindi cha nyuma nimewahi kuandika makala nzuri sana juu ya KUKATA TAMAA    na makala hiyo umesomwa na watu wengi sana,na huko  nilieleza sababu kadhaa zinazowafanya watu wakate tamaa mapema    katika maisha yao. Unaweza kuisoma sasa hapahapa addvaluenetwork ili kujifunza mengi. Lakini pamoja na hayo ngoja   nikwambie maana ya kukata tamaa ambayo ni ile hali ya kukosa tumaini la kuendelea mbele na kuona uwezo wako wa kupambana na changamoto hiyo ni mdogo kuliko tatizo lenyewe. Ukweli ni kwamba kila mtu anachangamoto zake ambazo hukutana nazo katika maisha ya kila siku. Zipo changamoto za fedha, changamoto za afya, changamoto za mahusiano au ndoa, changamoto binafsi, changamoto za kiroho na nyinginea

ACHA KUJARIBU, ANZA KUFANYA.

Image
  ACHA KUJARIBU ANZA KUFANYA. Hivi ulishawahi kuona mtu anauwezo wa kufanya au wa kukusaidia jambo lakini ukimwambia kufanya hivyo utashangaa anakwambia goja nijaribu . Wakati mwingine unakuta mtu anatamani kabisa kufanya au kufanikiwa jambo fulani, lakini utashangaa anakwambia ngoja nijaribu kama nitafanikiwa . Mwingine   akiwa darasani au kwenye kikao swali likiulizwa katika kulijibu utashangaa goja na mimi ni jaribu . Na maneno mengi tu ambayo hayaendi moja kwa moja katika kufanya badala yake watu hujificha katika kivuli cha   kujaribu huku wakijikuta wanashindwa kabisa kufanya. Wapo watu wenye mipango na mawazo lukuki tena adimu kutokea ambayo kufanikiwa kwayo ni swala la muda tu. Sasa badala ya kuyafanyia kazi utakuta mtu anakwambia sijui kama nitaweza labda ngoja nijaribu. Wengine wanatamani sana kufanikiwa eneo fulani mfano utakuta mwingine anatamani sana kuajiriwa badala ya kutuma maombi anasema ngoja nijaribu kutuma maombi. Penmgine utakuta mtu ameitwa na kwenye usaili lak

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.

Image
SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU. “ Sometimes your joy is the source of your smile, but sometimes your smile can be the source of your joy.” Wakati mwingine furaha yako ni chanzo cha tabasamu lako, lakini pia tabasamu lako linaweza kuwa chanzo cha furaha yako. Tunaishi kwenye dunia ambayo watu wamevurugwa na maisha, huku wakiwa bize au sirious na maisha yao.   kana kwamba kuona tabasamu na furaha yao imekuwa ni adimu sana. kwa kawaida tabasamu na kucheka huwa ni viashiria vionekanavyo katika kuonyesha au kuashiria furaha, licha ya kuwa vipo viashiria vingine lakini tabasamu na kicheko hutafsirika mapema kama viashiria vya furaha. Wakati mwingine mtu anaweza akacheka na kutabasamu lakini akawa na machungu ndani yake goja tuachane nayo leo hii. Tafti zinaonyesha kuwa mtoto mdogo mwenye umri wa miaka 4-6 hucheka mara 300-400 kwa siku huku mtu mzima hucheka mara 15 tu kwa siku huu ni utafri ambao haujathibitishwa. Lakini kilichothibitishwa ni kwamba kucheka na kutabasamu kunaimarisha mai

HIKI NDICHO HUJUI KUHUSU KULALAMIKA.

Image
  HIKI NDICHO HUJUI KUHUSU KULALAMIKA. Ndugu msomaji nakusalimu! Bila shaka u mzima   na kama sivyo Ikawe heri kwako. Karibu tena ndani ya addvaluenetwork tujifunza kwa pamoja ili kuongeza maarifa yatakayoongeza thamani ya kila mmoja. Kupitia mtanadano huu utajifunza mengi kuhusu uchumi, saikolojia, maendeleo binafsi, na   maisha kwa ujumla.  Kwani, wengi wameripoti kujifunza na kuponywa katika changamoto zao. Hivyo nikukaribishe sana na wewe upate kujifunza pamoja nasi. Uhakika wangu ni kwamba, hutabaki kama ulivyo mara tu baada ya kusoma hapa.  Na kama utaweza mwalike na rafiki yako, na rafiki yako amwalike rafiki yake na yeye amwalike rafiki yake pia ili sote tujifunze. Sasa leo nataka tujifunza kitu kimoja muhimu sana ambacho utapata kitu cha kusonga nacho. Kitu hiki ni kulalamika. Watu wengi wamekuwa na kasumba ya kulaumu watu wengine, hasa wanapokutana na ugumu wowote katika maisha yao au pengine mambo yao kutokwenda kama walivyo panga.  Hapo ndipo watatafuta watu wa kuwalau

TUMIA NJIA HII KUTATUA CHANGAMOTO YAKO.

Image
  TUMIA NJIA HII KUTATUA CHANGAMOTO YAKO. Hello ndugu msomaji! Ni matumaini yangu kuwa upo salama, vinginevyo Mungu akusaidie sana upate kuwa sawa. Nikukaribishe tena lkatika andiko hili tupate kujifunza kwa pamoja ili tuongeze thamani kisha tusonge   mbele. Ni wazi kuwa hakuna binadamu asiyepitia changamoto yeyote katika dunia hii. Kwenye biashara kuna chanagamoto zake, kwenye ndoa kuna changamoto zake, kwenye kilimo kuna changamoto zake, kwenye ufugaji kuna changamoto zake, kwenye uvuvi vivyo hivyo, kwenye elimu zipo pia, na sehemu zingine utakutana nazo sana. changamoto hizo zaweza kuwa; kufeli, kukata tamaa, maneno hasi, changamoto za afya, mahusiano, kazi, n.k .   Yote kwa yote aidha uwe mwema sana au katili sana utakutana nazo, uwe upole au mkali, uwe mtu maarufu au wa kawaida tu utakutana nazo, uwe unasali sana au husali utakutana nazo. Na katika hili tambua kuwa unapomwamini Mungu haimanishi kuwa hautapitia katika changamoto laahasha, bali hata utakapopitia katika magumu Mung

JIFUNZE KUJIFUNZA PART VIII.

Image
  JIFUNZE KUJIFUNZA   PART VIII. KANUNI ZINAZOENDESHA KUMBUKUMBU NDANI YA AKILI YAKO. Ndugu msomaji u hali gani! Bila sha haujambo   na unaendelea vyema, na kama si hivyo Mungu akupe wepesi katika hilo. Kama utakuwa unafuatilia somo hili la jifunze kujifunza utakumbuka kuwa   tuliishia part vii huko tumejifunza mambo   kibao na kama hujasoma au kufuatilia sehemu zilizopita ni wazi kuwa kuna vitu umekosa. Lakini habari njema kwako ni kuwa kupitia hapa hapa addvaluenetwork unakwenda kuyapata masomo yaliyopita hivyo fuatilia kupitia linki hapo chini. Kusoma part vii bonyeza hapa Kama ilivyo kwa bank kuhifadhi pesa, ghala kuhifadhi chakula, tank kuhifadhi maji, mtungi kuhifadhi gasi, zizi kuhifadhi mifugo, nyumba kuhifadhi watu na mali zao, flash kuhifadhi taarifa, ndivyo ilivyo kwa akili kuwa na MEMORY ya kuhifadhi taarifa na michakato mingine   ndani ya ubongo wa mwanadamu. Niseme tu kuwa hii ndiyo sehemu ambayo inatunza na kuhifadhi kumbukumbu zako, watu hukumbuka matukio mbali m

JIFUNZE KUJIFUNZA PART VII.

Image
                                                      JIFUNZE KUJIFUNZA PART VII. VIKWAZO KATIKA KUJIFUNZA . Rafiki wasalaamu! Karibu katika mwendelezo wa somo letu pendwa   la ajifunze kujifunza ambapo, tunazidi kuchanja mbuga na sehemu ya saba sasa, huku tukiwa tumejifunza mambo kedekede hapo nyuma. Na kama hujafuatilia nikusihi ufanye hivyo ili upate kujifunza mengi zaidi hapa hapa ADD VALUE NETWORK . kusoma part vi bonyeza hapa Leo   tunayo sehemu yetu nzuri ya saba ambapo tunakwenda kutazama kinaga ubaga   vikwazo na changamoto katika kujifunza. Kwani, watu wengi wanaofahamu na wasiofahamu kuwa wanapaswa kujifunza kila leo na pengine wanafahamu kabisa ni kipi wajifunze na wapi wajifunzie lakini bado wengi wao imekuwa ni changamoto kwao kujifunza vitu ambavyo wanatamani kuvifahamu lakini   kwakujua au kutokujua wanakutana na changamoto kibao ambazo huwafanya wasianze kabisa au pengine wasisonge mbele mara baada ya kuanzisha zoezi la kujifunza kwao. Kitu hiki kimekuwa kama ad

JIFUNZE KUJIFUNZA PART VI

Image
  JIFUNZE KUJIFUNZA PART VI NGUVU YA ZAWADI KATIKA KUJIFUNZA. Ndugu msomaji wasalaamu! Nikukaribishe tena katika mwendelezo wa somo letu pendwa la jifunze kujifunza , ambapo tumeona na kujifunza mengi sehemu zilizopita. Hadi sasa tupo katika sehemu ya sita. Lengo kubwa likiwa ni kufahamu   akili zetu, zinafanyaje kazi,   namna gani tunaweza kuzitumia, huku tukigundua kuwa Kujifunza kujifunza ni eneo muhimu sana ambalo limesahaulika sana katika jamiii zetu. Vitu kama hivi mara nyingi haviwekwi kabisa kwenye mitaala ya elemu, siyo afrika wala kule kwa mabeberu. Hivyo   kwasababu ya umuhimu wake ADD VALUE NETWORK imeamua kuzamia ili kukutafunia na kukuletea kwako kupitia hapahapa add value network kazi yako ni kumeza na kula tu! kusoma sehemu iliyopita bofya hapa  Sasa twende pamoja tujifunze kwa pamoja; Sehemu ya leo tunakwenda kuangalia nguvu ya zawadi katika kujifunza   kwakuwa tunazungumzia kuhusu zawadi, ni muhimu tukafahamu maana halisi ya zawadi. Katika hili kamusi ya kiswa

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.