HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

TUMIA NJIA HII KUTATUA CHANGAMOTO YAKO.

 

TUMIA NJIA HII KUTATUA CHANGAMOTO YAKO.

Hello ndugu msomaji! Ni matumaini yangu kuwa upo salama, vinginevyo Mungu akusaidie sana upate kuwa sawa. Nikukaribishe tena lkatika andiko hili tupate kujifunza kwa pamoja ili tuongeze thamani kisha tusonge  mbele. Ni wazi kuwa hakuna binadamu asiyepitia changamoto yeyote katika dunia hii. Kwenye biashara kuna chanagamoto zake, kwenye ndoa kuna changamoto zake, kwenye kilimo kuna changamoto zake, kwenye ufugaji kuna changamoto zake, kwenye uvuvi vivyo hivyo, kwenye elimu zipo pia, na sehemu zingine utakutana nazo sana. changamoto hizo zaweza kuwa; kufeli, kukata tamaa, maneno hasi, changamoto za afya, mahusiano, kazi, n.k .  Yote kwa yote aidha uwe mwema sana au katili sana utakutana nazo, uwe upole au mkali, uwe mtu maarufu au wa kawaida tu utakutana nazo, uwe unasali sana au husali utakutana nazo. Na katika hili tambua kuwa unapomwamini Mungu haimanishi kuwa hautapitia katika changamoto laahasha, bali hata utakapopitia katika magumu Mungu atakupa uwezo wa kushinda changamoto hizo.

Na leo kupitia hapahapa kwenye mtandao wetu pendwa wa ADD VALUE NETWORK tumekuletea njia moja mathubuti utakayo itumia katika kutatua matatizo na changamoto yeyote inayokusibu. Hivyo fuatana nami mwanzo hadi mwisho ili  kujifunza zaidi;

Njia hiyo ni SELF-COUNSELING  yaani, KUJISHAURI MWENYEWE. Hapa namaanisha kuwa, kuna namna mtu unaweza kujishauri mwenyewe hata ukafanikiwa kutatua tatizo yako ingawa inategemeana na aina na ukubwa wa tatizo hilo. Lakini kama utajua nguvu ya mawazo ambayo upo nayo utaweza kutoboa katika eneo hili. Kwani, kwa kawaida binadamu huwa  yanakuja mamilioni ya mawazo ndani yake, yakizunguka zunguka huku na kule  na kama ataamua kuyafanyia kazi ndani na kuyatekeleza  yanaweza kumvusha kwenda katika hatua anayo itaka. Sasa kupitia nguvu ya mawazo hayo mtu anaweza kuyatumia vyema ili kutatua matatizo yake.

JINSI YA KUFANYA.

Kama utakutana na changamoto au tatizo lolote ndani yako jiulize kuwa kama changamoto au tatizo hili lingempata rafiki yangu na akaja kwangu ili kutaka ushauri je, ningemshauri nini ili kuondokana na changamoto yake? Hapo ndipo utakapo shangaa na kuona jinsi utakapo pata wazo lililo bora kupitia mamilioni ya mawazo yanayo kuja ndani yako yakizunguka zunguka ili yafanyiwe kazi.

Labda nikuulize swali je, unachangamoto ya kujua ni biashara gani ufanye? Jibu ni rahisi tu, nalo ni kujiuza kuwa je rafiki yangu ninaye mwamini angekuja na changamoto kama hiii huku anataka mawazo yako ungemshauri nini? Hilo ndilo jibu fanyia kazi. Je, unachangamoto kuhusu mahusiano yako? Jibu ni rahisi tu, nalo ni kujiuza kuwa je rafiki yangu ninaye mwamini angekuja na changamoto kama hiii huku anataka mawazo yako ungemshauri nini? Hilo ndilo jibu fanyia kazi. Je, unachangamoto ya kukata tamaa mapema? Jibu ni rahisi tu, nalo ni kujiuza kuwa je rafiki yangu ninaye mwamini angekuja na changamoto kama hiii huku anataka mawazo yako ungemshauri nini? Hilo ndilo jibu fanyia kazi. Je, unachangamoto ya kutokuwa na nidhamu ya fedha na muda? Jibu ni rahisi tu, nalo ni kujiuza kuwa je rafiki yangu ninaye mwamini angekuja na changamoto kama hiii huku anataka mawazo yako ungemshauri nini? Hilo ndilo jibu fanyia kazi. Je, unachangamoto gani  inakusumbua? Jibu ni rahisi tu, nalo ni kujiuza kuwa je rafiki yangu ninaye mwamini angekuja na changamoto kama hiii huku anataka mawazo yako ungemshauri nini? Hilo ndilo jibu fanyia kazi.

Kupitia njia hii ya kujishauri mwenyewe kama itatumika vyema itakuwa msaada mkubwa sana katika kukabiliana na changamoto mbali mbali zinazo tukabili katika maisha ya kila siku. Na hapo utakuwa umeanza kuyafaidi mawazo yako.  Usiyadharau mawazo yako hebu jaribu njia hii itakusaidia sana, jiamini na yakubali mawazo yako  na anza kuyafanyia kazi.

Onyo!

kabla ya kuanza kulifanyia kazi wazo lako lipime kwanza kama ni wazo sahihi au siyo sahihi na kisha lithibitishe kwa kulifanyia kazi, ukiona limefanya kazi endana nalo na ukiona halijafanya kazi jaribu tena, likishindikana achana nalo kisha angalia wazo lingine si unajua yapo mamilioni ya mawazo eeh! Wakati mwingine ukiona mambo yamefika shingoni tafuta ushauri kwa wataalamu au ktafuta watu unao waamini watakusaidia katika hilo.

Ni imani yangu kuwa makala hii itakusaidia sana kitu kikubwa tu ni kwamba usiishie tu kusoma na kupongeza hapa bali soma na litakalo kupendeza anza kufanyia kazi mara moja. Matokeo utayapata naamini utaipenda.

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluenetwork. Karibu sana ujiongezee thamani yako.

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe.

Instagram>>migongo_elias.

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe.

 

 

 

 

 

 

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.