UMASKINI VS UTAJIRI: VYOTE HUANZIA AKILINI.
UMASKINI VS UTAJIRI: VYOTE HUANZIA AKILINI. Watu wengi hudhani kuwa umaskini na utajiri ni ukosefu au wingi wa pesa na mali. Kwa kiasi fulani hilo linaweza kuwa kweli, lakini kuna ukweli mkubwa zaidi ambao mara nyingi watu hawauoni. Ukweli ni huu ni: umaskini na utajiri huanzia akilini kabla ya kuonekana mfukoni. Nakumbuka Mentor wangu mmoja kutoka Kenya, Konji Oloyi, aliwahi kuniambia maneno ambayo sikuyasahau: "Poverty and wealth are in the mind; lack or abundance are just signs. Many people confuse these." Akimaanisha kuwa umaskini na utajiri upo kichwani. Ukosefu au utele wa pesa ni dalili tu. Ndugu yangu, umaskini huanza kichwani. Kadhalika utajiri nao huanza kichwani. Ukosefu wa pesa mfukoni unaweza kuwa dalili ya umaskini, lakini hata kuwa na pesa nyingi mfukoni kunaweza kuwa dalili ya utajiri. Ndiyo maana Napoleon Hill aliandika katika kitabu kinachoitwa Think and Grow Rich. Kwa lugha rahisi ni: FIKRA zako zina mchango mkubwa sana katika kile unachokuwa. ...