KABLA HUJAITA MTU MJINGA, SOMA HIZI TABIA 10 MOJAWAPO INAKUELEZEA WEWE MWENYEWE.
KABLA HUJAITA MTU MJINGA, SOMA HIZI TABIA 10 MOJAWAPO INAKUELEZEA WEWE MWENYEWE. Hapa boss naenda kuelezea tabia, ishara au vitu vinavyoonyesha mtu huyu ni mjinga, hana busara, hekima wala ujuzi. yaani hajastarabika. Soma hadi mwisho ujikague mwenyewe. 1. ANAZUNGUMZA ZAIDI KULIKO ANAVYOSIKILIZA. Mdomo wake daima uko wazi, masikio yake daima yamefungwa, muhimu kwake ni kuongea tu wala hata kama hajui anachoongea pia hatoi nafasi ya wengine kuzungumza, yaani ukitaka tuuongee tayari ashadakia . Mtu mwenye busara, hekima au ujuzi wa kweli anajua kwamba ukimya wake una thamani zaidi ya maneno yake mengi. Husikiliza kwanza, hufikiria pili, kisha huongea na pale anapoongea, kila neno lina uzito na maana. Pia ni watu wanaoskiliza sana wengine bila kuwa katiza. 2. ANAPINGA KILA KITU BILA USHAHIDI/HOJA YEYOTE. Unajua boss, Kubishana ni rahisi. Kutoa hoja ya nguvu hiyo ndiyo ngumu kwa watu wengi. Mtu asiye na hekima, busara au ujuzi hupinga kwa nguvu lakini hana kitu cha maa...