Posts

LEVEL ZA MAFANIKIO SEHEMU YA NNE

Image
  LEVEL ZA MAFANIKIO SEHEMU YA NNE. Baada ya kufika hatua ya Business Owner level kama tulivyoangalia sehemu ya tatu. Watu wengi huendelea kubaki palepale kwa kufanya biashara maisha yao yote. Lakini wachache sana hupiga hatua na kujiuliza swali hili muhimu: “Nawezaje kufanya pesa zangu zifanye kazi badala yangu yaani zinifanyie kazi?” Na hapo ndipo inakuwa ni ticket ya kupanda kwenda hatua inayofuata: INVESTOR LEVEL (PESA ZINAFANYA KAZI KWA AJILI YAKO). HII NI LEVEL YA KUBADILI MCHEZO mzima boss wangu. Hapa hutegemei tena: muda wako, nguvu zako wala uwepo wako. ๐Ÿ‘‰ Unategemea: MTAJI WAKO na MAARIFA YAKO boss. MAANA HALISI YA HII LEVEL Investor siyo tu mtu mwenye pesa ndugu angu. ๐Ÿ‘‰ Ni mtu anayejua: wapi pa kuweka pesa, lini aweke, kwa nini aweke na namna ya kupunguza hatari za uwekezaji. BOSS TOFAUTI KUBWA NA LEVEL ZILIZOPITA NI KWAMBA, Kwenye Slavery mode → unafanya kazi ya mtu kwa pesa boss. Self-employed → unafanya kazi yako mwenyewe ili upata pesa. Business own...

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KABLA YA KUWEKEZA.

Image
  MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KABLA YA KUWEKEZA. Watu wengi wanavutiwa sana na faida za uwekezaji, lakini wachache sana hujiuliza swali muhimu kabla ya kuwekeza: “Je, huu uwekezaji unanifaa kweli?” Ukweli ambao nimejifunza ni kwamba, si kila uwekezaji ni mzuri kwa kila mtu boss. Kwasababu wengine huingia kwenye biashara, hisa, kilimo, au miradi mbalimbali kwa sababu tu wameona watu wengine wanafanya na kupata fedha. Mwisho wa siku wanajikuta wakipoteza pesa, muda, na amani ya moyo kwa sababu hawakufanya tathmini sahihi kabla ya kuwekeza. Boss kabla hujaweka pesa zako sehemu yoyote, kuna mambo muhimu sana unapaswa kuyafikiria kwa kina. Haya ndiyo yanayotenganisha mwekezaji mwenye akili na mtu anayekurupuka. 1. LENGO LA UWEKEZAJI Boss kabla hujawekeza, jiulize hivi: ๐Ÿ‘‰ “Ninawekeza kwa ajili ya nini?” Pengine: Unajiandaa kwa maisha ya baadaye? Unataka kujenga nyumba? Unajiwekea akiba ya elimu ya watoto? Unataka uhuru wa kifedha? Au unatafuta kipato cha ziada? Boss hapa tu...

NGUVU YA KUELEWA NA KIDHIBITI HISIA ZAKO.

Image
  NGUVU YA KUELEWA NA KUDHIBITI HISIA ZAKO. Watu wengi wanadhani kuwa, kuwa na nguvu ni kidhibiti, kushikiria na kukandamiza hisia zao. Lakini nimekuja gundua ukweli ni kinyume chake kabisa boss. Nguvu ya kweli ni kuelewa hisia zako, kuzikubali, na kuziongoza bila kuzifanya zikudhibiti wala kukucontrol boss. Kuelewa hisia zako ni uwezo wa kutambua: Unajisikiaje, kwa nini unajisikia hivyo, Na unapaswa kufanya nini bila kuharibu hali Huu ndiyo msingi wa kile kinachoitwa akili ya kihisia (emotional intelligence). Wakati mwingine huu ndo ustadi unaotofautisha kati ya watu wanaofanikiwa na wanaoishia kujilaumu wao wenyewe. Ndugu yangu huu ni uf unguo ya utulivu wa ndani na maamuzi sahihi ya maisha. MARA NYINGI TUMEFUNDISHWA KUELEWA HISIA NI ADUI KUTOKA NDANI YETU:  LAKINI UKWELI NI KWAMBA HISIA SI ADUI, BALI NI UJUMBE. Hii niflow of energy inayokuja na ujumbe maalum kwa muhusika. Hisia si tatizo. Hisia ni lugha ya ndani ya nafsi yako boss. Hata hivyo kila hisia unayopata in...

LEVEL ZA MAFANIKIO SEHEMU YA TATU.

Image
  LEVEL ZA MAFANIKIO SEHEMU YA TATU. Baada ya kupitia: Hatua ya Utumwa (kuuza muda ku-survive au kujikimu) Hatua ya Kujiajiri (kujitegemea kwa ujuzi wako) Sasa kuna watu wachache wanaofika hapa na kugundua ukweli mkubwa na watofauti kidogo: “Siwezi kukua kwa kufanya kila kitu mwenyewe lazima nijenge mfumo kwani ntachoka sana ma sitapatq matokea makubwa.” Kusoma sehemu ya pili bonyeza hapa Kutokea  hapo ndipo wanapanda kwenda hatua ya tatu sasa boss wangu, ambayo ni: BUSINESS OWNER LEVEL HII NI LEVEL YA KUJENGA MFUMO WAKO MWENYEWE. Hapa hutengenezi tu kipato boss. Hapa boss,  Unakuwa na watu na unajenga mfumo wa kuzalisha kipato chako ndugu. Tofauti kubwa ni hii: Kwenye self-employed → unafanya kazi ili upate pesa. Business owner → mfumo pamojabna watu  wanafanya kazi ili uzalishe pesa wewe. DALILI KWAMBA UPO LEVEL HII Una timu au watu wanaokusaidia. Kuna kazi zinafanyika hata bila wewe kuwepo. Biashara ina structure (mfumo) ambao unajiendesha wenyewe....

MAKOSA YA KAWAIDA KATIKA UWEKEZAJI.

Image
  MAKOSA YA KAWAIDA KATIKA UWEKEZAJI. Uwekezaji siyo tu kuweka  rasilimali kama pesa, muda au nguvu sehemu fulani ni mchakato wa kimkakati wa kukuza thamani yako ili upate faida ya baadaye. Na katika uwekezaji lengo kuu huwa ni moja kupata FAIDA. Lakini ukweli ni kwamba, watu wengi wanaingia kwenye uwekezaji wakiwa na ndoto kubwa ya kupata faida, lakini wanatoka wakiwa na hasara, maumivu, na majuto boss. We unadhani ni kwa nini boss? Kwa sababu ya makosa ya msingi ambayo wengi huyafanya lakini  yanaweza kuepukika kabisa boss wangu. Leo tuyaweke wazi ili wewe usiwe miongoni mwa wanaopoteza. Kosa la kwanza. KUTAKA FAIDA YA HARAKA (GET RICH QUICK MENTALITY). Hii ndiyo sumu kubwa zaidi ndugu yangu katika uwekezaji. Watu wanataka mafanikio ya haraka bila kuvumilia mchakato wenyewe. Na ukweli ambao hauujui ni huu: Uwekezaji halisi unahitaji rasilimali, muda, nidhamu, na subira. Zingatia muda na subira bos Ukikimbilia faida za chapu chapu: Utadanganywa kwa urahisi, U...

NGUVU YA MAWAZO YAKO

Image
  NGUVU YA MAWAZO YAKO Mara nyingi tunadhani maisha yetu yanaamuliwa na mazingira, bahati, au watu wanaotuzunguka hili nilikaa nalo kwa muda mrefu sana. Hata hivyo nimekuja gundua, ukweli uliojificha ni huu: maisha yako yanaendeshwa na mawazo yako yaani, jinsi unavyofikiri boss. Ngoja nikwambie ndugu ndani yako kabisa, kuna sauti ya kimya inayokuambia wewe ni nani, unaweza nini, na una thamani gani, watu wanakuonaje n.k  na mara nyingi hata huihoji sababu ushaizoea. HIVI UNAZANI MAWAZO YAKO NI NANI? Jiulize kwa uaminifu tu: Unapoamka asubuhi, unajiambia nini? “Leo itakuwa ngumu?” “Sitafanikiwa?”, "mimi ni mbaya", "siwezi" “Maisha ni magumu sana?” n.k. Kama hujui hayo si ukweli. Hizo ni imani ulizojijengea  labda kutokana na uzoefu, mazingira, kumbukumbu, mawazo au watu uliowahi kuwasikiliza. Na shida kubwa katika hilo ni kwamba, ukirudia mawazo hayo kila siku, yanakuwa sehemu ya utambulisho wako wa maisha. Kingine boss, imani zilizofichwa ndizo zinazoendesh...

NGUZO ZA MAENDELEO BINAFSI SEHEMU YA KWANZA.

Image
  NGUZO ZA MAENDELEO BINAFSI SEHEMU YA KWANZA. Maendeleo binafsi (personal development) si jambo la kubahatisha, wala si tukio la siku moja boss. ๐Ÿ‘‰ Ni mchakato wa makusudi wa kujijenga kuboresha uwezo wako, tabia zako, maarifa yako, na maisha yako kwa ujumla. Hii haimaanishi kuwa na mafanikio ya kibinafsi au kuwa mtu mwingine tofauti, bali ni kuwa toleo bora la wewe mwenyewe. Becoming a better you. Na katika safari hii hupaswi kujiringanisha na mtu awaye yote. Ispokuwa kwako mwenyewe yaani, wewe wa leo na ww wa jana boss. Kumbuka ndugu, hii ni safari ya muda mrefu. Safari inayohitaji nidhamu, uamuzi, muda, tabia, na mwendelezo ndugu. Na katika safari hii, kuna nguzo kuu ambazo ndizo zinashikilia ukuaji wako wote. Leo tunaanza na nguzo ya kwanza ambayo ndiyo msingi wa kila kitu: NGUZO YA KWANZA: AKILI NA MAARIFA. Akili yako ndugu, ndiyo mtaji wako mkubwa kuliko kitu kingine chochote ulicho nacho. hebu rudia kusoma tena hapo. Ndugu kabla hujabadilisha maisha yako, lazima u...

USIWEKE MAYAI YOTE KWENYE KAPU MOJA.

Image
USIWEKE MAYAI YOTE KWENYE KAPU MOJA. Watu wengi wanapoanza safari ya uwekezaji, huwa na mtazamo mmoja hatari sana, ambao ni kuweka fedha zao zote sehemu moja wakiamini hapo ndipo “dili” lilipo na litatiki. Lakini ukweli ni huu: ๐Ÿ‘‰ Uwekezaji siyo kubahatisha kama tulivyoona huko nyuma bali ni uwezo wa kusimamia hatari. Na hapa ndipo kanuni ya UWEKEZAJI MSETO (DIVERSIFICATION): inapokuwa muhimu sana na inapoingia kazini boss. Swali muhimu unalowezajiuliza ni hili, KWANI KUNA HATARI YA KUWEKA KILA KITU SEHEMU MOJA? na mimi nitakujibu hivi, Fikiria umeweka pesa zako zote kwenye: Biashara moja, Kampuni moja, Au mradi mmoja au sehemu moja. Unajua nini kitatokea boss? Kama mambo yataenda vibaya: ๐Ÿ‘‰ Unapoteza kila kitu kwa wakati mmoja boss wangu. Hii ndiyo sababu watu wengi huanguka kifedha si kwa sababu hawakuwekeza, bali kwa sababu hawakusambaza pasa zao ili kuepuka hatari za uwekezaji. HII SIRI YA WAWEKEZAJI MAKINI. Nimekujagundua kwamba wawekezaji waliofanikiwa hawategemei...

KUISHI KUTOKEA NDANI: NGUVU YA KUJISIKILIZA WEWE MWENYEWE.

Image
  KUISHI KUTOKEA NDANI: NGUVU YA KUJISIKILIZA WEWE MWENYEWE. Mara nyingi sana nimegundua na kuona kwamba, maisha yetu huendeshwa na kelele za nje kuliko sauti ya ndani yetu. Hebu fikiria, jamii inaongea, watu wanashauri, mitandao inaonyesha kila aina ya maisha pengine yaliyo bora kuliko yako, na mazingira yanatupangia namna ya kufikiri na kuishi. Sasa hapo unajua nini kinatokea boss? Polepole bila hata kugundua, tunaanza kuishi maisha ambayo si yetu kabisa. Tunafanya maamuzi kwa sababu: “Watu wataonaje?”, “Jamii inasema hivi” “Hivi ndivyo wengine wanafanya” yaani mamjo lukuki. Na hapo ndipo wengi wanapopoteza mwelekeo wao halisi kabisa. Unajua nini boss wangu? : KUISHI KWA SAUTI ZA NJE Siyo shida sema tu kwamba; Dunia ya leo imejaa kelele nyingi sana vitu kama: Mitandao ya kijamii, marafiki na ndugu, Mila na desturi, Shinikizo la kufanana na wengine yaani vitu kedekede boss. Na hii imepelekea watu wengi wameacha: Uwezo wao wa kufikiri, Ubunifu wao, Maamuzi yao, hata hatim...

LEVEL ZA MAFQNIKIO (SEHEMU YA PILI)..

Image
  LEVEL ZA MAFANIKIO SEHEMU YA PILI. Baada ya kutoka kwenye Hatua ya kujikimu/utumwa (Slavery/survival  Level). Ambapo mtu anakuwa anapambana na mahitaji ya msingi nq hapo kipato chake kina weza kuwa ni kidogo au sawa na mahitaji yake. Kusoma sehemu ya kwanza bonyeza hapa Sasa hatua hii ni ya kuanza kujitegemea Mtu anaanza kuwema; “Siwezi kuendelea kuuza muda wangu milele lazima nijitengenezee mfumo wangu.” Na hapo ndipo anaingia hatua ya pili: HATUA YA KUJIAJIRI/ KUJITEGEMEA(SELF-EMPLOYMENT LEVEL) HII NI LEVEL YA KUAMKA Hapa mtu: Anaanza kujitegemea Anaanza kujitengenezea kipato chake Anaanza kutumia ujuzi wake moja kwa moja ๐Ÿ‘‰ Anaacha kutegemea mshahara pekee ๐Ÿ‘‰ Anaanza kujitafutia njia zake mwenyewe KWA MFANO HALISI WA HII LEVEL Hapa ndipo utakuta: Fundi anajifungulia gereji yake, Mwalimu anaanza tuition zake, Mjasiriamali mdogo anaanza biashara zake. Writer anaanza freelancing. ๐Ÿ‘‰ Hapa unaanza “kumiliki kazi yako boss”. UKWELI Kuhusu  HII LEVEL In...

MISINGI YA UWEKEZAJI (SEHEMU YA TATU): FAIDA (RETURN).

Image
  MISINGI YA UWEKEZAJI (SEHEMU YA TATU): FAIDA (RETURN). Katika safari ya uwekezaji, kuna mlolongo ambao haupaswi kuvunjwa kabisa kama unataka kupata matokeo halisi. Uwekezaji siyo bahati nasibu wala ubabaishaji, bali ni mfumo unaofuata kanuni maalum zilizowekwa boss. Kama tulivyoona hapo awali: Hatua ya kwanza ilikuwa kufanya utafiti wa kina (research). Hatua ya pili ilikuwa kulinda pesa/mtaji wako (capital protection). Kusoma sehemu ya pili bonyeza hapa Na leo nataka nikupeleke kwenye kipengele pendwa, ambacho watu wengi hukikimbilia kwanza bila kufuata misingi. Si kingine bali ni FAIDA (RETURN). Ukweli ni kwamba: Kila Mwekezaji Anatafuta Faida. Hakuna mtu anayeweka pesa zake kwa lengo la kupoteza. Kila uwekezaji una lengo moja kuu: kuongeza THAMANI ya FEDHA yako boss. Lakini pamoja na hayo, hapa ndipo wengi hukosea, Wanaanza kwa kuuliza: “Nitapata faida kiasi gani?” Badala ya kuuliza: “Je, huu uwekezaji ni salama? Na umechunguzwa?” Najua unaweza kujiuliza fida Sahih...

UFUNGUO WA KUJIFUNGULIA MAISHA YAKO.

Image
UFUNGUO WA KUJIFUNGULIA MAISHA YAKO. Mara nyingi sana watu hulichukulia swala la kujitambua kwa juu juu tu, na kwa mtazamo mdogo sana. Wengi hudhani KUJITAMBUA ni kujua tu jina lako, historia yako, au kusema “mimi ni mtu wa aina fulani” kisha wanaishia hapo tu. Kama ndivyo hivyo kuna ukweli wanamiss boss. Na ukweli ukweli wenyewe ni huu ๐Ÿ‘‡ Kujitambua ni zaidi ya hapo. Ni nguvu ya ndani ambayo huamua mwelekeo mzima wa maisha yako. Kama ingekuwa ni ujenzi basi hii ni RAMANI ya jengo la injinia. Na kama ingekuwa ni chombo cha moto hii ni INJINI yenyewe boss. Huenda ikiwa ini mlango basi huu ni UFUNGUO wenyewe wa maisha yako boss. Na leo nataka uone jambo hili kwa jicho jipya na tofauti  kabisa ndugu yangu. Labda nikuulize swali boss, kwani wewe kujitambua ni nini hasa? Ninajua unajibu lako, hebu kaa nalo kwanza na ikiwezekana utanijibu kwa comment boss. Ndugu yangu, kujitambua (Self Awareness) si kujua tu “mimi ni nani”, bali ni: 1. Kuelewa kwa kina hisia zako. Unapojisikia...

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29