TABIA ZAKO NDIZO ZINAZOAMUA HATIMA YAKO
TABIA ZAKO NDIZO ZINAZOAMUA HATIMA YAKO Watu wengi wanapozungumzia mafanikio, kufika mbali na kuwa watu wakubwa, mara nyingi huangalia vitu vikubwa kama vile; elimu, mtaji, connections, bahati na hata urithi. Lakini kuna ukweli ambao wengi hawautaki kuukubali ambao ni huu: MAFANIKIO yako yamejificha ndani ya TABIA zako za kila siku. Ndiyo TABIA zako. Siyo ndoto zako, siyo mipango yako, siyo marafiki zako, siyo juhudi zako, bali tabia zako ndizo zinazoamua utafika wapi kesho. Ukweli mchungu mwingine ni kwamba huwezi kuwa na maisha makubwa ukiwa na tabia ndogo, never. KAMA NDIVYO HIVYO, TABIA NI NINI BASI? Tabia ni yale mambo unayafanya kila siku bila hata kufikiria sana wala kutumia nguvu. Yale matendo na maamuzi madogo madogo unayorudia kila siku kuyafanya, kama vile; Unaamka saa ngapi? Unatumiaje muda wako au kupiga soga tu. Unasoma au unateleza tu mitandaoni Unadhibiti hisia zako au zinaongoza maisha yako Hivi vitu vinaonekana vidogo vidogo sana, lakini kw...