KWANINI NI NGUMU KUGUNDUA KUSUDI LA MAISHA YAKO?
KWANINI NI NGUMU KUGUNDUA KUSUDI LA MAISHA YAKO? Kuna vitu vinavyoleta furaha hapa duniani. Kula chakula unachokipenda… Kuwa na muda na watu unaowapenda(familiy, friends ect) Kufanya kazi unayoifurahia. Lakini zaidi ya vyote, kuna furaha ya kipekee sana, ambayo ni: 👉 kugundua na kuliishi #KUSUDI la maisha yako. Hata hivyo, ukweli mchungu ni huu, watu wengi bado hawajui sababu ya wao kuwepo hapa duniani. Ukijiuliza swali hili: “Kwanini nipo hapa duniani?” hili ni moja ya maswali magumu zaidi, lakini pia ni muhimu zaidi. Mbaya zaidi, Wengi hulikwepa. Lakini haliachi kuwatesa KIMYA KIMYA. Kwa nini basi ni ngumu kulijua kusudi lako? 1. KUIGA MAISHA YA WENGINE Jamii imejenga mfumo wa kufanana. Watu wanashinikizwa kusoma walichochaguliwa pengine na wazazi, kufanya kazi zilizopendekezwa, na kuishi maisha yanayokubalika na jamii. Matokeo yake, 👉 Wanaacha kusikiliza #SAUTI ya NDANI ya #MIOYO yao. Hili ni kosa kubwa. 2. USUMBUFU WA MAISHA Maisha yana kelele nyingi. Mitandao ya kija...