KUISHI KUTOKEA NDANI: NGUVU YA KUJISIKILIZA WEWE MWENYEWE.
KUISHI KUTOKEA NDANI: NGUVU YA KUJISIKILIZA WEWE MWENYEWE. Mara nyingi sana nimegundua na kuona kwamba, maisha yetu huendeshwa na kelele za nje kuliko sauti ya ndani yetu. Hebu fikiria, jamii inaongea, watu wanashauri, mitandao inaonyesha kila aina ya maisha pengine yaliyo bora kuliko yako, na mazingira yanatupangia namna ya kufikiri na kuishi. Sasa hapo unajua nini kinatokea boss? Polepole bila hata kugundua, tunaanza kuishi maisha ambayo si yetu kabisa. Tunafanya maamuzi kwa sababu: “Watu wataonaje?”, “Jamii inasema hivi” “Hivi ndivyo wengine wanafanya” yaani mamjo lukuki. Na hapo ndipo wengi wanapopoteza mwelekeo wao halisi kabisa. Unajua nini boss wangu? : KUISHI KWA SAUTI ZA NJE Siyo shida sema tu kwamba; Dunia ya leo imejaa kelele nyingi sana vitu kama: Mitandao ya kijamii, marafiki na ndugu, Mila na desturi, Shinikizo la kufanana na wengine yaani vitu kedekede boss. Na hii imepelekea watu wengi wameacha: Uwezo wao wa kufikiri, Ubunifu wao, Maamuzi yao, hata hatim...