YUPO MBADALA WAKO.
YUPO MBADALA WAKO. Kuna ukweli mmoja ambao wengi wetu hatupendi kuusikia, lakini ni muhimu sana leo tuuelewe; "Haijalishi wewe ni muhimu kiasi gani leo, siku moja nafasi yako itachukuliwa na mtu mwingine. Kwa kimombo ni kusema, No matter how important you're one day you'll be replaced." Unajua boss unaweza kuwa: mwenye elimu kubwa sana, mwenye kipaji cha kipekee, tajiri mkubwa, kiongozimzuri, mtaalamu sana, maarufu sana, mfanyabiashara mkubwa, au mtu anayependwa na wengi yaani, mtu wa watu. Lakini ukweli wa maisha ni kwamba hakuna anadumu milele except God and his promises. Siku moja utaondoka, na maisha yataendelea kama kawaida boss. Nachotakq kusema ni kwamba boss, Usilewe nafasi uliyopewa leo, kwa sababu siku moja itachukuliwa na mwingine na bado maisha yanaendelea kama kawa boss. UNAJUA BOSS HISTORIA IMEJAA MIFANO Kabla yetu walikuwepo watu: wenye majina makubwa, wenye ushawishi mkubwa, wenye mali mingi sana, wenye hekima ya kipekee, waliopendwa sana...