Posts

SIRI MUHIMU WANAYOITUMIA WATU WANAOSHINE.

Image
  SIRI MUHUMU WANAYOITUMIA WATU WANAOSHINE. Watu wengi wanapenda mafanikio, lakini ukweli ni kwamba wachache sana wanafika juu kwenye hayo mafanikio. Kila mtu anatamani: kuwa bora kwenye kazi yake, kung’ara kwenye kipaji chake, kutambulika kwenye kile anachofanya na mengine kibao. Lakini ukiangalia katika uhalisia bila kupepesa, 👉 Wengi hubaki kuwa watu wa kawaida (average persons). SWALI MUHIMU LA KUJIULIZA: Kwa nini watu wengi hubaki wa kawaida, badala ya KUSHINE? Hapo kuna sababu nyingi unaweza kutoa. Lakini leo nataka nikupe KIINI halisi ambacho wengi wanakipuuza: KUKOSA MWENDELEZO (CONSISTENCY) HAPA NDIPO WENGI WANAPOANGUKIA. Unakuta mtu: Leo anaanza kitu kwa nguvu Kesho anabadilisha mwelekeo, Baada ya muda anaanza kitu kingine kabisa. 👉 Hapo hakuna kitu kinakomaa. 👉 Walakuna kitu kinatoa matokeo. Kila analoamza anaishia njiani. MWENDELEZO(Consistency) NI NINI HASA? Mwendelezo siyo kufanya kitu kwa siku mbili au wiki moja au mwaka mmoja boss. 👉 Mwendel...

MAENEO 6 YA UWEKEZAJI YATAKAYOONGEZA THAMANI YAKO.

Image
  MAENEO 6 YA UWEKEZAJI YATAKAYOONGEZA THAMANI YAKO. Watu wengi wanaposikia neno UWEKEZAJI, mara nyingi akili zao hukimbilia fedha, mashamba, mifugo, hisa, majengo, ardhi n.k. Hii siyo MAKOSA, lakini ni sehemu ndogo tu ya UKWELI. Sasa hebu nikuulize swali rahisi tu hapa: Nikikupa milioni moja(1M) leo, utawekeza wapi? Majibu ya wengi yanafanana. Lakini, leo nataka nikufungulie mtazamo wa juu zaidi  uwekezaji ambao ukikosea hapa, hata uwe na fedha kiasi gani, bado unaweza KUKWAMA sehemu. Haya ndiyo maeneo 6 ya msingi ya uwekezaji wa kweli unaopaswa kuzingatia: 1. WEKEZA KWENYE UJUZI (SKILLS) Huu ndio uwekezaji usiopotea. Unaweza: Kupoteza kazi, Kuibiwa mali, Kuhama nchi Lakini huwezi kupoteza ujuzi wako. 👉 Ujuzi ni kama mashine ya kuchapisha pesa ndani ya akili yako. Watu wengi wanafikiri wanaajiriwa kwa sababu ya kazi wanayofanya si kweli. Unalipwa kwasababu ya  THAMANI unayotoa. Na thamani = ujuzi boss. Hebu fikria: Ni rahisi mtu kutumia saa 5 mitandaoni a...

USISAHAU KILICHOKULETA HAPO.

Image
  USISAHAU KILICHOKULETA  HAPO. Kuna makosa mawili makubwa ambayo watu wengi hufanya wanapoanza kuyaona mafanikio yao: wanasahau walikotoka, na wanasahau kilichowafikisha hapo. Haya ni makosa makubwa mawili, ni kesi ya kutokujitambua. Hapo ndipo safari yao huanza kushuka bila wao kujua yaani, kimya kimya. UKWELI AMBAO NIWACHACHE WANAUJUA, Mafanikio hayakuji kwako kwa bahati mbaya. Yalikuja kwa sababu ya vitu fulani ulivyofanya. Yamkini huenda; Ulijituma sana, Ulijinyima, Ulijifunza, Uliomba sana, ulisave sana, Ulijitoa zaidi kuliko wengine, Ulivumilia wakati mgumu. 👉 Hiyo ndiyo “formula” yako ya mafanikio. Lakini shida inaanza pale unapopata mafanikio walau kidogo, halafu ghafula unaanza kubadilika. UNAPOSAHAU KILICHOKULIPA, UNAPOTEZA MWELEKEO WAKO. Watu wengi wakianza kuona matokeo: Wanaacha nidhamu, Wanaacha kujifunza, Wanaanza kujiamini kupita kiasi, Wanasahau kujituma, Wanaanza maisha ya anasa mapema sana. Kisa wameona matokeo kidogo tu. Namatokeo yake,...

TABIA ZAKO NDIZO ZINAZOAMUA HATIMA YAKO

Image
  TABIA ZAKO NDIZO ZINAZOAMUA HATIMA YAKO Watu wengi wanapozungumzia mafanikio, kufika mbali na kuwa watu wakubwa, mara nyingi huangalia vitu vikubwa kama vile; elimu, mtaji, connections, bahati na hata urithi. Lakini kuna ukweli ambao wengi hawautaki kuukubali ambao ni huu: MAFANIKIO yako yamejificha ndani ya TABIA zako za kila siku. Ndiyo TABIA zako. Siyo ndoto zako, siyo mipango yako, siyo marafiki zako, siyo juhudi zako, bali tabia zako ndizo zinazoamua utafika wapi kesho. Ukweli mchungu mwingine ni kwamba huwezi kuwa na maisha makubwa ukiwa na tabia ndogo, never. KAMA NDIVYO HIVYO,  TABIA NI NINI BASI? Tabia ni yale mambo unayafanya kila siku bila hata kufikiria sana wala kutumia nguvu. Yale matendo na maamuzi madogo madogo unayorudia kila siku kuyafanya, kama vile; Unaamka saa ngapi? Unatumiaje muda wako au kupiga soga tu. Unasoma au unateleza tu  mitandaoni Unadhibiti hisia zako au zinaongoza maisha yako Hivi vitu vinaonekana vidogo vidogo sana, lakini kw...

MISINGI YA UWEKEZAJI: KWANINI WENGINE WANASHINDA NA WENGINE WANAPOTEZA PESA?

Image
  MISINGI YA UWEKEZAJI: KWA NINI WENGINE WANASHINDA NA WENGINE WANAPOTEZA PESA? Dunia inaendeshwa kwa kanuni zisizobadilika Na moja ya kanuni kuu inayotawala maisha ya binadamu ni KANUNI YA UWEKEZAJI. Ukweli mchungu ni huu: 👉 Dunia haikupi unachotaka. Bali, Inakupa kile ulichowekeza. Ni sawa kabisa na ile kanuni ya asili: “Apandacho mtu, ndicho atakachovuna.” Ukichagua kupanda maarifa — utavuna ujuzi. Ukichagua kupanda nidhamu — utavuna mafanikio. Ukichagua kupanda fedha kwa hekima — utavuna uhuru wa kifedha. Lakini… 👉 Ukipanda tamaa, uzembe, au kukurupuka — utavuna hasara. Kuna UCHUNGU mkubwa kwenye uwekezaji Katika eneo la fedha, maumivu ni makubwa zaidi. Watu wengi: Wamepoteza mitaji yao, wametapeliwa Wameingia kwenye “deals” zisizoeleweka Wamebaki na majuto na lawama zisizokoma. Na swali linabaki moja,  Tatizo ya haya yote  ni nini? 👉 Jibu kubwa ni moja pia: Kukosa uelewa wa misingi ya uwekezaji. Watu wanaingia kwenye uwekezaji kama bahati nasib...

KWANINI NI NGUMU KUGUNDUA KUSUDI LA MAISHA YAKO?

Image
  KWANINI NI NGUMU KUGUNDUA KUSUDI LA MAISHA YAKO? Kuna vitu vinavyoleta furaha hapa duniani. Kula chakula unachokipenda… Kuwa na muda na watu unaowapenda(familiy, friends ect) Kufanya kazi unayoifurahia. Lakini zaidi ya vyote, kuna furaha ya kipekee sana, ambayo ni: 👉 kugundua na kuliishi #KUSUDI la maisha yako. Hata hivyo, ukweli mchungu ni huu, watu wengi bado hawajui sababu ya wao kuwepo hapa duniani. Ukijiuliza swali hili: “Kwanini nipo hapa duniani?” hili ni moja ya maswali magumu zaidi, lakini pia ni muhimu zaidi. Mbaya zaidi, Wengi hulikwepa. Lakini haliachi kuwatesa KIMYA KIMYA. Kwa nini basi ni ngumu kulijua kusudi lako? 1. KUIGA MAISHA YA WENGINE Jamii imejenga mfumo wa kufanana. Watu wanashinikizwa kusoma walichochaguliwa pengine na wazazi, kufanya kazi zilizopendekezwa, na kuishi maisha yanayokubalika na jamii. Matokeo yake, 👉 Wanaacha kusikiliza #SAUTI ya NDANI ya #MIOYO yao.  Hili ni kosa kubwa. 2. USUMBUFU WA MAISHA Maisha yana kelele nyingi. Mitandao ya kija...

UMASKINI VS UTAJIRI: VYOTE HUANZIA AKILINI.

Image
  UMASKINI VS UTAJIRI: VYOTE HUANZIA AKILINI. Watu wengi hudhani kuwa umaskini na utajiri ni ukosefu au wingi wa pesa na mali. Kwa kiasi fulani hilo linaweza kuwa kweli, lakini kuna ukweli mkubwa zaidi ambao mara nyingi watu hawauoni. Ukweli ni huu ni: umaskini na utajiri huanzia akilini kabla ya kuonekana mfukoni. Nakumbuka Mentor wangu mmoja kutoka Kenya, Konji Oloyi, aliwahi kuniambia maneno ambayo sikuyasahau: "Poverty and wealth are in the mind; lack or abundance are just signs. Many people confuse these." Akimaanisha kuwa umaskini na utajiri upo kichwani. Ukosefu au utele wa pesa ni dalili tu. Ndugu yangu, umaskini huanza kichwani. Kadhalika utajiri nao huanza kichwani. Ukosefu wa pesa mfukoni unaweza kuwa dalili ya umaskini, lakini hata kuwa na pesa nyingi mfukoni kunaweza kuwa dalili ya utajiri. Ndiyo maana Napoleon Hill aliandika katika kitabu kinachoitwa Think and Grow Rich. Kwa lugha rahisi ni: FIKRA zako zina mchango mkubwa sana katika kile unachokuwa. ...

SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI MISINGI.

Image
  SIYO PESA PEKEE ZINAZOKUFANYA UWE MWEKEZAJI, NI  MISINGI. Watu wengi wanapofikiria UWEKEZAJI, jambo la kwanza linalokuja akilini mwao ni pesa nyingi. Ndiyo maana wengine husema, “Nikishapata pesa nyingi ndipo nitaanza KUWEKEZA.”. Lakini ukweli ni tofauti kidogo. Uwekezaji wa kweli hauanzi na pesa nyingi. Unaanza na MISINGI sahihi ya KIFEDHA. Watu wengi hupata na kuzalisha pesa siyo tatizo kwao, lakini hawajengi utajiri. Kwa nini? Kwa sababu hawajajifunza misingi ya kuitunza na kuikuza. Kila kitu kina misingi na kanuni zake. Kabla ya kufikiria uwekezaji mkubwa, jifunze kwanza mambo machache ya msingi. Jifunze kuishi chini ya kipato chako. Jifunze kuokoa hata kama ni kidogo. Jifunze kupanga matumizi yako. Na jifunze kuwa na subira. Kwa sababu uwekezaji si mbio za haraka. Ni safari ya uvumilivu. Ni kama kupanda mti. Unapanda mbegu leo. Unaimwagilia kila siku. Unaipa muda ikue. Halafu baada ya muda, inaanza kutoa kivuli  na baadaye matunda. Tatizo la wen...

USIISHI TU ISHI KWA KUSUDI.

Image
  USIISHI TU ISHI KWA KUSUDI. Kuna watu wengi wanaamka kila siku, wanafanya kazi, wanatafuta pesa, wanapambana na maisha. Lakini ndani yao kuna swali ambalo bado halijajibiwa. Ambalo ni, “NIMEKUJA DUNIANI KUFANYA NINI?” Kwa sababu ukweli ni huu: sio kila mtu anayeishi anaelewa kusudi la maisha yake hapa duniani. Wengine wanafuata mkondo wa dunia. Wengine wanaiga maisha ya wengine. Wengine wanapoteza miaka mingi wakikimbiza vitu ambavyo havina maana ya kudumu. Lakini maisha hubadilika na kuwa na maana pale unapogundua kwa nini upo hapa duniani. Kusudi la maisha sio tu kupata pesa. Sio tu kuwa maarufu. Sio tu kumiliki vitu vingi. Wala si kuwa na kazi nyingi. Bali, Kusudi la maisha ni kugundua ZAWADI (uwezo, kipaji, karama, nguvu n.k) uliyopewa na Mungu. na kuitumia kuleta MWANGA(wepesi) katika maisha yako na maisha ya wengine. Ndiyo maana watu wanaoishi kwa kusudi huwa na nguvu tofauti. Changamoto zinakuja, lakini hawaachi kufanya. Wanakosolewa, lakini bado wanaende...

KUACHA URITHI.

Image
  #KUACHA #URITHI. Watu wengi wanaishi wakifikiria leo tu. Lakini wachache wanaishi wakijenga urithi wa kesho. Ukweli ni huu ; Maisha ya mtu hayapimwi tu kwa muda aliokaa duniani, bali kwa athari na alama  aliyoiacha katika maisha ya wengine. Wengine wanaacha majumba. Wengine wanaacha mali. Wengine wanacha mashamba. Wengine wanaacha Magari. Na hilo ni jambo jema, na ni urithi mzuri. Lakini kuna urithi mkubwa zaidi kuliko mali. Urithi wa maadili. Urithi wa maneno ya kutia moyo. Urithi wa mfano wa maisha uliouonyesha. Urithi wa mifumo na mienendo ya maisha. Kuna mtu leo anapigana vita za maisha kwa ujasiri kwa sababu kuna mtu aliwahi kumwambia, “USIKATE TAMAA.” Kuna mtoto anajua KUHESHIMU kwa sababu kuna mtu aliwahi kumfundisha heshima. kuna mtu anajali #thamani na #utu wa watu sababu kuna mtu amewahi kumfundisha hivyo. Maneno madogo yanaweza kujenga maisha na HATIMA ya mtu. Na vitendo vidogo vinaweza kubadilisha #KIZAZI kizima. Ndiyo maana maisha hayapaswi kuishi ishi tu. yanap...

KUJILINGANISHA NI SUMU HATARI.

Image
  KUJILINGANISHA NI SUMU HATARI. Tatizo kubwa la kizazi hiki si kukosa UWEZO binafsi. Bali ni KUJILINGANISHA kupita kiasi. Hebu tazama kwa mfano, nafungua simu yako, unaona maisha ya wengine, yanaonekana yamepangwa. Wamefanikiwa. Wanasafiri. Wanaonekana kuwa na furaha sana. Wanavaa na kula vizuri. Halafu unaanza kujiuliza: “Mimi niko wapi?” mara unasema mimi si chochote. Mdogo mdogo, unajikuta unapima thamani yako kwa vipimo vya watu wengine. Hapo ndipo tatizo linapo anzia. Lakini ukweli ni huu;  👉 kila mtu ana safari yake, kila mtu anasababu yake. Ambayo yaweza kuwa nitofauti kabisa na wengine. Kuna anayekimbia haraka kwa sababu alianza mapema. Kuna anayepanda polepole kwa sababu anajenga msingi imara. Kuna anayeficha mapambano yake nyuma ya picha nzuri. Usilinganishe mwanzo wako na mwisho wa mtu mwingine. Si unajua maisha ni kama kitabu, ukurasa wako wa kwanza una weza kuwa ni wa mwisho kwa mwingine. Kila mtu anakitabu chake na kurasa zake. Maisha yako hayakuitwa KUIGA watu...

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

Image
  UKILIFAHAMU HILI KUHUSU WATU  UTAISHI VYEMA SANA MAISHANI. Kuna ujuzi mwingi muhimu ambao kila mtu anapaswa kujifunza ili kufanikiwa maishani: mauzo, masoko, fedha, utatuzi wa matatizo, mawasiliano, majadiliano, na mengine mengi. Lakini kuna ujuzi mmoja ambao ni zaidi ya hazina—ukiupata, unafungua milango mingi bila hata kugonga. 👉 Ujuzi huo ni KUWAFAHAMU WATU. Ukifanikiwa kuwafahamu watu—saikolojia yao, hisia zao, na namna wanavyotaka kutendewa—hakuna mahali utakwamia. Kwa nini? Kwa sababu kila kitu unachokitaka kipo mikononi mwa watu: fedha, ardhi, bidhaa, mitaji, fursa, ushirikiano, na huduma zote. Kwa kifupi: 👉 Mahusiano mazuri na watu ni bidhaa ADIMU yenye thamani kubwa sana. Na kama ni bidhaa, basi lazima ujifunze namna ya kuitengeneza, kuikuza na kuitunza. Katika sanaa hii ya kuishi na watu, kuna sheria mbili kuu zinazokuongoza. SHERIA YA KWANZA: THE GOLDEN RULE Kanuni hii inasema: “Watendee wengine kama unavyotaka kutendewa wewe.” Hii ni kanuni nzuri s...

HUWEZI KUBADILIKA BILA KUJITAMBUA.

Image
HUWEZI KUBADILIKA BILA KUJITAMBUA. Watu wengi hutamani kubadilisha maisha ya tabia, kipato, mahusiano, au jinsi wanavyojiona. Wengine husoma vitabu, huhudhuria semina, na kuweka malengo mapya kila mwaka. Lakini, pamoja na juhudi zote hizo, hujikuta wakirudia hali ileile. Sababu si kukosa bidii, no. Mara nyingi ni kukosa #KUJIJUA wao kama wao. Kujiboresha bila kujitambua ni kama kujenga bila ramani. Unapojaribu kubadilika bila kuelewa wewe ni nani, unaishia kuiga maisha ya wengine tu. Utaweka malengo yasiyoendana na hali yako, uwezo wako, au hali yako ya ndani. Ndiyo maana baadhi ya malengo huonekana mazuri kwa macho ya watu, lakini moyoni hayana uzito wowote. Unapoanza kuchoka haraka, si uvivu tu, wakati mwingine ni ishara kwamba njia uliyopo siyo yako. Kujitambua kunahitaji ujasiri wa kukubali ukweli kuhusu wewe. #Kujitambua siyo kujipongeza kila wakati. Ni kukubali ukweli wote mtamu na mchungu. Ni kuona #NGUVU zako bila kiburi, na #UDHAIFU wako bila kujilaumu.  Ni kujiuliza maswa...

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31 Ilipoishia………. Elvine alipoteza amani kuliko hata mkewe maana kila alipomtazama mkewe basi moyo wake ni kama ulikuwa unachomwa na mwiba uliojishikiza huko kwenye mishipa ya moyo. Nafsi yake ilitaabika na ndipo alipoamua kutafuta muda mzuri, baada ya chakula cha jioni, azungumze na mkewe, maana ule ukimya wa siku mbili ulikuwa adhabu kubwa sana kwake. Kusoma sehemu ya 30 bonyeza hapa Sasa inaendelea………. Elimina mamy naomba kujua kwanini hutaki kuniuliza kuhusu sababu ya haya yote? Maana najua unajua kuwa kuna mahali mimi nilikosea, sasa unapokaa kimya hivyo… kiukweli unazidi kunichanganya maana ni kama hutaki kujua, sasa unadhani mimi roho yangu itatulia kweli?. Hata kama ungekuwa wewe lazima usingepata amani, ungekuwa hata unawaza hivi nakuwaziaje, nakuonaje na ninajisikiaje ninapokuona, sasa kwanini wewe umekaa kimya, sema neno tafadhali? (Elvine alikuwa akiongea bila kumtazama mkewe usoni maana moyo wake haukuwa katika hali ya utulivu). Pamoja na ...

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.