MISINGI YA UWEKEZAJI (SEHEMU YA TATU): FAIDA (RETURN).
MISINGI YA UWEKEZAJI (SEHEMU YA TATU): FAIDA (RETURN). Katika safari ya uwekezaji, kuna mlolongo ambao haupaswi kuvunjwa kabisa kama unataka kupata matokeo halisi. Uwekezaji siyo bahati nasibu wala ubabaishaji, bali ni mfumo unaofuata kanuni maalum zilizowekwa boss. Kama tulivyoona hapo awali: Hatua ya kwanza ilikuwa kufanya utafiti wa kina (research). Hatua ya pili ilikuwa kulinda pesa/mtaji wako (capital protection). Kusoma sehemu ya pili bonyeza hapa Na leo nataka nikupeleke kwenye kipengele pendwa, ambacho watu wengi hukikimbilia kwanza bila kufuata misingi. Si kingine bali ni FAIDA (RETURN). Ukweli ni kwamba: Kila Mwekezaji Anatafuta Faida. Hakuna mtu anayeweka pesa zake kwa lengo la kupoteza. Kila uwekezaji una lengo moja kuu: kuongeza THAMANI ya FEDHA yako boss. Lakini pamoja na hayo, hapa ndipo wengi hukosea, Wanaanza kwa kuuliza: “Nitapata faida kiasi gani?” Badala ya kuuliza: “Je, huu uwekezaji ni salama? Na umechunguzwa?” Najua unaweza kujiuliza fida Sahih...