MATAMANIO 6 MAKUBWA YA KILA MWANADAMU.
MATAMANIO 6 MAKUBWA YA KILA MWANADAMU. Boss. Ukichunguza maisha ya watu kwa makini, utagundua jambo moja la kuvutia sana. Ingawa tunatofautiana kwa umri, jinsia, kabila, dini, elimu au kiwango cha kipato, kuna matamanio ya msingi yanayotuunganisha sote kama wanadamu. Kuelewa Kinachomsukuma Mwanadamu Kufikiri, Kuamua na Kuishi. Kwa kifupi, karibu kila kitu tunachofanya kinachochewa na moja au zaidi ya matamanio haya makuu. Leo tuyaangalie kwa undani kidogo. 1. USALAMA NA UHAKIKA WA MAISHA(Survival & Certainty). Hili ndilo tamanio la kwanza na la msingi kabisa kwa mwanadamu. Kabla ya kufikiria mafanikio, utajiri au ndoto kubwa, mtu huanza kwa kutafuta usalama na uhakika wa maisha yake kwanza. Yaani, anataka kuwa na uhakika wa: chakula, malazi, mavazi, afya njema, kipato cha kumwezesha kuishi boss. Lakini si hivyo tu boss. Binadamu pia hutafuta usalama wa: kihisia, kiakili, kifedha, na kijamii. Tunapenda kujua kuwa kesho yetu ina matumaini, wa siyo hofu. Ndiyo maana wat...