MAKOSA YA KAWAIDA KATIKA UWEKEZAJI.
MAKOSA YA KAWAIDA KATIKA UWEKEZAJI. Uwekezaji siyo tu kuweka rasilimali kama pesa, muda au nguvu sehemu fulani ni mchakato wa kimkakati wa kukuza thamani yako ili upate faida ya baadaye. Na katika uwekezaji lengo kuu huwa ni moja kupata FAIDA. Lakini ukweli ni kwamba, watu wengi wanaingia kwenye uwekezaji wakiwa na ndoto kubwa ya kupata faida, lakini wanatoka wakiwa na hasara, maumivu, na majuto boss. We unadhani ni kwa nini boss? Kwa sababu ya makosa ya msingi ambayo wengi huyafanya lakini yanaweza kuepukika kabisa boss wangu. Leo tuyaweke wazi ili wewe usiwe miongoni mwa wanaopoteza. Kosa la kwanza. KUTAKA FAIDA YA HARAKA (GET RICH QUICK MENTALITY). Hii ndiyo sumu kubwa zaidi ndugu yangu katika uwekezaji. Watu wanataka mafanikio ya haraka bila kuvumilia mchakato wenyewe. Na ukweli ambao hauujui ni huu: Uwekezaji halisi unahitaji rasilimali, muda, nidhamu, na subira. Zingatia muda na subira bos Ukikimbilia faida za chapu chapu: Utadanganywa kwa urahisi, U...