HUJAWAHI KUSHINDWA, NI VILE HUJATAMBUA TU NGUVU ZAKO.
HUJAWAHI KUSHINDWA, NI VILE HUJATAMBUA TU NGUVU ZAKO. Boss hivi unajua, watu wengi hutumia muda mwingi kufikiria udhaifu na mapungufu yao kuliko kutambua uwezo na zao za kweli. Mara nyingi utakuta wanajua: wanachoshindwa kukifanya, wanapokosea, na maeneo wanayodharika ndani yao. Hata hivyo jambo la kushangaza ni kwamba: Wengi hawajui kabisa nguvu zao halisi. Na hii ndiyo sababu watu wengi wanaishi maisha ya kawaida wakati ndani yao kuna nguvu ya ajabu na uwezo mkubwa ambao haujawahi kugundulika wala kutumika kikamilifu boss wangu. Hili ni kosa ndugu. SWALI LINALOKUJA HARAKA HARAKA NI KWAMBA. NGUVU YA KWELI NI NINI? Swali zuri boss, nami ntakujibu, Nguvu ya kweli si kitu unachoweza kufanya tu au kufanya kitu kwa nguvu kubwa hadi uchoke kabisa. Nguvu ya kweli ni kile: unachofanya kwa urahisi bila kutumia nguvu kubwa na bado kisikuchoshe bali kinakupa nguvu, furaha na unatamani kuendelea kufanya tu. Ni kile kitu, unachokifanya bila kujilazimisha sana Na watu...