WATU WENYE HESHIMA YA KWELI HUFANYA MAMBO HAYA 10.
WATU WENYE HESHIMA YA KWELI HUFANYA MAMBO HAYA 10. Mara nyingi watu hupima mafanikio kwa fedha, elimu, cheo au umaarufu. Lakini ukweli ni kwamba, mojawapo ya vitu vinavyomtofautisha mtu mwenye busara na mwenye hekima ni namna anavyowatendea watu wengine boss. Kwasababu tabia nzuri hazihitaji utajiri. Hazihitaji cheti. Hazihitaji nafasi kubwa katika jamii. Zinahitaji ufahamu, heshima, nidhamu na utu boss. Haya ni baadhi ya mambo madogo ambayo yanaweza kujenga au kuharibu taswira yako mbele ya watu. Yaani, mambo madogo yanayofichua ukomavu wako kwa watu na jamii. 11. MSIFIE MTU HADHARANI, MPINGE FARAGHANI. Ukiona mtu amefanya jambo zuri, msifie mbele ya watu moja kwa moja hata kama akiwa pekee yake siyo mbaya. Lakini unapohitaji kurekebisha kosa lake, fanya hivyo faraghani. Kumkosoa mtu hadharani mara nyingi huumiza heshima yake, humpa aibu na kumfanya awe na msimamo wa kujitetea badala ya kujifunza. Watu wengi husahau maneno uliyosema, lakini hawasahau aibu na jinsi ulivyo...