UFUNGUO WA KUJIFUNGULIA MAISHA YAKO.
UFUNGUO WA KUJIFUNGULIA MAISHA YAKO. Mara nyingi sana watu hulichukulia swala la kujitambua kwa juu juu tu, na kwa mtazamo mdogo sana. Wengi hudhani KUJITAMBUA ni kujua tu jina lako, historia yako, au kusema “mimi ni mtu wa aina fulani” kisha wanaishia hapo tu. Kama ndivyo hivyo kuna ukweli wanamiss boss. Na ukweli ukweli wenyewe ni huu 👇 Kujitambua ni zaidi ya hapo. Ni nguvu ya ndani ambayo huamua mwelekeo mzima wa maisha yako. Kama ingekuwa ni ujenzi basi hii ni RAMANI ya jengo la injinia. Na kama ingekuwa ni chombo cha moto hii ni INJINI yenyewe boss. Huenda ikiwa ini mlango basi huu ni UFUNGUO wenyewe wa maisha yako boss. Na leo nataka uone jambo hili kwa jicho jipya na tofauti kabisa ndugu yangu. Labda nikuulize swali boss, kwani wewe kujitambua ni nini hasa? Ninajua unajibu lako, hebu kaa nalo kwanza na ikiwezekana utanijibu kwa comment boss. Ndugu yangu, kujitambua (Self Awareness) si kujua tu “mimi ni nani”, bali ni: 1. Kuelewa kwa kina hisia zako. Unapojisikia...