USIWEKE MAYAI YOTE KWENYE KAPU MOJA.
USIWEKE MAYAI YOTE KWENYE KAPU MOJA. Watu wengi wanapoanza safari ya uwekezaji, huwa na mtazamo mmoja hatari sana, ambao ni kuweka fedha zao zote sehemu moja wakiamini hapo ndipo “dili” lilipo na litatiki. Lakini ukweli ni huu: ๐ Uwekezaji siyo kubahatisha kama tulivyoona huko nyuma bali ni uwezo wa kusimamia hatari. Na hapa ndipo kanuni ya UWEKEZAJI MSETO (DIVERSIFICATION): inapokuwa muhimu sana na inapoingia kazini boss. Swali muhimu unalowezajiuliza ni hili, KWANI KUNA HATARI YA KUWEKA KILA KITU SEHEMU MOJA? na mimi nitakujibu hivi, Fikiria umeweka pesa zako zote kwenye: Biashara moja, Kampuni moja, Au mradi mmoja au sehemu moja. Unajua nini kitatokea boss? Kama mambo yataenda vibaya: ๐ Unapoteza kila kitu kwa wakati mmoja boss wangu. Hii ndiyo sababu watu wengi huanguka kifedha si kwa sababu hawakuwekeza, bali kwa sababu hawakusambaza pasa zao ili kuepuka hatari za uwekezaji. HII SIRI YA WAWEKEZAJI MAKINI. Nimekujagundua kwamba wawekezaji waliofanikiwa hawategemei...