Posts

Showing posts from March, 2024

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23. Ilipoishia...... Alipofika nje, alimkuta Elimina katahamaki sana tena anahasira sana.  "Umefanya nini Elvine? Elimina aliuliza kwa ukali sana tena hadi macho yalikuwa mekundu kama damu kwaajili ya kujaa hasira.... Swali; kwanini Elimina anahasira? Na Elimina huyu anasiri gani na nyumba iliyoungua moto? Kusoma sehemu ya 22 bonyeza hapa   Sasa inaendelea...... Elvine alikuwa anatetemeka  kwa hofu ya yale anayoyaona lakini alistaajabu kuona ni kama mkewe hajali sana kuhusu yeye. Alimtazama kwa makini sana mkewe akiwa anajaribu kutafakari kwanini anaonekana kuwa na hasira juu yake. Elimina akajishitukia "Hey, wewe! Nini sasa unanitazama hivyo?" "Nakutafakari sipati majibu!' "Nimefanyaje kwani?" "Hamna ila sijajua kama umenihofia mimi au hilo swali lako linamaana gani? "Elvine baba sina maana hiyo uliyoelewa wewe kabisa. Shida yangu mimi umefanya nini mpaka unataka kuhatarisha maisha Yako namna hii. Hujui namna ga

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA 17.

Image
HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA KUMI NA SABA Ilipoishia.... Siku moja akiwa amelala aliota moto mkubwa unawaka ndani ya maji lakini ule moto ni kama unaofifia kwa kuzidiwa na yale maji. Alipoamka akaikumbuka ndoto aliyowahi kuota utotoni ikamkumbusha kuwa hatakiwi kuzima namna hiyo na akajikuta kakumbuka sana vile viusumbufu vya kivita na maadui. Lakini hakujua kumbe kuna bomu kubwa kaandaliwa.....  Kusoma sehemu ya 16 bonyeza hapa. *.   *.    *.   *.    *.    *.   *.  Elvine alikuwa ameketi juu ya mti katikati ya poli fulani akiwa na amani sana. Akiwa pale aliweza kuona umbali mrefu sana. Alishangaa baada ya kumuona mtoto wa kiume mwenye umri kama wa miaka 7 hivi anazunguka zunguka mule polini. Akacheka sana halafu akasema "Kuna vitoto vya ajabu Duniani jamani. Sasa angalia huyu mtoto anataka nini huku polini muda huu?" Akatabasamu akachuma embe lililoiva kwenye ule mti na kuanza kulila. Yule  mtoto alikuwa akijiimbia "ukutiukuti" mwenyewe. Elvine akamtazama kwa makini

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA 16.

Image
  SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”.   SEHEMU YA 16.  Ilipoishia.....      Sherehe zilianza na watu wengi sana walikuja tena wachungaji walikuwa wengi sana. Elvine alifurahi baada ya kumuona baba yake na mama yake wamekuja tena wakiwa wazima wa afya. Elvine pamoja na kufurahi lakini bado alikuwa na wasiwasi  k usoma sehemu iliyopita bonyeza hapa. Sasa inaendelea.... Alitazama Elimina namna alivyopenda akasema kimoyomoyo 'hakika malkia wangu usife mapema bado natamani kuona ulipendeza hivihivi daima'. Wakaingia kanisani ambapo aliyesimamia ibada ya send-off alikuwa ni mchungaji wa kanisa jilani. Lakini Elvine alikuwa na wasiwasi sana na yule mchungaji maana tangu alipofika alikuwa hawatazami watu usoni bali mda mwingi alitazama chini kama anayetunza sheria za familia.  Elvine hakutaka kujaji saana lakini kuna namna alimkazia macho sana yule mchungaji maana kwa mauzauza tu yanayomuwinda aliona ni lazima amchunguze kila mtu anayemsogelea. Ghafla alitazama pembeni

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.