Posts

Showing posts from August, 2025

KAMA UNASAHAU MARA KWA MARA, SOMA HAPA KWANZA.

Image
  KAMA UNASAHAU MARA KWA MARA, SOMA HAPA KWANZA. Boss! Siyo  kila mara, kusahau ni ishara ya Ubongo dhaifu, mara nyingi ni namna tunavyojifunza ndugu. Nimekutana na watu wengi wakisema: "Mimi sina akili kubwa." Wengine "Kumbukumbu yangu ni mbaya." Mara "Ubongo wangu hauhifadhi vitu." Lakini ukweli ni kwamba, mara nyingi tatizo si ukubwa wa akili yako wala uwezo wa ubongo wako. Tatizo ni kwamba watu wengi hawajawahi kufundishwa jinsi kumbukumbu (memory) inavyofanya kazi boss. Sikia ndugu; Ubongo wa binadamu umeumbwa kwa ustadi mkubwa. Kazi yake si kuhifadhi kila kitu unachokiona au kukisikia, bali ni kuchagua filtering taarifa muhimu na kuacha zisizo muhimu wala matumizi. Kwa hiyo, kusahau si kasoro ya ubongo ni sehemu ya kawaida ya jinsi unavyofanya kazi. Hebu tuangalie sababu kuu zinazowafanya watu kusahau mara kwa mara. 1. Kukariri Bila Kuelewa (memorising without understanding). Hili ndilo kosa kubwa zaidi ambalo wanafunzi na hata watu wazima...

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 30

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 30 Ilipoishia……... Kwa upande wa Elvine kilio chake kilitawaliwa na huzuni, hofu na woga wa kumpoteza mkewe, alitawaliwa na hasira dhidi yake mwenyewe kwa makosa aliyoyafanya maana aliona adhabu kubwa itaipata familia yake kwaajili yake, hali hii ya mkewe kupoteza, mtoto na kutopata mtoto ilizidisha maumivu na kila alipomkumbuka Eljini alihisi kupasuka. Kilio chake kiligubikwa na huruma kwa mateso aliyopitia mkewe wakati ambao yeye hakuwepo maana aliona kila tatizo la Elimina basi yeye ndio chanzo, hivyo alikuwa anaumia sana moyoni mwake…... Kusoma sehemu ya 29 bonyeza hapa Sasa inaendelea……... Baada ya kulia sana madaktari waliamua kuwatuliza na kuwainua pale chini. Eliudi alimwita Elvine pembeni na kumwambia anajambo la kuongea nae. Hivyo waliamua kutoka nje na kumuacha Elimina pale ndani akiwa na madaktari wengine ambao dhahiri walionekana kushangazwa na jambo ambalo hata Elimina mwenyewe hakujua ni nini hasa. Wakati Elvine na Eliudi wanatoka nje, ...

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

Image
  Nashukuru kwa kushiriki nami link ya Hadithi hii tamu na Nzuri ya Hatima ya Kimungu Sehemu ya 29. ๐Ÿ™ Nilichosoma katika sehemu hii, simulizi imeendelea  kwa mvuto mkubwa sana – linaonyesha mapambano ya ndani ya Elvine kati ya imani yake, hofu yakuwaza kumpoteza mkewe Elimina, na hatia ya makosa ya zamani. Kuna mambo yafuatayo nimeona  yaliyobeba msingi   wa  sehemu hii: 1. Mgongano wa nafsi ya Elvine ๐Ÿ‘‰Anapokuwa mbele ya Malaika Elvila, anatakiwa kufanya maamuzi magumu: kati ya mke na mtoto. ๐Ÿ‘‰Uamuzi wake unaonyesha upungufu wa mwanadamu, uchungu, na jinsi maumivu yanavyoweza kuathiri fikra na maamuzi. 2. Adhabu na Neema ๐Ÿ‘‰Kupotea kwa mtoto na kutozaa tena kwa Elimina ni matokeo ya makosa ya Elvine, lakini bado neema ya Mungu inaonekana kwa kumrejesha mkewe. ๐Ÿ‘‰Malaika anamkumbusha kuwa Mungu si mkatili, bali anamfundisha kupitia mateso na changamoto. 3. Ugeuzi wa Maisha (Turning Point) ๐Ÿ‘‰Elvine sasa anaitwa kuwa mchungaji wa kondoo wa Bwana, ishara ...

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 28

Image
 JACQUELINE JOHN & MWL MIGONGO ELIAS,Kwanza nichukue fursa hii kumshukuru Mungu ALIYE ziumba mbingu na Dunia Kwa kweli nimefurahi mno na tena mno Kwa makala yenu ya simulizi/ Hadithi Nzuri inayo conquer MOYO wangu hivyo ๐Ÿ‘๐Ÿ‘ ๐Ÿ‘‡ I love it♥️ Nimeisoma yote uliyonitumia, hii sehemu ya 28 ya "Hatima ya Kimungu" inabeba hatua kubwa ya hadithi na kuunganisha matukio ya kiroho na uhalisia kwa nguvu sana. Kwa ufupi, hapa kuna mambo yafuatayo yakupasa kujua ndani ya Hadithi hii  The points I have presented down a vivid picture and rich imagery for deep reflection, guiding the reader toward discernment and the pursuit of greater excellence. In this section of the narrative, I have endeavored to analyze, as thoroughly as I can, to illuminate what you are doing have done within your story. 1. Mateso ya Elimina na nguvu ya maombi • Elimina anaachwa na Edgar kwenye hali ya uchungu wa uzazi, milango imefungwa, hana msaada. • Anakumbwa na mwanga usoni, unaompa nguvu za kiroho kuomba kwa...

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29 Ilipoishia………. Jesus! Elvine alishtuka na mshale wa hatari ukagonga kichwani mwake. Alianza kuifuata ile damu ambayo ilimpeleka mpaka chumbani ambako alimkuta Elimina kalala chini huku ashika mtoto mkononi,mtoto kalala na Elimina kazimia. Damu zilikuwa zimemtoka nyingi sana Elimina hivyo hakuwa na nguvu tena. Elvine alipaniki asijue afanye kitu gani. Kusoma sehemu ya 28 bonyeza hapa. Sasa inaendelea………. Haraka alimchukua mtoto kutoka mikononi mwa Elimina kisha akachukua kitenge cha mkewe na kukitandika kitandani alafu akamlaza mtoto wake. Kijasho chembamba kilikuwa kikimtiririka, kwa woga alimsogelea Elimina na kuanza kumuamsha. Alipiga simu kwa daktari mmoja aliyekuwa akiitwa Eliudi kisha akamtaarifu kuhusu mkewe kujifungulia nyumbani na hatari iliyomkuta. Daktari Eliudi haraka aliagiza usafiri wa dharura (ambulance) kuja nyumbani kwa Elvine na baada ya dakika chache Elimina na mtoto walichukuliwa mpaka hospitali ya “The Lion” ambako walipewa hudum...

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 28

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 28 Ilipoishia……… Elimina alishikwa na uchungu wa ghafla mbele ya Edgar, lakini Edgar alianza kucheka kisha akasema “sasa Elimina mama, wacha mie niende nikanywe moja baridi huko kwa marafiki, alafu wewe liaaa liaaa ukichoka kufa na mwanao maana mlango nafunga dear…. Hospitali sio ya kwenda watu kama wewe. Au omba hata Mungu atume malaika waje wakusaidie”  Ilikuwa ni saa 7 mchana siku ya jumamosi sikuhiyo. Na isingekuwa rahisi kwa majirani kujua kinachoendelea pale ndani. Edger alitoka pale ndani na akafunga milango yote kisha akaondoka zake. Kusoma sehemu ya 27 bofya bapa. Sasa inaendeleaa…….. Elimina alishagundua kuwa tayari Edgar kaingiliwa na roho ya kishetani, hivyo anatumiwa kufanya vitu asivyovielewa kwahiyo sio kosa lake. Elimina alikosa nguvu na akawa anahangaika pekeyake pale ndani, wala hakuwa na msaada na tayari kiumbe cha Elvine kilikuwa kinabisha hodi duniani. Mbaya zaidi Elimina hakuwa na uzoefu wowote maana huyo ndiye alikuwa mwana ...

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.

Image
  UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27. First let me thanks GOD for giving me a unique chance to pass through this chapter by starting down to describe and express my internal feelings and emotional ideas down here๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡ ๐Ÿ”Kwa  Uchambuzi wa Kina ,, “Hatima ya Kimungu Sehemu ya 27” 1. Nafasi ya Maombi Katika Mapambano ya Kiroho Maombi ya Elimina yanapokea uzito mkubwa katika sehemu hii. Anaomba kwa imani na mamlaka, akituma moto na upanga kutoka mbinguni. Sauti yake inamfikia Elvine aliyepo mtini, ishara ya kuwa maombi ya dhati yanaweza kuvunja minyororo ya kiroho. ๐Ÿ‘ญMESEJI; SIKU ZOTE IMANI , rafiki Yako , ndugu Yako ama  mpenzi wako n.k inaweza kukutoa Kwenye jaribu usilo lijua kabisa HOJA YA PILI Mti wa Miujiza – Alama ya Njia ya Wokovu Mtini alipo Elvine, ambao hapo awali haukuwa na tunda wala uhai, sasa umechanua maembe na kuonekana kuwa na mwanga wa kipekee. Huu ni mti wa nuruni, unaosimamia neema ya Mungu na njia ya wokovu kwa Elvine. 1 Wakorintho 10:13 J...

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27. Ilipoishia……...               Elvine alikumbuka kila kitu, akajitambua na akakumbuka kila kilichotokea akiwa kwenye Ile ardhi, akajiuliza kuhusu Elimina na akatambua ukweli kuwa yule aliyenaye hawezi kuwa Elimina maana kuna vitu vingi alivyofanyiwa vibaya ambavyo Elimina asingeweza kufanya.... Kusoma sehemu ya 26 bonyeza hapa Sasa inaendelea…... Elvine akiwa pale mtini alikuwa akiwaza ni jambo gani litakaloendelea baada ya pale maana hakuwa na cha kufanya kwa haraka kutokana na mazingira yalivyo magumu kwake. Alitulia kidogo huku hofu imemkamata kisawasawa. Akaanza kusikia sauti ya Elimina anaomba sana tena anaomba maombi ya kupambana, Maombi; Mungu wa mbingu na nchi na ijulikane leo ya kuwa wewe ni Mungu wamiujiza. My husband Elvine has to come back no matter what. Namuombea nguvu mpya na ulinzi. Namuombea ujasiri katika hali anayopitia. Natuma moto kutoka mbinguni ukaangamize adui zake, natuma upanga ukatao kuwi...

Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31