HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31 Ilipoishia………. Elvine alipoteza amani kuliko hata mkewe maana kila alipomtazama mkewe basi moyo wake ni kama ulikuwa unachomwa na mwiba uliojishikiza huko kwenye mishipa ya moyo. Nafsi yake ilitaabika na ndipo alipoamua kutafuta muda mzuri, baada ya chakula cha jioni, azungumze na mkewe, maana ule ukimya wa siku mbili ulikuwa adhabu kubwa sana kwake. Kusoma sehemu ya 30 bonyeza hapa Sasa inaendelea………. Elimina mamy naomba kujua kwanini hutaki kuniuliza kuhusu sababu ya haya yote? Maana najua unajua kuwa kuna mahali mimi nilikosea, sasa unapokaa kimya hivyo… kiukweli unazidi kunichanganya maana ni kama hutaki kujua, sasa unadhani mimi roho yangu itatulia kweli?. Hata kama ungekuwa wewe lazima usingepata amani, ungekuwa hata unawaza hivi nakuwaziaje, nakuonaje na ninajisikiaje ninapokuona, sasa kwanini wewe umekaa kimya, sema neno tafadhali? (Elvine alikuwa akiongea bila kumtazama mkewe usoni maana moyo wake haukuwa katika hali ya utulivu). Pamoja na ...

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

 


Nashukuru kwa kushiriki nami link ya Hadithi hii tamu na Nzuri ya Hatima ya Kimungu Sehemu ya 29. 🙏

Nilichosoma katika sehemu hii, simulizi imeendelea  kwa mvuto mkubwa sana – linaonyesha mapambano ya ndani ya Elvine kati ya imani yake, hofu yakuwaza kumpoteza mkewe Elimina, na hatia ya makosa ya zamani. Kuna mambo yafuatayo nimeona  yaliyobeba msingi   wa  sehemu hii:

1. Mgongano wa nafsi ya Elvine

👉Anapokuwa mbele ya Malaika Elvila, anatakiwa kufanya maamuzi magumu: kati ya mke na mtoto.

👉Uamuzi wake unaonyesha upungufu wa mwanadamu, uchungu, na jinsi maumivu yanavyoweza kuathiri fikra na maamuzi.

2. Adhabu na Neema

👉Kupotea kwa mtoto na kutozaa tena kwa Elimina ni matokeo ya makosa ya Elvine, lakini bado neema ya Mungu inaonekana kwa kumrejesha mkewe.

👉Malaika anamkumbusha kuwa Mungu si mkatili, bali anamfundisha kupitia mateso na changamoto.

3. Ugeuzi wa Maisha (Turning Point)

👉Elvine sasa anaitwa kuwa mchungaji wa kondoo wa Bwana, ishara kwamba maisha yake yamepata mwelekeo mpya.

👉Huu ni mwanzo wa safari yake ya kiroho, kutoka katika hatia na huzuni kuelekea huduma ya kiungu.

4. Upendo wa ndoa

👉Muunganiko wa Elvine na Elimina unaelezwa kwa hisia kali sana – kilio chao, kumbatio lao, na maneno ya madaktari yanasisitiza kuwa wanapendana kwa dhati.

👉Hii inafundisha kuwa mapenzi ya kweli hupimwa kwenye majaribu makubwa.

Kwa mtazamo wa kifasihi na kimaana , sehemu hii imejaa:

Ustadi wa kusisimua Kwa msomaji (suspense) , Cha kutaka  kujua nini kitatokea baada ya Elvine kufanya maamuzi yasiyo na uhakika.

Maswali ya kimaadili na imani ,kati ya upendo wa familia na mapenzi ya Mungu.

Mafundisho ya kiimani , kuwa Mungu huruhusu mateso kwa ajili ya kutufundisha na kutuandaa kwa jukumu kubwa aidha LA kiroho au kimwili.

🙏Mr. MIGONGO ELIAS & JACQUELINE JOHN🙏

Here I have written a message  in both literary work  and spiritual matter, woven together with the eternal Word of God, so that it may carry the weight of the heart and the power of impact upon the reader and the listener.

🙏Mwanadamu usicheze na Mungu 🙏

Mungu si mtu, aseme uongo; Wala si mwanadamu, ajute; Iwapo amesema, hatalitenda? Iwapo amenena, hatalifikiliza?(Hesabu 23:19).

Anaposema, hufanyika; anapotoa ahadi, haina budi kutimia.

Njia zake ni za ajabu mno, hazichunguziki wala hazielezeki, kwa

macho ya mwili hayawezi kuyafikia, na akili za wanadamu haziwezi kuyafasiri.

Isaya 55:8-9  Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema Bwana.

 Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu. 

Yamkini leo unapita katika kivuli cha mauti, katika giza la huzuni, katika majaribu yasiyoelezeka. Yamkini machozi yamekuwa mkate wako mchana na usiku, na moyo wako umejaa maswali yasiyo na majibu. Lakini kumbuka: Mungu halali na pia, Mungu hajakuacha, Mungu hajanyamaza bure Katika pitapita zako yupo NAWE Kila saa.

“Zaburi 23:4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.

Amini, hakika ipo siku moja, kutakuwa vyema tu.

Kwani macho ya Mungu yameelekezwa juu yako, na rehema zake hazikomi.

Mapito yako ni darasa, mateso yako ni maandalizi, na machozi yako ni mbegu ya furaha ijayo.

Kwa hiyo mwanadamu, usidanganyike kwa kuichezea neema ya Mungu.

Ukihesabu magumu yako kama adhabu, kumbuka ni daraja la neema.

Ukiona giza mbele yako, jua ni kivuli cha mwanga unaokuja.

Kwa maana Mungu ni mwaminifu, na hajawahi kudanganya.

Anakuangalia, anakushika, na mwisho wake utashangilia.

In conclusion ;This part of Hatima ya Kimungu (Section 29) has deeply touched me. The blend of pain, love, faith, and sacrifice shows how fragile human life is, and how God uses trials to shape our destiny.

As a writer and a believer, I see in Elvine’s struggle the reflection of many of us when faced with impossible choices  torn between love, responsibility, and God’s will. His tears represent the weakness of humanity, but his new covenant with God reveals that redemption and transformation are always possible.

I truly admire the way this story reminds us that marriage, faith, and commitment to God can carry us through the darkest valleys.




DANIEL EMANUEL NGASA 


CONTACT;+255 683 227 7.

Kusoma sehemu ya 29 bonyeza hapa

Hadithi  hii imendaliwa na kuandikwa na JACQUELINE JOHN.

Mtunzi wa Hadithi (simulizi) .

 Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255789523850. Normal >>>>>+255747313148.

                            &, 

Imehaririwa na MIGONGO ELIAS. Mhariri.

Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255767653697. Normal >>>>>+255617653697.

Pamoja na;

ERICK MGAYA. Mhariri.

Mawasiliano :

Normal and WhatsApp no >>>>+255764032905

Tu follow kwenye.

Facebook page>>> Add Value Network.

                        GeT tO tHe NeXt LeVeL!

Kama umejifunza kitu shiriki nasi katika comment hapo chini, ili kuboresha na kujifunza zaidi.






Popular posts from this blog

MAAJABU YA AKIBA

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.