Posts

Showing posts from September, 2023

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23. Ilipoishia...... Alipofika nje, alimkuta Elimina katahamaki sana tena anahasira sana.  "Umefanya nini Elvine? Elimina aliuliza kwa ukali sana tena hadi macho yalikuwa mekundu kama damu kwaajili ya kujaa hasira.... Swali; kwanini Elimina anahasira? Na Elimina huyu anasiri gani na nyumba iliyoungua moto? Kusoma sehemu ya 22 bonyeza hapa   Sasa inaendelea...... Elvine alikuwa anatetemeka  kwa hofu ya yale anayoyaona lakini alistaajabu kuona ni kama mkewe hajali sana kuhusu yeye. Alimtazama kwa makini sana mkewe akiwa anajaribu kutafakari kwanini anaonekana kuwa na hasira juu yake. Elimina akajishitukia "Hey, wewe! Nini sasa unanitazama hivyo?" "Nakutafakari sipati majibu!' "Nimefanyaje kwani?" "Hamna ila sijajua kama umenihofia mimi au hilo swali lako linamaana gani? "Elvine baba sina maana hiyo uliyoelewa wewe kabisa. Shida yangu mimi umefanya nini mpaka unataka kuhatarisha maisha Yako namna hii. Hujui namna ga

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI NA TANO.

Image
SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”.   SEHEMU YA KUMI NA TANO.  Ilipoishia... Usisogee maana hapo unaposogea ndipo nataka kudondokea kwahiyo pishaaa!!" Kabla hajayatafakari yale maneno yule mtu alijiachia makusudi kabisa na kujitupa chini. Elvine alishangaa zaidi. Alitaka kusogea ili akatoe msaada lakini yule mtu ghafla alipotea.         Elvine alipata hofu zaidi. Akakimbia mpaka chumbani kwake na akajihisi kabisa hadi ile kiu imekata. Lakini alipofika chumbani kwake alipigwa na butwaa kwa kile alichokuwa anakiona mbele yake na wala hakuamini kwa haraka.... Kusoma sehemu ya 14 bonyeza hapa Inaendelea...     Alipotazama kitandani kwake alimuona kijana yule aliyekuwa kaanguka mchana na ndiye aliyemuona kajiangusha muda sio mrefu kutoka kwenye ngazi tena akiwa anacheka sana.       "Kumbe ni wewe? Unajua nilikuwa najiuliza sana kuwa ni kijana yupi ambaye anakaa hapa na anauwezo wa kufanya mambo makubwa. Kwakweli nimekupenda, nadhni kazi nimeikamilisha. Kwasasa nae

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI NA TATU.

Image
  SIMULIZI YA KUFURAHISHA,   “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI NA TATU.     Ilipoishia..   Aligundua kuwa kumbe Elimina anamachungu sana moyoni mwake. Aliacha kumfokea na kuanza kumwomba msamaha huku akitamani kujua tatizo ni nini hasa. Wakati akiwa anambembeleza alikaa pembeni ya Elimina kwenye sofa huku akisema samahani. Ghafla mama aliingia na kushangaa kwa kile alichokiona "Nyie watoto ni upuuzi gani mnafanya hapo?....." kusoma sehemu ya kumi na mbili bofya hapa   Sasa inaendelea....   Elvine hawakujua wamjibi nini maana walijua kabisa mama atakuwa kaelewa kwa tofauti sana.     "Samahani mama sio kama unavyofikiria. Ni kwamba Elimina hajisikii vizuri. Na alikuwa akilia na mimi sijui shida ni nini na ndio maana nilitaka aniambie" Elvine alijaribu kujitetea       "Jiandaeni kwaajili ya kikao cha familia akija baba yenu" mama aliongea kwa mkato kisha akaondoka na kuelekea chumbani.         Elimina naye baada ya mama kupita ali

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.