HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23. Ilipoishia...... Alipofika nje, alimkuta Elimina katahamaki sana tena anahasira sana.  "Umefanya nini Elvine? Elimina aliuliza kwa ukali sana tena hadi macho yalikuwa mekundu kama damu kwaajili ya kujaa hasira.... Swali; kwanini Elimina anahasira? Na Elimina huyu anasiri gani na nyumba iliyoungua moto? Kusoma sehemu ya 22 bonyeza hapa   Sasa inaendelea...... Elvine alikuwa anatetemeka  kwa hofu ya yale anayoyaona lakini alistaajabu kuona ni kama mkewe hajali sana kuhusu yeye. Alimtazama kwa makini sana mkewe akiwa anajaribu kutafakari kwanini anaonekana kuwa na hasira juu yake. Elimina akajishitukia "Hey, wewe! Nini sasa unanitazama hivyo?" "Nakutafakari sipati majibu!' "Nimefanyaje kwani?" "Hamna ila sijajua kama umenihofia mimi au hilo swali lako linamaana gani? "Elvine baba sina maana hiyo uliyoelewa wewe kabisa. Shida yangu mimi umefanya nini mpaka unataka kuhatarisha maisha Yako namna hii. Hujui namna ga

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI NA TATU.

 


SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”.

SEHEMU YA KUMI NA TATU.  

Ilipoishia..

 Aligundua kuwa kumbe Elimina anamachungu sana moyoni mwake. Aliacha kumfokea na kuanza kumwomba msamaha huku akitamani kujua tatizo ni nini hasa. Wakati akiwa anambembeleza alikaa pembeni ya Elimina kwenye sofa huku akisema samahani.

Ghafla mama aliingia na kushangaa kwa kile alichokiona

"Nyie watoto ni upuuzi gani mnafanya hapo?....."

kusoma sehemu ya kumi na mbili bofya hapa

 Sasa inaendelea....

 Elvine hawakujua wamjibi nini maana walijua kabisa mama atakuwa kaelewa kwa tofauti sana.

    "Samahani mama sio kama unavyofikiria. Ni kwamba Elimina hajisikii vizuri. Na alikuwa akilia na mimi sijui shida ni nini na ndio maana nilitaka aniambie" Elvine alijaribu kujitetea

      "Jiandaeni kwaajili ya kikao cha familia akija baba yenu" mama aliongea kwa mkato kisha akaondoka na kuelekea chumbani.

        Elimina naye baada ya mama kupita aliondoka na kwenda chumbani kwake kwahiyo Elvine akajikuta amebaki pekeyake pale sebuleni.

         Alikaa kwa muda akiwa hajui hata anachowaza. Ilipofika saa 6:00 aliamua kuondoka na kwenda kulala.

        Asubuhi aliamka na akawa anatamani sana kuongea na mama ili amuelekeze vizuri asije akaendelea kumtazama vibaya maana alishapata uwoga sana kuhusu mtazamo wa mama juu yake.

       Alitoka sebuleni na akamuona mama akienda jikoni. Alimfuata mpaka jikoni na akamkuta akiwa anawasha moto kwaajili ya kuandaa chai ya asubuhi.

        "Samahani mama naomba tuzungumze"

        "Kuhusu nini?"

        "Mama naomba unielewe. Sikuwa na maana mbaya kumzuia binti yako asilie maana kweli kabisa Elimina alikuwa akitia huruma. Halafu Elimina ni rafiki yangu tu mama naomba usiniwazie vibaya"

          "Kwani mimi nimesema nini? Mbona maelezo mengi?"

          "Mama Mimi naelewa wewe kama mzazi hupendi mwanao aharibikiwe lakini Nina jambo. Naomba uniwasilishie kwa baba pindi akirudi"

         "Nikuwasilishie kuhusu nini?"

.        "Nahitaji kuoa kwenye hii familia"

         "Na nilijua tu."

         "Naomba sana mama"

         "Ni kweli lakini kwanza lazima utambue kwanini Elimina anakuchukia na huwa anaumia sana pindi akikutazama halafu ndiyo ujue kama atakubali kuolewa na wewe"

          "Kwani kuna  jambo ambalo lilitokea wakati mimi sipo?"

          "Sina jibu sahihi lakini kamuulize yeye mwenyewe utapata jibu"

          "Mbona unanitisha mama?"

.         "Kwanini sasa?"

          "Ok sawa! Nitalifanyika kazi hilo"

          "Elvine alitoka jikoni huku akiwa anawaza, hivi ni nini kilichotokea? Ndio maana Elimina anaonekana hana amani kabisa. Nahisi kuna jambo zito sana hapa. Ngoja nipeleleze, na lazima nijue japo Elimina ni mgumu sana kueleza mambo yake kwangu"

            Elvine wakati akiwa katika mawazo hayo alijikuta akigongana na Elimina sebuleni.

          "Ooh! Sorry Elimina... Eti unausingizi?"

         "Kwanini?"

         "Naona unasinzia huku unatembea

         "Mmh! Kwanini?"

         "We unazani kwanini tumegongana?"

         "Basi hata wewe unasinzia ndio maana huoni mbele" Elimina aliongea kwa masihala kidogo.

           Elvine alicheka lakini Elimina alitabasamu kidogo na kuondoka.

           Ilopofika saa 7; mchana Elvine alikwenda kwa mama na kumwambia kuwa anahitaji kutoka na Elimina japo anahisi haitakuwa rahisi kwa Elimina kukubali kwahiyo anaomba mama amsaidie kumfanya Elimina aweze kukubali.

         Mama alimtazama sana Elvine kwa muda kabla hajakubali ombi lake. Kisha akamwambia.

          "Elvine, wewe ni nani hasa?"

          "Kwanini unauliza hivyo mama?

          "Unatakiwa kuondoka hapa nyumbani haraka maana watu wataanza kujaa hapa nyumbani hivi Karibuni"

         "Unaongea kuhusu nini mama"

         "Leo nilikuwa huko sokoni. Nikakutana na wamama wawili pamoja na vijana Kama wanne hivi wakiwa wanakuulizia.  Sasa waliponisimamisha sikuwa najua kama wataniuliza kuhusu wewe. Lakini nilishangaa waliponionyesha picha yako na kuniambia unamjua huyu? Mwanzo nilihisi polisi lakini baadaye nikajua tu kuwa wale sio polisi kwa namna walivyokuwa wanaonekana.

       Niliwajibu ndio. Baada ya jibu langu wale watu walifurahi sana. Na wakanishukuru sana. Waliomba niwaambie unapopatikana na mimi nikawaambia kuwa wewe ni kijana wangu. Mmoja wao alisema kuwa nnabahati sana kuishi na kijana kama wewe. Nilipouliza kwanini waliniambia wanahitaji kupafahamu kwangu. Nilikuja nao mpaka hapo nje. Lakini hawakuingia ndani. Tukiwa hapo nje ndipo walipoanza kunieleza kuhusu mambo uliyoyafanya wakati umefika Iringa. Nilistaajabu sana maana hata mimi nilisikiaga kwenye taarifa ya habari lakini sikujua kama ni wewe"

       "I am sorry mama kwakuwa sikuwahi kuwaeleza kuhusu suala hili. Lakini ni kweli mama. Mimi ninabaraka fulani za kipekee kutoka kwa Mungu na mara nyingi nimefanya mambo mengi sana ambayo hata mimi sikujua nimewezaje ila ni kwa nguvu za Mungu tu"

         "Sawa lakini najua wale watu watarudi. Na pindi wakirudi hawatakuja peke yao bali watakuja wengi sana na mwisho tunaweza jenga hospitali hapa"

         "Ni kweli lakini pasipo Elimina mimi hapa kuondoka itakuwa ngumu"

          Lile neno lilimpa kigugumizi mama na asijue cha kueleza. Wakati huo Elvine aliongea akiwa kamkazia macho mama.

        "Lakini katika taratibu zetu za kuoa binti wa kihehe lazima wazazi wako ndiyo wahusike"

        "Mimi hapa nipo mimi tu. Na kila kitu ni nyie na mimi ndiyo tutakao shughulikia. Maana hapa Tanzania mama wala baba hawapo. Labda mambo yakiwa sawa basi babu yangu atashughulikia kila kitu"

        "Sawa basi, lakini lazima ujue kwanza Elimina anawaza nini"

         "Naomba msaada wako basi mama eeh?"

         "Mmmmmh! we mtoto mbona unanitia majaribuni? Aya sawa basi"

          Mama na Elvine walitazamana kisha wakatabasamu na mwisho waliangua vicheko.

         Mama alitoka jikoni na kumuita Elimina kumueleza kuwa yeye anatoka kidogo kwahiyo anahitaji watoke wote pamoja na Elvine maana kuna mahali anataka awapeleke.

          Elimina akakubali kwahiyo akaenda kujiandaa. Wakati huo Elvine alikuwa kajificha jikoni anachungulia sebuleni. Mama alimpa ishara kuwa ajiandae haraka kutoka. Elvine alitoka mbio mpaka chumbani. Alipofika chumbani alichukua begi lake na kumwaga nguo zake zote kitandani.

          Alitazama suti zake na kila aliyoishika aliona kama haifai. Alianza hadi kuchanganyikiwa maana alijihisi kama hana nguo licha ya kuwa na nguo nyingi sana.

          "Sasa hapa nitavaa nini mimi jamani? Leo nataka niwe tofauti sana lakini naona kama ni ngumu kwangu. Daah!" Baadaye alipata wazo. Akachagua suti moja ya bluu ya kawaida tu Kisha akaipasi vizuri na akaanza kujiandaa kwaajili ya mtoko huo.

         Ilipofika saa 9:30 kila mmoja alikuwa tayari amejiandaa. Elimina ndiye aliyependeza kuliko wote siku hiyo hadi Elvine akajiona hajapendeza. Walipofika mlangoni kwaajili ya kutoka walikuja wageni wanne wakiwa wamebebe wagonjwa wawili.

         Wale watu walikuja kwa Elvine ili wamueleza kuwa wanahitaji msaada wale. Kwakweli Elvine alitamani kulia na kuwafukuza maana aliona mipango yake inaharibika.

          Alimtazama mama ambaye kwa wakati huo hakujibu neno bali alionekana wazi kabanwa na kicheko ila anajizuia tu. Elimina yeye hakuwa anaelewa chochote kwahiyo aliona ni sawa tu hivyo akafungua mlango na wageni wakaingia ndani.

          Elvine alikaa na wageni sebuleni na kuanza kuongea nao huku akiwa na maumivu moyoni.

            Wale watu waliianza kumueleza namna wagonjwa wao walivyoanza kuumwa. Elvine alijikuta kapata moyo wa huruma baada  ya wale watu kumueleza kuwa wale wagonjwa ni wazazi wao na walianza kuumwa baada ya mjomba wao kutamani mali zao na kuanza kulazimisha kuzichukua kwa nguvu. Lakini baada ya kunyimwa alisema tu lazima atazipata zile mali, na haikuchukuwa muda toka mjomba wao aseme hivyo wazazi wao walianza kuumwa. Na baada ya kuumwa walipolwa mali zote na mjomba wao maana hawakuwa na wakili wa kuwatetea na isitoshe hawakuwa wamesoma, kwahiyo hawakujua ni wapi wanaweza kudai haki zao.

        Wakati wale wageni wanaongea hayo. Elimina alikuwepo pembeni anasikiliza. Elimina alipata huruma sana na machozi yakamtoka. Elvine alipomtazama Elimina na kumuona analia alijikuta anatabasamu kimoyo moyo.

       Elimina alisogea pale na kuketi karibu  na wagonjwa lakini alikuwa hajui kabisa kuwa Elvine anauwezo gani kwahiyo alihisi wageni wale hasa walikuwa wanamuhitaji baba yake.

        "Poleni sana. Lakini yupo Mungu anayeweza kuponya na kuondoa huzuni zetu. Sisi tutawaombea japo mchungaji hayupo. Lakini imani zenu ndizo zitakazo waponya wazazi wenu maana sisi hatuwezi chochote bali ni Mungu tu" Elimina aliongea hivyo kwa kuonesha hisia na huruma.

          Elvine alikuwa akizidi kufurahia maneno ya kitumishi na hapo ndipo akaona kumbe yeye anaweza kuwa mchungaji. Maana Elimina alizungumza kama mama mtumishi.

          Elvine alijikuta kapata nguvu hata ya kuomba. Alisimama na kuanza kuomba. Na alipomaliza kuomba ndipo alipowagusa wagonjwa wale nao wakawa wazima.

          Elimina alishangaa kidogo maana hakuelewa namna wale wagonjwa walivyopona. Alimtazama sana Elvine ambaye bado alikuwa uweponi. Baada ya uponyaji wa watu wale basi waliondoka zao. Elvine alikwenda chumbani kwa mama kugonga wakati Elimina akiwasindikiza wageni kidogo na kuwatia moyo.

           "Mamaaa!! Sahizi bado mapema naomba tusiahirishe jamani"

           "Saa ngapi kwani"

           "Ni kumi na moja kasolo chache. Please mama"

           "Mmmh!! Tutaenda kesho, hapana mama haiwezekani. Basi nitakununulia zawadi nzuuuuri ila we nisaidie tu"

           "Aya nakuja" Elvine alifurahi sana baada ya jibu la mama.

           Baada ya dakika Kama tano mama alitoka na Elimina alikuwa karudi.

           "Aya twendeni wanangu"

           "Nikajua tumeahirisha maana muda umeend pia"

           "Kuna umuhimu wa kwenda leo hiyo sehemu. Kwahiyo twendeni"

            Basi walitoka pale nyumbani na kuondoka mpaka hotelini. Ambako aliagiza juice tu na wakaanza kupiga stori za hapa na pale. Elimina aliuliza. Kwanini wako pale. Mama alisema kuwa kuna mtu wanamsubiri.

         Elvine aliondoka na kusema kuwa atarudi sio muda mrefu. Elimina na mama yake walikaa pale na kuendelea na stori mbalimbali za kupoteza muda.

          Ilipofika saa moja kamili simu ya mama iliingia sms, aliitazama na kisha akatabasamu tu.

         "Sasa Elimina, mgeni wangu yupo mahali nazani hatokuja hapa, kwahiyo msubiri Elvine aje halafu mrudi nyumbani mimi nitawakuta"

         "Elvine toka aondoke mpaka sahizj hajarudi mimi nitajuaje kama anarudi? Pengine kashaenda hata nyumbani maana yule naye"

         "Hapana mimi aliniambia anakoenda kwahiyo najua atarudi. Usimuache maana si unajua yule bado ni mgeni hapa?"

         "Aya, sawa mama"

     Elimina alisubiri pale wakati mama anaondoka. Alikua kachukia maana kitendo cha kufika pale halafu Elvine kuondoka kilimkera sana.

     "Elimina nimerudi..." Sauti ya Elvine ilisikika nyuma ya Elimina.

      Elimina alipogeuka alishangaa sana namna ambavyo Elvine alivyokuwa anaonekana....

 Sehemu ya kumi na nne >>>>>Itaendelea jumatano. Usikose kufuatilia

Kupata mwendelezo wake bonyeza hapa

 Hadithi hii imendaliwa na kuandikwa na JACQUELINE JOHN.

Mwimbaji na mtunzi wa nyimbo, mashairi, Hadithi (simulizi) na ngonjera.

 Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255789523850. Normal >>>>>+255747313148.

                            Na, 

Imehaririwa na MIGONGO ELIAS. Mhariri.

Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255767653697. Normal >>>>>+255783327456.

                        GeT tO tHe NeXt LeVeL!

Kama umejifunza kitu shiriki nasi katika comment hapo chini, ili kujifunza na kuboresha zaidi.

 

 

 

         

 

          

    

 

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.