HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI NA MBILI.

 



SIMULIZI YA KUFURAHISHA,
 “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”.

SEHEMU YA KUMI NA MBILI. 

"Mmh! Mbona amekata tena simu huyu au anabip? Ngoja nimpigie" Elvine alianza kutabasamu huku maneno yaliyokuwa yameandikwa kwenye ile barua ya baba yake yakijirudia kichwani mwake.

    "ila kama ningekuwa mimi basi ningekushauri kuwa yule binti Elimina anaweza kuwa mke mzuri sana kwako, maana anaonekana kuwa na heshima sana na mwanzo nilipokuona naye nilizani unamalengo naye. "

kama hujasoma sehemu ya kumi na moja bonyeza hapa

     Alipiga simu lakini haikupokelewa. Akajaribu mara kadhaa lakini haikupokelewa. Aliamua kutuma meseji lakini nazo hazikujibiwa. Baadaye alipopiga tena simu haikuwa inapatikana. Aliumia sana amani ikapotea tena.

    "Huyu binti anashida gani? Si amepiga hapa jamani? Mbona hapokei simu yangu?"

     Alijiuliza maswali mengi lakini hakupata majibu. Aliamua kulala pale hotelini mpaka jioni. Alipoamka alipata wazo la kumpigia mchungaji Moses baba yake Elimina.

     "Hallo baba! Shikamoo"

     "Marahaba Elvine kijana wangu. Upo? Bwana yesu asifiwe"

      "Amina. za nyumbani?"

      "Ni njema tu. Mbona umetususa?"

      "Nitakuja baba"

      "Lini?"

      "Muda wowote tu"

      "Sawa karibu sana"

      "Samahani, hivi Elimina yupo?"

       "Haaa! kumbe huwa hamuongei bado mpaka leo mnaugomvi?"

       "Hapana, ni kwamba simu yake haipatikani"

       "Anhaaa labda imeisha chaji ila alikuwa nayo sio mda anaichezeachezea hapa, badae aliondoka sasa sijui labda yupo anaichajia huko chumbani kwake."

       "Anhaaa Asante baba, basi nitamtafuta baadaye"

       "Sawa. Uje bwana, mama yako kakumisi huku"

       "Nakuja wiki ijayo"

       "Waoh! Ngoja tukuandalie jogoo"

       "Asante baba"

       "Karibu sana"

       "Asante ubarikiwe baba"

       "Amina"

      Baada ya mazungumzo hayo Elvine alishusha pumzi na akachukua kadi ya pesa aliyoachiwa na baba yake kisha akaenda kwa babu yake Mr. Edward ambako alikuta bibi yake amekwisha kuzikwa masaa machache kabla ya yeye kwenda.

        Baadaye wakati akiwa katika mazungumzo na babu yake aliweza kutambulishwa ndugu wa mama yake na aliambiwa kuwa angewahi basi angeweza kumuona mama yake maana Mama yake na baba yake walikuwepo pale msibani toka asubuhi.

         Elvine alijilaumu sana kwanini hakwenda mapema nyumbani maana alihisi kuwa kama angeenda mapema pengine angekuwa na uwezo wa kuwazuia.

          Aliamua kuanza maisha mapya sasa pasipo kuiwaza familia yake maana aliona hakuna haja kwasababu wakati huu alikuwa na uhakika kuwa familia yake ipo salama.

           Siku iliyofuata mapema saa 12:00 aliamka cha kwanza alishika simu yake kwa lengo la kumtafuta Elimina. Simu iliita tu lakini haikupokelewa. Alianza kuhisi vibaya, na akahisi kuwa Elimina anamfanyia makusudi.

         Aliamua kuachana na simu kwa wakati huo maana aliona inamfanya akereke tu hivyo akaenda sebuleni. Alipotoka nje sebuleni aliwakuta watu wenye fedha zao wamekaa sebuleni na babu yake wakiwa wanakikao naye kifupi kwaajili ya kumpa mkono wa pole.

     "Aisee najua tu hawa watu hapa mkono wao wa pole sio wakitoto. Mmh! Kweli haya magepu maana izo pesa bora wangetoa tu kwawahitaji maana sioni umuhimu wa kumpa babu hela nyingi wakati yeye tu anahela hadi anaumwa" Elvine alijisemea kimoyo moyo huku akiwa anapita pale sebuleni na kutoka nje.

        Akiwa katika hayo mawazo yake aligongana na mtu mlangoni.

        "Ooh! Sorry sister (ooh, samahani dada), sijui hata nilikuwa natazama wapi?"

           "It's ok don't worry (ni sawa usijali). Najua utakuwa ni mshituko tu wa msiba ndiyo unaokusumbua" alijibu yule binti kwa tabasamu

         (Mmmh! Ungejua hata sio kwaajili ya msiba maana hata sijakaa sana na hawa watu na sikuwazoea) Elvine alimjibu yule binti kimoyo moyo pasipo kutoa neno.

           "Ooh! Eeh! Itakuwa labda ni msiba ndiyo. Samahani sana" Elvine alimjibu yule binti huku akijichekesha chekesha.

         "Hivi wewe na Mr. Antony undugu wenu upoje?"

          "Ni babu yangu"

           "Anhaaa! Unaitwa nani?"

           (Mmmh huyu binti vipi mbona ana maswali mengi inakuwa kama kituoni bwana? Halafu wafiwa hawasumbuliwagi, huyu binti sijui wawapi?) Elvine alilalamika kimoyo moyo

            "Naitwa Elvine"

            "Jina zuri sana, nashukuru kukufahamu. Mimi naitwa Eriviela ni mtoto wa mfanyabiashara pia"

            "Anhaaa Asante, nashukuru kukufahamu pia, kwaheri"

             "Mbona unaharaka Elvine unakwenda wapi?"

               (Hiiii, huyu binti pepo nini mbonaa anajipendekeza sana asee) "anhaa  eeh! Kuna mahali nawahi". Elvine alijibu huku alilalamika moyoni.

           "Vipi naweza ku......" Kabla hajamaliza kuongea Elvine aliamua kuondoka na kwenda zake. Alipofika nje alikutana na baba yake mjomba wake akiwa na mkewe aliwasalimia na wakaanza kupiga stori za hapa na pale.

          "Elvine hivi hujaoa eeeh?" Mjomba wa Elvine aliuliza ghafla wakiwa katika mazungumzo.

           "Hiii? Uncle bwana. Mbona ghafla umeuliza hivyo?"

           "Hapana, nataka kujua tu, ila unajua mama yako na baba yako bwana. Walioanaga ndoa ya ofisini"

           "Kwanini sasa?"

           "Huyo mzee kipindi hicho alikuwa anazingua sana bwana"

           "Nani? Babu Mr Edward?"

           "Eeh! Nani mwingine sasa?. Alitaka kumlazimisha mama yako aolewe na jamaa fulani wa kijinga sana".

           "Kwahiyo ikawaje sasa?"

           "Nitakusimulia siku nyingine, sahizi ngoja niende mahali fulani mara moja"

           Elvine alihisi kakatishwa simulizi moja tamu sana yenye maajabu ndani yake. Mjomba wake aliondoka na yeye akaagana na shemeji yake na kuamua kurudi chumbani kwake.

            Baada ya wiki moja watu walikuwa wamesha tawanyika na sasa kukawa kimya sana pale ndani. Wafanyakazi tu ndiyo waliokuwa wakionekana kupitapita napo ni kwautulivu na heshima kubwa. Babu yake alikuwa mnyonge sana muda mwingi.

          Siku moja Mr. Antony alimuita Elvine na kumwambia kuwa angependa sana kama Elvine angeoa na kumleta mkewe pale nyumbani maana kama akiwaona wajukuu zake huko mbeleni pengine atapata furaha.

          Elvine hakuwa na jibu sahihi lakumpa babu yake maana akilini mwake hakujua kama ni kweli anachokiwaza akilini mwake kinaweza kutimia.

         Alikwenda chumbani kwake na akawaza sana. Alikumbuka mambo mengi sana kuhusu Elimina, toka wakiwa China mpaka wanarudi Tanzania. Alitamani kumuona Elimina lakini bado moyoni mwake alikuwa akihisi hatia sana kwa yale aliyomfanyia binti yule. Alianza kutazama meseji mbalimbali ambazo walikuwa wakitumiana toka wakiwa China ambazo nyingine zilimchekesha sana. Lakini alikuja kushituka baada ya kukutana na meseji moja ambayo hakuwahi kuiona.

       "Inamaana kumbe kuna siku Elimina alinitafuta wakati nikiwa hapa Dar es salaam?. Mmh! Hi ni mbaya zaidi" Elvine alijihoji na kujilaumu sana

       Kesho yake alimwambia babu yake kuwa anasafari kidogo. Babu yake hakuwa na shida kabisa alimruhusu aende anakotaka kwenda.

       Elvine alipanda gari la kwenda Iringa. Lakini akiwa anapanda alimwambia dereva.

      "Kaka naomba uendeshe gari vizuri maana nahisi kama tusipokuwa makini tutapata ajali"

     Konda alijibu "ajali nazo ni mpango wa Mungu tu ili binadamu apumzike" konda na dereva walicheka kama utani lakini Elvine alikuwa anamaanisha kuwa anaiona ajali mbele.

      Walianza safari. Elvine alikaa nyuma kabisa ya gari. Gari ilikwenda kasi sana hadi abilia wakawa wanalalamika. Lakini kwa wale wanaopenda kuwahi kufika walikuwa wakichekelea tu na kufurahia mwendo ule.

        Walifanikiwa kufika Iringa lakini wakati wanaingia stendi Ghafla gari liliacha njia na kugongana na gari nyingine wakati dereva alipokuwa akitaka kumpisha mwenzie kwa pembeni na kumbe mbele kulikuwa na gari jingine.

        Gari ilianguka vibaya sana na wote waliokuwa ndani ya gari walipiga kelele lakini wakati huo Elvine alikuwa amelala kwahiyo hakuona kilichotokea na hata baada ya gari kuanguka wala  hakushituka. Waokozi walikuja na kuokoa watu wachache ambao waliweza kuishi lakini watu watatu walipoteza maisha.

         Dereva na konda waliumia sana lakini hawakufa. Elvine hakuumia popote lakini hakuwa anajitambua maana alikuwa bado katika usingizi mzito sana. Waokozi walihisi labda kaumia kwa ndani ndio maana kapoteza fahamu hivyo naye akapelekwa hospital kwaajili ya uchunguzi zaidi.

     Alikuja kushituka saa 12:30 jioni. Alishangaa kujikuta kalazwa maana hakuwa anaelewa kilichotokea. Alipoamka nesi mmoja alikuja na kumsalimu.

     "Unajisikiaje?"

     "Kwani nini kimetokea?"

     "Kwani hukuona wakati ajali inatokea?"

     "Ajali?"

     "Ila ni ajabu sana. Maana wewe peke yako hata mchubuko hukupata ila ulizimia tu"

     "Hapana bwana, Mimi. mbona nililala tu. Na hata ajali Sina taarifa nayo"

      "Kivipi?"

      "Lakini dereva alipohojiwa alisema kuwa kuna mtu alitabili ajali kabla haijatokea, au ni wewe"

     "Hapana mimi sikutabili ajari Bali nilimuasa tu aendeshe kwa uangalifu tusije kupata ajali"

      "Kwanini ulisema hivyo?"

      "Basi tu"

      "Basi maneno yako yalitimia"

       Elvine alistaajabu sana akaomba kuwaona waathirika wa ajali ile ambao hawakufa. Alipelekwa kwenye wodi ya wagonjwa mahututi. Alipofika aliwahurumia sana mpaka machozi yakamtoka. Alitembea tembea mule ndani huku akiwatazama wale wangonjwa. Wale wagonjwa waligeuka kumtazama japo kwa shida sana. Na kila aliyemtazama Elvine alipona hapohapo. Nesi aliogopa sana akaamua kukimbia mule ndani na kwenda kuita watu.

     Baada ya muda watu walijaa mule wodini na wakastaajabu maana wagonjwa wato wa siku hiyo walikuwa wazima kabisa. Elvine mwenyewe alijiogopa kidogo. Alipokuwa anatoka pale ndani kila mtu alikuwa anamshangaa. Aliamua kutimua mbio maana hakutaka awe maarufu kwa kitu alichokifanya asije akatukuzwa yeye.

      Alipotoka pale hospitali alielekea nyumbani kwa kina Elimina. Akiwa njiani alimuona Elimina kwa mbali, akiwa kashika simu. Akaona ampigie iwe kama 'surprise' lakini alishangaa sana baada ya kuona Elimina akiitaza simu mpaka inakata pasipo kuipokea.

     Alishangaa sana. Akapiga tena, lakini kadharika Elimina aliitazama simu pasipo kuipokea. Elvine alichukia sana, kwakuwa Elimina alionekana kama anayekwenda mahali fulani, aliamua kumuacha aende kwanza na yeye akaenda nyumbani ambako alipokelewa na mama na kuambiwa kuwa baba kasafiri kidogo kihuduma.

Akiwa anapiga stori pale sebuleni na mama, Elimina alirudi. Alishangaa sana kumuona Elvine pale sebuleni.

"Elvine?"

"Yes"

"Ooh, karibu sana"

"Asante sana"

Elimina aliondoka na kwenda zake chumbani kwake. Elvine alishangaa maana aliona kama kuna namna Elimina anampuuzia.

Siku iliyofuata asubuhi Elvine aliamka mapema sana. Alimkuta Elimina akiwa anadeki sebuleni. Akamsalimia, Elimina alijibu kwa sauti ya unyonge sana jambo ambalo hakulipenda.

"Unaumwa?"

"Hapana"

"Hivi bado hujanisamehe tu mpaka leo Elimina?"

"Kwa kosa gani?"

"Lolote"

"Ninakazi naomba unipishe kidogo, tutaongea badae"

"Lakini...." Kabla Elvine hajaendelea mama yake Elimina alikuja na kuwasalimu. Waliacha kuongea walichokuwa wanaongea na kumsalimu mama yule. Elvine aliamua kutoka nje lakini alianza kukata tamaa kuhusu Elimina na akawa na hasira sana lakini akajipa moyo.

Waliendelea kuishi pale ndani kibubububu maana kila muda Elimina alionesha kuwa bize na wala meseji hakujibu.

Siku moja muda wa jioni Elvine alikuwa na njaa maana mchana hakula kwasababu alikuwa kwenye mfungo. Alipomuona Elimina sebuleni alimuomba amsaidie kupika uji.

Elimina pasipo kujibu neno alisimama na kwenda kuandaa uji na akamletea na mikate lakini hakuwa anaongea wala kuonyesha tabasamu.

"Asante" Elvine alishukuru, Elimina alitabasamu kwa mbali sana Kisha akaketi na kuendelea na kutazama tv.

Elvine aliunywa uji ule huku akiusifia kimoyo moyo kwa namna ulivyokuwa mtamu.

"Elimina, unaonaje jumamosi tukatembee?" Elvine aliongea huku akitabasamu

"Sina muda" Elimina alijibu huku akiwa bize na tv.

Jibu lile lilimuuma sana Elvine maana hakutegemea kujibiwa vile

Elvine kwa hasira alisimama na kwenda mahali alipokaa Elimina. Alimshika mkono na kumsimamisha kwa nguvu.

Aya niambie sasa. Nimekukosea Nini? Niambie tatizo ni nini? Hivi unajua unachokifanya wewe.

"Sijui na sitaki kujua. Kwani wewe unajali nini? Hasa kuhusu mimi, nimeona uendelee na mambo yako. Na katu sitokusumbua" Elimina aliongea akiwa amelengwa na machozi.

Elvine alishangaa na akajikuta kamuachia huku alimshangaa maana baada ya sekunde chache Elimina alikua akilia.

Aligundua kuwa kumbe Elimina anamachungu sana moyoni mwake. Aliacha kumfokea na kuanza kumwomba msamaha huku akitamani kujua tatizo ni nini hasa. Wakati akiwa anambembeleza alikaa pembeni ya Elimina kwenye sofa huku akisema samahani.

Ghafla mama aliingia na kushangaa kwa kile alichokiona

"Nyie watoto ni upuuzi gani mnafanya hapo?"

kupata mwendelezo wake bonyeza hapa

Sehemu ya kumi na tatu itaendelea ijumaa >>>>>. Usikose kufuatilia.

Hadithi hii imendaliwa na kuandikwa na JACQUELINE JOHN.

Mwimbaji na mtunzi wa nyimbo, mashairi, Hadithi (simulizi) na ngonjera.

 Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255789523850. Normal >>>>>+255747313148.

                            Na, 

Imehaririwa na MIGONGO ELIAS. Mhariri.

Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255767653697. Normal >>>>>+255783327456.

                        GeT tO tHe NeXt LeVeL!

Kama umejifunza kitu shiriki nasi katika comment hapo chini, ili kujifunza na kuboresha zaidi.

 

    

 

 

 

 

 

 

    

     

    

         

 

 

       

  

 

 

 

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.