Posts

Showing posts from July, 2023

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23. Ilipoishia...... Alipofika nje, alimkuta Elimina katahamaki sana tena anahasira sana.  "Umefanya nini Elvine? Elimina aliuliza kwa ukali sana tena hadi macho yalikuwa mekundu kama damu kwaajili ya kujaa hasira.... Swali; kwanini Elimina anahasira? Na Elimina huyu anasiri gani na nyumba iliyoungua moto? Kusoma sehemu ya 22 bonyeza hapa   Sasa inaendelea...... Elvine alikuwa anatetemeka  kwa hofu ya yale anayoyaona lakini alistaajabu kuona ni kama mkewe hajali sana kuhusu yeye. Alimtazama kwa makini sana mkewe akiwa anajaribu kutafakari kwanini anaonekana kuwa na hasira juu yake. Elimina akajishitukia "Hey, wewe! Nini sasa unanitazama hivyo?" "Nakutafakari sipati majibu!' "Nimefanyaje kwani?" "Hamna ila sijajua kama umenihofia mimi au hilo swali lako linamaana gani? "Elvine baba sina maana hiyo uliyoelewa wewe kabisa. Shida yangu mimi umefanya nini mpaka unataka kuhatarisha maisha Yako namna hii. Hujui namna ga

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI NA MOJA.

Image
   SIMULIZI YA KUFURAHISHA,   “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI NA MOJA.   Ilipoishia....           Wakiwa pale ghafla mlango ulifunguliwa na aliyeingia alikuwa ni Emiliano. Editrin hakutarajia kwasababu Emiliano siku hiyo hakuja na gari  k ama siku zote hivyo walijisahau. Na pia walinzi hawakumzuia Emiliano kuingia kwakuwa walikuwa wakijua kuwa Emiliano ni mkwe wa ile familia na hawakuambiwa chochote kuhusu kutoroka kwa Editrin kwa mume wake.           "Editrin mke wangu" Emiliano aliita na wakati Editrin kashangaa pale. Emiliano akimkimbilia na kumkumbatia. Huku alionesha kufurahi sana kumuona Kupata sehemu ya kumi bofya hapa         Inaendelea......        "Editrin nisamehe kwa kila kitu lakini kumbuka kuwa mimi bado ni mumeo huwezi kunitelekeza kama hivi nakuomba sana nipo chini ya miguu yako rudi nyumbani" Emiliano aliongea huku akipiga magoti na kukumbatia miguu ya    Editrin        "Weeee!!! Naomba niache tena wewe unastahili kufa kabisa. Huwezi

JIFUNZE KUJIFUNZA PART IV.

Image
JIFUNZE KUJIFUNZA PART IV. JINSI AKILI YA BINADAMU UNAVYOWEZA KUIAMURU. “The greatest revolution in our generation is the discovery that human beings by changing the inner attitudes of their minds can change the outer aspects of their lives”. Maneno haya aliwahi kusema mwanasaikolojia maarufu nchini marekani Willium James. Akimaanisha kwamba mageuzi makubwa katika kizazi chetu ni kugundua kuwa kwa kubadili mtazamo wa ndani ya akili zetu, tunaweza kubadili mitazamo yetu ya maisha ya nje. Tupo katika mfululizo wa somo letu pendwa la JIFUNZE KUJIFUNZA na hii ikiwa ni part iv , kama utakuwa unafuatilia tumejifunza mengi huko nyuma, ikiwemo consicious, sub- conscious mind na mengine kibao. Na kama hujasoma kabisa, nikushauri usome tena kwa makini itakusaidia sana asee. Na, ikiwezekana umwalike na kumshirikisha jirani yako. Kusoma part iii bonyeza hapa Sasa leo tuna kwenda kujifunza ni kwa namna gani mtu anaweza kuiamuru akili yake kufanya chochote anacho kitaka, iwe ni maneno mazu

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI.

Image
  SIMULIZI YA KUFURAHISHA,   “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA KUMI.   Ilipoishia....   Ile nyumba haikuwa mbali na barabara hivyo akafika barabarani lakini kwa yale maumivu aliyokuwa nayo hakuweza kukimbia zaidi, alidondoka katikati ya barabara, akiwa pale alisikia sauti ya mama mmoja kwambali sana ikimwambia       "Kijana wangu nini shida amka! Nini kimekukuta? Haa! Mungu wangu. Mwanasheria!! hebu tumbebe huyu tumuwahishe hospitali kwanza, maana nahisi kavamiwa na vibaka wa mji wetu huu...."           kusoma sehemu ya tisa bonyeza hapa Sasa inaendelea....       Elvine alipoteza fahamu kwa muda, alipoamka alijikuta yupo hospitali na pembeni yake alimuona mama yake Editrin. Hakuamini kwa haraka kuwa yule ni mama yake maana alihisi anaota ndoto ya mchana. Alitulia kwa muda kidogo akiwa anamtazama mama yake pasipo kuongea chochote bali ni machozi tu ndiyo yaliyokuwa yakiongea kwa kutiririka kwa uchungu.        Editrin hakujua kwanini kijana yule alikuwa akilia

SIMULIZI YA KUFURAHISHA KUHUSU "HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA TISA.

Image
SIMULIZI YA KUFURAHISHA,   “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA TISA.     Ilipoishia...   "Mawazo unayoyawaza wewe, sio Bwana anavyokuwazia wewe" Elvila alisema huku kamkazia macho Elvine Niambie basi unamaana gani, Elvine alipiga magoti na kuanza kulia. kusoma sehemu iliyopita bonyeza hapa   Sasa inaendelea....   Elvine alilia na kutia huruma sana. Elvila akamwambia kulia sio suluhisho cha kufanya ni kujitahidi tu kujitambua yeye ni nani kwa Mungu na anatakiwa kufanya nini hiyo ndi y o njia pekee ya kusamehewa. Elvine aliposikia hivyo aliahidi kuwa hatakuwa m kaid i tena na ata yaf ua ta maelekezo yote atakayopewa, ila alihitaji kumuona mama yake kwanza.      Elvila hakujibu chochote bali alipotea ghafla k ama upepo. Elvine alishituka maana hakuelewa sehemu ambayo Elvila kapotelea. Elvine alikaa kitandani kwa muda huku akiwaza cha kufanya. Ilipofika jioni alitoka nje na kuanza kufanya kazi ya kutembelea nyumba za jirani na ile hoteli huku akishuhudia watu

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.