HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

JIFUNZE KUJIFUNZA PART IV.


JIFUNZE KUJIFUNZA PART IV.

JINSI AKILI YA BINADAMU UNAVYOWEZA KUIAMURU.

“The greatest revolution in our generation is the discovery that human beings by changing the inner attitudes of their minds can change the outer aspects of their lives”. Maneno haya aliwahi kusema mwanasaikolojia maarufu nchini marekani Willium James. Akimaanisha kwamba mageuzi makubwa katika kizazi chetu ni kugundua kuwa kwa kubadili mtazamo wa ndani ya akili zetu, tunaweza kubadili mitazamo yetu ya maisha ya nje.

Tupo katika mfululizo wa somo letu pendwa la JIFUNZE KUJIFUNZA na hii ikiwa ni part iv, kama utakuwa unafuatilia tumejifunza mengi huko nyuma, ikiwemo consicious, sub- conscious mind na mengine kibao. Na kama hujasoma kabisa, nikushauri usome tena kwa makini itakusaidia sana asee. Na, ikiwezekana umwalike na kumshirikisha jirani yako.

Kusoma part iii bonyeza hapa

Sasa leo tuna kwenda kujifunza ni kwa namna gani mtu anaweza kuiamuru akili yake kufanya chochote anacho kitaka, iwe ni maneno mazuri, tabia nzuri au pengine kuondokana na tabia mbaya ambayo mtu hazitaki. Kutoka part iv utaweza kupandikiza maneno yeyote yawe mazuri au mabaya kwenye akili yako, pia utakuwa na uwezo wa kupandikiza tabia yeyote unayoitaka mwenyewe na kufanya namna yeyote ya kuzungumza na ubongo au akili yako, hivyo nikusihi ufatane nami katika safiri ya somo hili muhimu.

Katika kupandikiza maneno au tabia yeyote kwenye akili yako ni kitu rahisi sana na hapo tunakwenda kutumia hatua hizi tatu ambazo ni

i.             Andaa sifa au tabia unazotaka mwenyewe;

ii.           Andika kwenye karatasi sifa zote unazotaka

iii.          Pandikiza kwenye akili  yako.

Karibu tujifunze kwa pamoja ni kwa namna gani hatu hizi tatu unaweza kuzifaulu hatua kwa hatua na hata kupandikiza sifa, maneno au tabia ambazo mwenyewe unaitaka.

Andaa sifa au tabia unazotaka uwe nazo mwenyewe;

 Katika hatua hii ni muhimu kukaa na kufikiria kwa mapana kuhusu maisha yako kwa ujumla, hapa utaweza kutengeneza maneo, sifa au tabia nzuri ambazo wewe unazitaka uwe nazo, pia ni muhimu kufahamu wewe ni nani wa sasa na unataka kuwa nani wa baadaye na hapo ndipo unaweza kutengeneza tabia yeyote unayoitaka. Mfano unaweza kuandaa na kujisemea maneno kama;

 i.             Mimi ni mwandishi bora duniani,

ii.           Mimi ni baba bora wa familia,

iii.          Mimi ni tajiri mkubwa,

iv.          Mimi ni jasiri na ninajiamini,

v.           Mimi ni mwenye ushawishi mkubwa duniani,

vi.          Mimi ni kiongozi bora duniani, nina afya njema,

vii.        Nina mahusiano yenye furaha na upendo mwingi.

Hiii ni mifano tu ya namna unavyo weza kuandaa maneono au sifa ambazo wewe unataka, haijarishi ni maneno kiasi gani utaweka kikubwa tu ni wewe kuangalia sifa au tabia unazozitaka mwenyewe, na kitu cha kuzingatia hapo ni kwamba sifa hizo ni muhimu zikahusisha kila nyanja ya maisha yako na hapa ni pamoja na afya yako, mahusiano yako, uchumi wako, biashara, familia, elimu na sehemu nyingine muhimu za maisha yako.

Vitu viwili muhimu vya kuzingatia unapo andaa sifa aua tabia unazozitaka.

a)  Zote ziwe katika wakati uliopo.

Kama utaangalia kwa makini sifa hapo juu zote zipo katika wakati uliopo. Hata wewe unashauriwa unapoandaa vigezo au sifa unazo zitaka ni lazima uviweke katika wakati uliopo yaani iwe kama tayari umeshapata au umeshakuwa mtu unaye taka. Hii ni kwasababu wanasaikolojia wengi wanasema kuwa Subconscious mind inaishi katika wakati uliopo tu. Mfano unaweza kusema mimi ni mchezaji bora ulimwenguni, mimi ni mfanyabiashara mkubwa duniani. Ninacho maanisha ni kwamba hata kama kitu unachokitaka hujakipata bado kiweke kama vile umeshakipata tayari.

b)   Zote ziwe chanya.

Hata ukiangalia mifano yetu hapo juu utakuja gundua kuwa yote ipo katika hali ya uchanya wala siyo hasi. Usiandike maneno ambayo yapo kinyume na unavyotaka, baadhi ya wanasaikolojia wanaamini kuwa subconscious mind inaelewa na kusikia maneno chanya pekee yake na haielewi wala kusikia maneno hasi kama vile “siyo”, mfano hauhitaji kusema mimi siyo masikini. Hapo SCM  haitaelewa neno siyo hivyo itatafsiri kama mimi ni masikini. Hivyo badala yake waweza kusema mimi ni tajiri, mimi ni sumaku ya fedha na mengine kama hayo.

 

Andika kwenye karatasi sifa zote unazozitaka.

Ukishajua sifa au tabia gani unatamani uwenazo ambazo pengine kwa sasa huna,  ni muhimu kuziandika kwenye daftali hapa pia itakubidi uwe na daftali na kalamu ilikuandika kama vile wewe unavyotaka uwe. Na hii, itarahisisha wewe kukumbuka kwa wepesi sifa gani umeweka na sifa gani umesahau. Unaweza kuandika na kuya kagua mara kwa mara na hapo unawea kuongeza mengine au kupunguza kutokana na mahitaji yako.

Anza kupandikiza ndani  ya SCM.

Kutoka katika sifa ulizoziandaa na kuziandika kwenye hatua ya kwanza na ya pili sasa ni hatua muhimu ya kuamuru na kupandikiza maneno au sifa hizo. Na hii ni rahisi sana kama utatuliza akili na kusafisha akili yako(relax), waweza kutafuta sehemu tulivu ukafanya hivyo mara kwa mara na hapo pia, unaweza kusoma kwa sauti au kimya kimya. Katika hali ya kutulia sana waweza kufumba macho au ukafumbua inategemeana na wewe mwenyewe.

Inashuriwa pia utumie muda wa kabla ya kulala au asubhi baada ya kuamka kwasababu muda huo Subconscious mind inakuwa makini sana kupokea kitu kipya, ndiyo  maana haishauriwi sana kusikilia, kutazama au kufuatilia taarifa mbaya asubhi badala yake utumie muda huo kupandikiza kitu kizuri na chenye manufaa ndani yako kwani wakati huo SCM inakuwa ACTIVE sana kupokea vitu. Hivyo ni muhimu kufahamu hali kama hiyo ili kufanya  kwa uhakika bila kubahatikasha.

Yote kwa yote haijalishi ni muda gani utapitia sifa na tabia ulizoziandaa kitu kikubwa ni kutafuta utulivu wa akili(relax) na kusafisha akili  na hii unaweza kufanyaa kwa kutafuta sehemu tulivu kisha fumba macho, vuta pumzi kwa nguvu na anza kuiachia kidogo kidogo huku ukihesabu 1 hadi 5. Hakikisha upo katika hali ya utulivu kwani utulivu yaani, relaxation ni mlango wa kufungulia SCM si unajua hii inatumia sana hisia basi na wewe uwe katika hali ya utulivu na hisia.

Na ufanyavyo hivyo hakikisha unajenga taswira ya kile unachokitaka na uwe kana kwamba unakiona. Weka matarajio hayo na pitia mara kwa mara kila siku kadiri utakavyo weza, rudia tena na tena hadi scm itakapo ikubali hali hiyo na kuwa mtu ndoto zako.

Kadiri utakavyo kuwa unafanya hivyo utakuwa unaona mabadiliko kidogo kidogo hadi picha uliyo ijenga ndani inakuwa uhalisia wako. Na utashangaa kuona tabia za nyuma unaanza kuachana nazo kabisa kwani, tunasema SCM haiwezi kushikiria tabia mbili zinazokinzana kwa wakati mmoja mfano uoga na ujasiri, umasikini na utajiri, enye akili na mjinga kwa hiyo itachangua kitu kimoja ambacho huwa unakifanyia kazi mara kwa mara  na hapo ndipo itakapoishinda tabia nyingine. Hapo utakuja kuona mtu alikuwa na tabia mbaya mf ulevi na mara baada ya kuweka mikakati ya kuacha na ulevi huo utashangaa huyu mtu anabadilika kabisa na watu wataesma huyu jamaa amebadilika kweli kweli. Katika hatu zote utaona madabiliko yanatokea na mabadiliko hayo yanawezaonekana au hayaonekani lakini mwisho wake matokeo huonekana.

Kitu kikubwa tufahamu kuwa kutengeneza sifa na tabia tunazo zitaka kwaajili ya kuzipandikiza kwenye akili zetu na kuwa sehemu ya maisha yetu au kuachana na baadhi ya tabia mbaya ambazo hatuzitaki. Siyo kazi nyepesi hivyo itahitaji muda, kurudia mara kwa mara (repeatation), patience(uvumilivu), kufanyia kazi na utekelezaji wa kile tunachokitaka kiwe ndani yetu. Yaani, ninachotaka uelewe ni kwamba kama utasema wewe ni mchezaji bora duniani anza kutafuta na kufanya vitu na mbinu zitakazo kufanya kuwa bora kama kufanya mazoezi n.k. vivyo hivyo kama wewe ni tajiri anza kuchukua hatua na kufanya kazi kwa bidiii matokeo utayapenda na hakika utakubali.

Kwa leo itoshe  kusema tuonane part v usiache kufuatilia.

kupata part v bofya hapa

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

 GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvalue. Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe.                                     

 


 

 

 

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.