HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31 Ilipoishia………. Elvine alipoteza amani kuliko hata mkewe maana kila alipomtazama mkewe basi moyo wake ni kama ulikuwa unachomwa na mwiba uliojishikiza huko kwenye mishipa ya moyo. Nafsi yake ilitaabika na ndipo alipoamua kutafuta muda mzuri, baada ya chakula cha jioni, azungumze na mkewe, maana ule ukimya wa siku mbili ulikuwa adhabu kubwa sana kwake. Kusoma sehemu ya 30 bonyeza hapa Sasa inaendelea………. Elimina mamy naomba kujua kwanini hutaki kuniuliza kuhusu sababu ya haya yote? Maana najua unajua kuwa kuna mahali mimi nilikosea, sasa unapokaa kimya hivyo… kiukweli unazidi kunichanganya maana ni kama hutaki kujua, sasa unadhani mimi roho yangu itatulia kweli?. Hata kama ungekuwa wewe lazima usingepata amani, ungekuwa hata unawaza hivi nakuwaziaje, nakuonaje na ninajisikiaje ninapokuona, sasa kwanini wewe umekaa kimya, sema neno tafadhali? (Elvine alikuwa akiongea bila kumtazama mkewe usoni maana moyo wake haukuwa katika hali ya utulivu). Pamoja na ...

JIFUNZE KUJIFUNZA PART III.

JIFUNZE KUJIFUNZA PART III.

JINSI AKILI YA BINADAMU INAVYOFANYA KAZI.

kusoma part II bonyeza hapa

U hali gani ndugu msomaji! Mimi niko vyema na ninaendelea vizuri kabisa. Kama utakuwa unafuatilia somo hili  la jifunze kujifunza kwa makini  nadhani leo tupo part 3 ambapo tuliamua tufahamu kinaga ubaga kwa namna gani akili ya mwanadamu hufanya kazi ilikuweza kulowea ndani kabisa ya somo letu la jifunze kujifunza.

Na, kama utakumbuka part 2 iliyopita tulizungumza kuhusu sehemu ya kwanza ya ubongo ambayo ni, Conscious mind (CM). Na hii, tulisema kuwa ni sehemu ya ubongo ambayo tupo na uelewa nayo . ni sehemu ya ubongo ambayo  inashughulika na matendo yote ya hiali ambayo mtu  anaweza kuyazuia au kuyaruhusu yafanyike, wakati mwingine wamombo wanasema its a logical portion of our mind, na inauwezo wa kufikri kwa mantiki(logically), kuchakata na kufanya maamuzi kupitia matukio. Mfano kujifunza kupitia makosa, kuweka malengo. Kwa ujumla tunaweza kusema mambo na matukio yote ambayo unaweza kufikri na kuamua kwa utashi wako mwenyewe mf, unaweza kuamua kutembea au usitembee, kusoma au usisome, kuoga au usioge, kukimbia au usikimbie, kupiga makofi au laah, kunyosha mkono na mengine kama hayo. Sehemu ya ubongo inayohusika na mawazo, na matendo ya hiali inaitwa conscious mind (CM).

Kwa kuwa conscioius mind ipo na mapungufu kadhaa(limitations) ambayo kama vile; Inaukomo wa kumbukumbu (limited memory) na Inaweza kufanya kitu kimoja tu kwa wakati mmoja (It can do only a single task at a time). Sasa hapo ndipo sehemu ya pili ya ubongo huingilia kati kuziba mapungufu ya conscious mind. Twende pamoja tuangalie ni kwa namna gani subconscious mind inavyofanya kazi.

SUB-CONSCIOUS MIND (SCM): Hii ni, sehemu ya ubongo ambayo hatuna uelewa nayo. Wazungu wanasema is the portion of our mind that we’re unaware of. Na hii, ni toufauti na conscious mind ambayo hufanya kazi pindi bindamu akiwa macho tu, lakini hii, hufanya kazi muda wote yaani, saa 24, siku saba za wiki. Inahusika na matendo yasiyo ya hiali kama vile; mapigo ya moyo, kupumua n.k., inahusika na hisia pamoja na tabia ya mtu husika. Pasipo kusaidiwa na conscious mind, hufanya kazi muda wote na inawasiliana na kila seli kwenye mwili wa mwanadamu huku ikipokea na kutuma taarifa na maelekezo mbalimbali akilwa macho au amelala ndiyo maana, hata kama mtu amelala ukimchoma sindano ana shituka au ukimwita mara kadhaa anaitika. nd Sub conscious mind huwa inajifunza na kupokea vitu kutoka kwa conscious mind kupitia kitendo cha kujirudia rudia (repeation) ambapo ndani yake huunda seli ya kitu hicho na kisha, baadaye kitu hicho kinakuwa ni sehemu yake. Kwa mfano mtoto anapo jifunza kutembea anaanza kidogo kidogo na kwa maelekezo na usimamizi maalumu. Kisha hufanya hivyo mara kwa mara na hapo ndipo seli zake huundwa hata kuanza kutembea au kukimbia pasipo kufikiria au kujiuliza uliza tena. Kitendo hiki chaweza kuambatana na maumivu kadhaa (painstaking process)

Sifa za sub-conscious mind

1.   Haina ukomo wa kumbukumbu (has no limited memory). Sub-conscious mind haina ukomo wa kumbukumbu kama ilivyo kwa conscious mind ambapo kama kitu kikikaa ndani ya sub-consciius mind kukisahau sahau inakuwa ngumu sana. kwani, huwa inageaka na kuwa tabia. Mfano, ukianza tabia ya kuwasema watu (kusengenya)  na ukafanya mara kwa mara utashangaa itakavyokuwa tabia yako ya kusengenya watu. Kwa ufupi, hii ni memori ya mtu ambayo inahifadhi matukio yote kutoka kipindi anazaliwa hadi anakufa ambayo mtu amewahi kuyafanya. Yaani, vitu alivyowahi kusikia na vitu alivyowahi kuona. Sasa utajiuliza sijui ni GB ngapi vile? Ndiyo maana, unaweza kukutana na mtu mara ya kwanza hata mkimaliza miaka mingi ikakata hamjaaonana siku ukimwona hata kama ulikuwa ulishasahau sub-consious mind itakukumbusha na kukwambia kuwa hii sura siyo ngeni machoni kwangu. Hii ni sawa na kusema kuwa, taarifa za mtu huyo zilikuwepo kwenye kompyuta ya ubongo wako.

2.   Ni sehemu ya ubongo inayo husika na hisia za mtu. Hisia za kila namna ndani ya mtu huweza kuzalishwa ndani ya ubongo, kuendeshwa na kuhifadhiwa hapa. Hisia hizi ni kama vile, upendo, wivu, chuki, hasira, furaha, nyinginezo. Amygdala ndipo hisia  hupatikana.

3.   Hufanya shughuli nyingi kwa wakati mmoja. Kwa kimombo tunaweza kusema “it can perform multiple tasks per time”. Sehemu hii haichagui ni kwa kiwango gani kazi zipo yenyewe hujali kufanya kazi hasa zile muhimu na ambazo imezihifadhi. Hii ni sawa na kusema hufanya kazi saa 24 hata kama mtu amelala huendelea kumeng’enya chakula, kusukuma damu, huendelea kupumua, huendelea kufanya kazi tu. Yaani, ni kama kompyuta ndani ya mtu.

4.   Inahifadhi tabia, hisia na imani. Kwa manahiyo, tabia, hisia na imani ambayo mtu ameshikilia na kuweka msimamo kwayo. Hii hutokana na vitu ambavyo ameshikilia ndani yake.

Katika hili, kwa kuwa ukifanya kitu kwa kurudia rudia tena kwa hisia hupandikizwa ndani yake na mwisho wake huwa tabia yake. Pasipo kujua wengi wamejikuta na tabia ambazo hata hawajui zimetoka wapi. Uhalisia ni kwamba watu wengi wamepandikizwa maneno machafu na mabaya kutoka utotoni na vimesemwa  kwa hisia hata kuingia ndani ya sub- conscious mind na kutengeneza picha ambayo hutoka nje kama tabia. Na ndiyo maana James Thomson alisema “your reality will altermately match the sub- conscious image you have of your self” tafsiri yake ni kusema “uhalisia wako utafanana na picha uliyo nayo kwenye ufahamu wako”. Kwahiyo, picha uliyo nayo ndani ya akili yako ndiyo hujulisha uwe mtu wa namna gani. Kama umejaza maneno hasi ndani yako sub-conscious mind yako itaanza kufanya hadi kufananania picha uliyo nayo ndani yako.

Katika upande huu ni sawa na kusema kama umejaza maneno ya utajiri ndani yako, sub-conscious mind itaanza kufanya na kufanania kile kilichomo ndani yako ambacho ni utajiri. Vivyo hivyo, kama uliambiwa kuwa wewe, ni mvivu, wewe ni masikini, wewe ni jasiri, muoga na mengine kama hayo, mambo hayo yalisemwa kwako kwa kurudia rudia hadi yakatengeneza picha ambayo ipo ndani ya SCM yako. Hata maandiko matakatifu yanasema “Maana aonavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo” soma(mithali23:7) hichi kitu ndo alikuwa anakisemea sasa.

Kwa maana hiyo, kama ukiona mtu anafanya mambo na tabia mbaya huna haja ya kutafuta mchawi ni nani. Bali ni maneno ya hovyo yaliyojazwa ndani ya SCM yake. Kwa kutokulitambua hilo  wazazi wamewatukana sana watoto wao wamesema maneno ya kikatili sana, majina ya ajabu sana  utakuta mzazi anamwambia mwanaye mbwa wewe, nyau, jambazi, maneno haya yamezalisha picha ambayo imewajeruhi hata ukubwani.

Hivi ulisha wahi kujiuliza kuwa kwanini maswala ya imani, tabia na hisia ni ngumu sana kuyashinda au kuyaacha? Pengine ni ngumu sana kubadilisha hisia za mtu, au tabia za mtu, imani ya mtu ndo usiseme sasa. Hii ni kwasababu,  tabia, imani, na hisia hukaa ndani ya sub-conscious mind ambayo hatuna uelewa nayo ni tofauti na conscious mind tunayoifahamu na kuamua juu yake. Ndiyo maana ni rahisi sana mtu kumchoma mtu kisu kwaajili ya mapenzi, au kumuua mtu kwaajili ya imani yake, au utashangaa mtu anatamani sana kuacha ulevi au uchawi lakini hawezi kuacha hii ni sababu ile ya sub-conscious mind ambayo hujiongoza yenyewe. Lakini unaweza kuiendesha na kuiamuru Scm kwa vyovyote unavyotaka mwenyewe kwa kupitia maneno. Na hata kuwa vile wewe unavyotaka. Kama unatabia au maneno hasi ndani yako unaweza kuyaondosha kwa wepesi kabisa na kuweka tabia yeyote unayotaka mwenyewe.

Nadhani tumeona japo kwa uchache kuhusu CM na SCM kwa namna zilivyo na zinavyo husiana. Ya kwamba, kitu ili kiingie SCM kinaanzia kwenye CM ambapo mtu mwenyewe anaamua kujizoesha pengine hata kuzoeshwa na watu bila yeye kujua mara kwa mara na hata kuwa tabia yake ambayo ipo kwenye SCM. Kumbuka neno kurudia rudia ni muhimu sana. hapo ndiyo utakuja kuona waswahili wanasema mazoea hujenga tabia. Part 4 tutaona njia rahisi ya kupandikiza maneno au tabia yeyote unayo itaka, au kuondosha tabia yeyote usiyoitaka ndani yako na hapo utashangaa itakuwa ni rahisi sana kwako na kwa watu wanaokuzunguka kuwasaidia kujenga tabia wanazozipenda au kuachana na tabia wasizozipenda katika maisha yao. Hivyo usikose kufuatilia masomo haya mazuri na ikiwezekana mshirikishe na rafiki yako si unajua kizuri kula na mwenziyo!    

kusoma sehemu inayofuata bonyeza hapa  

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvalue. Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe.                                     

 


Popular posts from this blog

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31