MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

JIFUNZE KUJIFUNZA PART II

JIFUNZE KUJIFUNZA PART II

JINSI UBONGO WA MWANADAMU UNAVYOFANYA KAZI.

Kama hujasoma part I bonyeza hapa.

Kabla hatuja zamia mbali sana kwenye somo letu la jifunze kujifunza, ni muhimu tuelewe kwanza ni kwa namna gani ubongo wa mwanadamu unavyofanya kazi. Kwa kuwa ubongo ni sehemu muhimu sana na inahusika katika kujifunza, ni muhimu tufahamu ni kwa jinsi gani unafanya kazi. Kutokana na kamusi sanifu ya kiswahili ubongo ni ogani laini na tepetevu yenye mishipa ya fahamu iliyopo ndani ya fuvu la kichwa yenye kazi ya kudhibiti fikra, kumbukumbu, hisia na shughuli za mwili. Na hii ndiyo nyumba ya akili. Lakini akili ni uwezo wa mtu wa kujua Kitu au jambo. Akili ni kitu muhimu sana kwa binadamu hasa katika mada yetu ya jifunze kujifunza

Kama akili ya binadamu ingefananishwa na mashine ingekuwa ni mfano wa mashine tata  yaani, complex machine na huu ni mfano tu, na uhalisia ni kwamba inazidi hapo. Ubongo kwakweli unavitu vingi na vya ajabu mno! Na kama ningeambiwa kufananisha ubongo na mfumo bado isingefaa.

Na kama mtu akijua namna ubongo wa mwanadamu unavyofanya kazi, atafanikiwa sana kufikia malengo yake, kuwa mbunifu, ataweza kujifunza kwa haraka, atabadili namna anavyojioona ataweza kuondosha tabia mbaya na kujenga tabia nzuri ambazo mtu huyo anataka awenazo. Kiujumla mtu akifahamu namna mfumo wake wa akili unavyofanya kazi ataweza kufanya makubwa sana na hata kuwa mfano  wa kuigwa  katika dunia hii. Kutenda miujiza ni swala la kawaida sana, lakini siyo miujiza ya kutoa pepo hahahahahahaa!

Tafti zinaonyesha kuwa watu wote waliofanya mambo makubwana yaajabu duniani, wametumia chini ya asilimia 10% tu! Ya akili zao. Na hii, inamaanisha kwamba watu wana uwezo mkubwa sana lakini bado hawajaufahamu na wala hawautumii kabisa. Ndiyo maana charles aliwahi kusema “mind is like a ten speed bicycle; most of us have gears we never use.” Kwa tafsiri yake ni sawa na kusema akili  ni kama baiskeili yenye spidi kumi na na miongoni mwetu tuna gia lakini hatujawahi kuzitumia kabisa.

Katika hili nimepokea malalamishi kutoka kwa watu wengi sana wakidai kuwa hawana akili, wanauwezo  mdogo, wengine wakidai kuwa hawana vipaji, hawana uwezo wowote, hawana bahati na vitu vingine kama hivyo. Naomba nikwambie kuwa, jambo hili ni uongo na siyo kweli kabisa. Hakuna mtu ambaye hana akili dunia hii hayupo! Hakuna mtu ambaye hana kipaji, ambaye hana akili, hawa wote hawapo. Watu wote tunaakili na uwezo mkubwa, na wa kipekee ndani yetu, sema tu shida ni namna gani tunazitumia akili zetu. Katika hili tuseme kuwa “if you’re intelligent you’re good at using your mind in many different ways.” Yaani kama una akili unajua kutumia vyema ubongo wako katika namna tofauti tofauti. Ukiona mtu anakuzidi akili, ujue anakuzidi kuitumia tu! Akili, ukiona mtu anakipaji na uwezo mkubwa amekuzidi kutumia akili tu! Changamka asee. Kama hivyo ndivyo, ni muhimu tukafahamu namna gani akili zetu zinafanya kazi ili tuweze kujifunza kwa wepesi sana. Si unajua kujifunza kujifunza wengi hawajafundishwa eeh!

Goja turudi kwenye akili kwanza ambayo wazungu wanaiita intelligence (mind) ambapo napenda mtu mmoja amewahi kuielezea na kusema “intelligence is what you use when you don’t know what you want to do.” Yaani, akili ni kile unacho tumia pindi hujui nini unataka kufanya. Hii ni dhana pana sana, na hapa nifupishe kwa kusema kwamba, akili ya binadamu imegawanyika katika makundi makuu mawili ambayo ni, Conscious mind na Subconscious mind. Hapa ijulikane kuwa inaweza kugawanywa kwa namna tofauti tofauti, lakini hapa goja tutumie hizi mbili mana yake ndizo kuu. Na kwa leo tutaangalia kuhusu conscious mind kwanza. Hata hivyo ifahamike kuwa tuna ubongo mmoja lakini umegawanyaka katika sehemu kuu mbili katika utendaji kazi wake.

Conscious mind, hii ni sehemu ya ubongo ambayo tupo na uelewa nayo . ni sehemu ya ubongo ambayo  inashughulika na matendo yote ya hiali ambayo mtu mtu anaweza kuyazuia au kuyaruhusu yafanyike, wakati mwingine wamombo wanasema its a logical portion of our mind, na inauwezo wa kufikri kwa mantiki(logically), kuchakata na kufanya maamuzi kupitia matukio. Mfano kujifunza kupitia makosa, kuweka malengo. Kwa ujumla tunaweza kusema mambo na matukio yote ambayo unaweza kufikri na kuamua kwa utashi wako mwenyewe mfano, unaweza kuamua kutembea, kusoma kuoga, kukimbia, kupiga makofi, kunyosha mkono na mengine kama hayo. Sehemu ya ubongo inayohusika na mawazo, na matendo ya hiali inaitwa conscious mind. Sehemu hii hutusaidia kuyaweka pamoja mawazo na mipango ili kuyatekeleza kama tulivyoamua(kupanga). Lakini pia, sehemu hii ni muhimu sana katika kufanya maamuzi na kuchukua hatua.

Mapungufu(limitations) ya conscious mind

Pamoja na umuhimu wote huo, conscious mind bado haijajikamilisha kwani, bado inamapungufu kadhaa katika utendaji kazi wake ambayo ni;

1.   Inaukomo wa kumbukumbu (limited memory). Kuna namna akili zetu huwa zinasahau hata kwa vitu ambavyo tunavifahamu au tulishawahi kuviona mfano; ulishawahi kumwona mtu anatafuta shoka lipo begani? , Anatafuta funguo zipo mkononi?, Anasahau majina ya watu, au alipo weka ile buku tano? Mifano ya matukio kama haya hutokea kwasababu vilifanyika kwenye conscious mind ambayo inalimited memory.

2.   Inaweza kufanya kitu kimoja tu kwa wakati mmoja. (It can do only a single task at a time).

Ukweli katika sehemu hii ya ubongo inahusika sana na kazi moja tu kwa wakati mmoja. Yaani haiwezi kubeba kazi mbili kwa muda uleule na kama mtu akijaribu kubeba mambo mawili kwa wakati mmoja itaachana na jambo lingine na kushughulika na jambo moja tu ambalo mara nyingi  linakuwa linafurahisha au jepesi. Mfano unaweza ukawa unalima huku mtu anakupigisha stori, hapo akili itachagua kitu kimoja mara nyingi huwa chepesi na kukomaa nacho ahapo yaweza kuwa ni kupiga stori, au unaweza kuwa unasoma huku unachati, hapa lazima tu utatelekeza kimoja wapo. Na hapa ndipo usemi wa mshika mawili moja humponyoka.Wakati mwingine conscious maana yake ni kwamba huwezi kufanya chochote nje ya ufahamu wako. Mambo haya pia yamezungumzwa na mwanasaikolojia James Thomson.

Ndugu ninachotaka uelewe kwanza, namna akili yako ilivyo na jinsi inavyofanya kazi hapo ndipo utajua namna gani ucheze nayo, uifanyishe vipi mazoezi na hata kuiamuru jinsi wewe upendavyo. Harafu wakati mwingine akili yako ni kama kompyuta ujue!, Ambayo hufanya kazi kulingana na utaalamu wa mtumiaji. Kama unajua kutype tu basi kompyuta yako itakuwa na uwezo wa kutype tu, kama unauwezo wa kuangalia muvi tu basi kompyuta yako itakuwa na uwezo wa kuangalia muvi. Ndivyo ilivyo kwa akili yako inafanya mambo madogo au ya kawaida kwasababu uwezo wako wa kuitumia umeisha hapo. Lakini ukweli ni kwamba, akili yako ni kubwa sana kuliko unavyofikri inaweza kufanya mambo makubwa na yaajabu sana. Tatizo litakuja palepale hujui namna gani ya kuitumia.

Rafiki masomo haya ni mfululizo ambayo yamelenga kukufahamisha namna ya kujifunza kwa kutumia akili yako, kuifahamu akili yako na hata  kufanya makubwa pindi utakapojua uwezo ulionao na hata kuitumia akili yako. Hivyo, usikose kufuatilia.

kupata part III bonyeza hapa

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvalue. Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe.

Popular posts from this blog

PANDE ZA MAFANIKIO

MAAJABU YA AKIBA

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.