MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

JIFUNZE KUJIFUNZA (PART 1)

JIFUNZE KUJIFUNZA (PART 1)

Siku moja nikawa nimetulia natafakari  nikawaza na kuwazua kuhusu binadamu. Nikaona kuwa ni kawaida kabisa kwa binadamu yeyote kuzaliwa, kulelewa, kwenda shule au kutokwenda kabisa, kuoa/kuolewa wakati mwingine kutokuoa/kuolewa kabisa, kufanya kazi, kuzeeka na hata kufa. Lakini unaweza kufa hata kabla ya wakati wa kuzeeka kwako. Nikagundua kuwa katikati ya utoto na uzee/ kifo. Mwanadamu huyu atajikuta amefahamu vitu vingi sana. Aidha kwa kujifunza mwenyewe kwa kuona kusikia au kwa njia yeyote ile, au kwa kufundishwa na watu wengine nyumbani au kwa kwenda shule.

Kwa kifupi  tumejifunza au tumefundishwa mambo kemkemu. Ukienda shule za St. Kayumba utafundishwa habari ya 3K  yaani, kusoma, kuandika, na kuhesabu. Na, ukibahatika ukapanda magari ya njano utafundishwa kuhusu, 3Rs yaani, Reading, wRiting, and aRithmetic. Hata kwa wale hawakukanyaga kabisa umande wa asubuhi nao wamejikuta wamejifunza vitu vingi sana huko nyumbani na mtaani pia.

Kwahiyo utaona tumefundishwa vitu vingi sana lakini, utagundua kuwa kunakitu hatufundishwi kabisa  siyo st. Kayumba wala kule kwenye magari ya njano ama nyumbani kule mtaani. Na kitu hiki ni kujifunza. Kitu kufundishwa kujifunza ni ngumu sana kufundishwa hata mashule. Ndiyo maana, utakuta watoto wanakunywa madude na kukariri kwa kwenda mbele bila kujua ni namna gani  njia nzuri na rahisi ya kujifunza na kuelewa kwa haraka. Mtu mmoja alisema Learning how to learn, is the key skill and the brain is the key organ. Ingekuwa nakalimani ningesema kujifunza jinsi ya kujifunza ni ujuzi muhimu  na ubongo ni ogani yake muhimu. Huu ujuzi kwa kimombo ndiyo tunauita LEARNACY . Ukiachana na Reading, wRiting, and aRithmetic LEARNACY bado inakosekana  na haipatikani kabisa kwa watu wengi duniani.  

Kwakuwa toka enzi na enzi tumekaririshwa kuhusu 3RS, sasa hapa hapa tutajifunza kwa habari ya 5Rs zinazokosekana katika maisha ya kujifunza kwa mwanadamu yeyote yule. Na katika hili, utashangaa utakavyo jifunza namna na njia rahisi  sana za kujifunza kwa haraka na kufanya kazi kwa ubora yaani, unakuwa smarter. Na hapa tutaungana na Mwandishi Bill Lucas huku tukirejerea katika kitabu chake kimoja makini kinachoitwa Power up your mind learn faster work smarter. Mr Bill ambaye pia ameelezea  kuhusu 5Rs ambazo ni, Resourcefulness, Remembering, Resilience, reflectiveness and responsiveness. Katika hili tutajifunza kinaga ubaga mambo kedekede,  tutajifunza namna sahihi ya kutumia akili na ubongo wako katika kujifunza kitu chochote kwa haraka bila kutumia nguvu kubwa, hapo ndipo utafahamu namna nzuri ya kucheza na kuuamru ubongo wako katika kujifunza kitu chochote unachotaka.

Learnacy ni ujuzi muhimu sana ambao ningependekeza kila mtu aweze kujifunza, kwani tunaishi kwenye dunia ambayo kujifunza ni hitaji la msingi kwa kila mtu katika kupiga hatua yeyote ile ya mafanikio anayoyataka. Hata hivyo kujifunza namna nzuri ya kujifunza kwa wepesi na muda mfupi bado ni tatizo kwa walio wengi, badala yake watu wamebaki kukariri na kutumia nguvu, na akili nyingi kuliko uhalisia wa namna ambavyo mabo yanatakiwa yawe. Najua unaweza kuwa ulihangaika sana juu ya namna gani ya kujifunza na pengine ni kutokana na mifumo ya elimu uliyo fundishwa nayo au namna ulivyo lelewa na mambo mengine kibao. Sasa na wewe umefikiwa ni suala la muda tu!

Na hapa ni utangulizi tu,unao lenga kukuandaa na kukuweka tayari kupokea mambo hayo mhimu utakayo kwenda kujifunza, ambapo utabadili kabisa maisha yako ya kujifunza. Ili kupiga hatua kila utakapo hitaji kujifunza. Kuwa tayari sasa na usikose kufuatilia mfululizo wa mafundisho haya ili upate kujenga uwezo huu muhimu sana.

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluetz. Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe


Comments (2)

Loading... Logging you in...
  • Logged in as
Masaga mlekwa's avatar

Masaga mlekwa · 92 weeks ago

Ubarikiwe sana kaka elias kwa mafundisho mazuri,,🙏🙏,
Nasubir next part
1 reply · active 92 weeks ago
Amen amen stay tuned

Post a new comment

Comments by

Popular posts from this blog

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

VITU 9 MUHIMU KWA MTU YEYOTE KUJIFUNZA KWENYE MAHAFALI.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.