HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

JIFUNZE KUJIFUNZA (PART 1)

JIFUNZE KUJIFUNZA (PART 1)

Siku moja nikawa nimetulia natafakari  nikawaza na kuwazua kuhusu binadamu. Nikaona kuwa ni kawaida kabisa kwa binadamu yeyote kuzaliwa, kulelewa, kwenda shule au kutokwenda kabisa, kuoa/kuolewa wakati mwingine kutokuoa/kuolewa kabisa, kufanya kazi, kuzeeka na hata kufa. Lakini unaweza kufa hata kabla ya wakati wa kuzeeka kwako. Nikagundua kuwa katikati ya utoto na uzee/ kifo. Mwanadamu huyu atajikuta amefahamu vitu vingi sana. Aidha kwa kujifunza mwenyewe kwa kuona kusikia au kwa njia yeyote ile, au kwa kufundishwa na watu wengine nyumbani au kwa kwenda shule.

Kwa kifupi  tumejifunza au tumefundishwa mambo kemkemu. Ukienda shule za St. Kayumba utafundishwa habari ya 3K  yaani, kusoma, kuandika, na kuhesabu. Na, ukibahatika ukapanda magari ya njano utafundishwa kuhusu, 3Rs yaani, Reading, wRiting, and aRithmetic. Hata kwa wale hawakukanyaga kabisa umande wa asubuhi nao wamejikuta wamejifunza vitu vingi sana huko nyumbani na mtaani pia.

Kwahiyo utaona tumefundishwa vitu vingi sana lakini, utagundua kuwa kunakitu hatufundishwi kabisa  siyo st. Kayumba wala kule kwenye magari ya njano ama nyumbani kule mtaani. Na kitu hiki ni kujifunza. Kitu kufundishwa kujifunza ni ngumu sana kufundishwa hata mashule. Ndiyo maana, utakuta watoto wanakunywa madude na kukariri kwa kwenda mbele bila kujua ni namna gani  njia nzuri na rahisi ya kujifunza na kuelewa kwa haraka. Mtu mmoja alisema Learning how to learn, is the key skill and the brain is the key organ. Ingekuwa nakalimani ningesema kujifunza jinsi ya kujifunza ni ujuzi muhimu  na ubongo ni ogani yake muhimu. Huu ujuzi kwa kimombo ndiyo tunauita LEARNACY . Ukiachana na Reading, wRiting, and aRithmetic LEARNACY bado inakosekana  na haipatikani kabisa kwa watu wengi duniani.  

Kwakuwa toka enzi na enzi tumekaririshwa kuhusu 3RS, sasa hapa hapa tutajifunza kwa habari ya 5Rs zinazokosekana katika maisha ya kujifunza kwa mwanadamu yeyote yule. Na katika hili, utashangaa utakavyo jifunza namna na njia rahisi  sana za kujifunza kwa haraka na kufanya kazi kwa ubora yaani, unakuwa smarter. Na hapa tutaungana na Mwandishi Bill Lucas huku tukirejerea katika kitabu chake kimoja makini kinachoitwa Power up your mind learn faster work smarter. Mr Bill ambaye pia ameelezea  kuhusu 5Rs ambazo ni, Resourcefulness, Remembering, Resilience, reflectiveness and responsiveness. Katika hili tutajifunza kinaga ubaga mambo kedekede,  tutajifunza namna sahihi ya kutumia akili na ubongo wako katika kujifunza kitu chochote kwa haraka bila kutumia nguvu kubwa, hapo ndipo utafahamu namna nzuri ya kucheza na kuuamru ubongo wako katika kujifunza kitu chochote unachotaka.

Learnacy ni ujuzi muhimu sana ambao ningependekeza kila mtu aweze kujifunza, kwani tunaishi kwenye dunia ambayo kujifunza ni hitaji la msingi kwa kila mtu katika kupiga hatua yeyote ile ya mafanikio anayoyataka. Hata hivyo kujifunza namna nzuri ya kujifunza kwa wepesi na muda mfupi bado ni tatizo kwa walio wengi, badala yake watu wamebaki kukariri na kutumia nguvu, na akili nyingi kuliko uhalisia wa namna ambavyo mabo yanatakiwa yawe. Najua unaweza kuwa ulihangaika sana juu ya namna gani ya kujifunza na pengine ni kutokana na mifumo ya elimu uliyo fundishwa nayo au namna ulivyo lelewa na mambo mengine kibao. Sasa na wewe umefikiwa ni suala la muda tu!

Na hapa ni utangulizi tu,unao lenga kukuandaa na kukuweka tayari kupokea mambo hayo mhimu utakayo kwenda kujifunza, ambapo utabadili kabisa maisha yako ya kujifunza. Ili kupiga hatua kila utakapo hitaji kujifunza. Kuwa tayari sasa na usikose kufuatilia mfululizo wa mafundisho haya ili upate kujenga uwezo huu muhimu sana.

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluetz. Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe


Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.