MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

JIFUNZE KUJIFUNZA PART V

 

JIFUNZE KUJIFUNZA PART V

SIFA NA SHERIA ZA AKILI YA MWANADAMU KATIKA KUJIFUNZA.

Hallo uhali gani ndugu msomaji! Ni matumaini yangu kuwa unaendelea vyema vinginevyo Mungu akusaidie sana. Nikukaribishe tena katika mfululizo wa somo letu pendwa la JIFUNZE KUJIFUNZA na leo tupo katika (part/sehemu) ya tano. Somo hili watu wengi wamekubali kuwa ni ufunguo tosha wa akili na maisha yao kwa ujumla. Hivyo ni muhimu sana, kwako kujumuika nasi ili kujifunza pamoja nikukaribishe sana.

Kama umefuatilia somo hili tumezungumza mengi sana juu ya namna gani akili ya binadamu inavyofanya kazi, mugawanyo wa akili ya binadamu katika utendaji kazi wake, namna gani unaweza kuuamuru ubongo wako na namna nzuri ya kupandikiza tabiia au sifa yeyote kwenye ubongo wako  na mengine kibao. Kama hujasoma huko nyuma ni wazi kuwa umekosa mengi, lakini habari njema ni kwamba unaweza kufuatilia somo hili toka mwanzo kupitia linki hapa chini.

kusoma part iv bonyeza hapa

Sasa leo nahitaji tupige hatua kidogo kwa kuangalia sifa na sheria kadhaa za akili yako katika kujifunza, ili kujua namna nzuri ya kujifunza kwa wepesi chochote utakacho. Bila shaka kwa kufamu tabia, sifa na nini akili yako inapendelea utaweza kujifunza kwa haraka na wepesi zaidi. Hivyo fuatana nami tujifunze kwa pamoja  sifa hizi;

Namba moja: Akili yako inapenda taarifa.

Binadamu ameumbiwa milango mitano ya fahamu yaani, pua, ulimi, ngozi, masikio na macho. kwaajili ya kupitisha taarifa kutoka mazingira ya nje kwenda ndani. Ndani ya ubongo wa mwanadamu kuna homoni kadhaa zinazohusika na kuleta furaha ndani yake pindi anajifunza kitu kipya, dopamine na cytokinin hutoa kemikali za furaha juu ya mtu. Ukweli ukijifunza kitu kipya utafurahia kutokana na kuwepo kwa homoni hizo. Ndiyo maana, mfano boss wako, mpenzi wako, au mtu yeyote akikuahidi kukwambia kitu, unakuwa na shauku sana ya kupata kusikia na kujua ni kitu gani hicho. Hivi ulisha wahi kujiuliza kwanini walevi huwa wanaenda kulewa baa wakati wanauwezo wa kunywa na kulewa nyumbani? Ni muhimu katika kujifunza tafuta taarifa mpya  chanya, kwa kusoma vitabu, kusikiliza video, na kujifunza kutoka kwenye vyanzo vingine muhimu. Usiwekeze kupata taarifa mbaya au hasi.

Namba mbili: Akili yako inapenda miunganiko (connections).

Kwenye ubongo wa mwanadamu kuna Axons na  dendrites ambazo zimeungana pamoja ilikuwezesha na kujifunza kuweze kupita kwa wepesi kutoka neuron moja kwenda neuron nyingine. Vivyo hivyo katika kujifunza mtu anapojifunza taarifa mpya, pamoja na kuwa ubongo wake hufurahia sana lakini kipindi cha kujifunza huwa inafanya muunganiko wa taarifa mbali mbali  katika kipindi hiki utakuta mtu anaelewa kitu hadi anaanza kusema anhaa, kumbe au ndiyo maana, n.k. wakati mwingine unakuta mtu anakuelezea au kukusimulia tukio/hadithi fulani lakini utashangaa kunapicha ya mazingira fulani unakuwa umeijenga juu ya hiyo hadithi mahali ilipo tokea wahusika na mandhari. Au kama ulisha wahi kuangalia muvi utaanza kubashiri na kutabiri jinsi kipande kinachofuata itakavyo kuwa kuhusu muvi hiyo. Kitu hiki tunasema connecting the dots.

Namba tatu: Akili yako inapenda kuiga.

Ukweli ni kwamba asilimia kubwa ya kujifunza kwa mwanadamu hufanyika kutokana na kuwatazama wengine yaani, kwa kuona hapo ndipo kuiga huanzaia. Na hii utaona kuwa tumezaliwa na kukua  huku tumejifunza mambo mengi kwa kuwaiga wengine wanavyofanya mfano ulizaliwa hujui kuongea wala kufanya kazi, lakini ulijifunza kutoka kwa wazazi wako na watu wengine  kwa namna wanavyofanya na wewe ukajikuta umefahamu kuongea na kufanya mambo mengine. Hivi ulishawahi kuona darasani wanafunzi wamefananisha majibu wote? Utashangaa kuona kipanga wa darasa akijaza njia fulani darasa lote litajaza njia hiyo. Tumejifunza elimu lugha na hata maisha kwa kuwaiga wengine. Hii ndiyo imekuja kuzalisha kanuni moja inaitwa copy cut principle ambayo inadai kuwa kitu chochote mtu yeyote akikianziasha baada ya miezi sita kitaenea maeneo mbali mbali kama anavyofanya yeye. Kwa maana hii ndiyo maana watu huwa wanakuwa na mentors, coaches na wakufunzi mbali mbali kwaajili ya kujifunza kwao. Jitahidi kujifunza kutoka kwa watu na usiwaige watu!

Namba nne: Akili yako hunawili na kufanya kazi kupitia mifumo(patterns).

Kama utakumbuka habari ya conscious mind na subconscious mind na sifa kubwa na kupandikiza sifa au maneno tunafanya kwamurudio rudio repteation kitu hiki hutengeneza njia au mifumo /partterns. Ambapo baadaye hugeuka na kuwa njia yake na mtu hufanya jambo hilo kama kawaida. Kitu hiki kujenga mazoea na mwisho huwa kama tabia, mfano hivi ni nani alikwambia kuwa moto ni hatari? Au baadhi ya wanyama au wadudu ni hatari? Hii ni mifumo parterns ambao mfumo huwa hujijengea na kuufuata katika maisha ya kila siku. Ndiyo maana wanafunzi husoma na kupitia notisi zao kabla ya kuingia kwenye mtihani. Hivi kwanini mtu akizungumza lugha yako unamwelewa? Au akikuita jina lako unageuka na kuitika, hii ni kwasababu ya patterns ambazo akili yako imejifanyia kwa mara ya kwanza unajifunza yaani ilikuwa inatengeneza njia. Unaweza usielewe kitu fulani au somo au lugha fulani si kwasababu huna akili bali ni vile tu hujatengeneza njia ya hicho kitu, changamka!

Namba nne: Akili yako haifanyi kazi vizuri kwenye stress.

Lucas Bill aliandika kuwa “When your brain is under severe stress, it can only think of survival”. Waswahili husema  akili yako iikiwa katika mawazo makali, huwa inawezakufikiri kujinusuru tu.  Wataalamu wanashauri sana usifanye maamuzi yatakayo gharimu maisha yako ukiwa na stress (msongo wa mawazo) akili yako haifanyi vyema katika kipindi hiki, msongo wa mawazo na hatari zingine zikitokea au zikitarajiwa kutokea akili ya mtu huwaza namna ya kujiokoa tu na sivinginevyo, na hii hutokana na kuwepo kwa homoni kama adrenaline ambazo huajilia nguvu ya kupambana na hatari au kuikwepa hatari. Na katika kipindi hiki utashangaa kiwete kuruka kwenye kiti pale hatari inapotokea.

 

Ndugu msomaji yapo mengi sana ya kufahamu kuhusu ubongo wetu kuliko vile tunavyofahamu kuhusu injini za magari na mifumo mingine mikubwa duniani ndiyo maana Bill alisema “When it comes to our mind, most of us know less about it than we do about the engine of our car.”  Yaani lipokuja suala la akili watu wengi tunafahamu kidogo kuhusu akili kuliko tunavyofahamu kuhusu injini za magari mbalimbali.Kwa maana hiyo tuendelee kufuatilia na kujifunza kwa manani juu ya hili. Ukiyafahamu haya utaweza kutumia vyema akili yako katika kujifunza na kufanya jambo chanya kwako na kwa wepesi sana si unajua hakuna mtu ambaye hana akila kama wengine wanavyo jiitaga kwamba hawana akili.

kusoma mwendelezo wake bonyeza hapa 

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluetz. Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Instagram>>migongo_elias. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe. 

 

Comments (2)

Loading... Logging you in...
  • Logged in as
Ubarikiwe saana mwl wangu unaedeal na kufingua fikra za watu nikiwemo Mimi lengo kuu ikiwa ni kuongeza ufahamu na kutatua changamoto zinazotukumba wanadamu. Mungu azidi kukutumia
1 reply · active 90 weeks ago
Amen amen nashukuru Sana rafiki

Post a new comment

Comments by

Popular posts from this blog

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

VITU 9 MUHIMU KWA MTU YEYOTE KUJIFUNZA KWENYE MAHAFALI.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.