MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

JIFUNZE KUJIFUNZA PART VI

 


JIFUNZE KUJIFUNZA PART VI

NGUVU YA ZAWADI KATIKA KUJIFUNZA.

Ndugu msomaji wasalaamu! Nikukaribishe tena katika mwendelezo wa somo letu pendwa la jifunze kujifunza, ambapo tumeona na kujifunza mengi sehemu zilizopita. Hadi sasa tupo katika sehemu ya sita. Lengo kubwa likiwa ni kufahamu  akili zetu, zinafanyaje kazi,  namna gani tunaweza kuzitumia, huku tukigundua kuwa Kujifunza kujifunza ni eneo muhimu sana ambalo limesahaulika sana katika jamiii zetu. Vitu kama hivi mara nyingi haviwekwi kabisa kwenye mitaala ya elemu, siyo afrika wala kule kwa mabeberu. Hivyo  kwasababu ya umuhimu wake ADD VALUE NETWORK imeamua kuzamia ili kukutafunia na kukuletea kwako kupitia hapahapa add value network kazi yako ni kumeza na kula tu!

kusoma sehemu iliyopita bofya hapa

 Sasa twende pamoja tujifunze kwa pamoja;

Sehemu ya leo tunakwenda kuangalia nguvu ya zawadi katika kujifunza  kwakuwa tunazungumzia kuhusu zawadi, ni muhimu tukafahamu maana halisi ya zawadi. Katika hili kamusi ya kiswahili inasema kuwa, “zawadi ni kitu chochote ambacho anapewa mtu aliyeshinda jambo fulani au kwaajili ya kuonyesha urafiki, upendo, au shukurani kwake.”

Wakati mwingine Lucas Bill alisema “we only reward or value what our theories tell us are mportant”, kwamba huwa tunazawadia au kuthamini kile ambacho nadharia zetu hutuambia kuwa ni cha muhimu. Kumbe watu wakati mwingine hutoa zawadi kwaajili ya kuonyesha thamani au umuhimu wa kitu au mtu katika maisha ya mtu.

Tumeona mashirika, familia, taasisi, na sehemu zingine watu hutoa zawadi kedekede kwa wafanyakazi wake ambao hufanya vizuri zaidi katika kufanya kazi. Na lengo likiwa ni kutambua juhudi zao na mchango wao katika kampuni husika. Lakini imekuwa tofauti kabisa katika kujifunza wengi hawajui umuhimu wa kujifunza ndiyo maana hawalipi kipaumbele eneo hili.

Ujue zawadi inanguvu katika kutia hamasa eeh! Ndiyo maana maandiko matakatifu yanasema “zawadi ya mtu humpatia nafasi; humleta mbele ya watu wakuu” soma mithali 18:16, kuna namna fulani hivi mtu akikupa zawadi labda tusema ya birthay, au shelehe anakuwa kama amekukopesha vile yaani nawewe unakuwa unatafuta namna ya kumlipa zawadi yake siku akiwa na tukio. Tunasema the best gain is to lose. Yaani, njia bora ya kupata kitu ni kutoa kitu.

Goja nikutonye kidogo kuhusu mfumo wa akili yako,  mfumo wa akili yako hufanya kazi katika mifumo miwili ambayo ni limbic system  mfumo huu unahusika na  raha pamoja na starehe hapa raha na starehe zote mtu anazozipata huratibiwa na mfumo huu, mfumo huu hukomaa akiwa anazaliwa ndiyo maana watoto hupenda kulala na kubebwa. Mfumo wa pili ni  cortex system huu ni mufumo ambao unahusika na kufanya maamuzi na kuratibu shughuli zingine za mwili. Mfumo huu ni tofauti na limbic ambao hukomaa kadiri mtu anavyokua. Kama akili haitaongozwa kufanya mambo yenye tija hukimbilia kufanya mambo ya raha na furaha tu! Mfano kulala, kukaa, kuangalia tv, kuchati na mengine kama hayo.

Pia katika kujifunza ni muhimu kuwa na zawadi pindi unapojifunza na zawadi ya weza kuwa ni nzuri kama kutoa kitu upendacho au kukupa raha mfano kucheza, kutoka out, au kuchati endapo tu utajifunza kitu kipya. Je wewe huwa unajipongeza kila ukijifunza kitu kipya? Basi anza leo, waweza kusema leo sitachati au kuingia online hadi nisome kitabu fulani, au leo sitenda kutembea hadi njifunze kitu fulani na ukifanikisha waweza kuchati, kutembea au kula kama zawadi. Lakini pia, yawezakuwa kwa mfumo wa adhabu kama hutokamilisha lengo ni kutia hamasa nakuushinda limbic system ambao unahitaji kudekezwa.

Kujifunza ninaakokuzungumzia hapa siyo kule darasani tu, bali hata namna ya kufahamu au kujifunza chochote katika maisha yetu ya kila siku. Na zawadi nninayoizungumzia hapa ni hamasa. Na lengo lake ni kumotivate yaani, kuhamasisha.

Na hamasa hii imegawanyika katika aina kuu mbili ambazo ni hamasa ya ndani(intrinsic motivation) ambayo ni sawa na zawadi kutoka ndani, na hamasa ya nje (extrinsic motivation) ni sawa na  zawadi kutoka nje

Zawadi kutoka ndani ni hii huzalishwa kutoka ndani ya mtu husika mara baada ya kujifunza kitu kipya. kama tiulivyoona katika sehemu ya  nne ya somo letu. Kutokana na kuwepo kwa homoni kama dopamine n.k  zinazotoa furaha pindi mtu anapojifunza kitu kipya. Hii ni zawadi kubwa mnoo kwanza unapata kufahamu vitu vingi, pili unaongeza thamani yako, unapunguza au kuondosha msongo wa mawazo  hivyo utajikuta umepata furaha na amani ya moyo baada ya kujifunza. Hamasa hii ni msukumo kutoka ndani unaomsukuma mtu kujifunza au kufahamu kitu kutokana na umuhumu wake wa hapo baadaye.

Zawadi kutoka nje hii huchochewa na vishawishi kutoka nje ya mtu utakuta vitu kama pesa, chakula, mavazi, mali, na vitu vingine kama hivyo. Na hiii hutumiwa sana na taasisi mbali mbali kwaajil ya kuhamasisha wafanyakazi wake ilikufanya zaidi ya pale. Hata wapendanao huitumia sana hii zawadi au hamasa hii huwa ni nzuri na huwafanya watu kufanya kazi kwa bidii huku wakitegemea kupewa chochote kitu. Lakini changamoto yake ni moja hasa pale unapofanya kitu kwa hamasa toka nje, pindi utakapokosa au kuondokewa na hamasa hutokuwa na hamasa ya kuendelea au kusonga mbele na katika hili ni seme kuwa usianze kufanya au kuanzisha kitu kwa msukumo wa nje bali, tumia msukumo na hamasa ya ndani kitu hicho kitadumu.  Yaani, usianzishe biashara kwasababu rafiki yako anafanya biashara, usiaanzishe kitu et kwasababu  jirani yako anafanya bali fanya kwakuwa unamsukumo na hicho kitu kisha jifunze kwa watu waliofanikiwa katika eneo hilo.

Kanuni ya hamasa katika kujifunza 

Watu wengi wamefundishwa vitu vingi hata huko shuleni lakini wakati mwengine vitu hivyo havitumiki kabisa katika maisha yao pengine hii ni kutokana kutokufahamu kanuni ya hamasa katika kujifunza kujifunza, na kanuni  hii  Andrea Spurling and Jim Smith walipendekeza namna nzuri ya kuangalia hamasa na kuitumia katika kujifunza, hebu tuangalie kwa pamoja kanuni hii;

R + V + P + I = M 

Motivation halisi yaani, hamasa katika kujifunza  inabeba vitu vinne ambavyo ni,

 R = Readiness. Hiki  ni kiwango cha utayari wa kujifunza. Ifahamike kuwa unapijifunza kitu hakili yako ni muhimu iwe tayari katika kujifunza, mazingira pia yawe tayari n.k  hata unapofanya kitu, ni muhimu kuwa na utayari kwani hii itakuongezea hamasa na uthubutu wa kusonga mbele. Je unataka kusoma vitabu? Kuwatayari. Unataka kufanya biashara? Kuwa tayari, unataka kujifunza kingereza? Kuwa tayari. Unataka kujifunza kompyuta? Kuwa tayari nasema kuwa tayari.

V = Value : hii in thamani na faida ya kujifunza. Wakati mwingine na mara zote tunajifunza ili kuongeza  maarifa yatakayo onngeza thamani katika maisha yetu. Si unajua watu muhimu katika jamii zetu ni wale wanatoa thamani eeh. Wakati mwingine kabla hujaamua kujifunza kitu au kufanya kitu ni muhimu kuangalia ni thamani  gani utaipata kwa kufanya kitu hicho , si unajua hata kuwasaidia watu kunafaida eeh.

P = probability of learning being successful. Hii ni uwezekano wa kufanikiwa na kufikia unachokitaka. Hapa ni sawa na kusema uwezekano wa  kitu unachojifunza kuhusiana na jamii au mazingira upo au laah. Njia za kujifunza zinahusiana na ninachojifunza au ninachokitaka?

I = Impact of the learning on your life. Hapa tunasema kitu unachojifunza unaweza kukitumia itumia  ilikilete matokeo tarajiwa kwako na kwa jamii? Hapa swali hili litaamua tujifunze nini na tuache nini kitakacho tunufaisha sisi na jamiii zetu wala siyo kila kitu kusoma soma tu.

M =  is the amount of motivation you have toward a particular learning opportunity. Kiwango cha hamasa unachokipata juu ya fursa ya kujifunza.  Na hii inabebwa na vitu vinne tajwa hapo juu.

Hivyo kama utaweka utayari kujifunza, na kama kitu unachojifunza kipo na thamani kwako na kwa ulimwengu kwa ujumla, na kama utakuwa na uwezo wa kukifanya na kukifikia kitu unchokifanya au kujifunza,  na kama  kujifunza kwako kutakuwa na matokeo chanya kwako na kwa jamii nzima nadhani utakuwa umehamasika kwa upande chanya. Tena , msukumo kutoka ndani intrinsic motivation hii itakupa nguvu ya kuthubutu na kuanza kufanya, na hapo ndipo utatumia hamasa ya nje kujiongezea thamani na kusonga mbele hali hii itakupeleka mbali sana na hutakuwa mtu wa kawaida. Na hapo ndipo utakuwa umetumia zawadi kubwa katika kujifunza.

Kupata mwendelezo wake bofya hapa

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluetz. Karibu sana ujiongezee thamani yako.

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe.

Instagram>>migongo_elias.

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe.

 

Comments (4)

Loading... Logging you in...
  • Logged in as
Ubarikiwe sana kwa SoMo zuri mwl.
1 reply · active 88 weeks ago
Amen amen Sana Ndugu
Jofrey Joram Andeshi's avatar

Jofrey Joram Andeshi · 88 weeks ago

Nakusalimu. mkuu, umenigusa tena, barikiwa sana.. amen.
1 reply · active 88 weeks ago
Barikiwa Sana rafiki tuendelee kujifunza

Post a new comment

Comments by

Popular posts from this blog

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

VITU 9 MUHIMU KWA MTU YEYOTE KUJIFUNZA KWENYE MAHAFALI.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.