HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

JIFUNZE KUJIFUNZA PART VII.

 

                                                    JIFUNZE KUJIFUNZA PART VII.

VIKWAZO KATIKA KUJIFUNZA .

Rafiki wasalaamu! Karibu katika mwendelezo wa somo letu pendwa  la ajifunze kujifunza ambapo, tunazidi kuchanja mbuga na sehemu ya saba sasa, huku tukiwa tumejifunza mambo kedekede hapo nyuma. Na kama hujafuatilia nikusihi ufanye hivyo ili upate kujifunza mengi zaidi hapa hapa ADD VALUE NETWORK.

kusoma part vi bonyeza hapa

Leo  tunayo sehemu yetu nzuri ya saba ambapo tunakwenda kutazama kinaga ubaga  vikwazo na changamoto katika kujifunza. Kwani, watu wengi wanaofahamu na wasiofahamu kuwa wanapaswa kujifunza kila leo na pengine wanafahamu kabisa ni kipi wajifunze na wapi wajifunzie lakini bado wengi wao imekuwa ni changamoto kwao kujifunza vitu ambavyo wanatamani kuvifahamu lakini  kwakujua au kutokujua wanakutana na changamoto kibao ambazo huwafanya wasianze kabisa au pengine wasisonge mbele mara baada ya kuanzisha zoezi la kujifunza kwao. Kitu hiki kimekuwa kama adui wa kujifunza na kusonga mbele kwa watu wengi katika mambo yao ambayo hutamani kuyafanya au kusonga mbele kwayo.

Kwasababu huwezi kupigana na adui yako ikiwa humfahamu au hujui ni njia gani au uwezo gani yupo nao katika pambano hilo. Si unajua kumfahamu vizuri adui yako tayari ni ushindi kwa asilimia 50% wa vita yako! Kwa kugundua hilo Addvaluenetwork imeamua kuzamia kindaki ndaki ili kubaini vikwazo hivyo na kuviweka wazi iliuvifahamu na kisha uchukue hatua, na hapo ndipo utakapo kuwa mshindi wa vikwazo vyako na utakuwa umetoboa  katika kujifunza kwako. Vikwazo hivyo ni pamoja na ;

..............................................................

Umri umeenda sana kujifunza; hii utakutana nayo sana hasa kwa watu wenye umri wa makamo au wazee wakidai kuwa wao hawana haja ya kujifunza kwani umri wao umeenda sana hakuna haja ya kujifunza. Hiki tunaweza kukiita ni kikwazo hasa katika eneo la kujifunza.  Ukweli ni kwamba kadiri mtu anavyokua ndivyo cell zake hufa na kuzoofu, lakini  ubongo hufanya kazi kwa connnections na patterns kama tulivyoona siku ile, kwahiyo kadiri unavyo jifunza vitu vipya na kuufanyisha mazoezi akili yako hunawili na kuwa imara zaidi. Ndiyo maana maarifa pekee yanaweza kukufanya kuwa kijana hata kama unamiaka 80, au mzee hata kama unamiaka  20. Au haukusikia wahenga waliposema kuwa elimu haina mwisho? Na kwa maisha na akili ya mwanadamu ilivyo ni kwamba upende usipende utajifunza tu. Sasa kama ni hivyo kwanini usijifunze kujifunza kwa hiali yako mwenyewe pengine ukawa mzee mwenye busara zake??

..............................................................

Kukosa muda wa kujifunza;  muda imekuwa ni kisingizio kwa watu wengi, na wengi wakisema hawana muda wa kujifunza, kuanzisha au kufanya vitu vyao vya msingi walivyopanga kufanya. Na wakati mwingine utashangaa kuona mtu analalamika muda wa kufanya mambo yake ya msingi haupo, lakini utaona ana muda wa kutosha kupiga soga kijiweni, kushinda mtandaoni kutafuta umbea. Hapa ni muhimu kuelewa kuwa muda hautoshi  kufanya kila kitu lakini unatosha kufanya vitu vya muhimu.  Hivyo jitahidi kuweka vipaumbele vya nini ufanye na kipi usifanye, kipi uanze nacho na kipi kifuate. Tambua muda haujawahi kutosha.

..............................................................

Maneno hasi kutoka kwa watu; utake usitake kama ukitaka kuanzisha kitu, kufanya au kujifunza kitu chochote utakutana na maneno hasi kama vile, utaweza kweli, wengi wameshindwa , hautafika mbali, achana na hicho kitu na maneno mengine hasi kama hayo ambayo kwa uhalisia yatakukatisha tamaa au kukuvunjua moyo ili tu usisonge mbele na mpango wako hasa katika kujifunza au kufanya kitu chochote chenye tija kwa maisha yako. Bila kujua maneno mengine yatakuja kama ushauri tena kutoka kwa watu, wakati mwingine watu wako wa karibu kabisa, pengine unaweza kuwa na mpango wa kujifunza lugha za kigeni au mpango wa kuanzisha biashara, kampuni n.k  tambua kuwa utakutana na maneno lukuki ya kukurudisha nyuma, nikwambie tu usiwape sikio lako.  Hata katika maneno na ushauri tambua kuwa maneno na ushauri mara nyingi hutolewa bure lakini, kuwa makini kuchagua unaofaa tu.

..............................................................

Ukosefu wa rasilimali; kwa kweli katika sehemu yeyote ile hakukosi kuwa na changamoto. Ilwe ni shambani, shuleni, katika biashara, safari na sehemu zingine, changamoto hazikosi kabisa. Hata katika suala letu la kujifunza utakutana na uhaba wa vifaa na rasilimali za kujifunzia ambapo yaweza kuwa vitabu, fedha, muda, wakufunzi, sehemu, n.k. mfano pengine mtu anataka kujenga tabia ya kusoma vitabu utashangaa analalamika kua hana vitabu vya kusoma. Ukweli  ni kwamba pamoja na kuwepo kwa changamoto kama hizo loakini  katika karne hii mambo yamerahisishwa sana kwani vitabu na rasilimali zingine zinapatika kwa urahisi sana pengine mtandaoni  kwa bei ndogo sana tena wakati mwingine  bure kabisa  kwa hiyo ushindwe mwenyewe tu, tena kunakozi na masomo ambayo gharama zake zipo chini sana  na utakapo jifunza na kufuatilia mwanzo mwisha huta baki kama ulvyo.  Tatizo ni kwamba watu tuko bize mitandaoni lakini hakuna tunachopata zaidi ya habari nyepesi nyepesi. Unaweza ukawa unailalamikia mitandao ya kijamii kuwa imeharibu na kupoteza muda wako mwingi kumbe wewe ndo changamoto hujui usome nini na uache nini unapakia kila kitu  goja hili nalo ni somo la wakati mwingine lakini muhimu kuliko ni kubadilika

Yaani, anza na kile upo nacha kwa wakati huo tena hapohapo ulipo utashangaa mengine utakavyokuwa unayapata mbele ya safari, huna haja ya kulalamika huna mtaji anza na kidogo ulicho nacho, hunahaja ya kulalamika kwamba huna vitabu wakati upo kwenye magurupu 30 ya wasap. Anza na kile upo nacho....

..............................................................

Ujuaji wa kujiona kama unajua kila kitu; Kuna namna hii imekuwa kama kikwazo katika kusonga mbele, kwani kuna wakati mtu anatakiwa kujifunza na pengine kutengeneza sabuni, kulima, kompyuta, udereva na vitu vingine ambavyo ni muhimu sana kwake lakini utashangaa, kuona akijitapa na kudai kuwa yeye anajua kila kitu, hivyo hana haja ya kujifunza wala kujiimarisha mwenyewe katika maisha yake sasa kitu kama hicho haki siyo kizuri, wakati mwingine utakuta eti kwasababu mtu anadigrii fulani, ataanza kubweteka na kushindwa kujifunza vitu vingine ambavyo ni muhimu kwake katika kusonga mbele , na hapo atajiona kama anajua kila kitu na hana haja ya kujifunza vitu vingine. Kitu hiki siyo kizuri kwani unatakiwa, kujifunza kila siku si una jua ubongo wako unapenda taarifa eeh! Kama ni hivyo huna haja ya kuridhika na kitu kimoja tu ulichosoma badala yake endelea kujinoa na kujiimarisha kila iitwapo leo.

..............................................................

Mazingira hayaruhusu kujifunza; kuna nyakati utapita na utashangaa kuona kuwa mazingira hayaruhusu, kujifunza, hayaruhusu kuanzisha biashara, hayaruhusu kufanya kitu ulichojipangia kufanya, nimekuwa nikipokea changamoto hii kutoka kwa watu wengi sana wakisema kuwa siku hizi hawasom vitabu mazingira ya nyumbani hayaruhusu, mazingira  hayaruhusu kufungua biashara,  na vitu vingine  kama hivyo.  Kwa  kweli nyakati kama hizi zipo si unajua siyo kila siku ni jumapil eeh! Lakini tambua kuwa hakuna siku hata moja mambo yatakuja yakamilike yote sawa kabisa kwa asilimia 100 kama unavyotaka ili uanze,. Pengine utasubiri sana kitu kama hicho na wala kisitokee. Lakini pamoja na mazingira kugoma na kutokuwa kama unavyotaka ndiyo uanze kitu kikubwa hapo ni kuanza na kile ulicho nacho mengine yatakukuta mbele kwa mbele. Lakini  wakati mwingine ukiona mambo yamegoma kabisa waweza kubadili mazingira na kuendelea na kazi lakini isiwe kiivyo. Pambana hadi kieleweke inawezekana.

Kwaleo itakuwa vyema kama tukisema itoshe lakini tutaendelea kujifunza mengi  na mazuri ya kujenga. Na vikwazo hivyo katika kujifunza au kufanya mipango yetu vipo vingi sana na hivi ni kwa uchache tu zichukue ikawe ni changamoto kwako katika kujifunza na kuzifanyia kazi. Na kama zipo nyingine usiache kushiriki nasi kupitia comments hapo chini au tutumie ujume kupitia namba hapo chini, uwe na wakati mwema asee.

 Kupata meendelezo wake bofya hapa

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluetz. Karibu sana ujiongezee thamani yako.

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe.

Instagram>>migongo_elias.

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe.

 

 

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.