HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

SIMULIZI YA KUFURAHISHA KUHUSU "HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA TISA.

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”.

SEHEMU YA TISA.  

Ilipoishia...

 "Mawazo unayoyawaza wewe, sio Bwana anavyokuwazia wewe" Elvila alisema huku kamkazia macho Elvine

Niambie basi unamaana gani, Elvine alipiga magoti na kuanza kulia.

kusoma sehemu iliyopita bonyeza hapa

 Sasa inaendelea....

 Elvine alilia na kutia huruma sana. Elvila akamwambia kulia sio suluhisho cha kufanya ni kujitahidi tu kujitambua yeye ni nani kwa Mungu na anatakiwa kufanya nini hiyo ndiyo njia pekee ya kusamehewa. Elvine aliposikia hivyo aliahidi kuwa hatakuwa mkaidi tena na atayafuata maelekezo yote atakayopewa, ila alihitaji kumuona mama yake kwanza.

     Elvila hakujibu chochote bali alipotea ghafla kama upepo. Elvine alishituka maana hakuelewa sehemu ambayo Elvila kapotelea. Elvine alikaa kitandani kwa muda huku akiwaza cha kufanya. Ilipofika jioni alitoka nje na kuanza kufanya kazi ya kutembelea nyumba za jirani na ile hoteli huku akishuhudia watu habari za Yesu.

      Alipofika kwenye nyumba moja alimkuta mtoto mmoja amelala anaumwa sana. Na yule mtoto alionekana naweza hata kuongea. Mama yake baada ya kugundua kuwa Elvine ni mtumishi wa Mungu alianza kulia na akapiga magoti kwa Elvine huku akilia.

     "Wewe si mtumishi wa Mungu mchungaji? Tafadhari sana naomba msaidie mwanangu, najua nyie walokole mnaponyaga watu. Mwanangu mimi kalogwa tena na mama yangu, yaani bibi yake baada ya mimi kukataa kwenda kumfanyia matambiko mtoto wangu. Na sikutaka afanyiwe matambiko maana sijui hayo matambiko yao yanamaana gani, niliogopa wasije wakamfanya mwanangu mchawi. Sasa nilipokataa tu mama alisema atanikomesha, na tangu hapo mwanangu hajawahi amka hapo kitandani na anawiki mbili sasa."

      Maelekezo ya yule mama yalimfanya Elvine amuonee huruma sana yule mtoto.  Lakini akawaza afanye nini. Aliwaza yule mama alikuja akamshika miguu na akasema hatoruhusu Elvine atoke pale ndani kama mwanaye hajapona maana ni mtoto wake wa pekee aliyenaye na mumewe alikwisha fariki.

         "Mmmh! Huyu mama vipi tena mbona ananitisha"Elvine aliwaza moyoni.

         "Mama mimi sio mponyaji. Mponyaji ni Mungu"

          "Hapana mimi naimani unaweza kumfanya mwanangu apone, naomba sana mchungaji, mwanangu hana hatia"

       Elvine alihisi kuchanganyikiwa, akamsogelea yule mtoto na kuanza kumuombea. Aliomba masaa mawili lakini hakuna kilichotokea na mwisho akawa amechoka sana. Alitaka akimbie lakini yule mama hakutoka hata dakika moja na alikuwa kamkazia macho ili muujiza unapotokea asiwe wa mwisho kuona. Elvine alikuwa amevaa tai, lakini akaona ile tai inamkaba sana akaitoa na kuiweka kwenye begi lake dogo alilokuwa amebeba. Alihisi anaonewa sana maana aliona hana msaada.

       Baadaye akaona hawezi kabisa kuendelea. Akatoka mbio mule ndani na kuanza kukimbia. Alipofika nje ya ile nyumba alimsikia yula mama akilia sana. Ghafla alisikia sauti ikimwambia,

      "Kwanini unakimbia, imani ya yule mama inatosha sana kumponya kijana wake, tatizo lipo kwako, ongeza imani yako na umthibitishe Yesu wako"

        Elvine alisimama kama dakika tano pale nje, kisha akarudi tena ndani. Na wakati huu alikuwa kajiweka tayari kuhakikisha mtoto anapona ili shetani aaibike. Aliporudi alimkuta yule mama amemkumbatia mtoto wake. Alimsogelea na kumwambia "Bwana atafanya".

      Yale maneno yalimtia moyo sana yule mama hivyo akafuta machozi na kusogea pembeni. Elvine alimshika mtoto yule kichwani na akasema tu "walivyovituma kwako, vitawarudia, na Bwana atawanyamazisha kimya wote wanaokuwazia mabaya. Amka mtoto mzuri ukawaoneshe kuwa yupo Mungu mwenye mawazo tofauti na wanadamu"

Ghafla yule mtoto aliamka pale kitandani, tena akiwa mzima  kabisa. Hata Elvine hakuelewa vizuri kilichotokea. Yule mama alifurahi sana. Elvine alipotaka kuondoka yule mama akamwambia Elvine kuwa anataka kuokoka, Elvine alifurahi sana maana aliona kafanya jambo ambalo hajawahi kulifanya la kamvua mtu mmoja kutoka dhambini. Baadaye alipotaka kuondoka yule mama alimwambia Elvine kuwa yupo tayari kumpa chochote anachotaka lakini Elvine alikataa. Yule mtoto alikuja na kumkumbatia Elvine na akasema anaomba amuombee ili asilogwe tena. Elvine alimuombea yule mtoto na akamtabiria baraka nyingi sana yule mtoto, kisha akaondoka kurudi hotelini.

      Alipofika hoteli aliingia chumbani kwake na akashangilia sana, aliweka muziki wa nyimbo za dini na kucheza sana maana hakuamini kama Mungu kamtumia yeye kumponya mtu, alicheza na akaimba sana mule ndani: ukweli hakuwa anajua kucheza lakini alikuwa akirukaruka tu.

        Asubuhi alipoamka akajikuta amechoka sana, na kichwa kikawa kinamuuma sana. Aliamka na kijianda vizuri, baada ya kunywa chai ya pale hotelini alitoka na kuanza kumtafuta mama yake mtaani kwa kutumia picha aliyokuwa nayo kwenye simu yake. Alitafuta sana lakini hakufanikiwa.

      Taarifa zilimfika Emiliano kuwa kuna mtu mwingine anamtafuta Editrin. Alituma watu wakaja kumteka Elvine; Elvine alishangaa ghafla wakati anaendelea kuzunguka mtaani mida ya saa 1:30 usiku gari lilisimama pembeni yake na wakatoka vijana wenye nguvu wakamshika na kumuingiza kwenye gari.

        Alichukuliwa na kupelekwa sehemu ambayo hakuwa anaijua. Alipelekwa kwenye nyumba moja nzuri sana lakini mule ndani kulikuwa kunatisha sana. Kulikuwa na giza, taa zilipowashwa zilikuwa zikitoa mwanga hafifu sana. Aliogopa sana maana hakuwa anajua kama anaweza kuwa na ugomvi na mtu, alihisi labda wale watu wamemfananisha. Alifikishwa kwenye chumba fulani na kufungwa kamba akiwa kakalishwa kwenye kiti.

       Alikaa pale kwa muda mrefu hadi ilipofika saa 5 usiku ndipo Emiliano alipokuja. Elvine Alishangaa sana kumuona baba yake wa kambo pale. Emiliano alipofika kabla ya kuuliza chochote alishika mbao pana sana iliyokuwepo pale pembeni na kuanza kumpiga nayo Elvine. Elvine alilia kwa maumivu makali hakujua sababu ya kupigwa. Baada ya Emiliano kuridhika ndipo akamsogelea na kumuuliza

      "wewe ni nani? Na kwanini unamtafuta mke wangu?"

     "Mimi ni mtoto wa Editrin"

     "What?"

.    "Ndio"

     Emiliano alicheka sana na akaanza upya kumpiga mpaka alipoona Elvine kazimia ndipo aliporidhika na kuondoka.

      Elvine alirudisha fahamu siku iliyofuata baada ya kumwagiwa maji ya barafu. Alipotazama alikutana na sura ya Emiliano tena mbele yake. Akiwa amekaa kwenye kiti pia wametazamana. Alikuwa anaogopa sana.

        "Kwahiyo kumbe haukufa?" Emiliano aliuliza.

        "Sikudanganyi mheshimiwa Editrin ni mama yangu, japo tulipotezana muda sana." Elvine aliongea kwa hofu sana.

       "Najua hudanganyi. Siku zile ulipopotea nikajua ulikufa maana nakuchukia sana"

       "Unanijua Mimi toka zamani"

        Emiliano alicheka sana na akaanza kumsimulia mambo yaliyotokea wakati Elvine hajazaliwa na wakati akiwa mtoto.

......

        *Emiliano alikuwa akimpenda sana Editrin toka wakiwa shule. Baada ya kurudi kutoka marekani masomoni alikuta Editrin kaolewa. Hakuwa tayari kukubali kirahisi kumpoteza Editrin hivyo aliwatuma watu wakaenda kumteka Edwin mume wa Editrin. Alipomteka alimwambia achaguwe kati ya kumuacha Editrin au kufa. Edwin alikataa kumuacha mkewe hivyo Emiliano aliagiza Edwin akatupwe kwenye maji akiwa mzima. Walimfunga kamba na wakamfungia na jiwe kubwa mwilini. Wakati wanaenda kumtupa walichukua simu ya Edwin na walimvua saa, kisha wakaenda kumtupa baharini. Baadaye taarifa za kupotea kwa Edwin zilisambaa sana, na Editrin alimtafuta mumewe sana. Baada ya kusikia kuwa Editrin anamtafuta mumewake. Emiliano alimteka mtu mwingine na kumchoma moto na akamvalisha saa ya Edwin na kumtegeshea ile simu ya Edwin mfukoni ili polisi waweze kumpata.

      Emiliano alifanya hivyo ili kumfanya Editrin ajue kuwa mumewe amekwisha fariki, hivyo aache kumtafuta Edwin. Baada ya Editrin kumzika mtu ambaye alidhania kuwa ni Edwin, alirudi kukaa kwa baba yake Mr. Edward. Akiwa pale Emiliano alimfuata Mr. Edward na kumwambia kuwa yupo tayari kumuoa Editrin kwa gharama yoyote. Na kwakuwa baba yake alikuwa kashuka kidogo kiuchumi baada ya familia ya Esau kujiondoa ushirika kwenye kampuni yake baada ya Editrin kuolewa na mtu mwingine, Edward akaona ni jambo jema kumfanya Editrin aolewe na Emiliano, lakini Editrin hakuwa tayari kuolewa kwaajili ya mtoto wake yaani Elvine, na kwakuwa alihisi kuwa baba yake atamuozesha kwa Esau aliamua kutoroka.

       Emiliano alichukia sana baada ya kupata taarifa za kutoroka kwa Editrin lakini hakuwa na namna ya kufanya. Alimtafuta lakini hakumpata.

       Baada ya miaka kama 14, alifanikiwa kufahamu kuwa Editrin yupo Iringa,  na aliweza kujua suala hilo baada ya kumfatilia Edger kwa muda mrefu. Hivyo siku ambayo Edger alipafahamu nyumbani kwa Editrin naye pia aliweza kupafahamu. Alipofanikiwa kupajua mahali wanapoishi Editrin na mwanaye. Alipanga kumuua Elvine ili apate nafasi ya kumuoa Editrin lakini alikuja kupata taarifa kuwa Elvine kapotea kwahiyo akawatuma watumishi wake wazidi kumfatilia Editrin na pindi wakipata taarifa za muonekana kwa Elvine wahakikishe wanamuua mtoto huyo.

      Baada ya siku kadhaa kupita alikwenda Iringa. Siku aliyokwenda yeye, Eliana pia mama wa Editrin alikuwa kapata taarifa za binti kuchanganyikiwa hivyo Eliana alitangulia kufika. Wakati Emiliano anafika sehemu ambayo Editrin alikuwa kahifadhiwa alimuona mtoto Efraim akiwa kamkumbatia Editrin, akajua ndiyo Elvine kapatikana kumbe Efraim alikuwa akimuaga Editrin kama mama wa rafiki yake kipenzi Elvine alikuwa akilia kwa uchungu maana alimkumbuka sana Elvine.

         Emiliano aliiwaagiza wafanyakazi kazi wake wamuue yule mtoto. Siku iliyofuata walimvizia Efraim akiwa anatoka dukani na kumgonga na gari hivyo Efraim alipoteza maisha. Lakini baada ya Editrin kuja Dar es salaam ndipo alipogundua kuwa yule mtoto waliomuua sio sahihi.

        Na mara hii baada ya Editrin kuja tena Dar es salaam aliamua kuja kama kijana mwema sana, na haikumgharimu sana hivyo akatimiza lengo lake kirahisi sana.

       Emiliano alieleza kuwa akiwa marekani alimchumbia binti mmoja wa kizungu, lakini kwakuwa hakuwa anampenda alimuua baada tu ya yule binti kupata ujauzito wake.

        Na pia Esau alimuua maana aliona anamsumbua mkewake maana Esau pia alikuwa akimpenda Editrin. Esau alikuwa mkorofi sana lakini alikuwa muoga sana kuua.*

      .....

   Emiliano alimaliza kusimulia hadithi yake kwa kujitapa kuwa yeye ni mkatili na hana huruma japo watu hawawezi kumgundua kwakuwa anasura nzuri ya kitumishi.

     "Kwani unachotaka kwetu ni nini?"

     "Hakuna chochote, nampenda mke wangu Editrin, lakini wewe lazima nikuue kabla Editrin hajakupata maana najua atabadilisha mawazo na atakuwa tayari kuniweka hatari mimi"

      "Vipi kama baba yangu akawa ajafa"

      "Nini wewe? Baba yako nani?"

      "Natamani baba yangu angekuwa hajafa ili uje uaibike"

       "Haiwezi tokea"

       "Sawa! lakini mimi sina hatia naomba niondoke"

       "Leo hutoki hapa"

       "kwanini?"

       "Hutakiwi kuishi wewe Mr pastor, maana mama yako alikuwa anasema mtumishi wake umepotea, hahahhah!"

       "Natoka hapa leo baba mdogo"

        "Hutoki Elvine"

        "Natoka, na nikitoka nitahakikisha nakufunga wewe"

        "Hivi unajiamini nini wewe kijana"

        "Mungu hawezi kuruhusu nife wakati kazi yake sijaitimiza, hata kama iwaje hapa nitatoka tu",

       Emiliano alipata hasira sana, hivyo akawagiza watu wake wampige sana Elvine. Elvine alipigwa hadi akazimia tena, Emiliano aliwaachia maagizo watu wake kuwa wasimuue kwanza mpaka kesho atakapokuja tena, kisha akaondoka.

      Usiku Elvine alishituka na akasikia mtu akimwambia "haya ondoka sasa". Alishangaa maana alijikuta kasimama mlangoni na hana kamba, hakujua hata kafikaje pale mlangoni. Alifungua mlango akataka kutoka lakini ghafla wale majambazi wakamsikia,

      "Simama hapo, unaenda wapi? Na kwanza umejifunguaje?" Wale walinzi walishangaa kidogo naye akawa anawashangaa maana walikua na siraha za moto hivyo akaogopa kukimbia maana alijua atashambuliwa. Ghafla wakatokea watu wanne warefu sana waliovaa mavazi ya rangi nyeupe iliyong'aa sana pia walikuwa na mapanga ya moto, wakamzunguka Elvine.

    

      Wale watu waliogopa sana mmoja akapiga risasi lakini cha ajabu ni kuwa ile risasi ilibadilika na kuwa ua jeupe kwahiyo lilipofika kwa Elvine lilimpiga lakini kwakuwa ni ua hakuumia. Wale watu walikimbia kwa kupitia madirisha huku wakipiga kelele za hofu. Elvine hakuwaona wale malaika hivyo hakujua kwanini wale watu wamekimbia ma wala ile risasi hakuiona bali alisikia mlio tu, alipoona wale watu wamekimbia na yeye akaanza kukimbia.

Ile nyumba haikuwa mbali na barabara hivyo akafika barabarani lakini kwa yale maumivu aliyokuwa nayo hakuweza kukimbia zaidi, alidondoka katikati ya barabara, akiwa pale alisikia sauti ya mama mmoja kwambali sana ikimwambia

      "Kijana wangu nini shida amka! Nini kimekukuta? Haa! Mungu wangu. Mwanasheria!! hebu tumbebe huyu tumuwaishe hospitali kwanza, maana nahisi kavamiwa na vibaka wa mji wetu huu...."

       

Sehemu ya kumi itaendelea >>>>>. Usikose kufuatilia.

kupata mwendelezo wake bonyeza hapa

Hadithi hii imendaliwa na kuandikwa na JACQUELINE JOHN.

Mwimbaji na mtunzi wa nyimbo, mashairi, Hadithi (simulizi) na ngonjera.

 Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255789523850. Normal >>>>>+255747313148.

                            Na, 

Imehaririwa na MIGONGO ELIAS. Mhariri.

Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255767653697. Normal >>>>>+255783327456.

                        GeT tO tHe NeXt LeVeL!

Kama umejifunza kitu shiriki nasi katika comment hapo chini, ili kujifunza na kuboresha zaidi.

 

    

 

 

 

 

 

 


Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.