HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA NANE.

 

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”.

SEHEMU YA NANE.  

Ilipoishia.... 

Walipokumbuka hili wote walicheka. Wakati huo kumbe mama alikuwa mbele yao. Akawauliza "nyie maadui wawili mnafanya nini sasa hivi hapa nje na usiku wote huu?"

Walishituka sana na wakawa wanawaza namna ya kujitetea.. 

Sasa inaendelea..

Kama hujasoma sehemu ya saba bonyeza hapa

    "Ni kwamba tuuu!!!

"Mama usituelewe vibaya tulikuwa tunaagana tu, kwahiyo nilipomkuta Elimina hapa nikaona nimuage" Elvine alieleza.

"Na wewe Elimina ulikuwa unafanya nini nje saizi usiku?"

     "Nilikuwa na...."

     "Alisema anajisikia vibaya kidogo kwahiyo anapunga upepo"

     "We Elvine vipi mbona unamsemea kwani yeye hawezi kujieleza?"

      "Kwanza nyie mmeanza lini kuongea, nyie si mnatuigizia mmenuniana?"

      "Mama samahani, umeelewa vibaya, mimi naomba nikalale tu" Elimina alisimama kisha akaingia ndani kulala.

   Mama alitabasamu tu kisha akamtazama Elvine. Wote wakatabasamu.

   "Usijali kijana wangu nilikuwa nawatania tu, napenda muwe na amani, lakini pia kwa kipindi ulichokuwa hapa nimejikuta nakupenda sana mwanangu. Na ninakuombea sana ukafanikiwe kumpata mama yako"

   "Asante sana mama."

   Asubuhi Elvine alikuwa tayari kwa safari, hivyo Elimina alimsindikiza stendi Elvine. Wakiwa wanasubiri gari, ghafla yule baba anayefanana na Elvine alikuja na kusimamisha gari karibu yao.

     "Hey Elvine unarudi nyumbani China nini?"

"Hapana, naenda apo Dar, father!"

    "Waooh! Sio mbaya kama nitakupa lifti maana pia naelekea huko."

     Elvine alifurahi sana , kwasababu ya ile furaha, alijikuta bila hata ya  kuamuaga vizuri Elimina, alichukua begi lake dogo alilokuwa amebeba na kuingia kwenye gari. Elimina alijisikia vibaya sana. Hivyo naye akaondoka kwa hasira.

       Wakati gari inaanza kuondoka Elvine akakumbuka kuwa hajamuaga vizuri Elimina, hivyo aliomba kushuka kwenye mara moja. Alitegemea kumuona Elimina lakini hakuweza, aliaangaza tena huku na huko lakini aligundua kuwa Elimina amekwisha ondoka. Alijisikia vibaya pia lakini hakuwa na namna zaidi ya kurudi kwenye gari na safari ikaanza.

     Wakiwa kwenye gari Elvine alitamani sana kujua jina la baba yule, hivyo akawa anamsumbua kwa maswali.

    "Elvine kijana wangu, kwanini unataka kujua jina langu?"

    "Nothing, napenda tu!"

"Si nilikwambia uniite pacha au baba? *

"Ni kweli lakini ingekuwa vizuri kama ningejua pia."

     "Sawa, naitwa Edu!"

     "Ooh! Na ilikuwaje akapoteana na huyo unayemtafuta."

     "Ooh! Ni stori ndefu, ila usijali nikimpata nitakwambia"

     Waliendelea na stori mbalimbali za kuhusu maisha. Walifika Dar es salaam mchana. Elvine alisema anakwenda kumuona mama yake anayekaa maeneo ya "Mlimani city". Yule baba alimpeleka Elvine Mlimani city kisha wakaagana.

      Elvine aliposhuka alitafuta hotel na kwenda kupumzika. Aligundua amebakiwa na kiasi kidogo cha pesa. Hivyo alipokuwa pale hotel alipiga simu kwa baba yake Mr. Ezhu yang wa China na kumueleza hatua aliyofikia na kisha akamueleza shida yake. Ezhu yang alituma fedha haraka sana. Lakini alimwambia kuwa Elvila analia sana maana anajihisi mpweke sana pindi akitoka shuleni. Elvine aliuliza kwanini Elvila hajawahi kumtafuta yeye hata kwenye simu? na mara nyingi alipokuwa akimtafuta Elvila alikuwa hapokei simu yake?, lakini Ezhu yang akamwambia Elvila hataki kusikia sauti bali anahitaji kumuona Elvine kaka yake kwa macho, na anasema Kama kweli Elvine anampenda basi aende kumuona. Elvine akaahidi kuwa baada ya kumpata mama yake atakwenda China kuwasalimia.

     Siku iliyofuata Elvine alianza kutafuta nyumba ya Emiliano, lakini haikuwa rahisi sana. Alitafuta kwa muda wa siku mbili bila mafanikio.

     Siku ya tatu akiwa amesimama pembeni ya nyumba moja ya kifahari sana akiwaza namna ya kuingia aliona gari inaingia kwenye ile nyumba. Alipotazama ndani alimuona mama yake, Emiliano pamoja na Emily mdogo wake Emiliano.

    Kitendo cha kumuona mama yake, Ilikuwa kama kapigwa ganzi na akashindwa hata kusogea, aliishia kushangaa. Gari ile iliingia ndani. Elvine alijikuta analia na akaogopa hata kuingia ndani. Alibaki pale nje kwa muda huku akiwa hajui cha kufanya.

    Aliamua kuondoka ili akajipange namna ya kuingia kwenye ile nyumba na kujitambulisha. Alirejea kwenye hoteli aliyokuwa anakaa huku akiwa na uchungu sana maana alijua kabisa kuwa sio rahisi mama yake kumtambua yeye.

     Kesho yake aliamka mapema sana na akajiandaa vizuri, kisha akaelekea kwenye ile nyumba. Alipofika nje alibisha hodi kupitia kengere ya hodi pale mlangoni. Geti lilijifungua lenyewe na mbele yake alikutana na walinzi matano.

  "Tukusaidie nini kijana?"

  "Samahani mwenye nyumba yupo?"

  "Nani?"

  "Madam Editrin"

   "Unaahadi naye?"

   "Hapana ila nahitaji kumuona"

   "Ondoka haraka usijeukabeba kesi"

   "Kwanini?"

   Akiwa haelewi kinachoendelea Emiliano alitoka ndani akiwa na polisi wawili. Emiliano alipofika pale alimshangaa sana Elvine, akamuuliza "we nani?" Elvine alianza alisema anahitaji kuonana na Editrin kwakuwa anajambo la kumwambia. Emiliano aliposikia hivyo aliwaambia wale polisi wamkamate Elvine maana atakuwa anajua kitu. Elvine hakuelewa kwanini kakamatwa.

      Alipofika polisi aliuliza kosa lake. Ndipo alipoambiwa kuwa Emiliano kuchanganyikiwa baada ya mkewe kupotea usiku ulipopita.

"Kapotea? Kivipi yani? Jana si walikuwa pamoja? "

"Uliwaona wapi?"

"Pale kwao"

"We ulikwenda kufanya nini. We ni mpelelezi wa maisha ya watu?"

Elvine alikosa jibu. Yule afande akamwambia "maneno yako yatakufunga dogo, usije ukatoa maelezo kama hayo polisi, sema mimi nakuona kama mtoto wa Mungu hivi, yaani huna kosa lakini hiyo sentensi uliyoisema inautata kidogo. Ila usijali mimi nimekupenda tu, kwahiyo nakutoa hapa halafu Emiliano nitamwambia kuwa ushahidi unaonesha hauna kosa, ok?"

"Asante sana... Asante sana aisee.."

      Elvine aliachiliwa na kurudi zake hotel. Alistaajabu sana, kwanini mama yake apotee wakati kama huu.

 

*.   *    *    *    *    *   *   *   *  

MASAA 18 YALIYOPITA

 

Editrin baada ya kutoka kanisani na mumewe alikuwa kachoka sana, alikwenda chumbani kupumzika. Mumewe aliaaga anakwenda mahali. Alichelewa sana kurudi. Aliporudi alioga kisha akapanda kitandani kulala. Baada ya Emiliano kulala, Editrin aliamka maana usingizi ulipaa, alipoamka aliamua akafue nguo za mumewe jambo ambalo hajawahi kulifanya hata siku moja, maana siku zote ni wafanyakazi tu ndiyo wafuaji wa nguo, nao walikuwa wakifua kwa kutumia mashine za kufulia.

     Alizibeba zile nguo hadi sehemu ya kufulia, kabla hajaanza kuzifua alizikagua mifukoni kuona kama kuna chochote ambacho kipo kwenye mifuko. Hakuona chochote. Lakini wakati mkono wake upo kwenye mfuko wa mwisho alihisi mfuko ule umeloa na akagusa kitu mule mfukoni.

   "Mmh! Emiliano naye anawekaje vitu mfukoni hadi mfuko unalo......" Kabla hajamaliza alipigwa na mshtuko baada ya kutoa ule mkono na kugundua kuwa ni kidole cha mtu chenye damu mbichi kabisa.

    Alitupa lile koti pembeni yake, aliogopa mno, akajiziba mdomo ili asitoe sauti, alijiuliza maswali mengi mno moyoni kwa dakika chache tu. Alitoa machozi, akajuta, akashangaa, anajilaumu, akajing'ata vidole kwa uchungu mkubwa. Aliona pale ndani sio sehemu salama kwake. Akiwa anawaza kukimbia aligundua kuwa haitokuwa rahisi sana maana ni usiku wa saa 6:30, kwahiyo walinzi wangemzuia. Alikwenda kwenye store na kujifungia huko.

     Usiku wa saa 8 Emiliano alishituka kutoka usingizini, alishangaa baada ya kugundua kuwa Editrin hayupo. Alitoka sebuleni huku akiita, hakuna aliyejibu. Aliita sana lakini kulikuwa kimya, alipofika kwenye chumba cha kufulia nguo alishangaa kuziona nguo zake zimetupwa pale chini hivyo akagundua kuwa Editrin kaona kile kidole kwenye suti yake.

     Alishituka sana, akaondoka mpaka kwenye chumba cha mfanyakazi mmoja aliyeitwa Ekhi. Ekhi alikuwa ni mfanyakazi wa muda mrefu sana mule ndani na ndiye aliyekuwa mfuaji wa nguo zake siku zote. Ekhi alikuwa anajua siri nyingi za bosi kwahiyo alikwisha zoea kuna vitu vya ajabu sana.

      Wakati huo Emiliano anakwenda kwa Ekhi, Editrin pia aliamua kutoka kwenye kile chumba ili aende kwa Ekhi kumuuliza vizuri kuhusu alichokiona kama kimewahi jitokeza kabla. Alipotoka tu kwenye kile chumba alimuona Emiliano anaingia kwenye chumba cha Ekhi. Alinyata na kusimama mlangoni kusikiliza.

     Alisikia Emiliano akimfokea Ekhi maana alikwisha mwambia kuwa akirudi tu kutoka kazini, Ekhi anatakiwa kuchukuwa nguo na kwenda kuzifua haijalishi saa ngapi wala muda gani. Ekhi alijitetea kuwa siku hiyo alipitiwa na usingizini mapema sana, kwahiyo hakujua kama bosi karudi. Mwisho Editrin alisikia Emiliano akisema "usinilaumu mimi, haya ni makosa yako na hii ndiyo adhabu yako". Ekhi alipiga kelele lakini hazikuwa zinafika mbali kutokana na uwepo wa 'singbord'. Editrin alisikia mlio wa lisasi akiwa pale mlangoni, na ndipo alipogundua kuwa mumewe ni mkatili kama mnyama. Hakutegemea wala kuwaza hata siku moja. Alikuwa akimuamini sana Emiliano kwa namna alivyokuwa mpole na mkarimu.

      Alitoka mbio pale mlangoni na akawahi getini ambako aliwakuta walinzi wamelala. Alimshukuru sana Mungu maana ilikuwa rahisi sana kutoroka. Alifanikiwa kukimbia pale ndani na kwenda kusikojulikana.

    Emiliano alituma walinzi wamtafute kila mahali lakini hawakumpata usiku ule. Emiliano alichanganyikiwa maana aliwaza mambo mengi sana hasa juu ya hatari inayokuja baada ya Editrin kukimbia.

    Asubuhi alipiga simu kwa mama yake mkwe Eliana, lakini aliambiwa kuwa Editrin hajafika nyumbani. Alitoa taarifa polisi, hivyo polisi walikuja pale nyumbani asubuhi kuchukua maelezo. Aliwaambia polisi kuwa mkewe amepotea kwenye mazingira ya kutatanisha kwahiyo anaomba msaada wa kumtafuta.

    *   *   *   *    *    *    *    *  *   *

   Elvine baada ya kutoka polisi alifika hoteli na akaanza kumuomba Mungu kwa uchungu sana. Akiwa anaomba alisikia sauti ikimwambia kuwa mama atamuona, lakini kwanza kuna jambo anatakiwa kulifanya kwanza.

      Alijiuliza ni jambo gani hilo. Aliambiwa aondoke pale ndani na akazunguke kwenye nyumba za karibu kushudia. Hakuamini na alihisi kaanza kuwa kichaa.

   "Hivi ni sauti ya Mungu kweli? Yaani mama yangu kapotea halafu mimi nikawashuhudie watu! Naenda kuongea nini kwanza? Kwanza mimi mwenyewe ni mchanga kiroho, nimeokoka hata mwezi sijamaliza" alijiongelesha sana baadaye akasema "mimi siwezi kutofautisha sauti ya Mungu na mapepo kama huyu ni Mungu kweli, basi amshushe malaika hapa ndipo nitaamini vinginevyo siendi mahali mimi"

   Akiwa katika kusema maneno hayo ghafla alihisi kaguswa na mtu begani na mtu aliyekuwa nyuma yake. Alianza kuogopa na akaanza kujisemea kimoyo moyo "eeh, Mungu mimi nilikuwa natania tu! Nani huyu sasa!". Aliwaza sana, kwanza yupo hoteli, chumbani anakaa peke yake, hana mwenyeji, hajaagiza chochote, na mlango kafunga na funguo.

    Elvine alikuwa anaogopa hata kugeuka nyuma, japo ulikuwa ni mchana lakini yeye alihisi kama ni usiku na yupo pekeyake kwahiyo hana msaada.

    "Geuka na unitazame"

    "We... Ni... nani?

    "Usiogope, Ukigeuka utanijua"

    Kwa woga aligeuka, alishangaa kumuona Elvila wa utotoni tena akiwa bado mtoto vilevile.

    "Wewe......!!"

    "Nimekuja tena kwako, si umehitaji kuniona?"

    "Nani? Mimi? Akha!"

    "Mungu anakupenda sana Elvine"

    "Najua"

    "Kwanini sasa unakuwa mkaidi?"

     "Aaa hapana, kwani nimesema siendi sasa? Naenda mbona. naenda mimi tena sasa hivi."

    "Kaokoe maisha ya mtu kwanza, kuhusu yakwako Mungu atayasumbukia. Mama yupo sehemu salama."

"Niahidi kitu"

"Sawa, najua unachotaka kusema, baada ya kazi hii, basi utampata mama yako, lakini..."

"Lakini nini?"

"Hutokaa naye mapema hivyo"

"Kwanini?"

"Kwasababu wewe ni mkaidi na hiyo ndiyo itakuwa adhabu yako"

Kwamba, mnataka kumuua mama yangu au? Niambie vizuri, sijaelewa hapo!, Kama anakufa basi na mimi sitowasikiliza tena, kweli nawaambia na wala sitosali tena.

"Mawazo unayoyawaza wewe, sio Bwana anayokuwazia wewe" Elvila alisema huku kamkazia macho Elvine

Niambie basi unamaana gani, Elvine alipiga magoti na kuanza kulia 

Sehemu ya tisa itaendelea ijumaa >>>>>. Usikose kufuatilia.

kusoma mwendelezo wake bonyeza hapa

Hadithi hii imendaliwa na kuandikwa na JACQUELINE JOHN.

Mwimbaji na mtunzi wa nyimbo, mashairi, Hadithi (simulizi) na ngonjera.

 Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255789523850. Normal >>>>>+255747313148.

                            Na, 

Imehaririwa na MIGONGO ELIAS. Mhariri.

Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255767653697. Normal >>>>>+255783327456.

                        GeT tO tHe NeXt LeVeL!

Kama umejifunza kitu shiriki nasi katika comment hapo chini, ili kujifunza na kuboresha zaidi.

 

 

 

   

 

 

 

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.