HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31 Ilipoishia………. Elvine alipoteza amani kuliko hata mkewe maana kila alipomtazama mkewe basi moyo wake ni kama ulikuwa unachomwa na mwiba uliojishikiza huko kwenye mishipa ya moyo. Nafsi yake ilitaabika na ndipo alipoamua kutafuta muda mzuri, baada ya chakula cha jioni, azungumze na mkewe, maana ule ukimya wa siku mbili ulikuwa adhabu kubwa sana kwake. Kusoma sehemu ya 30 bonyeza hapa Sasa inaendelea………. Elimina mamy naomba kujua kwanini hutaki kuniuliza kuhusu sababu ya haya yote? Maana najua unajua kuwa kuna mahali mimi nilikosea, sasa unapokaa kimya hivyo… kiukweli unazidi kunichanganya maana ni kama hutaki kujua, sasa unadhani mimi roho yangu itatulia kweli?. Hata kama ungekuwa wewe lazima usingepata amani, ungekuwa hata unawaza hivi nakuwaziaje, nakuonaje na ninajisikiaje ninapokuona, sasa kwanini wewe umekaa kimya, sema neno tafadhali? (Elvine alikuwa akiongea bila kumtazama mkewe usoni maana moyo wake haukuwa katika hali ya utulivu). Pamoja na ...

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA SABA.

 

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”.

SEHEMU YA SABA. 

Ilipoishia.....

Kule chumbani Elimina aliamua kunywa panado na mseto(dawa za malaria) ambavyo jumla yake vilikuwa ni vidonge 47. Wakati huku sebuleni maongezi yakiwa yanaendea mama Elimina aliona aende chumbani kwa binti yake akamfariji, lakini oooh!! Hakuamini kabisa alichokiona baada ya kuingia chumbani.

Kusoma sehemu ya sita bonyeza hapa

 Sasa inaendelea 

Mama Elimina hakuamini wala hakufikria kama binti yake angeweza kufanya uamuzi kama ule. Yule mama alipiga kelele kama aliepatwa na kichaa baada ya kumkuta binti yake kalala chini huku akitokwa na povu mdomoni.

     Kelele zile ziliwashitua sana Elvine na mchungaji Moses ambao walikuwa bado katika mazungumzo sebuleni, baada ya kusikia kelele na wao wakaamua kukimbilia kelele zilikosikika ili wakajue ni nini kilichotokea. Walipofika hawakuamini kabisa. Elvine alishituka hadi akaajikuta kaishiwa nguvu, akakaa chini kwasababu ya uoga maana hakuwaza kama Elimina angekuwa anampenda yeye kiasi kile.

      Mchungaji Moses alipoona hali ile alitoka nje haraka na kwabahati nzuri walikuwa na ng'ombe wawili wa maziwa hivyo aliwahi kwenda kukamua maziwa na kuja nayo haraka mule chumbani. Wakati huo mama Elimina alikuwa akilia huku akisema. "Elvine umeniulia binti yangu".

     Elvine alianza kulia huku akitetemeka maana hakujua hata cha kufanya. Na kwa dakika chache alizokuwa pale akilia alijikuta kakumbuka namna binti Elimina alivyokuwa mwema kwake toka walipokutana China. Aliumia sana na akajuta kudanganya alijisemea tu kimoyo moyo "kwanini mimi lakini, kwanini nimefanya hivi?.

      Baba alikuja na maziwa na haraka akamnywesha binti yake ambaye tayari alikuwa kwenye hali mbaya sana. Elimina hakuwa mtoto pekee bali alikuwa na kaka zake wawili ambao walikuwa tayari wanafamilia zao kwahiyo yeye alikuwa ni mtoto pekee wa kike ambaye yupo nyumbani katika ile familia.

      Yale maziwa yalikuwa msaada mkubwa sana maana kidogo Elimina alionekana kama anayerudi kwenye hali ya kawaida. Elvine wakati akiwa pale mlangoni alipokuwa kasimama alisikia kama mtu anamnong'oneza kwa sauti ya chini sana "omba uongozwe sara ya toba na mchungaji Moses".

      Alishituka na akageuka pande zote aone ni nani aliyemwambia vile, lakini hakuona mtu. Alishangaa sana na akashindwa kusema kwani alikuwa ameogopa sana maana alijua sio rahisi kueleweka kwa namna wazazi walivyokuwa wamechanganyikiwa kuhusu binti yao.

      Baadaye Elimina alipelekwa hospitali na akapewa huduma nzuri zaidi za kimatibabu, lakini hakuweza kuamka. Walikaa wiki nzima lakini Elimina hakuamka.

      Siku moja Elvine alikwenda hospitali peke yake muda wa jioni kumuona Elimina. Alipofika alishangaa sana kuona wagonjwa wote wamelala na licha ya kuwa ulikuwa ni muda wa kuona wagonjwa, lakini hakuna hata mtu mmoja aliyekuja pale hospitali kumtazama mgonjwa wake.

       Aliingia kwenye wodi ile huku akiwa na hofu kidogo maana ule utulivu wa mule ndani ulimtisha kidogo. Alipofika kwenye kitanda cha Elimina alimkuta Elimina bado hajitambui kabisa. Ile hali ilimuumiza sana na akajikuta akilia huku akimuomba Elimina msamaha japo alijua kabisa Elimina hasikii chochote.

    Ilikwa saa 12:30 lakini hakuna hata muuguzi aliyekuja mule ndani. Ghafla Elimina aliamka na kukaa kitako vizuri pale kitandani. Elvine alishituka maana Elimina aliamka ghafla sana.

     Wakati anashangaa akaamua kumuuliza, "unaendeaje?" Elimina hakujibu bali alikuwa akimtazama tu.

  "Elimina nisamehe sana rafiki yangu, sikujua kama hili litatokea, am really sorry, nisamehe Elimina" Elvine aliongea kwa uchungu sana.

 "Kwanini unalia?" Elimina alimuuliza kwa upole sana. Ile sauti ilimshitua sana maana haikuwa sauti ya Elimina japo aliyeongea alikuwa ni Elimina. Lakini hakujali sana maana alihisi labda ni sauti ya kigonjwa.

   "Najua nimekosa kwako hata kwa Mungu"

   "Sasa kwanini hukutii?"

   "Sikutii nini?"

   "Ulikosea tangu mwanzo, kwahiyo unatakiwa kurudi kwenye njia, Elvine uliyekusudiwa ni wewe kwanini usitubu kwa Mungu wako kwanza? Hivi unajua namna Mungu anakuhitaji wewe? Hivi unajua kuwa umebeba huduma kubwa sana? Hivi unajua unakusudi la Mungu na jukumu la kutimiza ukiwa duniani? Mungu anakutaka wewe Elvine. Kaombe msamaha maana wewe ndiyo sababu ya Elimina kuto kuamka maana hukutii sauti ya Mungu ile siku"

     Elvine aliogopa sana, maana katika yote yaliyoongelewa hakuna alichoelewa zaidi aliishika sentensi ya mwisho "wewe ndiyo sababu ya Elimina kuto kuamka" maana ilithibitisha kuwa muongeaji sio Elimina.

    Alimuogopa sana Elimina na akaamua kukimbia kutoka nje. Alipofika mlangoni ndipo akakutana na watu wakiwa wamechelewa sana kuja kuwaona wagonjwa wao. Elvine hakujali walitoka mbio sana jambo ambalo liliwashangaza sana watu.

   Alifika mahali na akawa amechoka sana, ghafla alisalimiwa,

  "Hey Elvine ni wewe, unaendeaje kijana wangu?" Ile sentensi iliingia hadi ndani ya moyo hadi yeye alishangaa maana alijihisi tofauti sana.

   "Ooh! Shikamoo, ni wewe kumbe? Za toka sikuile?"

   "Marahaba Elvine. Njema tu! Vipi mbona kama unaharaka sana?

   "Hapana ni kidogo tu"

   "Anhaa! Hivi unakaa wapi kijana wangu?"

   "Nakaa hapo tu mbele hata sio mbali".

   "Ok! Nahisi unaswali kwangu, hebu uliza". Elvine alishangaa sana maana yule baba alikuwa ndiye aliyekutana naye siku ya kwanza alipofika Tanzania. Kweli alikuwa anatamani kuuliza swali japo hakujua ni nani atakaye muuliza.

   "Oh, ni kweli, umejuaje?"

   "Watu wa rohoni hutambuana rohoni, mimi nakuona kama unahuduma na nguvu kubwa sana ya Mungu, lakini ni kama wewe hujajua hilo"

    "Mmmh! Sielewi hata, mimi unahuduma gani, kwani naonekanaje?"

    "Hivi tangu ukiwa mdogo hujawahi kufanya tukio la ajabu au lakushangaza?"

   "Ajabu kivipi?"

   "Kama muujiza hivi"

   "Hapana sikumbuki"

   "Ok sijui labda kweli hujawahi, lakini mimi nahisi kama unajukumu la kufanya, haya uliza swali sasa"

   "Eti sauti ya Mungu ipoje na unaijuaje?"

   "Swali zuri sana. Mungu sikuzote huwa hashuki mwenyewe Duniani, bali hutumia watu, vitu na mazingira. Pia tunaijua sauti ya Mungu kwa uongozi wa Roho mtakatifu"

    "Na vipi kama utakutana na mtu unayejua lakini akatumia sauti ambayo sio yake? Yaweza kuwa sauti ya Mungu hiyo?"

    "Inawezekana maana sikuzote Mungu hupenda kuonesha upekee wake kutokana na namna anavyopenda yeye, vipi imekutokea hiyo hali?"

     Elvine aliitikia kwa kichwa

    "Ooh, unauhakika kuwa hiyo sauti iliyotumika ni ngeni kwako?".

    "Yes! Ok yote ni mapenzi ya Mungu."

   "Halafu samahani baba, wewe unaitwa nani?"

    "Oh! Jina langu sio muhimu, ila ningependa uniite pacha maana mimi na wewe tunafanana au niite hata baba."

    "Sawa, vipi kuhusu mtu unayemtafuta umempata?

     "Hapana bado sijampata ila najua sio muda nitampata"

"Ni nani kwani?"

"Ni rafiki wa moyo wangu anaitwa Eddy"

"Anhaa! Sawa basi Mungu akusaidie"

"Amina"

    Baada ya mazungumzo ya muda mrefu waliagana kisha Elvine akarejea nyumbani. Elvine toka tukio la Elimina kunywa vidonge alikuwa akiishi pale ndani kwa woga sana maana hakujua wale wazazi wanawaza nini juu yake.

     Alipofika nyumbani aliingia chumbani kwake na kulala. Akiwa kalala aliota ndoto. Katika ndoto alisikia akiitwa na alipoamka alimkuta mdogo wake wa China Elvila, wakati anashangaa mdogo wake kafikaje Tanzania alimuona Elvila mwingine ambaye alikutana naye akiwa mtoto lakini cha ajabu bado alikuwa mtoto vilevile.

       Yule Elvila wa utotoni mwake akamwambia. "Unaelewa maana ya hili jambo?"

   "Hapana, sasa mimi ntaelewaje hapa"

   "Maana yake ni kuwa hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu". Akiwa anashangaa mdogo wake alimuita "kakaaaa". Alishituka kutoka usingizini na ndipo alipogundua kuwa sauti aliyokuwa akiitumia Elimina ilikuwa ni ya mdogo wake Elvila wa China. Elvine alimuogopa sana Mungu.

     Alitazama saa, ilikuwa ni saa 3:12 usiku akaona hawezi tena kulala, hivyo akaamka na kutoka sebuleni, ambako alimkuta baba yake aliamini bado hajalala.

      "Baba samahani"

      "Usijali kijana wangu, nini shida?"

      "Naomba kuokoka"

      "Waoh! Kumbe hujawahi kuokoka?"

      "Ndiyo! maana huko nilikokuwa wazazi wangu walionilea hawakuwa wanafahamu chochote kuhusu Mungu."

     "Sawa, nimefurahi sana. Mchungaji Moses alimuongoza sara ya toba Elvine na kisha akamuombea, lakini alishangaa maana alikuwa akiwiwa kumwombea kuwa Mungu amtumie Elvine jinsi apendavyo".   Baada ya Elvine kuombewa alipata amani sana na hata alipokwenda kulala, aliota ndoto za kupaa tu mawinguni akiwa na malaikwa wa zamu.

     Asubuhi walipigiwa simu na wakaambiwa kuwa, Elimina aliamka toka usiku na sasa wanaweza kwenda kumchukua hospitali. Wazazi walifurahi sana lakini Elvine alizidi kumuogopa sana Mungu maana alijua kuwa Mungu anamthibitishia kuwa alihitaji yeye atubu makosa yake. Mchungaji Moses alikwenda hospitali kumchukua Elimina.

     Elimina alipofika tu nyumbani mama yake alikuwa na hasira sana kwahiyo alimpiga makofi kwa hasira sana huku akimwambia kwanini amewaaibisha kiasi kile, maana waumini walitamani kujua sana kwanini Elimina kanywa sumu lakini wazazi walidanganya tu kuwa binti yao alipokuwa akija Tanzania alipoteza baadhi ya vyeti vyake vya masomo ndiyo maana akanywa vidonge.

       Elimina alilia sana na akaanza kumchukia sana Elvine.

       Siku iliyofuata asubuhi Elvine aliamka na akawa anamsubiri Elimina aamke ili amsaidie kwenda kumtafuta mama yake. Labda watapata taarifa yoyote. Elimina alipoamka alimkuta Elvine kakaa sebuleni anamsubiri yeye. Elimina hakuongea wala kusalimia bali alipita kama hajaona mtu mpaka jikoni na kuanza kuandaa chai. Elvine aliogopa sana maana kwa muonekano tu wa Elimina ulionesha kabisa hataki mazoea. Alijikaza na kutuliza moyo.

      Muda wa chai ulipofika wote wakaja kunywa chai. Lakini mchungaji Moses na mkewe waligundua kuwa binti yao hana furaha kabisa kumuona Elvine mbele yake. Wazazi wakapeana ishara na kujifanya wameshiba kisha wakaondoka mezani.

      Elvine aliona atumie nafasi hiyo kuomba msamaha.

     "Elimina naomba unisamehe sana please!"

     "Kwalipi"?

      "Elimina najua unanichukia lakini mimi nilichukulia kawaida tu maana nilichokuwa nawaza wakati huo ni kufika Tanzania tu nimwone mama"

     "Kwahiyo unasubiri nini hapa? Si uende kwa mama yako?"

     "Elimina nahitaji msaada wako sana"

     "Mmh! Mimi tena?"

     "Tafadhari sana, naomba usinichukie hivyo, tumefundishwa kusamehe sisi kama watoto wa Mungu"

    "Nani mtoto wa Mungu? Wewe?"

    "Sisi sote"

    "Kama na wewe ni mtoto wa Mungu basi dunia imeisha"

    "Elimina please, nisaidie kumpata mama, pindi nikimpata mama sitakusumbua tena, nakuahidi!"

    "Kamtafute mwenyewe, achana na na maisha yangu kabisa. Elimina baada ya kuongea maneno hayo aliondoka na kwenda chumbani kwake akamuacha Elvine pale sebuleni akiwa amekosa amani kabisa.

    Ulipofika muda wa chakula cha mchana, Elimina hakuja kula kabisa, na ilipofika jioni Elimina alikuja lakini hakuinua kichwa kumtazama mtu. Kwa upande wa Elvine naye alionekana hana amani hivyo naye aliinama tu muda wa chakula wala hakutazama mtu. Wazazi walikwisha jua kuwa watoto hawa hawana furaha tena.

       Siku iliyofuata asubuhii mchungaji na mkewe waliamua kuwaita na kukaa nao ili wawapatanishe lakini ikawa ngumu sana. Baadaye wazazi waliamua kumwambia Elimina amsadie mwenzie kumtafuta mama yake hata kama anamchukia. Kwa kulazimishwa aliamua kukubali japo sio kwakupenda.

     Asubuhi walijiandaa mpaka mtaa ambao mchungaji Moses aliwaeleza kuwa ndiko mama yake alipohifadhiwaga baada ya kuchanganyikiwa. Lakini haikuwa rahisi maana hawakuweza kuipata iyo nyumba maana wengi walikuwa ni wahamiaji wapya katika mtaa ule hivyo walirudi pasipo mafanikio. Siku iliyofuata walikwenda tena lakini bado hawakufanikiwa wiki nzima walitafuta lakini hawakuweza kuipata nyumba hiyo. Walichunguza wiki mbili lakini hawakufanikiwa. Utafutaji wao ulifanyika kila mmoja akiwa haongei na mwenzie. Njia nzima walikuwa kimya Elimina kazi yake ilikuwa ni kuongoza njia na Elvine kazi yake ilikuwa ni kuulizia na kutoa maelezo kuhusu mama yake kwa watu. Jambo hili liliifanya kazi kuwa ngumu na kuchosha sana.

Mchungaji Moses aliamua kutangaza kanisani kama kuna mtu yeyote anayejua taarifa za Editrin basi amsadie Elvine. Baada ya ibada mama mmoja alikwenda kwa mchungaji na akaomba kuonana na Elvine. Elvine aliitwa.

Yule mama alimuuliza Elvine "hunikumbuki mimi?"

"Sina uhakika ila sura yako sio ngeni kwangu"

"Mimi ni mama Efraim"

"Anhaa!! Nimekukumbuka tayari, vipi Efraim yuko wapi?

"Yule mama hakujibu ila alitikisa kichwa tu kuonesha anasikitika"

"Mbona una...?"

"Efraim alifariki muda sana"

"Hapana, kwanini sasa? Kwanini?"

"Aligongwa na gari"

"Haiwezekani!! Haiwezekani kabisa"

Elvine taarifa zile zilimuhuzunisha sana na alishindwa kujizuia kutoa machozi, maana Efraim alikuwa ni rafiki yake pekee wa utotoni waliopendana sana.

Yule mama alimtuliza Elvine kisha akamwambia kuwa yeye ndiye aliyekuwa akikaa na mama yake baada ya mama yake kuchanganyikiwa lakini kuna mama alikuja kumchukua na kuondoka naye maana alikuwa ni mama yake Editrin yaani Bibi yake yeye Elvine.

"Bibi? Mbona mama hakuwahi niambia kuwa tuna ndugu?"

"Mwenyewe hakuwahi niambia lakini hiyo siku ndiyo nilijua. Lakini pia, nilisikia kaolewa na tajiri mmoja aitwaye Emiliano na ndoa yake ilirushwa kwenye runinga."

Mmmh! Mama yangu kaolewa kumbe! Natumai anaishi maisha ya raha huko.

Baada ya maongezi hayo. Elvine alimuuliza mchungaji Moses kama anamfahamu Emiliano. Mchungaji Moses alisema ndiyo anamfamu maana Emiliano ni tajiri anayefahamika sana. Taarifa zile zilimsaidia sana Elvine. Usiku hakulala kabisa, alianza kufuatilia mtandaoni kuhusu Emiliano na mwisho alifanikiwa kuiona ndoa iliyofungwa kati ya mama yake na Emiliano kupitia YouTube. Alilia sana baada ya kumwona mama yake.

Asubuhi muda wa chakula Elvine aliwashukuru sana familia ya mchungaji kwa msaada wao, kisha akasema kuwa siku inayofuata ataondoka na kuelekea Dar es salaam maana amepafahamu mahali ambapo ataweza kumpata mama yake.

"Unaondoka? Umepafahamuje kwa mama yako? Na mbona mimi sina taarifa?" Elimina alihoji kwa mshangao.

!" We shida yako ni nini? We si ulisema hutaki kumwona kijana wa watu hapa? Mwache aondoke kwa amani sasa, ni kweli alikosea tena sana lakini si kaomba msamaha, hata yeye alikuwa na matatizo ndiyo maana akakutumia wewe". Aliongea mchungaji Moses kwa upole tu.

"Ooh! Kumbe wote mpo upande wake haya sawa" Elimina aliondoka pale mezani na kwenda chumbani. Mama yake Elimina alikuwa akiwatazama tu wala hakusema neno. Baada ya Elimina kuondoka yule mama akaanza kucheka. Alipoulizwa anacheka nini alisema hamna kitu.

Ilipofika saa 4:30 usiku Elvine akawa anapanga nguo zake ili kesho aanze safari lakini alishangaa kuona Elimina akimtumia "safari njema". Hakuamini maana haijawahi tokea toka afike pale ndani kupokea sms ya Elimina. Alitabasamu na akajibu "Asante sana, uko wapi nataka nikuage"

"Nipo nje!" Elimina alijibu

Elvine alifurahi sana, akatoka nje na kumkuta Elimina kakaa kwenye kiti.

"Mbona upo nje usiku wote huu?"

"Nimekaa tu"

"Ooh! Sio salama kwa afya yako."

"We ni nani hata unihofie mimi"

"Samahani"

"Never mind"

"Ok, nisamehe kwa kila kitu pia nimekusamehe, halafu kuhusu ile siku sitoikumbuka tena"

Elimina alijikuta katabasamu na akakumbuka kuwa kuna siku alimtelekeza Elvine mtaani wakati wanamtafuta Editrin kwahiyo Elvine alipotea akatangatanga sana mtaani, Elimina alirudi nyumbani usiku lakini hakumkuta Elimina alipoulizwa Elvine yuko wapi alidanganya kuwa kamuacha mahali kuna kitu anafanya. Kwahiyo ikabidi arudi kumtafuta na alimkuta Elvine kakaa mahali hajui hata aende wapi.

Walipokumbuka hili wote walicheka. Wakati huo kumbe mama alikuwa mbele yao. Akawauliza "nyie maadui wawili mnafanya nini sasa hivi hapa nje na usiku wote huu?"

Walishituka sana na wakawa wanawaza namna ya kujitetea... 

Sehemu ya nane itaendelea jumatano >>>>>. Usikose kufuatilia.

Kupata mwendelezo wake bonyeza hapa

Hadithi hii imendaliwa na kuandikwa na JACQUELINE JOHN.

Mwimbaji na mtunzi wa nyimbo, mashairi, Hadithi (simulizi) na ngonjera.

 Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255789523850. Normal >>>>>+255747313148.

                            Na, 

Imehaririwa na MIGONGO ELIAS. Mhariri.

Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255767653697. Normal >>>>>+255783327456.

                        GeT tO tHe NeXt LeVeL!

Kama umejifunza kitu shiriki nasi katika comment hapo chini, ili kujifunza na kuboresha zaidi.

 

 

 

 

 

 

 

    

 

  

 

 

 

 

Popular posts from this blog

MAAJABU YA AKIBA

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.