MAAJABU YA AKIBA

MAAJABU YA AKIBA

Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa.

Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili.

Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,

 Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula.

Ni muhimu kujiwekea akiba ya kile kidogo unachokipata kwa sasa kwani kitakuwa na faida nyingi sana sasa na hapo baadaye.

Zipo aina kadhaa za akiba ambazo inampasa mtu kuwa nazo, kama ifuatavyo;

AINA YA KWANZA: AKIBA YA ROHO NA NAFSI YAKO;

Kwakuwa mafanikio na ukuaji muhimu huanzia ndani ya mtu, hivyo ni muhimu sana kwa kila mtu kuwekeza vilivyo katika nafsi na roho yake, ili akijiwekea akiba ya kutosha basi atapata matokeo yake.  Unawezakufanya hivyo kwa maombi, kusoma na kujifunza neno; kuwasaidia na kujitoa kwa wahitaji na kazi zote kwaajili ya utukufu wa Mungu.

 

Akiba muhimu pia katika eneo hili kwa watu wote ni kumwamini Yesu kuwa bwana na mwokozi wa Maisha yako. mwanadamu yafaa ujiwekee akiba kwa kumpokea Yesu na kufanya yote yampendezayo ili kujifaidia mwenyewe na kizai chako.

 

AINA YA PILI: AKIBA YA MALI AU FEDHA;

Ni muhimu kukumbuka kujiwekea sehemu ya fedha au mali unayoipata kila siku kwa ajili ya baadaye ili kupambana na changamoto mpya zitakazoibuka mfano utasikia; utasikia bei ya hiki imepanda au ada imeongezeka au kodi imeongezeka au namna yoyote ya mabadiliko hayo yanakuwa yanahitaji fedha zaidi.

 

Ajabu ni kwamba utakuta pamoja na hayo kutokea lakini uchumi wako hauongezeki na wakati fulani ni kama unashuka usipo kuwa makini unaweza kujikuta umekuwa mtu wa kuomba misaada kila wakati sababu haukufikiria kuhusu kesho.

 

Hebu tazama viumbe hawa wa ajabu chungu ni watu wasio na nguvu lakini hujiwekea chakula wakati wa hari (mithali 30:25) ni muhimu sana kutambua majira na nyakati za Maisha.

 

Chungu analijua hilo ndio maana hujiwekea akiba, mara nyingi tunapata sana fedha au mali kwa wingi hadi unaweza kujiulliza ulikuwa wapi siku zote huko nyuma kufanikiwa?  Huu ni wakati wako wa kufurahia na kuwa makini sana.

 

Kuna kanuni moja inaitwa ``bread and seed``   hujaribu kutueleza wakati unafikiri umepewa chakula pekee toka kwa Mungu yeye huona amekupa chakula na mbegu hivyo hautakiwi kula mbegu kwani utashindwa kuleta matokeo pindi chakula kitakapoisha utahitaji kuvuna kilichopatikana kwa mbegu kama hukujiwekea akiba huu ndo wakati ambao utaona ni kama kitu hakiendi na hauna pesa             ``usisahau  akiba ni mfano wa mbegu hivyo haiwezi kukuletea matunda isipo pandwa kwa upande wa pili akiba isipo wekezwa haiwezi kukusaidia wakati wa shida fulani``

Na muhimu ni kuwa hatuishii kuiweka tu hii akiba bali tunaenda hatua ya Zaida mbele kwa kuiwekeza ili ilete matokeo makubwa tarajiwa.

 

AINA YA TATU: AKIBA YA MUDA;

Wataalamu wa mikakati ya maisha au life strategists husema muda ni mali kama ni mali tumeangalia hapo juu lazima tuweke akiba ya mali tulizo nazo. Namna ya kuweka akiba ya muda ni kuto kupoteza muda kwa vitu visivyo na umuhimu kwa maisha yako mfano kuangalia tu TV bila ratiba maalumu, kushinda unalala bila sababu yoyote, Kukesha ukiwa una chart au unaperuzi mitandaoni billa ya sababu maalumu.  Ikumbukwe rasilimali muhimu ambayo tumepewa kwa usawa ni muda. Hapa kila mmoja ana 24 na utofauti unakuja kwa namna kila mtu anavyoutumia muda wake.

 

Unaweza kufanya vitu kama; kusoma vitabu ili kujipatia maarifa fulani lakini pia kujiunza   ujuzi mpya au new skills zitakazo kusaidia katika maisha yako, kama namna nzuri ya kuukomboa wakati wako’

 

AINA YA NNE: AKIBA YA MAHUSIANO;

Mahusiano mazuri na watu yanaweza kutumika kama bidhaa ya kupata mahitaji ya mtu husika.  Mara nyingi mtu akijikusanyia watu muhimu wengi basi atakuwa na akiba njema iliyomzu nguka.

 

Kila mtu hutamani kuona anathaminiwa, anapendwa na anajaliwa na watu wake wa karibu akiba ya mahusiano ambayo wewe binafsi unaijenga kwa ajili ya kukusaidia wewe mwenyewe. Njia rahisi ya kujiwekea akiba kwa watu ni kwa kuongeza thamani kwao kwa kuwatafuta na kuwajulia hali au kuwasaidia katika yale matatizo au shida wanazozipitia na wakati fulani kujaribu kuomba ushauri wao kwa mambo sumbufu kwako.

Haya yote yanabebwa na vitu vitatu katika kuweka akiba ya mahusiano ambavyo ni upendo, uaminifu na heshima au nidhamu kwa mume, mke, wazazi, ndugu, jamaa na marafiki na watu wote.    

Mwandishi>> Erick Mgaya.+255 764 032 905

Mhariri >>> Migongo Elias. +255767653697


Ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu... Kama ndiyo waweza fanya yafuatayo.

1. Washirikishe wengine ujumbe huu wajifunze pia.

2. Unawezaa kutembelea ukurasa wetu wa Facebook Add Value Network. Au wasilina nami kwa masomo mengine ili kujifunza zaidi.

Let us sign out🖐️

Add Value Network
SeE yOu NeXt LeVeL 💪

 



Comment (1)

Loading... Logging you in...
  • Logged in as
🙌 This is cute bro....🩷

Post a new comment

Comments by

Popular posts from this blog

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

VITU 9 MUHIMU KWA MTU YEYOTE KUJIFUNZA KWENYE MAHAFALI.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.