HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31 Ilipoishia………. Elvine alipoteza amani kuliko hata mkewe maana kila alipomtazama mkewe basi moyo wake ni kama ulikuwa unachomwa na mwiba uliojishikiza huko kwenye mishipa ya moyo. Nafsi yake ilitaabika na ndipo alipoamua kutafuta muda mzuri, baada ya chakula cha jioni, azungumze na mkewe, maana ule ukimya wa siku mbili ulikuwa adhabu kubwa sana kwake. Kusoma sehemu ya 30 bonyeza hapa Sasa inaendelea………. Elimina mamy naomba kujua kwanini hutaki kuniuliza kuhusu sababu ya haya yote? Maana najua unajua kuwa kuna mahali mimi nilikosea, sasa unapokaa kimya hivyo… kiukweli unazidi kunichanganya maana ni kama hutaki kujua, sasa unadhani mimi roho yangu itatulia kweli?. Hata kama ungekuwa wewe lazima usingepata amani, ungekuwa hata unawaza hivi nakuwaziaje, nakuonaje na ninajisikiaje ninapokuona, sasa kwanini wewe umekaa kimya, sema neno tafadhali? (Elvine alikuwa akiongea bila kumtazama mkewe usoni maana moyo wake haukuwa katika hali ya utulivu). Pamoja na ...

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”. SEHEMU YA SITA.

 

SIMULIZI YA KUFURAHISHA, “KUHUSU HATIMA YA KIMUNGU”.

SEHEMU YA SITA. 

Ilipoishia.....

Mungu nisamehe kwa huu uamuzi lakini no matter what, lazima nimjue aliye na mtoto wangu na aliyemuua mume wangu. Mungu ni rehemu Kwahaya maamuzi lakini naomba baraka zako maana siwezi kukaa kimya tena. Mpaka hapa nilipofikia basi inatosha Mimi kuumia, maana nahisi hata mtoto wangu hawa watu ndio wanajua aliko. Huu ndiyo mwanzo, nipo tayari kufa, maana Sina cha kupoteza.  nisamehe sana ila niruhusu tu mimi nifanye hivi please..."

Kama hujasoma sehemu iliyopita bonyeza hapa.

 Sasa inaendelea....

    Editrin alijiapiza kulipa kisasi kwa wote waliosababisha familia yake sambaratika. Alionekana kama mtu aliyedhamilia kufanya jambo fulani ili aweze kutimiza kisasi chake.

    Alipotoka kanisani alirudi nyumbani, ambako alimkuta baba yake kawahi sana kurudi jambo ambalo halikuwa la kawaida kutokea. Mr. Edward baada ya kumwona Editrin, alionekana kama aliyefurahi kumwona binti yake karudi salama nyumbani. Alishusha pumzi nzito kisha akasimama na kuanza kuondoka kuelekea chumbani kwake.

    "Baba!"

    "Yes Editrin"

    "Hauna chochote cha kuniambia?"

    "Kama nini?"

    "Mbona kama unahofu kuhusu mimi sikuizi?"

    "Unamaana gani?"

    "Ok, sawa, kama huna cha kuniambia, basi mimi ninacho cha kukuambia". Mr. Edward aliahirisha safari yake na kuja kukaa tena mahali alipokuwa amekaa mwanzo. Editrin naye alisogea karibu na baba yake kisha akaketi.

     "Nataka kutimiza haja yako"

     "Ipi?"

    Nataka kuolewa, tena mtu ambaye wewe unataka". Mr. Edward alishituka kidogo kisha naye akauliza

   "Ninayemtaka? Nani?"

   "Yeyote tu, nimechoka kukaa hapa ndani, tena kwa wakati kama huu ambao mimi na wewe hatuelewani bora nikaolewe"

   "Nipe muda wa kufikiria kuhusu hilo". Mr. Edward alisimama na kuelekea chumbani kwake akiwa kama asiyeamini kitu, Editrin katamka kwa mdomo wake.

   Usiku huo Mr. Edward aliwaza sana, usingizi ulipaa na akawaza ni nani ampe binti yake. Kwa upande wa Editrin alikosa usingizi pia maana aliwaza namna ya kulipiza kisasi maana alihisi kabisa Esau atakuwa ndiye muhusika wa kifo cha mumewe.

     Asubuhi Mr. Edward aliondoka mapema sana na hakujulikana alikokwenda. Alirudi jioni akiwa na kijana mmoja aliyeitwa Emiliano. Emiliano alikuwa kijana aliyejulikana sana jijini Dar es salaam kwani alifahamika kwa namna alivyokuwa tajiri. Emiliano alikuwa ni kijana mdogo sana aliyemiliki kampuni ya ndege za masafa marefu yaani, kutoka Dar es salaam kwenda Marekani, China na India. Aliweza kumiliki kampuni hiyo baada ya wazazi wake kupoteza maisha kwa ajali ya gari. Alikuwa akiishi na mdogo wake aliyeitwa Emily maana ndiye ndugu pekee aliyekuwa naye, na hakuwahi kuwaza kuoa maana alipohojiwa na waandishi wa habari alisema sababu kubwa ni kuwa alihofia kumtelekeza mdogo wake.

      Emiliano na Editrin walisoma pamoja katika shule ya sekondari st. Claudy, na walikuja kutengana baada ya yeye kwenda kusoma India mara baada ya kumaliza form four.

     Editrin alishangaa sana kumuona Emiliano, na hakujua baba yake kamtoa wapi kijana yule. Hakujua kwanini Emiliano yupo kwao na wala hakutaka kuuliza. Emiliano alionyesha kufurahia sana kumuona Editrin.

     Baada ya chakula cha jioni Editrin na Emiliano walipata muda wa kukumbushana vihoja na matukio mbalimbali ya shule. Emiliano alikuwa kijana mstaarabu sana na mpole mno toka akiwa shule.

     Walipiga stori kwa muda mrefu sana mpaka wakajikuta 'wametoboa ozon' maana ilifika saa 11:30 asubuhi wakiwa bado subuleni wanachekacheka tu.

      Walishituka  na kuagana kwa kicheko baada ya kugundua wamekesha usiku kucha. Kila mmoja alikwenda kulala chumbani kwake na hakuna aliyeamka mpaka ilipofika saa 9:15 alasiri. Mr. Edward alifurahi kuona binti yake anafuraha sasa hivyo akaadhimia kumwozesha Editrin kwa Emiliano.

    Emiliano alikaa kwao kwa muda wa siku tano na hakuna aliyejua kwanini  yupo pale zaidi ya Mr. Edward. Baada ya siku tano kupita Editrin aliitwa na kuambiwa kuwa Emiliano yupo pale kwakuwa alihitaji kumuoa. Alishangaa maana hakujua kama itakuwa hivi maana adhima yake ilikuwa ni kuolewa na Esau ili aweze kupata nafasi ya kulipiza kisasi chake. Kwake hili lilikuwa jambo gumu kukubaliana nalo. Wakati akiwa anasitasita kutoa jibu baba yake alimpa stori fupi kuhusu Emiliano.

    "Emiliano akiwa shule alimpenda sana Editrin kwakuwa walikuwa wadogo aliona atajiaibisha tu, hivyo hakusema lolote. Walipomaliza sekondari Emiliano alipelekwa kusoma India na familia yake. Baada ya kurudi alikwenda kwa Mr. Edward na kumwambia kuwa anampenda Editrin na yupo tayari kumuoa, lakini alisikitishwa sana na taarifa alizopewa maana Editrin alikuwa amekwisha olewa na Edwin. Kiukweli alilia sana mbele ya Mr. Edward lakini Edward akamwambia Editrin kalazimisha ndoa.

       Kwakua hakuwa na chakufanya aliamua kukubali lakini alisema yupo tayari kumsubiria Editrin maana ndiyo binti pekee anayeweza kuishi na mdogo wake Emily vizuri vinginevyo basi yeye hatoweza kuoa.

     Stori hii ilimshangaza sana Editrin. Na ndipo alipoamua kukubali kuolewa na Emiliano na akaona itakuwa vizuri kama atamtumia Emiliano kumsaidia kulipiza kisasi chake.

      Editrin alimwambia Emiliano kuwa atakuwa tayari kuolewa naye kama atakuwa tayari kuokoka na kuanza kusali maana alitaka kufunga ndoa ya kanisani tena kwa heshima sana. Emiliano hakuwa na shida kabisa, alikwenda jumapili kanisani na kuokoka. Ndoa ikafungwa.

      Esau baada ya kusikia zile habari alichukia mno na akaanza kumsumbua Mr. Edward kwa fujo mbalimbali.

        Siku moja baada ya Emiliano kuja kumtembelea baba mkwe wake alitekwa na Esau na kupigwa sana. Esau baada ya kumpiga sana Emiliano alisema tu "unabahati mimi siwezi kuua mtu maana leo ungekuwa mwisho wako" baada ya maneno hayo alimchukua Emiliano na kwenda kumtupa karibu na ofisi ya Mr. Edward.

 

Kwanamna Emiliano alivyokuwa akijulikana watu walimtambuana kumuwahisha hospitali. Baada ya kupona aliulizwa kuwa ni nani kamfanyia vile, lakini alisema hata yeye hamjui. Ukweli ni kuwa hakuwa tayari kusema.

      Editrin alikaa miaka mingi sana na Emiliano lakini hakuweza kupata mtoto jambo ambalo lilisababisha kukosekana kwa furaha ndani ya familia ile.

      Siku moja Editrin aliota ndoto na ndani ya ndoto hiyo alimuona Edwin akimuita huku akisema "huwezi kupotea kama hivi Editrin, huwezi!". Ndoto ile ilimshangaza sana na ikamkosesha amani  kabisa. Alipomsimulia Emiliano, Emiliano alionyesha hali ya kukosa amani pia.

     Waliishi miaka yote bila mtoto na wakati huo walikuwa wakiishi na Emily mdogo wake Emiliano. Emily na Editrin walikuwa wanapendana sana na hawakuwahi kugombana.

     Siku moja Editrin akiwa nyumbani pekeyake baada ya mumewe na Emily kuondoka, alitoka nje ya geti kwaajili ya kuzungukazunguka nje ya nyumba yao. Ghafla alitaka kutekwa lakini kwa msaada wa walinzi wa nyumba yao ambao hakuwa mbali naye waliokuwa na silaha waliweza kumsaidia.

      Emiliano alipopata taarifa alirudi nyumbani haraka sana na alionyesha kuumia kana kwamba yeye ndiye aliyekuwa kavamiwa.

    Baada ya tukio lile kupita Emiliano aliongeza ulinzi kwa mkewe maana alihofia kuwa Esau ndiyo chanzo cha haya yote. Editrin aliamua kumsimulia Emiliano kuhusu kifo cha Edwin na kupotea kwa mumewe na mwisho alisema kuwa anahisi Esau ndiye aliyehusika.

      Emiliano alimuuliza Editrin swali "hivi ukithibitisha kuwa Esau ndiye aliyemuua mume wako utamfanyaje?".

      "Namfunga jela yaani lazima alipe"

       "Kwani huwezi kumsamehe?"

       "Hapana siwezi kumwacha kirahisi hivyo"

      "Kwani wewe bado unampenda Edwin au unanipenda mimi?. Kila siku humu ndani ni Edwin tu, kwani huwezi kumsahau Edwin?, Basi nenda kamtafute huyo Edwin na mtoto wako". Emiliano aliongea kwa kufoka hadi Editrin akashangaa.

       Baada ya miaka sita kupita Editrin alipewa taarifa kuwa Esau kafa pia. Tena kafa kwa kuuwawa na watu waliosemekana kuwa ni majambazi. Kwake taarifa zile zilimvutia maana aliona kama Mungu kamsaidia kulipa kisasi chake, hivyo alisema "kwakweli malipo ni hapahapa duniani'.

       Aliamua kuanza maisha kwa amani sasa, aliamua kumsamehe baba yake na kuachilia kila kitu. Wakiwa wanaendelea na maisha siku moja usiku aligumdua kitu ambacho hakuamini kabisa na kikamfanya atoroke pale ndani usiku na kukimbia mtaani huku akilia sana.

      *    *.    *.   *.    *.         *.          *

 

Elvine alirudi nyumbani akiwa na hasira sana. Na alipofika nyumbani alikwenda sebuleni na kukaa sebuleni akiwa na mawazo sana. Ghafla alikuja mdogo wake Elvila na kumkumbatia akiwa na furaha sana. Kwaasila na uchungu aliokuwa nao alimfokea mdogo wake na kumwambia hataki usumbufu. Elvine Alishangaa sana naye kwaasila alizila na kuondoka.

       Wakati anajutia kitendo cha kumfokea Elvila, baba yake alitoka. Elvine baada ya kumuona tu Mr. Ezhu yang alisimama na kumkunja baba yake kwa kumkaba, huku akihoji "where is my really mother?(yuko wapi mama yangu wa kweli?).

       Mr. Ezhu yang alishangaa sana. Wakati Elvine akiwa katika hali hiyo ya hasira mama yake Exhao alikuja pale sebuleni kwakile alichokiona alipiga kelele ambazo ziliwafanya watu watumishi wa mule ndani kuja kutoa msaada.

     Baada ya ugomvi huo kuisha Mr & Mrs Ezhu yang waliona hakuna haja ya kumficha ukweli Elvine tena maana tayari Elvine alikuwa na mawazo mabaya juu yao. Walimsimulia ukweli wote pasipo kumficha jambo. Elvine alilia mno na akasema baada ya kumaliza tu chuo alihitaji kurudi Tanzania. Wazazi wale waliumia sana maana hawatamani kumwacha Elvine aondoke lakini hawakuweza kumzuia tena.

        Elvine alikwenda kwa rafiki yake Elimina na kumsimulia kila alichosimuliwa na wazazi wake wale wa kichina. Elimina alimuuliza kama ataweza kupakumbuka nyumbani kwao siku akirudiTanzania. Elvine alisema hana uhakika maana tayari ni miaka mingi sana imepita.

        Walipomaliza chuo Elvine alimwambia Elimina kuwa watakwenda wote Tanzania. Elimina alikuwa na uzito kidogo kukubali maana alihofia pindi akifika Tanzania na Elvine wazazi wake watamuhoji maswali mengi. Kwahiyo akaanza kumkwepa.

      Elvine aligundua kwanini Elimina anamkwepa maana kila alipokaa naye na kumweleza kuwa anahitaji waende wote Tanzania. Elimina alikuja na maswali mengi mara utafikia wapi?, Unakwakufikia?, Unakukumbuka kwenu vizuri?, Kwanini usimwambiye baba yako Mr. Ezhu yang ndiyo akurudishe alipokutoa?....

     Elvine aliamua kumtumia Elimina vibaya, maana alijua kabisa kuwa Elimina anaifahamu Iringa vizuri na istoshe walikuwa wakisali kanisa moja. Elvine alianzisha mazoea sana na Elimina na akaanza kumjali kiasi ambacho Elimina alihisi anapendwa sana, lakini Elvine alikuwa akiigiza ili tu afike kwa mama yake.

     Siku waliyokuwa wakihitumu chuo kikuu Elvine alimwambia Elimina kuwa anahitaji kumuoa pindi wakifika Tanzania. Elimina alishangaa sana na akafurahi pia. Aliamua kutoa taarifa kwao kuwa amepata mchumba na anakwenda naye kwao maana pia mchumba wake ni mtanzania.

      Baba yake alimshangaa sana na kisha akamuuliza swali kuwa mbona imekuwa mapema sana kumkubali mtu huyo! Na pia alimwambia asikurupuke amwombe Mungu ili Mungu ndiye athibitishe hilo jambo lake, lakini Elimina alisema anauhakika na pia Mungu kasema naye pia kuhusu hilo.

 

 

       Siku zilifika za wao kuondoka china, Elvine aliwaaga Mr & Mrs Ezhu yang na Elvila mdogo wake ambaye alikuwa akilia sana maana alimzoea sana Elvine. Lakini Elvine alimuahidi Elvila kuwa atarudi tena kumchukua waende wote Tanzania.

     Elvine na Elimina waliondoka mpaka Tanzania, waliposhuka uwanja wa ndege wa Tanzania, walikutana na baba mmoja ambaye naye alionekana ni mgeni pale. Elvine alimshangaa sana yule baba maana Elimina alimwambia kuwa anafanana sana na yule baba. Yule baba alishangaa kuona kuna mtu anamtazama sana. Akaamua kumsogelea yule kijana na kumuuliza sababu ya yeye kumtazama vile. Elvine alimwambia kuwa anahisi wanafanana sana. Yule baba alicheka sana na akasema "Duniani kuna Mungu, na ndiye kaumba watu, kwahiyo msemo wa duniani wawili wawili unaweza kuwa wa kweli".

      Yule baba alionekana ni mwenye pesa sana na alisema kuwa katokea Marekani. Kwa muda mfupi walizoeana na yule baba akawapa lifti kwenye gari lake maana na yeye alisema anakwenda Iringa kwasababu kuna mtu anaenda kumtafuta huko. Elimina aliuliza "ni nani?" Yule baba alitabasamu na  kusema ni rafiki yangu tu.

      Walifika Iringa stendi na ndipo walipoachana, lakini walipeana namba kwaajili ya mawasiliano zaidi. Elvine alifika nyumbani kwa kina Elimina na kupokelewa vizuri sana. Elvine alijua kuwa itakuwa nahisi sana kumpata mama yake akiwa pale kwa mchungaji Moses. Alisubiri jumapili kwa hamu akiwa na . Matarajio ya kumuona mama yake.

     Jumapili ilipofika walikwenda kanisani, muda wote wa ibada alikuwa akiangaza macho yake kumtafuta mama yake lakini hakujua kuwa mama yake alikwisha ondoka Iringa muda mrefu sana. Alipoona hajamuona mama yake aliamua kusema ukweli. Wakiwa katika chakula cha jioni Elvine aliulizwa na baba yake Elimina kama kweli anamalengo na binti yao.

     Elvine alishindwa kujibu na akainamisha kichwa chini na kutikisa kichwa ikiwa ni ishara ya kukataa. Elimina hakuamini kabisa kinachotokea pale, Elvine aliwaeleza kuwa alimdanganya Elimina kwasababu alihitaji mtu wakumfikisha Tanzania. Na akasema alifanya hivyo baada ya kujua kuwa Elimina ni mtoto wa mchungaji anayelea kanisa ambalo yeye na mama yake walikuwa wakisali, hivyo alihisi itakuwa rahisi sana yeye kumpata mama yake akiwa kwa kina Elimina maana kutokana na maendeleo haikuwa rahisi sana kupafahamu kwao.

      Elimina alitoka pale sebuleni na kukimbilia chumbani kwake, ambako huko alilia sana. Mchungaji Moses alimuuliza jina la mama yake na Elvine akataja kuwa alikuwa akiitwa Editrin. Mchungaji na mkewe walishituka sana na wakaanza kumuuliza maswali ya mfululizo. "Ulikuwa wapi siku zote hizo? Nini kilitokea? Ulifikaje China we mtoto? Na mengine mengi.

Baadaye walimueleza namna mama yake alivyochanyikiwa baada ya yeye kupotea. Na pia walimwambia kuwa mama yake alikuja kumchukua na familia yake na hawajui taarifa zake maana ni miaka mingi imepita.

 Kule chumbani Elimina aliamua kunywa panado na mseto(dawa za malaria) ambavyo jumla yake vilikuwa ni vidonge 47. Wakati huku subuleni maongezi yakiwa yanaendea mama Elimina aliona aende chumbani kwa binti yake akamfariji, lakini oooh!! Hakuamini kabisa alichokiona baada ya kuingia chumbani....

 

       Sehemu ya sita itaendelea jumatatu >>>>>. Usikose kufuatilia.

Kupata mwendelezo wake bofya hapa.

           Hadithi hii imendaliwa na kuandikwa na JACQUELINE JOHN.

             Mwimbaji na mtunzi wa nyimbo, mashairi, Hadithi (simulizi) na ngonjera.

 Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255789523850. Normal >>>>>+255747313148.

          Hadithi hii Imehaririwa na MIGONGO ELIAS. Mhariri.

Mawasiliano:

Whatsapno. >>>>> +255767653697. Normal >>>>>+255783327456.

                                  GeT tO tHe NeXt LeVeL!

Kama umejifunza kitu shiriki nasi katika comment hapo chini, ili kujifunza na kuboresha zaidi.

Popular posts from this blog

MAAJABU YA AKIBA

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.