MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

HIKI NDICHO HUJUI KUHUSU KULALAMIKA.

 

HIKI NDICHO HUJUI KUHUSU KULALAMIKA.

Ndugu msomaji nakusalimu! Bila shaka u mzima  na kama sivyo Ikawe heri kwako. Karibu tena ndani ya addvaluenetwork tujifunza kwa pamoja ili kuongeza maarifa yatakayoongeza thamani ya kila mmoja.

Kupitia mtanadano huu utajifunza mengi kuhusu uchumi, saikolojia, maendeleo binafsi, na  maisha kwa ujumla. 

Kwani, wengi wameripoti kujifunza na kuponywa katika changamoto zao. Hivyo nikukaribishe sana na wewe upate kujifunza pamoja nasi. Uhakika wangu ni kwamba, hutabaki kama ulivyo mara tu baada ya kusoma hapa. 

Na kama utaweza mwalike na rafiki yako, na rafiki yako amwalike rafiki yake na yeye amwalike rafiki yake pia ili sote tujifunze.

Sasa leo nataka tujifunza kitu kimoja muhimu sana ambacho utapata kitu cha kusonga nacho. Kitu hiki ni kulalamika.

Watu wengi wamekuwa na kasumba ya kulaumu watu wengine, hasa wanapokutana na ugumu wowote katika maisha yao au pengine mambo yao kutokwenda kama walivyo panga. 

Hapo ndipo watatafuta watu wa kuwalaumu mwanzo mwisho,  huku wakidai kuwa wao ni chanzo cha kushindwa kwao. 

Atalaumu wazazi wake, pengine kwa kutokumsomesha, kumlea au kufariki kwao, atalaumu serikali kwa kutokumwajiri, atalaumu ndugu zake, atalaumu mke/mme wake, atalaumu, watoto wake, atalaumu viongozi, atalaumu  rafiki zake na wengine huenda mbali sana kwa kumlaumu hadi Mungu kwa kuzaliwa Nchi aliyozaliwa, kwa kuzaliwa na wazazi aliozaliwa nao, kwa kuwa na hali aliyo nayo kwa sasa. Yaani, atalaumu kila kitu. 

Kitu hiki siyo sawa, ndiyo maana leo addvaluenetwork imeamua kukusogezea karibu mada hii ili uongeze maarifa yatakayo ongeza thamani yako.

Nyuma ya kulalamika kuna mambo mengi ambayo pengine unayafahamu au huyafahamu, kuhusu kulalamika ambayo leo ningependa ujifunze kwayo. 

Hivyo twende pamoja;

Jambo la kwanza;

Unalaumu mtu ambaye unaamini ana uwezo na mamlaka kuliko wewe. 

Kwa kawaida unapolaumu mtu yeyote katika kila gumu unalokutana nalo, maana yake unachukua mamlaka na uwezo wako  wa kupambana na gumu hilo unauhamisha na kumpa unayemlalamikia. 

By the way huwezi kulaumu huku ukasonga mbele. Hata katika maisha kiujumla, kitu usicho kijua ni kwamba unamamlaka, nguvu na uwezo mkubwa wa kukabiliana na changamoto yako.

Kama utaamua kuwalaumu wengine juu ya tatizo lako, ni sawa na kuuambia ubongo wako kuwa uwezo, nguvu na mamlaka hiyo husitahili kuwa nayo hivyo unachukua na kuhamisha kwa mtu mwingine. Ambaye unamlaumu. 

Hebu jiulize kupitia kulaumu changamoto hiyo utaitatua kweli? Kama ni ndiyo endelea kulaumu, vinginevyo acha siasa mara moja tafuta suluhisho ya changamoto yako asee.

Jambo la pili;

Unapolaumu wengine hata fursa ndogo ambazo ungeweza kuzifanya hutaweza kuzifanya kabisa

Unauwezo mkubwa wa kushughulika na changamoto zako mwenyewe. Na pindi utakapouhamishia uwezo huo kwa mtu mwingine ambaye unamlaumu, ubongo na akili yako itabaki kwenye freezing state  ile hali ya kuganda na kushindwa kuchaji ili kufikiria njia mbadala ya kutatua shida yako. 

Kwa maana kulalamika hakufanyi usonge mbele isipokuwa utabaki katika hali hiyo hiyo miaka nenda miaka rudi ukilaumu watu. 

Mbaya zaidi utashangaa kuona watu wengine wakikatiza wanafanya jambo kama lako na kufanikiwa huku wewe umebaki kulaumu tu, vinginevyo labda wakuonee huruma.

Jambo la tatu;

Kulamu wengine hakusaidii kutatua tatizo lako. 

Kuna namna watu tunategemeana katika kuendelea kwetu kwenye maisha yetu ya kila siku. Sasa hii sio pointi ya kuwalaumu wengine kuwa, hawajafanya katika kutatua changamoto yako.

Ni kweli lakini tambua kuwa hatutatui magumu yetu kwa kuwalaumu watu badala yake kwa kutafuta shuruhisho la nini kifanyike ili kuimarisha au kutatua changamoto hiyo.  

Halafu ngoja nikwambie, katika patternaship yeyote mambo kama hayaendi vyema kabla ya kuwalaumu na kuwarushia mpira wengine hebu jiulize kuwa wewe umechangia kwa kiasi gani kutokea kwa tatizo hilo, kuvunjika kwa mahusiano haya au kuanguka kwa biashara yako.

Baada ya hapo jiulize pia, umejifunza nini? Na utabadilika kwa namna gani ili kuepuka kuteswa na changamoto moja miaka yote?. 

Ukisha shughulika na wewe kwanza ndipo unaweza kuangalia na mwenzako yeye kachangia kwa kiasi gani katika hili. Hapo ndipo mtapata muda wa kuyajenga na kuimarisha biashara yenu, ndoa yenu, mahusiano yenu, kazi yenu n.k .

Mara nyingi nimekuja gundua kuwa si watu tunao walaumu ndiyo chanzo cha kushuka kwetu kama wengi wanavyodhani, bali tatizo lipo kwetu wenyewe na  asilimia kubwa ya watu tunao walaumu na kuwa lalamikia hatukupaswa kabisa kuwa laumu.

Na kama hujui ukipenda kulalamika kwa kila kitu kwenye maisha yako, utapoteza watu wengi sana kwa sababu watu hawapendi kulaumiwa na mara nyingi hujitahidi kujitenga na walalamikaji.

Ndugu yangu yapo mengi katika hili lakini nachotaka ufahamu ni kwamba maisha yako ni jumkumu lako mwenyewe kwa asilimia mia. 

Kulaumu watu hakutasaidia wewe kusonga mbele badala yake utajichelewesha na kupoteza muda tu bure.  

Katika hili usitegemee mtu kutoka nchi za mbali ili kujakukufanyia jambo lako, usitegemee mtu atakuja na kukufanyia hiyo biashara yako, hiyo elimu yako, wala hilo jambo ufanyalo badala yake watu watakuja kwako kama daraja tu la wewe kupita na kujifunza kwao jukumu la kuamua na kujifunza kwao kisha kufanya mwenyewe ni lako mwenyewe. 

Wakati mwengine wao ni kutoa funzo na ushauri kwako ukiamua kuufuata ni wewe usipoamua ni wewe, si unajua maneno na ushauri mara nyingi huyolewa bure, lakini kuwa makini kuchagua unao faa tu.

ukibakikulaumu na kuwalalamikia watu  utabaki kama ulivyo asee.  Badilika pambana kwa nafasi yako, jifunze kwa watu, kisha usonge mbele.

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi, maendeleo binafsi, na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluenetwork. Karibu sana ujiongezee thamani yako.

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

Facebook page>> Add Value Network

Kama umejifunza kitu, andika "KUNA MAHALI NAENDA".

 

Comments (15)

Loading... Logging you in...
  • Logged in as
Victorine's avatar

Victorine · 86 weeks ago

Thanks for good and encouraging words lets meet to the next level
1 reply · active 86 weeks ago
Thank you too Madame stay tuned yet more
Scholastica's avatar

Scholastica · 86 weeks ago

Asante kwa ujumbe mzuri,,,Atleast nmepata funzo kutokana na hii mada ,,,,Mungu anisaidie nipone na hili janga la kuwalalamikia wengine🙇🏿‍♀🙇🏿‍♀🙇🏿‍♀
1 reply · active 86 weeks ago
Nafurahi kusikia hivyo lakini Mungu akusaidie sana katika hilo
🙋🙋🙋👍
1 reply · active 86 weeks ago
Amen amen
Asanteh kwa ujumbe mzuri mwl wangu.
1 reply · active 86 weeks ago
Ahsante nashukuru Sana rafiki
Ahsant sana Kwa somo zuri nimejifunza kitu katika hili somo mungu akuinue zaid utuletee masomo mengine 🙏
1 reply · active 86 weeks ago
Ahsante nashukuru Sana rafiki, ubarikiwe mnoo
Joga heke's avatar

Joga heke · 50 weeks ago

Thanks
Mwl. Kasunzu's avatar

Mwl. Kasunzu · 50 weeks ago

Asante saana!
1 reply · active 49 weeks ago
Elias Migongo's avatar

Elias Migongo · 49 weeks ago

Amen amen
deusmsafiri's avatar

deusmsafiri · 49 weeks ago

Much respect my brother...✊✊🤝
1 reply · active 49 weeks ago
Migongo Elias's avatar

Migongo Elias · 49 weeks ago

Thanks much rafiki

Post a new comment

Comments by

Popular posts from this blog

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

VITU 9 MUHIMU KWA MTU YEYOTE KUJIFUNZA KWENYE MAHAFALI.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.