MAAJABU YA AKIBA

Hivi ulishawahi kuona mtu anauwezo wa kufanya au wa
kukusaidia jambo lakini ukimwambia kufanya hivyo utashangaa anakwambia goja nijaribu.
Wakati mwingine unakuta mtu anatamani kabisa kufanya au kufanikiwa jambo fulani,
lakini utashangaa anakwambia ngoja nijaribu kama nitafanikiwa. Mwingine akiwa darasani au kwenye kikao swali likiulizwa
katika kulijibu utashangaa goja na mimi ni jaribu. Na maneno mengi tu ambayo
hayaendi moja kwa moja katika kufanya badala yake watu hujificha katika kivuli
cha kujaribu huku wakijikuta wanashindwa
kabisa kufanya.
Wapo watu wenye mipango na mawazo lukuki tena adimu kutokea
ambayo kufanikiwa kwayo ni swala la muda tu. Sasa badala ya kuyafanyia kazi
utakuta mtu anakwambia sijui kama nitaweza labda ngoja nijaribu. Wengine wanatamani
sana kufanikiwa eneo fulani mfano utakuta mwingine anatamani sana kuajiriwa
badala ya kutuma maombi anasema ngoja nijaribu kutuma maombi. Penmgine utakuta mtu ameitwa na
kwenye usaili lakini utakuta anasema ngoja nikajaribu lakini sijui kama
nitapita. Yaani, amejijengea notion fulani ya kujaribu jaribu tu ambayo uhalisia
wake siyo nzuri.
Na hapa na kwenda kukuambia kwanini
hupaswi kujaribu, kisha tutaona badala ya kujaribu tunapaswa kufanya nini;
1.
KUJARIBU NI SAWA NA KUSHINDWA.
Wazungu wanasema trying implies failure.
Ukweli ni kwamba mtu anayejaribu na anayefanya kabisa huwa hawafanani hata
katika usiliasi utakuta aliye zamilia kufanya yupo siliasi huku anayejaribu
ataonekana kama yuko siliasi lakini mwisho wa siku ataishia tu kujaribu na
hataumia kwa kushindwa kwake kwasababu alikuwa anajaribu. Kwahiyo mara nyingi
mtu anaye jaribu huwa na uwezekano mkubwa sana wa kushindwa yaani kufeli kuliko
yule anayefanya kwa kuzamilia kabisa. Pamoja na kwamba wapo wanaojaribu na
kufanikiwa mazima kabisa huku wapo aliozamilia kufanya na wakashindwa pia. Lakini,
bado takwimu na chunguzi zinaonyesha kuwa watu walio ingia kwenye biashara,
kilimo, ugugaji, uandishi, michezo, utangazaji, ualimu na sehemu zingine kwa
lengo la kujaribu wengi wao waliishia kushindwa huku wale waliojitoa kimasomaso
kufanya asilimia kubwa walifanikiwa katika
kufanya kwao.
Usikubali kuingia katika biashara, kilimo,
ushirika, aua kazi yeyote kwa lengo la kujaribu huku ukitegemea kufanya vizuri
zaidi.
2.
TAARIFA HII HUINGIA NDANI YA UBONGO
WAKO.
Uhalisia ni kwamba chechote
unachokifanya kimetokana na fikra ulizokuwa nazo ndani mwako. Hivyo hata wewe
ukiwa na fikra za kujaribu jaribu ubongo wako utapata taarifa hiyo na kupelekea
msukumo wa kufanya kile unachokiwaza. Yaani nasema kuwa ukiingia na fikra za
kujaribu kufanya kazi, biashara, kusoma, kuajiri/kuajiriwa. Kuoa/kuolewa akili
yako itakusukuma na kukwambia kuwa upo katika hali ya kujaribu tu ko hata ukishindwa
haina shida. Na kweli unaishia kujaribu tu na wakati mwingine kushindwa kabisa.
Kuwa makini asee!
3.
UNAKUWA HUNA UHAKIKA WA KUFANIKIWA.
Kama tunavyofahamu kujaribu ni kama kubahatisha yaani, kupata au kukosa hivyo hata wewe unapojaribu maana yake unakuwa huna uhakika wa kile unafanya ya kwamba utafanikiwa au utafeli, ni kama vile unabeti vile si unajua unaweza kupata au mkeka ukachanika eeh! Hivyo kwa uhakika zaidi achana na kubahatisha badala yake amua kufanya kabisa vinginevyo usifanye tu nakushauri.
NINI CHA KUFANYA?
Marc
Reklau amewahi kusema “Try
not. Do or do not. There is no try.” Yaani, usijaribu. Fanya au usifanye. Hakuna
kujaribu. Ninachojua ni kwamba kujaribu hakutakupeleka
kokote si unajua kwanza unakuwa huna uhakika na kile unafanya. Hivyo badala
ya kuwa mtu wa kujaribu jaribu katika kazi zako amua kujitoa kimasomaso kufanya
kile unatamani na siyo kujaribu.
Pia uondoe msamiati jaribu kwenye kazi na
maneno yako. Ninachotaka ujue ni kwamba usipoteze muda wako kujaribu
kwa kana kwamba huna uhakika na kile unafanya katika kazi zako. Kama unafanya
fanya kweli kweli na kama hufanyi nalolifahamike kabisa. Vinginevyo kujaribu ni
marufuku kama marufuku zingine.
Kabla ya kufanya kazi yeyote au kushirikishwa
kitu chochote kaa chini kisha jiulize kuwa unafanya au haufanyi. Maswala ya kujaribu
waachie watu ambao hawana uhakia na maisha yao ambapo wewe siyo mmoja wao. Labda
nikuulize rafiki kuwa unataka ufanye biashara? Basi usijaribu nenda kafanye,
unataka ufanye kilimo? Nenda kafanye hakuna kujaribu, unataka kuwa dalali nenda
kafanye usijaribu asee, unataka kufanya kazi gani? Amua kufanya usilete habari
za kujaribu jaribu hapa hapa vinginevyo acha kufanya hiyo kazi. Harafu Kama hujui, wakati unajaribu wenzako wanafanya kabisa.
Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza
kitu.
na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya
kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia
mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.
GeT tO ThE nExT
lEvEl!
Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS
Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na
Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluenetwork.
Karibu sana ujiongezee thamani yako.
Kwa mawasiliano;
Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456
Email>> eliasmigongo120@gmail.com.
Facebook>> MIGONGO ELIAS.
LinkedIn>>Migongoe.
Instagram>>migongo_elias.
Pinterest>>eliasmigongo.
Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi
kujifunza pamoja nawe.
Sort by: Date Rating Last Activity
Comments by IntenseDebate
Posting anonymously.
BeHumanBeKind · 85 weeks ago
Migongo · 85 weeks ago
Catherine · 85 weeks ago
Elias · 85 weeks ago
Chyo · 85 weeks ago
Elias Migongo · 84 weeks ago
masaga · 52 weeks ago
Migongo · 51 weeks ago