MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

ACHA KUJARIBU, ANZA KUFANYA.

 

ACHA KUJARIBU ANZA KUFANYA.

Hivi ulishawahi kuona mtu anauwezo wa kufanya au wa kukusaidia jambo lakini ukimwambia kufanya hivyo utashangaa anakwambia goja nijaribu. Wakati mwingine unakuta mtu anatamani kabisa kufanya au kufanikiwa jambo fulani, lakini utashangaa anakwambia ngoja nijaribu kama nitafanikiwa. Mwingine  akiwa darasani au kwenye kikao swali likiulizwa katika kulijibu utashangaa goja na mimi ni jaribu. Na maneno mengi tu ambayo hayaendi moja kwa moja katika kufanya badala yake watu hujificha katika kivuli cha  kujaribu huku wakijikuta wanashindwa kabisa kufanya.

Wapo watu wenye mipango na mawazo lukuki tena adimu kutokea ambayo kufanikiwa kwayo ni swala la muda tu. Sasa badala ya kuyafanyia kazi utakuta mtu anakwambia sijui kama nitaweza labda ngoja nijaribu. Wengine wanatamani sana kufanikiwa eneo fulani mfano utakuta mwingine anatamani sana kuajiriwa badala ya kutuma maombi anasema ngoja nijaribu kutuma maombi. Penmgine utakuta mtu ameitwa na kwenye usaili lakini utakuta anasema ngoja nikajaribu lakini sijui kama nitapita. Yaani, amejijengea notion fulani ya kujaribu jaribu tu ambayo uhalisia wake siyo nzuri.

Na hapa na kwenda kukuambia kwanini hupaswi kujaribu, kisha tutaona badala ya kujaribu tunapaswa kufanya nini;

1.   KUJARIBU NI SAWA NA KUSHINDWA.

Wazungu wanasema trying implies failure. Ukweli ni kwamba mtu anayejaribu na anayefanya kabisa huwa hawafanani hata katika usiliasi utakuta aliye zamilia kufanya yupo siliasi huku anayejaribu ataonekana kama yuko siliasi lakini mwisho wa siku ataishia tu kujaribu na hataumia kwa kushindwa kwake kwasababu alikuwa anajaribu. Kwahiyo mara nyingi mtu anaye jaribu huwa na uwezekano mkubwa sana wa kushindwa yaani kufeli kuliko yule anayefanya kwa kuzamilia kabisa. Pamoja na kwamba wapo wanaojaribu na kufanikiwa mazima kabisa huku wapo aliozamilia kufanya na wakashindwa pia. Lakini, bado takwimu na chunguzi zinaonyesha kuwa watu walio ingia kwenye biashara, kilimo, ugugaji, uandishi, michezo, utangazaji, ualimu na sehemu zingine kwa lengo la kujaribu wengi wao waliishia kushindwa huku wale waliojitoa kimasomaso kufanya  asilimia kubwa walifanikiwa katika kufanya kwao.

Usikubali kuingia katika biashara, kilimo, ushirika, aua kazi yeyote kwa lengo la kujaribu huku ukitegemea kufanya vizuri zaidi.

2.   TAARIFA HII HUINGIA NDANI YA UBONGO WAKO.

Uhalisia ni kwamba chechote unachokifanya kimetokana na fikra ulizokuwa nazo ndani mwako. Hivyo hata wewe ukiwa na fikra za kujaribu jaribu ubongo wako utapata taarifa hiyo na kupelekea msukumo wa kufanya kile unachokiwaza. Yaani nasema kuwa ukiingia na fikra za kujaribu kufanya kazi, biashara, kusoma, kuajiri/kuajiriwa. Kuoa/kuolewa akili yako itakusukuma na kukwambia kuwa upo katika hali ya kujaribu tu ko hata ukishindwa haina shida. Na kweli unaishia kujaribu tu na wakati mwingine kushindwa kabisa. Kuwa makini asee!

3.   UNAKUWA HUNA UHAKIKA WA KUFANIKIWA.

Kama tunavyofahamu kujaribu ni kama kubahatisha yaani, kupata au kukosa hivyo hata wewe unapojaribu maana yake unakuwa huna uhakika wa kile unafanya ya kwamba utafanikiwa au utafeli, ni kama vile unabeti vile si unajua unaweza kupata au mkeka ukachanika eeh! Hivyo kwa uhakika zaidi achana na kubahatisha badala yake amua kufanya kabisa vinginevyo usifanye tu nakushauri.

NINI CHA KUFANYA?

Marc Reklau  amewahi kusema “Try not. Do or do not. There is no try.” Yaani, usijaribu. Fanya au usifanye. Hakuna kujaribu. Ninachojua ni kwamba kujaribu hakutakupeleka kokote si unajua kwanza unakuwa huna uhakika na kile unafanya. Hivyo badala ya kuwa mtu wa kujaribu jaribu katika kazi zako amua kujitoa kimasomaso kufanya kile unatamani na siyo kujaribu.

Pia uondoe msamiati jaribu kwenye kazi na maneno yako. Ninachotaka ujue ni kwamba usipoteze muda wako kujaribu kwa kana kwamba huna uhakika na kile unafanya katika kazi zako. Kama unafanya fanya kweli kweli na kama hufanyi nalolifahamike kabisa. Vinginevyo kujaribu ni marufuku kama marufuku zingine.

Kabla ya kufanya kazi yeyote au kushirikishwa kitu chochote kaa chini kisha jiulize kuwa unafanya au  haufanyi. Maswala ya kujaribu waachie watu ambao hawana uhakia na maisha yao ambapo wewe siyo mmoja wao. Labda nikuulize rafiki kuwa unataka ufanye biashara? Basi usijaribu nenda kafanye, unataka ufanye kilimo? Nenda kafanye hakuna kujaribu, unataka kuwa dalali nenda kafanye usijaribu asee, unataka kufanya kazi gani? Amua kufanya usilete habari za kujaribu jaribu hapa hapa vinginevyo acha kufanya hiyo kazi. Harafu Kama hujui, wakati unajaribu wenzako wanafanya kabisa.

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluenetwork. Karibu sana ujiongezee thamani yako.

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe.

Instagram>>migongo_elias.

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe.

 

 

 

Comments (8)

Loading... Logging you in...
  • Logged in as
BeHumanBeKind 's avatar

BeHumanBeKind · 85 weeks ago

Asante Mr.Migongo Elias
1 reply · active 85 weeks ago
Ahsante nashukuru Sana rafiki ubarikiwe mnoo
Catherine's avatar

Catherine · 85 weeks ago

Safiii👏👏
1 reply · active 85 weeks ago
Ahsante Sana rafiki
Ubarikiwe sana ndguang kwa makala nzuri, hakuna kujaribu zaidi ni kufanya. Nimelielewa sana SoMo hili.
1 reply · active 84 weeks ago
Elias Migongo's avatar

Elias Migongo · 84 weeks ago

Ahsante nashukuru sana.
asantee ubarikiwe
1 reply · active 51 weeks ago
Amen Sana aseee

Post a new comment

Comments by

Popular posts from this blog

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

VITU 9 MUHIMU KWA MTU YEYOTE KUJIFUNZA KWENYE MAHAFALI.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.