MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.

Sometimes your joy is the source of your smile, but sometimes your smile can be the source of your joy.” Wakati mwingine furaha yako ni chanzo cha tabasamu lako, lakini pia tabasamu lako linaweza kuwa chanzo cha furaha yako. Tunaishi kwenye dunia ambayo watu wamevurugwa na maisha, huku wakiwa bize au sirious na maisha yao.  kana kwamba kuona tabasamu na furaha yao imekuwa ni adimu sana. kwa kawaida tabasamu na kucheka huwa ni viashiria vionekanavyo katika kuonyesha au kuashiria furaha, licha ya kuwa vipo viashiria vingine lakini tabasamu na kicheko hutafsirika mapema kama viashiria vya furaha. Wakati mwingine mtu anaweza akacheka na kutabasamu lakini akawa na machungu ndani yake goja tuachane nayo leo hii.

Tafti zinaonyesha kuwa mtoto mdogo mwenye umri wa miaka 4-6 hucheka mara 300-400 kwa siku huku mtu mzima hucheka mara 15 tu kwa siku huu ni utafri ambao haujathibitishwa. Lakini kilichothibitishwa ni kwamba kucheka na kutabasamu kunaimarisha maisha yako, afya yako, hali ya ubongo wako na hata ubunifu wako. Pamoja na kwamba kunawatu hucheka na kutabasamu kwa musimu yaani mara chache sana watu hawa ni tofauti sana na watu wanaocheka na kutabasamu mara kwa mara. Kwani huwa ni wepesi wa kusongwa na msongo wa mawazo wakati mwingine hata ugumu wa maisha ingawaje hawezi kusema, hii ni sawa na sumu ndani ya mtu ambayo kiafya siyo nzuri.

Tabasamu kadiri unavyoweza hata kama hauna sababu ya kutabasamu we tabasamu tu, kwani unapotabasamu unapeleka taarifa chanya kwenye ubongo wako ambayo huimarisha utendaji kazi wa ubongo na kuleta furaha zaidi. Kitu kama hichi Marc Reklau amewahi kusema “When you smile your entire body sends out the message “Life is great” to the world.” Tafsiri yake ni kwamba unapo tabasamu mwili wako unapeleka ujumbe “Maisha ni mkuu” kwenye dunia.

Vitu ambavyo huvijui kuhusu kutabasamu ni kwamba;

1.   Ukitabasamu unachilia homoni ya serotonin (ambayo hutufanya tujisikia vizuri). Ndiyo maana mtu akitabasamu anaonekana hanashida wala changamoto.

2.   Ukitabasamu unaachilia homoni ya  endorphins (ambayo hupunguza maumivu). Hii humfanya mtu asahau matatizo na kutua mzigo wa shida zake huku akifurahi na kuondoa stress. Hivi ulisha wahi kuvurugwa ukajisikia maumivu ndani yako, na ukaenda kuangalia hata comedy? Utashangaa kuona unaanza kucheka na kusahau kabisa maumivu yale hii ni kuwepo kwa homoni hii.

3.   Hupunguza mganzamizo wa damu(blood presure). Hii ni kutoka na na kuwepo kwa homoni hizo hapo juu ambazo husaidia kuondosha stress.

4.    Huongeza ufanisi wa utendaji kazi wa kinga ya mwili

5.   Humfanya mtu kuonekana hana shida wala changamoto za maisha.

6.   Humfanya mtu kuonekana mwepesi kufikika na kubadilishana mawazo nae. Watu wa aina hii ni tofauti kabisa na wale wenye kuwa serious muda wote kwani huogopeka sana.

Wana saikolojia husema kuwa tabasamu ni moja ya njia muhimu sana za kuongeza mvuto na ushawishi wa mtu  kwa watu wanao mzunguka, aidha wawe ni wale wanaomfahamu au wasio mfahamu lakini pindi atakapo tabasamu huonekana kama wanafahamiana kabisa. Unaweza kufanya hivyo pindi unapokutana na watu hata ambao hujawahi kukutana nao utashangaa kuona nao wanavyo tabasamu.

Kutabasamu au kucheka siyo lazima na wala mtu asipo tabasamu wala kucheka atakufa hapana! Kutokana na faida hapo juu na nyingine lukuki ambazo hatujazijadili hapa unaweza kuchagua kutabasamu. Kwani hakuna gharama yeyote inayohitajika ili kutabasamu, pili  unapotabasamu unayapa thamani na maana  maisha yako. Kama ni hivyo kwanini usichague kutabasamu na kufurahi hivi kutabasamu na kucheka ni shingapi kwani?

Na kama hujawahi kutabasamu wala hujazoea kabisa unaweza kuanza kutabasamu mara nyingi kadiri unavyo weza napo fanya hivyo kwa kutumia kioo chako  kisha jitazame kabla hujatabasamu. Halafu tabasamu huku ukiwa umejitazama kwa kioo hapo utachagua yule wa kwanza kabla ya kutabasamu na yule wa pili baada ya kutabasamu ni yupi amekaa poa? Kisha fanya hivyo mara kwa mara kila siku.

Pamoja na hayo kuna mahali pa kutabasamu, kucheka na kufurahi na siyo kila sehemu na kila wakati na kwa kila mtu inatakiwa utabasamu. Onyesha kufurahi lakini tambua kuwa kila jambu na wakati wake.

Najua hujatoka kama ulivyo ingia hivyo ulicho kipata anza kukifanyia kazi na kile hujakipenda achana nacho hicho siyo chako.

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluenetwork. Karibu sana ujiongezee thamani yako.

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe.

Instagram>>migongo_elias.

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe.

 

 


Comments (23)

Loading... Logging you in...
  • Logged in as
Suzan Phares's avatar

Suzan Phares · 84 weeks ago

Smile for better life😊😍!! Be blessed
1 reply · active 84 weeks ago
Amen stay blessed you too
Wow!! Enjoyed the lesson Mr.
1 reply · active 84 weeks ago
Am glad that you think so
Ubarikiwe sana kwa makala nzuri mwl wngu.
2 replies · active 84 weeks ago
Amen amen nashukuru ndugu
I learnt Mr Migongo👏🏻😁😁😁
1 reply · active 84 weeks ago
Great great Nuru
Japhary Seth's avatar

Japhary Seth · 84 weeks ago

Good message
1 reply · active 84 weeks ago
Thank you sir
Elisha W Ndidi's avatar

Elisha W Ndidi · 83 weeks ago

here we learn to take next step
Hatua Funzo
1 reply · active 78 weeks ago
Blessed be you HatuaFunzo
Nimejifunza kweli kaka angu barikiwa sanaaaaa,Mungu nisaidie tabasamu ndani ya nyuso yangu lizidi
1 reply · active 50 weeks ago
Amen amen rafiki
Nimejifunza kumbe ukitabasamu unaonekana wa tofauti kidogo unakuwa huogopeki na mm nitaanza kujifunza kutabasamu
1 reply · active 48 weeks ago
Migongo Elias's avatar

Migongo Elias · 48 weeks ago

Kwel kabisa you just smile Trice
Kumbe!!! Nitaanza kutabasamu mwalimu wangu 😆😆
1 reply · active 40 weeks ago
Yes inasaidia sana asee
Mhenga bf's avatar

Mhenga bf · 40 weeks ago

Thanks,,nimeadd value kuhusu Siri iliyopo ktk tabasamu.
1 reply · active 40 weeks ago
Ahsante kwa mrejesho, Mhenga bf.
Rachel gakay's avatar

Rachel gakay · 32 weeks ago

Waoooooooh adorable fact🙏
Ubarikiwe

Post a new comment

Comments by

Popular posts from this blog

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

VITU 9 MUHIMU KWA MTU YEYOTE KUJIFUNZA KWENYE MAHAFALI.