HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 23. Ilipoishia...... Alipofika nje, alimkuta Elimina katahamaki sana tena anahasira sana.  "Umefanya nini Elvine? Elimina aliuliza kwa ukali sana tena hadi macho yalikuwa mekundu kama damu kwaajili ya kujaa hasira.... Swali; kwanini Elimina anahasira? Na Elimina huyu anasiri gani na nyumba iliyoungua moto? Kusoma sehemu ya 22 bonyeza hapa   Sasa inaendelea...... Elvine alikuwa anatetemeka  kwa hofu ya yale anayoyaona lakini alistaajabu kuona ni kama mkewe hajali sana kuhusu yeye. Alimtazama kwa makini sana mkewe akiwa anajaribu kutafakari kwanini anaonekana kuwa na hasira juu yake. Elimina akajishitukia "Hey, wewe! Nini sasa unanitazama hivyo?" "Nakutafakari sipati majibu!' "Nimefanyaje kwani?" "Hamna ila sijajua kama umenihofia mimi au hilo swali lako linamaana gani? "Elvine baba sina maana hiyo uliyoelewa wewe kabisa. Shida yangu mimi umefanya nini mpaka unataka kuhatarisha maisha Yako namna hii. Hujui namna ga

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.

Sometimes your joy is the source of your smile, but sometimes your smile can be the source of your joy.” Wakati mwingine furaha yako ni chanzo cha tabasamu lako, lakini pia tabasamu lako linaweza kuwa chanzo cha furaha yako. Tunaishi kwenye dunia ambayo watu wamevurugwa na maisha, huku wakiwa bize au sirious na maisha yao.  kana kwamba kuona tabasamu na furaha yao imekuwa ni adimu sana. kwa kawaida tabasamu na kucheka huwa ni viashiria vionekanavyo katika kuonyesha au kuashiria furaha, licha ya kuwa vipo viashiria vingine lakini tabasamu na kicheko hutafsirika mapema kama viashiria vya furaha. Wakati mwingine mtu anaweza akacheka na kutabasamu lakini akawa na machungu ndani yake goja tuachane nayo leo hii.

Tafti zinaonyesha kuwa mtoto mdogo mwenye umri wa miaka 4-6 hucheka mara 300-400 kwa siku huku mtu mzima hucheka mara 15 tu kwa siku huu ni utafri ambao haujathibitishwa. Lakini kilichothibitishwa ni kwamba kucheka na kutabasamu kunaimarisha maisha yako, afya yako, hali ya ubongo wako na hata ubunifu wako. Pamoja na kwamba kunawatu hucheka na kutabasamu kwa musimu yaani mara chache sana watu hawa ni tofauti sana na watu wanaocheka na kutabasamu mara kwa mara. Kwani huwa ni wepesi wa kusongwa na msongo wa mawazo wakati mwingine hata ugumu wa maisha ingawaje hawezi kusema, hii ni sawa na sumu ndani ya mtu ambayo kiafya siyo nzuri.

Tabasamu kadiri unavyoweza hata kama hauna sababu ya kutabasamu we tabasamu tu, kwani unapotabasamu unapeleka taarifa chanya kwenye ubongo wako ambayo huimarisha utendaji kazi wa ubongo na kuleta furaha zaidi. Kitu kama hichi Marc Reklau amewahi kusema “When you smile your entire body sends out the message “Life is great” to the world.” Tafsiri yake ni kwamba unapo tabasamu mwili wako unapeleka ujumbe “Maisha ni mkuu” kwenye dunia.

Vitu ambavyo huvijui kuhusu kutabasamu ni kwamba;

1.   Ukitabasamu unachilia homoni ya serotonin (ambayo hutufanya tujisikia vizuri). Ndiyo maana mtu akitabasamu anaonekana hanashida wala changamoto.

2.   Ukitabasamu unaachilia homoni ya  endorphins (ambayo hupunguza maumivu). Hii humfanya mtu asahau matatizo na kutua mzigo wa shida zake huku akifurahi na kuondoa stress. Hivi ulisha wahi kuvurugwa ukajisikia maumivu ndani yako, na ukaenda kuangalia hata comedy? Utashangaa kuona unaanza kucheka na kusahau kabisa maumivu yale hii ni kuwepo kwa homoni hii.

3.   Hupunguza mganzamizo wa damu(blood presure). Hii ni kutoka na na kuwepo kwa homoni hizo hapo juu ambazo husaidia kuondosha stress.

4.    Huongeza ufanisi wa utendaji kazi wa kinga ya mwili

5.   Humfanya mtu kuonekana hana shida wala changamoto za maisha.

6.   Humfanya mtu kuonekana mwepesi kufikika na kubadilishana mawazo nae. Watu wa aina hii ni tofauti kabisa na wale wenye kuwa serious muda wote kwani huogopeka sana.

Wana saikolojia husema kuwa tabasamu ni moja ya njia muhimu sana za kuongeza mvuto na ushawishi wa mtu  kwa watu wanao mzunguka, aidha wawe ni wale wanaomfahamu au wasio mfahamu lakini pindi atakapo tabasamu huonekana kama wanafahamiana kabisa. Unaweza kufanya hivyo pindi unapokutana na watu hata ambao hujawahi kukutana nao utashangaa kuona nao wanavyo tabasamu.

Kutabasamu au kucheka siyo lazima na wala mtu asipo tabasamu wala kucheka atakufa hapana! Kutokana na faida hapo juu na nyingine lukuki ambazo hatujazijadili hapa unaweza kuchagua kutabasamu. Kwani hakuna gharama yeyote inayohitajika ili kutabasamu, pili  unapotabasamu unayapa thamani na maana  maisha yako. Kama ni hivyo kwanini usichague kutabasamu na kufurahi hivi kutabasamu na kucheka ni shingapi kwani?

Na kama hujawahi kutabasamu wala hujazoea kabisa unaweza kuanza kutabasamu mara nyingi kadiri unavyo weza napo fanya hivyo kwa kutumia kioo chako  kisha jitazame kabla hujatabasamu. Halafu tabasamu huku ukiwa umejitazama kwa kioo hapo utachagua yule wa kwanza kabla ya kutabasamu na yule wa pili baada ya kutabasamu ni yupi amekaa poa? Kisha fanya hivyo mara kwa mara kila siku.

Pamoja na hayo kuna mahali pa kutabasamu, kucheka na kufurahi na siyo kila sehemu na kila wakati na kwa kila mtu inatakiwa utabasamu. Onyesha kufurahi lakini tambua kuwa kila jambu na wakati wake.

Najua hujatoka kama ulivyo ingia hivyo ulicho kipata anza kukifanyia kazi na kile hujakipenda achana nacho hicho siyo chako.

Rafiki, ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuondokana na adha hii sasa waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii, imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa Mtandao wa addvaluenetwork. Karibu sana ujiongezee thamani yako.

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe.

Instagram>>migongo_elias.

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu, niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe.

 

 


Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.