HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

KANUNI MAKINI YA KUPAMBANIA NDOTO YAKO:

                   

 KANUNI MAKINI YA KUPAMBANIA NDOTO YAKO:

Kuna njia nyingi sana tumeambiwa na kufundishwa kwa namna tofautitofauti sana ilikupambana na maisha yetu hasa katika kuyafikia malengo na mafanikio yetu.na kwa bahati nzuri au mbaya njia hizo zimekuwa zikiwasaidia wengi na wengine kuwahalibia kabisa na wengine kuwaboresha huku wengine zikiwabomoa kabisa .kiuhalisia hakuna njia ambayo imethibitishwa na kutumika kuwa ni njia bora kwa 100% ambayo inaleta mafanikio kwa watu wote kwa kweli bado sijaona.kwasababu njia ambayo ilimfanikisha John akiitumia Anna kwa namna ileile inaweza kumfilisi na kumharibia kabisa,njia iliyo mfilisi Huyu ndiyo itakayo mfanikisha yule.Unaweza ukaambiwa  weka malengo,amka mapema ,weka vipa umbele,fanya kazi kwa bidii,fanya mambo kwa utofauti,fanya kwa ubora,jifunze vitu vipya kila siku ,ajabu ni kwamba unaweza kufanya yote hayo na ukapata matokeo tofauti kabisa na ulivyo tarajia sababu zipo nyingi sana naomba tutaelezana wakati mwingine  lakini leo wacha nikupe hii kwanza.

Pamoja na kwamba hakuna njia ambayo kwa 100% inaleta matoke sawa kwa wote leo nataka nikufundishe njia na kanuni moja ambayo ukiitumia kikamilifu na kwa uaminifu matokeo mazuri  utayapata naamini utanipenda.Kanuni hii imezunguzwa na waandishi kadhaa akiwemo Amos Mwanasaikolojia na mtaalamu wa elimu maalumu.

Na katika kanuni hii nazungumza na mtu ambaye tayari ana malengo na Ndoto zake yaani kiufupi anajua yeye ni nani na anataka kuwa nani .lakini kama wewe huna malengo na hujui unataka kuwa nani mwongozo unakuja siku si nyingi au kwa kuharakisha waweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja naamini nitakusaidia sana kwani wengi wemeripoti kusaika sana. kanuni hii imegawanyika katika sehemu kuu nne kama nilivyo ielezea hapa chini .

a)   KUANGUKA:

Katika safari ya kuyaendea mafanikio yako kuna njia itabidi uipitie na njia hii si nyepesi kama unavyo dhani kwani kuna misukosuko na changamoto lukuki sana ambazo zitakutaka kukata tamaa,kurudi nyuma ,kujihisi huwezi wala husitahili na lengo ni kukufanya usiishi ndoto yako.hizo ni pamoja na maneno ya watu,kufeli,kukosa mtaji,kukosa msaada na mengine mengi.kwa vyovyote vile utaanguka na kufeli mara kadhaa ,nataka kukwambia hii ni sehemu ya maisha na ni hatua muhimu sana katika kuya fikia mafanikio yako kwani hata unao waona wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa hawakuanza juu moja kwa moja na kufika hapo walipo  kwa mbahati mbaya bali walianguka mara nyingi sana wakapalangana hadi kufikia hapo walipo leo.yaani hakuna namna ukakwepa kufanya makosa hapa dunia kikubwa tu usikate tamaa . kwani “makosa yanatuongezea uzoefu na uzoefu unatupunguzia makosa hivyo usiogope kufanya makosa”.

 b)   JIFUNZE:

Kunamsemo mmoja maarufiu sana nao unasema “kama hautajifunza kutokana na makosa/matatizo unayokutana nayo basi utateseka na tatizo moja miaka nenda miaka rudi”.watu wengi wamekuwa na tabia mbaya ya kulaumu na kulalamikia sana matatizo yanapokuja ,ndugu naomba kukutaarifu kuwa matatizo unayokutana nayo yanakuwa yamebeba tahadhari na ujumbe maalumu kwaajili yako.kubwa Zaidi ni kukufundisha kuwa njia hii siyo sahihi hivyo ukipuuzia na kuona kuwa ni upuuzi hutojifunza chochote na badala yake utakuwa ni mtu wa kulalamika kwa kila gumu unalo pitia ,hii itapelekea kuteseka na changamoto hiyohiyo kila wakati.Hivyo penda kujiuliza kwanini hili limenitokea na je nimejifunza nini kutoka katika hili.yaani “failure teaching us a way by showing us which isn’t the way” makosa yanatufundisha njia kwa kutuonyesha njia gani siyo sawa.

c)   INUKA:

Kwasababu kila changamoto na gumu unalopitia linalo funzo na ujumbe maalumu kwaajili yako hivyo jitahidi kupata ujumbe na kujifunza kutokana na ujumbe huo na kisha chukua hatua kwa kuinuka na kuanza tena kwa kasi mpya ,ari mpya na nguvu mpya.kosa ambalo hutakiwi kulifanya ni kuanza upya pasipo kupata funzo kwa kilicho kuangusha ukifanya hivyo utalia na kitu kimoja siku zote za maisha yako.jiulize kitu gani kimenifanya nishindwe kupata nilicho kitarajia kisha kitafute chukua hatua ya kujifunza kwa watu waliofanikiwa,jifunze mtandaoni na jifunze kwa kusoma vitabu kisha pata ufumbuzi na anza upya .kuanguka siyo shida shida ni kubaki umelala pasipo kuanza upya .rafiki anza anza anza anza inawezekana tena.

d)   SONGA MBELE:

Moja ya kitu muhimu unapaswa kukifanyia kazi na kuwa sehemu ya maisha yako ni kusonga mbele yaani kuwa na mwendelezo pale ulipo ishia waingeleza wanasema consistency. kuendelea kufanya kazi kila siku bila kukata tamaa hata kama matokeo hayaji kama ulivyo kusudia kwani utakutana na vitu vingi sana vya kukurudisha nyuma usikubali kukata tamaa.endelea kufanya kazi na ufanyia kazi kila mara.Inawezekana na hapa inatakiwa uwe mtu wa kujifunza kila kukicha kwani ubongo wetu unahitajika kuoshwa na kusafishwa kila siku ili uwe na afya bora kama ilivyo miili yetu vinginevyo kusonga mbele itakuwa ni tatizo kubwa kwako.

Naamini umejifunza kitu ni furaha yangu kuona umesaidika katika hili na kuona ukisonga mbele katika maisha yako. Hivyo katika safari ya kuyafikia mafanikio yako utakutana na magumu,makosa,changamoto nyingi sana ili zikurudishe nyuma na pengine utaanguka mara kwa mara tena hata mara nyingi sana ,kama ni ndoto yako kweli nakusihi usikubali kubaki umeanguka hakikisha unajifunza kwa changamoto hiyo kisah anza upya tena inuka kwa kasi mpya,ari mpya na nguvu mpya rafiki! usikate tamaa hadi itokee mwisho kabisa kuwa mtu wa kuendelea mbele kila siku songa mbele pambana kila siku uwe bora kuliko jana  utatoboa .

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia,Uchumi na Maisha.  Mwanzilishi na Mwendeshaji wa   mtandao wa addvaluetz  karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Sim na Whatsapp >>+255783327456 / +255767653697.

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu,niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe.

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.