HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

SAMEHE KWA FAIDA YAKO MWENYEWE!.


  SAMEHE KWA FAIDA YAKO MWENYEWE.

Mtu mmoja alisikika akisema nimekusamehe lakini sitakusahau katika maisha yangu kwa hichi ulicho nitendea!

Kama utakuwa mfuatariaji na mdadsi wa mambo na watu utagundua kuwa suala la kusamehe limekuwa ni changamoto kubwa sana kwa watu wengi. Wengi wamebaki na vinyongo, visasi, machungu, na hasira kupita kiasi kuhusu ulio  wakosea au kutokuwasamehe.

Mwalimu mmoja aliwaagiza wanafunzi wake kila mmoja aje na nyanya kulingana na idadi ya watu anaowachukia. Wanafunzi walikuja nazo siku iliyofuata, wengine walikuja na nyanya moja, wengine mbili, wengine tano, na wengine nyanya za kutosha  na walipo kuja nazo aliwaambia waandike  majina ya watu wanaowachukia ko, waziache kwenye mikoba yao na mwalimu aliwaambia watakuwa wanakuja nazo kila siku bila  kuzitupa au kuziacha. Baada ya siku kadhaa wanafunzi walianza kulalamika kuwa mzigo umekuwa mzito na umekuwa ni ngumu kuja nao kwani zilikuwa zimeshaanza kuoza na kunuka hivyo yalikuwa yanaharibu daftari zao na walimwomba sana mwalimu wao awaambie wayatupe ili kuepuka kuchafuka na kuharibu daftari zao halafu kwanza mzigo ulikuwa ni mzito hasa kwa wale waliokuja na nyanya nyingi. 

Hivyo ndivyo ilivyo hata katika maisha ya kawaida kumchukia mtu ni kujibebesha mzigo mzito sana ambao hata wewe mwenyewe kuubeba ni taabu sana. Na kushindwa kusamehe ni sawa na kunywa sumu wewe ili afe mtu mwingine. Hiki kitu hakiwezekani. Linapokuja suala la kusamehe tunasamehe kwa faida yetu wenyewe hata kama waliotukosea ni wao.

Tatizo kubwa la watu hasa linapokuja suala la kusamehe, wengi wanashindwa kufanya hivyo kwasababu wanajua kuwa watawanufaisha wengine na matokeo yake wana baki na vinyongo, hasira, na chuki ya kudumu mioyo mwao. Ndugu yangu, hapa ni sawa na kunywa sumu ili afe unayemchukia, katika hili utasubiri sana, hasa ukikutana mtu kama mimi ambaye huwa sijali unisamehe au usinisamehe ni sawa tu, lakini ni lazima nije kukuomba msamaha kiroho safi kabisa sasa suala la kusamehe ni lako juu yako  mwenyewe.

Kusamehe ni kujipenda mwenyewe . Haijarishi mtu amekutenda makubwa kiasi gani jukumu la kuomba msamaha ni lake ndiyo lakini,  wajibu wako wewe ni kusamehe. Ndiyo maana hata maandiko yanasema samehe saba mara sabini, hiki ni kiwango kikubwa saba cha kusamehe lakini maana yake ni kwamba tunalo jukumu la kusamehe kila tunapo hitajika kufanya hivyo. Pamoja na kusamehe pia tunatakiwa kuomba msamaha kwa kila tunapokosea au kwenda kinyume. Samahani ni neno dogo sana lakini matokeo yake ni makubwa sana. Kipindi tunasoma hiki kitu tulikiita msuli sisimizi matokeo tembo yaani unasoma kidogo tu unafauli sana kama vile jiniazi ani.

Ukishindwa kusamehe unajizibia Baraka na utashindwa kufungua ukurasa mpya. Ili kuanza upya unahitaji kuachilia maumivu vinyongo na hasira hapo ndipo utaanza ukurasa mpya. Sasa swali la kujiuliza utawezaje kuanza ukurasa mpya hali ya kwamba bado umeng’ang’ania ukurasa wa zamani hiki kitu ni ngumu kutokea.

Mwandishi mmoja alisema when we begin to release the negative emotional we begin to release pains. Yaani, tunapoanza kuachilia mawazo hasi tunaanza kuachilia maumivu.

Joel nanauka anasema “Unaposamehe haimaanishi kuwa unakubaliana na makosa uliyofanyiwa ila inamaanisha unajua umuhimu wa kuanza upya na kusonga mbele kwenye maisha yako”.

Usiposamehe hutauona ufalme wa Mungu. Watu wengi tunasubiria kuuona ufalme wa Mungu kwa namna yoyote ile hata kwa kuchelewa sana ilimradi tu! tufike lakini ukweli ni kwamba tabia ya kusamehe ni ya Mungu mwenyewe na Mtu asipo samehe hatauona ufalme wa Mungu soma utusamehe deni zetu kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu (mathayo 6:12).

Rafiki yangu kusamehe ni kwa faida yako. William Shakespeare alisema, “Tusitwishe mzigo mzito kumbukumbu zetu kwa jambo zito ambalo limepita”. Jambo likisha fanyika huwezi kulibadilisha kwa kubadilisha matokeo yake badala yake ni kujipanga umpya kwa kugundua ni wapi umekosea na kisha kurekebisha.

Oprah Winfrey, aliposema: “Learn to Forgive and Let it go” (Jifunze kusamehe na kuachilia). 

Pamoja na kuwepo kwa maumivu makali sana ya kuwasamehe watu lakini pia suluhisho kubwa katika hili ni kusamehe na kuachilia hii ni njia moja ya kupatau ponyaji wa kudumu ili usonge mbele.

Unaposamehe haimaanishi kuwa unakubaliana na makosa uliyofanyiwa ila inamaanisha unajua umuhimu wa kuanza upya na kusonga mbele kwenye maisha yako.

Jaribu Leo kukumbuka kila mtu ambaye unajua hujamsamehe na umekuwa na kila sababu ya kutokumsamehe. Tangaza msamaha katika moyo wako, kisha tangaza msamaha kwa kusema pia kwa kumtaja jina: “  fulani, nimekusamehe.”. 

Nipende kukujuza kuwa unaposamehe haimanishi kuwa hautasahau, hapana kusamehe unasamehe kwa moyo wote sema tukio hilo litabaki kama kumbu kumbu kama yalivyo matukio mengine ya kufurahisha au kuhuzunisha hatujayasahau hadi leo na hii haimaanishi kuwa hatuja samehe ,tunasamehe lakini ubongo sababu kazi yake ni kutunza kumbukumbu basi tukio hilo ni ngumu kufutika hivyo kukumbuka tukio husika hakuhusiani kabisa na kusamehe .

Tambua kuwa watu dhaifu hawawezi kusamehe, kusamehe ni ishara ya ujasiri, na wewe ni mtu jasiri.

samehe kwa faida yako. 

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri &Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha.  Mwanzilishi na Mwendeshaji wa   mtandao wa addvaluetz  karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Sim na Whatsapp >>+255783327456 / +255767653697.

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu,niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe. 

 

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.