KAMA UNASAHAU MARA KWA MARA, SOMA HAPA KWANZA.

Image
  KAMA UNASAHAU MARA KWA MARA, SOMA HAPA KWANZA. Boss! Siyo  kila mara, kusahau ni ishara ya Ubongo dhaifu, mara nyingi ni namna tunavyojifunza ndugu. Nimekutana na watu wengi wakisema: "Mimi sina akili kubwa." Wengine "Kumbukumbu yangu ni mbaya." Mara "Ubongo wangu hauhifadhi vitu." Lakini ukweli ni kwamba, mara nyingi tatizo si ukubwa wa akili yako wala uwezo wa ubongo wako. Tatizo ni kwamba watu wengi hawajawahi kufundishwa jinsi kumbukumbu (memory) inavyofanya kazi boss. Sikia ndugu; Ubongo wa binadamu umeumbwa kwa ustadi mkubwa. Kazi yake si kuhifadhi kila kitu unachokiona au kukisikia, bali ni kuchagua filtering taarifa muhimu na kuacha zisizo muhimu wala matumizi. Kwa hiyo, kusahau si kasoro ya ubongo ni sehemu ya kawaida ya jinsi unavyofanya kazi. Hebu tuangalie sababu kuu zinazowafanya watu kusahau mara kwa mara. 1. Kukariri Bila Kuelewa (memorising without understanding). Hili ndilo kosa kubwa zaidi ambalo wanafunzi na hata watu wazima...

MFANO WA FAMILIA YA KUIGWA.

MFANO WA FAMILIA YA KUIGWA.
Ngazi ya familia ni ngazi muhimu sana kwa maendeleo ya Kila mtu. Pamoja na kuwepo ngazi nyingi na kubwa pengine kuliko hata familia, kwa  mfano tunazo ngazi kama Makundi au marafiki ,Shule /vyuo, jamii, Taifa n.k. ngazi ya familia bado ni ngazi muhimu sana katika kutengeneza malezi na mwongozo bora kwa mtoto ili kuyafikia malengo na maono yake. 

Lakini asilimia kubwa familia nyingi hazija litambua hili, kwani utajikuta baba yuko bize na kazi zake kweli kweli mama naye ndo kwanza ni yeye na vikoba  hata kaka na dada wanapo kuakua tu Kila mmoja anajua yake house gelo ndo mama, baba, dada na kaka wa watoto yeye ndo anajua wale nini wavaaje. Na wengine kuepuka taharuki zote hizo mtoto akifikisha miaka miwili tu anapelekwa boarding au nursery akajifunze kimombo ili kuja kuwakera wazazi na na wengine kwa kuwasemesha kingereza mwanzo mwisho akati hawakijui hata!, na kwa jeuri sasa nao wanatamba kweli mtaani kuwa mtoto ana mwaga ngeli balaa hahahaha!.

Sipingi kitu kama hichi lakini, ukweli ni kwamba kama familia, kuna mahali kuna muyumbo fulani, lazima tukubali yaani inafika wakati wazazi hawajui chochote kuhusu mtoto wao. Wanachojua ni kutoa hela ya twisheni, pipi na maandazi lakini, tukija kwa swala zima la kumfahamu mtoto wao kiundani bado ni kimbembe na matokeo yake wazazi wana walazimisha watoto wao kwenda kusoma na kusomea vitu vya ajabu kweli ambavyo hata wao wenyewe tu hawavijui kabisa.Tunapata kesi za  ajabu kweli yaani eti kisa mzazi anapenda kitu fulani na, alishindwa kikitimiza ndo anataka watoto wake waje wamtimizie,  hii inakubalika kweli jamani. Mimi nasema Hiki kitu hakikikubaliki kabisa Kwani "WATU HATUFANANI NA HATUWEZI KUFANANA". Ni muhimu kujua kwamba kila mtu ana ndoto yake na ipo tofauti kabisa na mtu mingine. Wazazi kuna mahala wana kwama kabisa imefika wakati Kila majukumu kuhusu watoto wao wamewaachia waalimu na watu wa mitaani kuwafahamu na kuamua, na kutengeneza hatima za wanao hili ni tatizo kubwa sana aseee. 

Sasa naandiki hivi mzazi wa  familia yenye KUIGWA kiujumla unayo kazi ya kushughulika na watoto wako in and out yaani, nje na ndani kwa sababu ipo sababu kubwa sana ya mtoto wako kupitia kwako hadi ukamzaa kuna watu wengi sana wanamlilia na kumwomba Mungu awape watoto lakini Mungu aliona kuwa wewe unafaa kumlea na kumsaidia mtoto huyo kutimiza kusudi la kuumbwa kwake. Kwani kuna uwezekano mkubwa sana kuwa angezaliwa kwingine na mtu mwingine kabisa .Goja nikuulize swali hivi wazazi wa Obama , Magufuli, Mesi na watu wengine mashuhuri walikuwa wanajua kuwa mtoto wao atakuja kuwa  raisi au mchezaji maarufu ulimwenguni???.na kama wangekuwa wanafahamu wangewalea kama wazazi wa leo wanavyo walea na kuwatwisha majukumu yao watu wengine??. 

Rafiki familia na wazazi wa KUIGWA ni wale ambao wanawasaidia watoto wao kujifahamu, kujitafuta, kujitambua, na kujua kusudi la kuumbwa kwao katika ulimwengu huu, mikakati na njia lukuki  za kuzifikia ndoto zao.

Wanafanya hivi kwa kuwajengea hofu ya mungunidhamu ya fedha, muda, Kujifunza maarifa mapya kila wakati, tabia ya kusomea nao vitabu hapa ndipo kuna siri kubwa goja tutalijadili siku nyingine hili. Pia wanahakikisha wanakuwa nao kwa ukaribu sana kwa kujua nini wanapenda na kipi hawapendelei yaani ukiwa mzazi wa namna hii utayafanya maisha yawe mepesi sana asee, si unajua hawajui wao ni akinanani na wapo hapa kwa Dunia kufanya nini hii issue imekuwa gumuzo mtaani na watu maisha hayaendeki kwa sababu watu hawajui ndoto na hatima zao na wazazi  wanaishi kama wanyama wengine  kwakweli wanachochea sana moto huu na hii ni shida sana tubadilike jamani.

Je ungependa kuwa mzazi wa familia yenye KUIGWA?? Fanya hayo mambo ya familia zenye kuigwa hufanya  na matokeo utayapata naamini utanipenda.

Mungu akubariki sana nakutakia familia yenye heri kwako.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa  mtandao wa addvaluetz  karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Sim na Whatsapp >>+255783327456 / +255767653697.

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu,niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe


Popular posts from this blog