UKIDHIBITI MANENO YAKO, UTAANZA KUDHIBITI MAISHA YAKO.

Image
  UKIDHIBITI MANENO YAKO, UTAANZA KUDHIBITI MAISHA YAKO. Watu wengi hudharau nguvu ya maneno. Wanafikiri maneno ni sauti tu zinazopita. Lakini ukweli ni kwamba: Maneno yana nguvu ya tena nguvu ya; kujenga au kubomoa, kuponya au kuumiza, kuhamasisha au kudhoofisha, na hata kubadilisha kabisa maisha ya mtu boss. Inshort Nguvu ya Maneno Yako Inaweza Kujenga au Kuharibu Maisha Yako au ya watu wengine. Ndiyo maana kuna dhana muhimu sana inayoitwa “Impeccable Word” yaani kutumia maneno kwa uangalifu, ukweli, uadilifu na usafi wa ndani boss. Kwa lugha rahisi: 👉 kuwa mwangalifu na kile unachosema kwa wengine na kwa nafsi yako mwenyewe. Boss najua bado unajiuliza IMPECCABLE WORD NI NINI HASA kama nikivyolitumia hapo juu? Vizuri nami nitajibu, Kwa lugha rahisi ni: kusema ukweli, kutotumia maneno kuharibu wengine au kujiharibu mwenyewe,  kutosengenya, Kuepuka lugha ya sumu, kutosema vitu usivyoamini au kutokujiharibu mentally kupitia maneno yako mwenyewe boss. Si unajua wewe...

MFANO WA FAMILIA YA KUIGWA.

MFANO WA FAMILIA YA KUIGWA.
Ngazi ya familia ni ngazi muhimu sana kwa maendeleo ya Kila mtu. Pamoja na kuwepo ngazi nyingi na kubwa pengine kuliko hata familia, kwa  mfano tunazo ngazi kama Makundi au marafiki ,Shule /vyuo, jamii, Taifa n.k. ngazi ya familia bado ni ngazi muhimu sana katika kutengeneza malezi na mwongozo bora kwa mtoto ili kuyafikia malengo na maono yake. 

Lakini asilimia kubwa familia nyingi hazija litambua hili, kwani utajikuta baba yuko bize na kazi zake kweli kweli mama naye ndo kwanza ni yeye na vikoba  hata kaka na dada wanapo kuakua tu Kila mmoja anajua yake house gelo ndo mama, baba, dada na kaka wa watoto yeye ndo anajua wale nini wavaaje. Na wengine kuepuka taharuki zote hizo mtoto akifikisha miaka miwili tu anapelekwa boarding au nursery akajifunze kimombo ili kuja kuwakera wazazi na na wengine kwa kuwasemesha kingereza mwanzo mwisho akati hawakijui hata!, na kwa jeuri sasa nao wanatamba kweli mtaani kuwa mtoto ana mwaga ngeli balaa hahahaha!.

Sipingi kitu kama hichi lakini, ukweli ni kwamba kama familia, kuna mahali kuna muyumbo fulani, lazima tukubali yaani inafika wakati wazazi hawajui chochote kuhusu mtoto wao. Wanachojua ni kutoa hela ya twisheni, pipi na maandazi lakini, tukija kwa swala zima la kumfahamu mtoto wao kiundani bado ni kimbembe na matokeo yake wazazi wana walazimisha watoto wao kwenda kusoma na kusomea vitu vya ajabu kweli ambavyo hata wao wenyewe tu hawavijui kabisa.Tunapata kesi za  ajabu kweli yaani eti kisa mzazi anapenda kitu fulani na, alishindwa kikitimiza ndo anataka watoto wake waje wamtimizie,  hii inakubalika kweli jamani. Mimi nasema Hiki kitu hakikikubaliki kabisa Kwani "WATU HATUFANANI NA HATUWEZI KUFANANA". Ni muhimu kujua kwamba kila mtu ana ndoto yake na ipo tofauti kabisa na mtu mingine. Wazazi kuna mahala wana kwama kabisa imefika wakati Kila majukumu kuhusu watoto wao wamewaachia waalimu na watu wa mitaani kuwafahamu na kuamua, na kutengeneza hatima za wanao hili ni tatizo kubwa sana aseee. 

Sasa naandiki hivi mzazi wa  familia yenye KUIGWA kiujumla unayo kazi ya kushughulika na watoto wako in and out yaani, nje na ndani kwa sababu ipo sababu kubwa sana ya mtoto wako kupitia kwako hadi ukamzaa kuna watu wengi sana wanamlilia na kumwomba Mungu awape watoto lakini Mungu aliona kuwa wewe unafaa kumlea na kumsaidia mtoto huyo kutimiza kusudi la kuumbwa kwake. Kwani kuna uwezekano mkubwa sana kuwa angezaliwa kwingine na mtu mwingine kabisa .Goja nikuulize swali hivi wazazi wa Obama , Magufuli, Mesi na watu wengine mashuhuri walikuwa wanajua kuwa mtoto wao atakuja kuwa  raisi au mchezaji maarufu ulimwenguni???.na kama wangekuwa wanafahamu wangewalea kama wazazi wa leo wanavyo walea na kuwatwisha majukumu yao watu wengine??. 

Rafiki familia na wazazi wa KUIGWA ni wale ambao wanawasaidia watoto wao kujifahamu, kujitafuta, kujitambua, na kujua kusudi la kuumbwa kwao katika ulimwengu huu, mikakati na njia lukuki  za kuzifikia ndoto zao.

Wanafanya hivi kwa kuwajengea hofu ya mungunidhamu ya fedha, muda, Kujifunza maarifa mapya kila wakati, tabia ya kusomea nao vitabu hapa ndipo kuna siri kubwa goja tutalijadili siku nyingine hili. Pia wanahakikisha wanakuwa nao kwa ukaribu sana kwa kujua nini wanapenda na kipi hawapendelei yaani ukiwa mzazi wa namna hii utayafanya maisha yawe mepesi sana asee, si unajua hawajui wao ni akinanani na wapo hapa kwa Dunia kufanya nini hii issue imekuwa gumuzo mtaani na watu maisha hayaendeki kwa sababu watu hawajui ndoto na hatima zao na wazazi  wanaishi kama wanyama wengine  kwakweli wanachochea sana moto huu na hii ni shida sana tubadilike jamani.

Je ungependa kuwa mzazi wa familia yenye KUIGWA?? Fanya hayo mambo ya familia zenye kuigwa hufanya  na matokeo utayapata naamini utanipenda.

Mungu akubariki sana nakutakia familia yenye heri kwako.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha. Mwanzilishi na Mwendeshaji wa  mtandao wa addvaluetz  karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Sim na Whatsapp >>+255783327456 / +255767653697.

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu,niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe


Popular posts from this blog

UKIJUA HILI KUHUSU WATU UTAFANIKIWA SANA.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29