HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

NJIA 7 ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

 


NJIA ZA KUOSHA UBONGO WAKO.

Hivi ulisha wahi kwenda hospitali na kupata ushauri wa daktari juu ya afya ya mwili wako? Au basi ulisha wahi kumsikia mtu yeyoye pengine rafiki, ndugu, mke, kaka yako au mtu yeyote akisimulia kuhusu ushauri wa daktari katika kutunza na kuimarisha afya ya mwili wake? 

Bila shaka ulisha wahi na kama bado usihamaki, kwani utaelewa tu. 

Ukweli ni kwamba mara nyingi watu wamekuwa na utaratibu wa kwenda hospitali kwaajili ya afya za miili yao na hapo watapewa dawa za kutosha, ili kujiponya na malazi yanayo wasibu. 

Na mara nyingi hupewa dawa za kutumia, wengine huchomwa  sindano, wengine kupewa masharti ya namna ya kutumia dawa hizo wengine huambiwa kula baadhi ya vyakula wengine mazoezi n.k

Kwa kawaida mwanadamu ameundwa na sehemu kuu mbili, nazo ni utu wa nje na utu wa ndani

Utu wa nje ndio huu mwili ambao unashikika yaani, huu mwili wa damu na nyama. 

Ili kuuimarisha mwili huu wanadamu wamekuwa wakifanya vitu kama mazoezi, kula vizuri na vitu vinavyofanana na hivyo.

Sasa kama ilivyo katika utu wa nje ambao umeundwa na damu, nyama, mifupa na misuli, ndivyo ulivyo na utu wa ndani huu unaundwa na akili (mind) ambao kiungo chake muhimu ni UBONGO

Hii ni sehemu muhimu sana katika mwili wa mwanadamu kadharika nayo inahitaji kuwepewa lishe bora , kufanyishwa mazoezi yaimarishayo na kuoshwa kwa maji safi na salama.

Pia nichukue nafasi hii kukujuza kuwa mwanadamu yeyote anahitaji kuwa na aina kuu tatu za afya nazo ni afya ya akili, afya ya mwili na afya ya Roho yake mwenyewe. 

Leo tutazungumzia sana afya ya akili ambayo ni muhimu sana mtu kuwa nayo katika kutimiza malengo na kufikia ndoto yake. Kwa kuwa afya hii ya akili imebebwa na inategemea sana kiungo ubongo tutakwenda kuzungumza njia mbalimbali ambazo mtu anaweza kuzitumia ilikuosha akili iliyo ndani ya ubongo wake  yaani, namna gani utaweza kuusafisha ubongo wako kama kiungo kibeba akili yako.

Ili ubongo na akili yako viweze kufanya kazi ipasavyo vinahitajika kusafishwa na kuoshwa kwa njia mbalimbali. 

Hivyo zifuatavyo ni njia lukuki zitakazo kusaidia ili kuiosha akili yako nazo ni;

1.   KULA CHAKULA NA LISHE BORA;

Kama ilivyo kwa mwili unahitaji sana rishe bora ili kuuimarisha, kadharika  akili inahitaji rishe na chakula bora kuiimarisha. 

Kwani, kuna vyakula vingi sana vimeripotiwa kutibu magonjwa ya akili na kuongeza utendaji kazi wa akili katika ubora wake. 

Vyakula kama matunda, mbogamboga, carbohaydrate na vyakula vingine. Kama vikiliwa kwa utaratibu husaidia sana kuimarisha afya ya mwili ambayo inamahusiano ya moja kwa moja na afya ya akili pengine baadhi ya vyakula vina matokeo ya moja kwa moja katika akili kwa kuimarisha misuli ya ubongo ambao ndiyo nyumba ya akili. 

2.   KUJIFUNZA VITU VIPYA.

Kadiri mtu anvyo jifunza vitu vipya kila siku na kila wakati, ubongo wake unazalisha hormone kama vile endorphins na dopamine ambazo husaidia sana katika uzalisha na kuchochea furaha katika mwili wake ambayo husaidia kuondoa mawazo na msongo wa mawazo katika maisha yake.

 Kadri uanavyokuwa na furaha ndivyo ambavyo ubongo wako unakuwa huru  katika kufanya kazi. 

Kwa hiyo kadiri unavyojifunza au kufanya vitu vipya na kuvifanikisha ubongo wako unakuwa katika hatua nzuri sana ya kusonga mbele na kuwa na afya njema.

 Hivyo ndugu kuwa na utamaduni wa kujifunza kitu kipya kila siku. 

Fanya hivi kwa kuuliza watu,kusoma mtandaoni,kusoma vitabu, kutembea, kusikiliza muziki, kuhudhuria semina na kuyafanyia kazi yale utakayojifunza, matokeo utayapata mwenyewe.

                       3.   KUTAFAKARI

Kutafakari ni kufikiri kwa utulivu na umakini kuhusu jambo fulani hasa unapo lenga kujifunza zaidi au kupata suluhisho juu ya changamoto inayo kuhusu . 

Wagojwa wengi sana marekani wameripotiwa kutibiwa kutokana na kutafakari kwa umakini na kwa kiina.njia hii huipa majukumu ubongo ya moja kwa moja katika kulijua na kulitatua tatizo husika . 

Kwa hiyo tafuta sehemu tulivu ili kuzungumza na akili yako na utashangaa utakavyoona unapata mawazo makubwa na suruhu bora kuwahi kutokea. 

kwani kwa kawaida katika kila dakika mwanadamu kuna zaidi ya maelfu ya mawazo ambayo humujia.Na njia rahisi ya kuya faidi ni kupitia kutafakari . 

Fanya kutafakari kuwa ni utaratibu wako kila siku  kwa kutafuta sehemu tulivu au fanya hivyo usiku wakati wengine wamelala kama matajiri na mabilionea wafanyavyo hapa dunia. 

4.   MICHEZO NA MAZOEZI YA VIONGO.

Nji mwili wako unavyopata mazoezi ya viungo ndivyo unavyozidi kutanua na kuimarisha misuri yake. hii inafanya mtu kuwa na furaha muda mwingi.  

Kama afya yako ya mwili ikiimarika hata misuli ya ubongo nayo huimalika. Na swala linguine hapa ni michezo.

Michezo ya pamoja kama mpira kuimba kuigiza, kucheza magemu huchangia sana kuifanyisha mazoezi akili yako.

Hivyo ndugu chagua kuimalisha afya yako ya ubongo kwa kufanya mazoezi walau mara 4 kwa wiki itakusaidia sana kwani mazoezi huimaliza misuli na kuondoa uzembe usio wa lazima . 

Asilimia kubwa ya wakurugenzi mahili duniani hufanya michezo na mazoezi ya viungo wanajua siri hii fanya hivyo na wewe leo. 

5.   KUTATUA MATATIZO NA KUFANYA MAZOEZI YA UBONGO.

Mtoto mmoja alikuwa akipewa kazi ngumu na kuwafanyia maswali magumu ya home work watoto wenzake alikuwa akifanyiwa hivyo na mama wa kambo na lengo kubwa ilikuwa ni kumkomoa. 

Lakini kadri muda ulivyozidi kusonga ndivyo alivyokuwa na uwezo mkubwa sana wa kukabiliana na matatizo na changamoto za maisha na watoto wengine waliokuwa wanadekezwa walikuwa na uwezo mdogo sana  wa akili. 

Hii itoshe tu kusema kadri unavyo tatua changamoto kubwa na nyingi kwenye maisha yako ndivyo unavyo ongeza uwezo wako wa kufikiri . 

Na kitu kingine katika hili ni kufanya mazoezi ya akili na ubongo , ubongo wako unaweza ukaufanyisha mazoezi kama vile kuvuta kumbu kumbu ya matukio ya nyuma na majina ya watu, kucheza magemu magumu, kutafakari na kujifunza lugha mpya hii itakusaidia sana. 

6.   KUULIZA MASWALI NA KUWA MDADSI

Uchunguzi ulifanyika na kuonyesha kuwa watu wenye akili na ubongo makini wanatabia zinazofanana kabisa, ile tabia ya kuwa wachunguzi wa mambo na wanasifa ya kuuliza maswali sana. 

kitu hiki kimedhibitishwa kuwa ni moja ya njia ya kujifunza vitu vipya kutoka kwa watu na mazingira mbalimbali ambapo hali hii humfanya mtu kuongeza uwezo wa akili yake kuweza kufanya kazi vizuri. 

Hivyo ndugu yangu kama unataka na wewe kula meza moja na watu wanao upiga mwingi katika maswala haya jifunze kuwa mdadsi, uliza maswali itakusaidia kuwa na taarifa nyingi na kufahamu vitu vingi vitakavyo kufanya kuwa mtu muhimu sana kwa dunia ya leo si unajua dunila ya sasa ni dunia ya taarifa, ujuzi na maarifa neeh!

7.   SOMA VITABU NA MAKALA MBALI MBALI.

Kipengele hiki kwa kawaida kilitakiwa kiwe katika ile point ya kujifunza ,lakini kutokana na umuhimu na uzito wake wacha tuipe mji ijitegemee. 

Rafiki njia rahisi ya kujifunza kwa makosa ya watu walio tutangulia ni kusoma vitabu. kurudia makosa ambayo watu wengi huko nyuma waliyafanya huku ungeweza kuyaepuka kwa kusoma vitabu huu ni ujinga. 

kama tunavyojua kuwa chanzo kikubwa cha taarifa na maarifa ni kwenye maandishi ingawa vipo vyanzo vingi lakini hii imeshika hatamu kutoka enzi na enzi.

 kusoma vitabu kutakuongezea wingi wa maarifa, utajifunza vitu vipya vingi, utatatua matatizo yako, utakula meza moja na wasomi, wanasheria, waalimu, wajasiliamali, wandishi na watu mashuhuri waliopita. 

Hii nayo itakupa furaha na kukupunguzia msongo wa mawazo kwa kuwa msongo wa mawazo una athari kubwa sana katika akili na ubongo wa mwanadamu.

Na isitoshe tabia hii inapunguza msongo wa,mawazo kwa 68%. Nikushauri tu rafiki jenga tabia ya kusoma vitabu hautakuja kujuta kamwe watu wengi walioshindikana wameripoti kubadilishwa kabisa kupitia kusoma vitabu. 

Ifanye kuwa ni tabia ya pili ya maisha yako na kama unachangamoto katika hili naomba wasiliana na mimi moja kwa moja naamini utasaidika. 

Ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu rafiki!

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi, maendeleo binafsi na Maisha.  

Mwanzilishi na Mwendeshaji wa   mtandao wa addvaluenetwork.  

karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Sim na Whatsapp >>+255783327456 / +255767653697.

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS|| Add Value Network.

Kama umejifunza kitu,niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe. 

 

 

 

Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.