HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

KWANINI UNATESEKA NA MADENI YASIYO KOMA?

 

KWANINI UNATESEKA NA MADENI YASIYO KOMA? 

Kabla ya kwenda mbali Zaidi ni muhimu tujue maana ya maneno haya mawili nayo ni Mkopo na Deni. Mkopo ni aina ya fedha ambayo mtu au taasisi inachukua  kutoka kwenye chanzo kingine cha fedha kwa masharti fulani ya kurudisha fedha hizo kwa muda fulani na kwa kiwango cha riba. Mkopo unaweza kutolewa na benki au taasisi nyingine za kifedha, serikali, au hata mtu binafsi. Sasa pale mtu anaposhindwa kutimiza masharti na makubaliano ya mkopo huo. Hapo ndipo inageuka na kuwa deni  na kwa wingi ni madeni. Madeni si mabaya sana, kama yatakuwa yamefanyika kwa utaratibu maalum wa lengo la kuongeza thamani yake kila baada ya muda fulani. Lakini, kama si hivyo yatakuwa ni mabaya sana kuwahi kutokea.

Pamoja na hayo zipo sababu nyingi sana zinazowapelekea watu wengi kuingia kwenye madeni yasiyoisha na mbaya zaidi wamefanya kila linalowezekana ili kuondokana na madeni hayo lakini imekuwa changamoto isiyoisha kwao. Hili nalo bado ni tatizo kubwa sana. Leo nataka nikushirikishe sababu ambazo watu wengi zimewapelekea kuingia kwenye madeni yasiyo isha. Na sababu hizi, zimezungumzwa na waandishi mbali mbali ndani na nje ya nchi akiwemo Joel nanauka kwenye kitabu chake cha jinsi ya kuondokana na madeni. na wengine wengi hivyo soma hadi mwisho naimani utasaidika sana.

SABABU ZINAZO SABABISHA WATU KUINGIA KWENYE MADENI YASIYO KOMA. 

1.   KUISHI JUU YA KIPATO CHAKO.

Kwa kawaida kadiri unavyoongeza kipato ndivyo na matumizi yako yanazidi kuongezeka zaidi. Angalia tu hata katika maisha ya watu waliokuwa na kipato cha kawaida walikuwa na matumizi na wailiishi maisha ya kawaida sana, Lakini, kadiri vipato na pesa zao zinavyozidi kuongezeka na matumizi yao yanazidi kuongezeka pia. Hiki kitu ndicho alichokizungumzia bwana parkson mtaalamu wa masuala ya fedha. Watu wengi wamekuwa wakiishi katika kundi hili, yaani pesa kidogo tu ashabadilisha kila kitu anabadili mighahawa ya kula ,anasomesha shule za gharama kuliko uwezo wake ,anaanza kujionyesha kuwa tayari yeye kashafanikiwa, anatumia na kuishi maisha ya juu sana kwa kuwaonyesha watu kuwa ashafanikiwa tayari, hali hii ni mbaya na imesababisha watu wengi kuingia kwenye madeni yasiyoisha .

Ndugu yangu usipende kujipandisha hadhi na kuishi juu ya uwezo wako. Hivyo, Inakupasa uishi chini ya kipato chako pia ishi maisha kulingana na hali yako ya sasa. kwani maisha unayo yatamani na kuyaigilizia utayafikia tu kama utafanya kazi kwa bidii na ubora.

2.    KUZOEA MADENI.

Kuna watu wameyazoea madeni na kuyafanya kuwa ni sehemu ya maisha yao. Utakuta mtu kila kitu yeye ni kukopa tu. Hela ya kalo ana kopa , chakula anakopa, bili za maji, umeme anakopa hela ya nguo anakopa yaani, ameshakuwa mtu wa kuhamisha deni kutoka kwa mtu huyu na kwenda kwa mdeni mpya. Na wengine wana misemo yao kabisa wakisema “hata mabilionea wenyewe wana kopa” mwingine utakuta anasema kama nchi inadaiwa trioni kadhaa mimi ni nani nisikope ?? Rafiki mikopo siyo mibaya tatizo ni kwamba, unakopa kwaajili ya nini? Kama mkopo wako haukuzalishii pesa au faida yeyote labda ni kwaajili ya matumizi ya kawaida tu mfano kulipa ada,kodi madeni n.k hapo jiandae kuingia kwenye dimbwi kubwa la madeni.

3.   ULEVI WA POMBE.

Tunawafahamu watu wengi kwenye mazingira yetu ambao wao pombe imekuwa kisukumo kikubwa Cha kuingia kwenye madeni lukuki. Tafiti zinaonyesha kuwa watu wengi wanaojihusisha na ulevyi wa pombe imekuwa ngumu sana kwao kuendelea katika maendeleo yeyote yale hii  ni kwasababu pombe inaathiri ubongo wa binadamu moja kwa moja, ndiyo maana walevi wengi hupoteza uwezo wao wa kumbu kumbu, uwezo wa kufikiri , uwezo wa kupanga mipango ya maendeleo na mafanikio yao, yaani anakuwa anawaza pombe tu anakuwa katika URAIBU, Hapo anaweza kukopa kwaajili ya pombe anaweza kuuza mali na vitu vyake vya thamani kwaajili ya pombe hali hii ni mbaya sana na mtu wa namna hii inampasa abadilishe sehemu za kutembelea na marafiki wa kuambatana nao na kama tatizo litakuwa kubwa sana watafute wataalamu wa saikolojia  au wasiliana nami moja kwa moja kwa mawasiliano hapo chini kwa msaada zaidi. 

4.   KUSHINDWA KUSEMA HAPANA.

Steve jobs mkurugenzi na mwanzilishi wa kampuni ya APPLE aliulizwa nini maana ya focus alijibu na kusema “focus ni uwezo wa kusema hapana kwa mambo ambayo yapo nje na malengo yako”.

Watu wengi sana wemeingia kwenye madeni ya kuwatosha kwasababu tu ya kushindwa kusema hapa. Wengine wamelazimishwa hata kununua vitu ambavyo hawakuvihitaji wala havikuwa kwenye malengo yao kwa kushindwa tu kusema hapana. Wengine wamelazimisha kuahidi vitu ambavyo hawawezi hata kuvilipa eti kwa kushindwa tu kusema hapana. Ndugu, kama kitu huna uwezo nacho sema nashukuru kwa kuniamini na kunishirikisha kitu hiki lakini kwa sasa sitaweza kwasababu 1,2,3 hivyo naomba tufanye wakati mwingine.

5. KUTOKUWA NA ELIMU YA FEDHA.

Pamoja na kwamba karibuni kila kitu kinatumia na kinahitaji fedha katika dunia ya leo, lakini ajabu ni kwamba elimu ya fedha bado haifundishwi mashuleni na hata vyuoni hili limepelekea watu wengi kuwa wajinga wa fedha yaani hawajui usahihi na nini wafanye ili kuzalisha pesa,kutunza fedha na kuwekeza fedha kwa kukosa elimu hii watu wamekuwa wahanga wa uchumi na kushindwa kuyaendesha maisha yao kwa vipato vyao badala yake wanakimbilia kwenye mikopo na kuzalisha madeni ya kuwatosha.

6.   UNUNUZI WA VITU HOLELA (SHOPAHOLIC)

Ulisha wahi kuona mtu yeye kila kitu akikutana nacho kinauzwa tu atatamani kununua wakati huohuo hata kama ni pipi hata kama yeye ni wa kiume zikapita nguo za kike zinauzwa atatamani tu anunue akampe hata mtoto wa binamu yake ,kitu hichi ndicho kinaitwa SHOPAHOLIC yaani, ulevi wa kununua vitu bila mipangilio. Hawa watu pesa inakuwa kama inawawasha na hawawezi kutulia na pesa na utawajua tu wakiwa na pesa hawezi kutulia watakuwa bize kweli kweli ni mwendo wa kukupungia mkono tu kwa mbali anapotea ,akimaliza pesa sasa anakuwa mpole sana tena mdogo kama pilitoni hahahaha.

Kama na wewe ni mmoja wao nikushauri uweke budget ya matumizi ya pesa zako kabla ya kuzitumia na kama pia unaweza kuwa unatembea na pesa ya kukutosha tu kwa wakati huo ili kuepuka tamaa na vishawishi wa pesa.

 

kwa uchache hizi ndizo baadhi ya sababu ambazo watu wengi zimekuwa zikiwa vuta na kuwaweka katika madeni makubwa na yasiyo lipika  pasipo hata wao kujua. zifahamu sababu  hizi kwa undani kisha uziepuke ili usiwe mmoja wao wanaoteswa na kulizwa na madeni kila kukicha. 

naamini umejifunza kitu na mungu akubariki sana.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia, Uchumi na Maisha.  Mwanzilishi na Mwendeshaji wa   mtandao wa addvaluetz  karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;Sim na Whatsapp >>+255783327456 / +255767653697.

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu,niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe


Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.