HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

TATUA TATIZO LOLOTE UNALOPITIA KWA NJIA HIZI!

 


TATUA TATIZO LOLOTE KWA NJIA HIZI!

Siku zote ukiishi katika dunia hii kila kukicha utakutanana na migogoro na matatizo ya kutosha.Yaani, ukikwepa upande huu utakutananayo tu upande wa pili. Kumbe matatizo katika dunia hii ni sehemu ya maisha. watu wengi hawakubaliani na ukweli huu matokeo yake matatizo yamekuwa yakiwashangaza kila leo. Nimewahi kukutana na usemi mmoja ambao sina budi kukujuza nawewe leo. Nao ni huu “kuishi duniani huku ukitegemea kuishi bila matatizo ni chanzo cha matatizo yote.”, kuna watu wana amini kuwa wao hawajaumbwa kukutana na matatizo yeyote hapa duniani, hapo utakuta mtu anasema  “hivi kwanini mimi tu Mungu yanipate haya ”. Ajabu kweli yaani matatizo anataka yawapate watu wengine tu ila yeye hapana, ndugu ilihali unakaa kwa hii dunia hiki kitu ni ngumu kukikwepa asee.

Ndugu yangu kama unakaa kwenye hii dunia matatizo yatakuja tu aidha upende au usipende, uwe mwema au mbaya kiasi gani ,mcha Mungu au muovu kiasi gani, uwe tajiri au uwe masikini, uwe mchapa kazi au uwe mvivu, matatizo yatakuja tu na kila mtu anamatatizo yake. Hapa namaanisha hakuna mtu asiyekuwa na matatizo ingawaje matatizo yanatofautiana baina ya mtu na mtu, ndiyo maana linaweza kuwa ni tatizo kwa mtu y lakini kwa mtu x wala! Kitu kikubwa hapa ni kukubali kuwa matati hapa duniani hayakwepeki na ni sehemu ya maisha  baada ya kukubali kisha ni kujua njia gani nzuri ya kukabiliana nayo na kuchukua hatua ilikupambana nayo haraka iwezekanavyo, vinginevyo utapata maumivu ya kudumu na yasiyoisha kabisa.

NJIA RAHISI ZA KUKABILIANA NA TATIZO LOLOTE KATIKA MAISHA YAKO.

1.   LIFAHAMU TATIZO LENYEWE.

Hata katika mapambano  ya kivita au mapambano yeyote yale mfano vita, mpira, mbio, ngumi n.k kumfahamu tu adui yako uimara na udhaifu wake utakuta umeukaribia ushindi wako kwa 50% .Msemo huu wazungu huusema kuwa” knowing your enemy your about to win the battle”. yaani, kumfahamtu adui yako ni kuukalibia ushindi. Rafiki fanya namna yeyote ulifahamu tatizo lako kabla ya kusonga mbele kupambana nalo vinginevyo utatia aibu kubwa sana . Hapo ni sawa na kukimbiza upepo.  Kwa mfano wewe ni mfanyakazi umeajiliwa unaingia ofisin upo na mgogoro wa mara kwa mara na boss wako, badala ya kuamua kuacha kazi au kumkimbia boss ilikuepuka migogoro na boss wako hapo cha kufanya  fahamu kwanza shida iko wapi. Utakuja kugundua kuwa upo kwenye mgogoro wa kutukannwa na kufokewa sana na boss wako, na hili ndilo tatizo lenyewe sasa.

2.   TAMBUA CHANZO CHA TATIZO.

Hii ni hatua ya pili baada ya kugundua tatizo lako ni nini,na hapa lazima ufahamu kwa kina chimbuko au chanzo cha tatizo lako.kuna msemo mmoja unasewma” kutatua tatizo bila kujua chanzo chake ni chanzo cha matatizo yote “.Ili utatue tatizo lako kwa urahisi ni lazima ufahamu kitu gani kilichopelekea kuwepo kwa tatizo lako au chanzo chake ni kipi hasa.Mfano katika tatizo letu hapo juu la migogoro wa kufokewa na boss wako ni lazima ujiulize  chanzo cha mgogoro wa kufokewa na kutukanwa huu ni nini hasa?. kwa mfano unaweza kugundua kuwa chanzo chake ni kufanya kazi chini ya kiwango hiki ndicho chanzo chenyewe cha tatizo lako .hivyo kwa kufahamu kuwa upo na mgogoro wa kufokewa na boss wako hilo ni tatizo tayari na kufahamu chanzo cha mgogoro huo ambao ni kufanya kazi chini ya kiwango au kuchelewa kazini hapo unakuwa umeshagundua tatizo na chanzo cha tatizo lako.

3.   FAHAMU NJIA SAHIHI YA KUKABILIANA NA TATIZO LAKO.

Kufahamu tatizo na chanzo chake ni hatua nzuri sana ya kuliendea na kulitatua tatizo lako kitu kikubwa sasa ni kuhakikisha unatafuta njia nzuri na sahihi Zaidi itakayo kusaidia kulitatua tatizo lako fanya hivi kwa kusoma vitabu na kufuatilia tatizo lako katika mitandao ya kijamii kama vile geogle, fb, youtube n.k au kuwauliza watu ambao unahisi ni sahihi kwako na unawaamini kuwauliza ili kukupa ushauri na hatua zingine katika kutatua tatizo lako.angalizo katika hili ni kwamba usishirikishe kila mtu tatizo lako.katika kupata ushauri kuna watu wengine ni wanafiki wapo kufurahia kufeli kwako kwahiyo ukimpa nafasi katika hili anakumaliza kabisa.Aidha si kila ushauri unapaswa kuufanyia kazi kwa maana ushauri na maneno hutolewa bure lakini kuwa makini kuchukua ule unao kufaa tu. Ndiyo maana raisi Kiwete wa awamu ya nne Tanzania amewahi “kusema akili za kuambiwa changanya na za kwako”.

Nimalizie kusema unapochagua njia bora ya kutatua tatizo lako jitahidi uwe na machaguo mengi zaidi ya njia moja na ugundue uzuri na ubaya wa kila njia ya kuliendea tatizo lako. Mfano katika tatizo letu hapo juu njia za kutatua tatizo Hilo zaweza kuwa, kuacha kazi, kumkimbia boss, kujiongezea maarifa na kubobea katika eneo husika. Mfano mwingine labda huna hela Hilo ni tatizo tayari na njia za kulitatua zinaweza kuwa, kwenda kuiba na kukaba, kwenda kutafuta kazi ya kufanya mfano kibarua, kutwa n.k, kuongeza vyazo vya kipata  n.k

Sasa ukiangalia karibia katika kila tatizo Kuna chaguzi kibao za kulitatulia lakini, Hoja yangu hapo ni kuchagua njia iliyo bora zaidi. Siyo bora tu yaani bora zaidi, na hapo utakuwa umeupiga mwingi na Kama ni ng'ombe  ushaila yote kasoro tu mkia na mkia wenyewe ndo unaofuata hapo.

 

4.   FANYIA KAZI NJIA BORA KUTATUA TATIZO LAKO.

Kufahamu tatizo na njia ya kulitatua ni jambo moja, kuifanyia kazi njia hiyo katika kulitatua tatizo lako ni jambo lingine kabisa . Hoja ni kwamba watu wengi wanaojua njia sahihi hasa za kuleta mabadiliko katika maisha yao wengi wao hawazifanyii kazi kabisa na hali wakitegemea matokeo tofauti , hili nalo ni tatizo haswaa. Ndugu yangu utekelezaji “implementation”ni hatua muhimu sana katika kuleta mabadiliko yoyote unayo yataka hapa duniani hata kama yawe ni mabaya au mazuri. Hivyo tafuta njia yako sahihi zaidi ya kutatua tatizo lako chukua hatua mara moja kuifanyia kazi ili kuleta matokeo ambayo unayahitaji katika maisha yako, na matokeo utayapata naamini utafurahia.

Aidha nikutakie kila lililo jema katika kutatua changamoto na matatizo yako na nimaombi yangu ufanikiwe sana


 K
atua tatizo lako inawezekana.

SeE yOu NeXt LeVeL!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia,Uchumi na Maisha.  Mwanzilishi na Mwendeshaji wa   mtandao wa Add ADDVALUENETWORK. Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp/Sim >>+255767653697 / +255783327456.

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu,niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe. 

 




Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.