HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31 Ilipoishia………. Elvine alipoteza amani kuliko hata mkewe maana kila alipomtazama mkewe basi moyo wake ni kama ulikuwa unachomwa na mwiba uliojishikiza huko kwenye mishipa ya moyo. Nafsi yake ilitaabika na ndipo alipoamua kutafuta muda mzuri, baada ya chakula cha jioni, azungumze na mkewe, maana ule ukimya wa siku mbili ulikuwa adhabu kubwa sana kwake. Kusoma sehemu ya 30 bonyeza hapa Sasa inaendelea………. Elimina mamy naomba kujua kwanini hutaki kuniuliza kuhusu sababu ya haya yote? Maana najua unajua kuwa kuna mahali mimi nilikosea, sasa unapokaa kimya hivyo… kiukweli unazidi kunichanganya maana ni kama hutaki kujua, sasa unadhani mimi roho yangu itatulia kweli?. Hata kama ungekuwa wewe lazima usingepata amani, ungekuwa hata unawaza hivi nakuwaziaje, nakuonaje na ninajisikiaje ninapokuona, sasa kwanini wewe umekaa kimya, sema neno tafadhali? (Elvine alikuwa akiongea bila kumtazama mkewe usoni maana moyo wake haukuwa katika hali ya utulivu). Pamoja na ...

TUMIA NJIA HII KUPATA PESA KWA URAHISI ZAIDI

PESA HAITAFUTWI TUMIA NJIA HII KUPATA PESA KWA URAHISI ZAIDI

Mtu mmoja alikuwa na mpango wa kufuga nyuki pamoja na vipepeo. Aliamua kutengeneza sehemu ya kuwahifadhi,yaani mabanda hivyo, aliweka mkakakati wa kuwakamata  nyuki na vipepeo.Alitumia njia ya kuwafukuza na kukamata mmoja baada ya mwingine.Alijua zoezi litakuwa jepesi sana lakini kiuhalisia mambo yalimwendea kinyume kabisa na matarajio yake.Kwasababu ilikuwa vigumu kuliko kawaida hasa pale ilipokuja suala zima la kukamata nyuki aliambulia kukamata wachache sana na wengi wao waliishia  kumuuma na kusepa zao kabisa.Kwasababu usalama ulikuwa ni sifuri yaani oo.

Bwana mmoja akiwa anapita njiani alimwona huyo mtu mzima akifukuzia wadudu wadogo kama hao alishangaa sana.lakini uzalendo ulimshinda akaamua kumhoji kwanini anafanya hivyo kitu gani kimemusukuma kuwafukuzia hao wadudu alijibu akasema nina kamata vipepeo kwaajili ya kuchavusha mimea yangu  nitakayo ipanda mana hawa ni wazuri sana wa kupandikiza  mimea na hivyo kuzuia mimea kuzaa mapooza au kutokuzaa kabisa hapo baadae, hivyo nawakusanya mapema mapema na kwa wingi ili nijekuvuna mazao mengi na yakutosha . Aliendele kwa kusema lakini pia nakamata hawa nyuki kwasababu nyuki wanazalisha asali  tamu sana ambayo naweza kutumia kama dawa,chakula na kujipatia pesa kutokana na kuuza asali kama biashara nyingine, aliendelea kuseama lakini pia hawa nyuki watasaidiana  na hawa vipepeo kuchavusha mimea ninayo kwenda kulima kwa wingi sana ili niweze  kujipatia mazao mengi naya kutosha .

Mpita njia huyu alimwambia na kusema ndugu hakika unampango mzuri sana hasa huu wa kujiongezea kipato chako kupitia kilimo na ufugaji wa nyuki  ndiyo maana umeamua kupanua na kuongeza mashamba hata kuamua kuweka mkakati mzuri wa kuhakikisha unakamata wadudu wengi wa kuwezesha uchavushaji na uzalishaji wa mazao mengi ya kutosha hata nyuki kwa asali, ni uamuzi wa kupongezwa kabisa yaani niseme hongera sana ndugu yangu.lakini kwa hii njia unayoitumia ya kuwakamata wadudu hawa ilikukamilisha mkakati wako huu umeyakanyaga yaani unasukuma kupandisha maji kwenye mlima mkali  wakati wahenga walisema maji hayapandi mlima na hewa haijazi kibubu ,jamaa aliduaa na kuvuta umakini wa kusikia kutoka kwa huyu mpita njia  labda akawa na njia mpya na nyepesi ya kukamilisha zoezi lake hivyo aliiuliza na kusema njia gani iliyo sahihi ya kuwakamata vipepeo na nyuki maana kwa hii njia kweli nimeuona moto!.

Alijibu na kusema rafiki huna haja ya kuhangaika kuwakamata na kufukuzana na wadudu wadogo wadogo namna hii hali u mkubwa kiasi hiki  ,sasa sikia ukitaka kumkamata kuku huna haja ya kufukuzana naye  unaweza ukavunjika mguu bure na zama hizi tulizo nazo unaweza kugongwa na gari barabarani kabisa kwa kumfukuza kuku.basi ili umkamate kuku yakupasa kumwaga mahindi au mchele kidogo tu karibu nawe ili aje ale kisha umkamate kiulainiiii kabisa.Jamaa akadakia na kusema ndiyo maana jilani yangu huwa akitaka kukamata kuku kwaajili ya kuchinja huwa anawarushia mchele na kuwakamata.Hali hii ni toufauti na sisi huwa tunafukuza mguu kwa mguu hadi kuku anakamatika mpita njia akasema  Ujanja ni kuchgua hakika!.

Jamaa akauliza kwa hiyo hata hawa nyuki na vipepeo niwarushie mahindi na mchele vipi watakuja kweli ingali hawali mchele na mahindi?.Mpita njia akasema wawezatumia njia hiyohiyo lakini usifanye hivyo.

Yaani badala ya kukimbizana na kufukuzana na vipepeo pamoja na nyuki hawa unaweza kutengeneza bustani ya maua mazuri na kuitunza vizuri vipepeo na nyuki wakaja kwa wingi tena wakaja wao wenyewe .pia unaweza kupanda msitu wa miti na kuweka mizinga ndani na pembeni yake na hao nyuki watakuja kwa wingi kwenye bustani kutumia maua na kisha kwenda kupumzika kwenye mstu na mizinga iliyo jilani na bustani tayari kwa kutengeneza asali. kufanya hivyo utakuwa umepiga ndege wawili kwa jiwe moja tu yaani unakuwa umefanikisha zoezi lako la kufuga vipepeo na nyuki pia utakua umejipatia bustani ya bure kabisa  hapo ndipo utapata wadudu wa kuchavusha mimea ya shambani kwako na kupata nyuki wa kuzalisha na kutengeneza asali kwa wingi ya chakula ,dawa na biashara n.k kwa kulima bustani peke yake.

Kilahisi kabisa unakuwa umemkamata kuku kwa kumpa mchele na mahindi tu. Jamaa alishukuru kwa ushauri ule na alienda kuufanyia kazi mara moja alikuja kushangaa lengo lake la kupata mazao mengi na kujipatia asali kwa wingi analifikia kwa urahisi sana.

UJUMBE.

Watu wengi wamekuwa wakifakamia na kutafuta pesa na mali kwa njia ambazo siyo sahihi na hatarishi sana badala la kutengeneza vitega uchumi vya kuuvutia utajiri na pesa  .zingatia kuwa pesa haitafutwi rafiki yangu ila inavutwa na vivutio vyake kama ilivyo katika watalii kuvutwa na vivutio vya utalii,hivyo acha kutafuta pesa tengeneza njia za kuitega na kuivutia pesa itakuja tu yenyewe .mitego na vivutio vyenyewe ni kama biashara sahihi,kilimo,uvuvi,maarifa,uandishi n.k.

Mungu akubariki sana.

rafiki! ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine unatamani ujue zaidi kuhusu Uchumi wako wasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia,Uchumi na Maisha.Mwanzilishi na Mwendeshaji wa   Mtandao wa addvaluetz.Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu,niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe  


Popular posts from this blog

MAAJABU YA AKIBA

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.