MAAJABU YA AKIBA

Image
MAAJABU YA AKIBA Akiba (saving) ni kiasi cha fedha au rasilimali ambacho kimewekwa kwa matumizi ya baadaye, hata sasa kingeweza kutumika lakini umuhimu wake kwa kutumika baadaye ni mkubwa kuliko matumizi yake ya sasa. Hata katika biblia ``Mwanzo 41:35-36`` kama umewahi soma utaona Farao baada ya kutafsiriwa ndoto yake na kufahamu kuwa, imempasa kuweka akiba alilifanya hilo kwa uharaka ili kuhakikisha linaendelea vizuri ndio akamweka Yusufu kama msimamizi wa hili. Farao aliona kabisa kuwa nidhamu yake ya kujiwekea akiba haipo sawa hivo alihitaji msaidizi wa kumsaidia kama yeye alivyokuwa ndivyo tulivyo baadhi yetu siku za leo hatuwezi kujiwekea akiba ya vile tulivyo navyo. yaani huwa tunapenda kusema kesho itajisumbukia yenyewe,  Hata hivyo tangu zamani hata leo mataifa mbalimbali yamekuwa yakijiwekea akiba kwa manufaa na matumizi ya baadaye. Ukiangalia nabii Samweli alikuwa akijiwekea akiba na aliitoa pale Sauli alipomtembelea wakaila ile akiba ya chakula. Ni muhimu kujiw...

SABABU 5 KWANINI WATU WANASHINDWA KUTEKELEZA MIKAKATI WALIYO JIWEKEA?


SABABU 5 KWANINI WATU WANASHINDWA KUTEKELEZA MIKAKATI WALIYO JIWEKEA?

Siku moja nilikuwa naongea na mtu mmoja. Katika mazungumzo yetu, ambayo, yalitumia muda mrefu kidogo. Kimya kilitawala muda kuashiria kuwa mada zimeisha na kusubiri mada yingine mezani. Baadaye, nilichomekea swali na kumuuliza kuhusu mipango yake ya maisha ndani ya mwaka tuliokuwa tumeuanza maana ilikuwa ni mwanzoni kabisa mwa mwaka 2022. Naye alijibu akanieleza mipango na mikakati yake ambayo alipanga kuitekeleza ndani ya mwaka mmoja . Ukweli nilimpenda bure, kwa namna ambayo alikuwa ameandaa mipango na mikakati ya kuukabili mwaka huo mpya. Kwa mipango ile mtu yeyote angeweza kutoboa kama angeifanyia kazi. Kwa kufupisha sana nilimpongeza na kumtakia utekelezaji mwema ndani ya huo mwaka. Niseme tu kuwa, saa zilienda,siku zikaenda, wiki ndo usiseme na miezi ilikatika hadi mwaka ukaelekea ukingoni. Nilipo kutananaye nikamuuliza vipi rafiki umefikia wapi, akajibu akasema, we acha tu! Mambo yaliingiliana na mipango ikavurugika kwa hiyo sijafanikisha lolote. Mipango na mikakati niliyojiwekea haijafanikiwa kabisa, kwahiyo, najipanga nianze kwa kasi ya ajabu sana mwaka ujao.

Kisa hiki ndicho kimenisukuma kuandika Makala hii leo kwamba, kwanini watu wengi wanakuwa na mipango mingi sana na wanajiwekea ratiba ili kuitimiza lakini mwishoni inakuwa ngumu sana kuitimiza. swali hili tunakwenda kulijibu hapa.

Martin Meadows kwenye kitabu chake cha Daily self-Discipline ameelezea sababu tano ambazo zinasababisha watu wengi kushindwa kuweka nidhamu ya utekelezaji wa mipango na mikakati yake fuatana nami sasa;

1.   AINA MBAYA YA HAMASA (THE WRONG KIND OF MOTIVATION).

Hivi ulisha wahi kusikiliza hamasa fulani hivi labda ya uchumi na ukatoka unajiona kabisa kama vile unamagari, una nyumba, ndege na vitu vingine vikubwa? Naomba tuelewane hapo kwamba sipingi hamasa apana! Lakini nachotaka uelewe ni kuwa kuna aina mbili za hamasa au motisha mwandishi ameelezea kwa kusema motisha ya ndani (intrinsic motivation) hii, inatokea mtu anapotenda mambo bila malipo na vishawishi kutoka nje.

Na aina ya pili ni hamasa ya nje(extrinsic motivation). Hii, hutokea mtu anapofanya mambo yake kutokana  na vishawishi au malipo ya nje. Kwa hiyo siku zote mtu akifanya maamuzi kulingana na motisha ya nje ataanza vizuri kabisa lakini kwa sababu haikuwa ndani yake atakapo kosa tu hamasa na msukumo wa kufanya kitu hicho atashindwa kuendelea mbele. 

Ndugu, tumia hamasa ya nje kama kichocheo cha hamasa ya ndani katika kufanya maamuzi na mambo mengine. Hii itakusaidia sana usifanye kitu ili watu wakuone, ili watu wakusifie, ili uwe maarufu au ili watu wakupende bali fanya kulingana na hamasa na musukumo wa ndani ilikutimiza hatima na ndoto zako.

2.   MATARAJIO MABAYA (WRONG EXPECTATIONS).

Ni kawaida ya watu wengi kutarajia makubwa na kutaka mambo yaje kama walivyo panga wao. Watu wengi hutaka mambo waliyo jipangia yaje kwenye uhalisia kama yalivyo na huku wanasahau kupigia gharama zote muhimu zinazohitajika. Lakini, pamoja na hayo naomba nikuambie kuwa, kwa kweli mambo huwa hayaji kama ulivyopanga bali, mambo hutokea kama yalivyopangwa.  Siyo kama unavyo taka wewe. Sasa mtu akipata matokea tofauti na alivyotarajia macho yanakuwa juujuu hadi hukata tamaa na kushindwa kuendelea kabisa.

3.   KUKOSA MSAADA (LACK OF SUPPORT).

Ukweli ni kwamba, tunaishi duniani kwa kutegemeana. Ndiyo maana hakuna mtu aliye kamilika hivyo, utahitaji msaada wa mawazo, maarifa, nguvu, fedha n.k kutoka kwa watu wengine. Shida inakuja pale mtu anapotaka kufanya au kuanzisha kitu huku anategemea watu wengine katika kufanikisha jambo au ndoto yake. Sasa, anapokosa msaada huo na kutengwa na watu huacha mara moja.

Ndugu, nipende kukushauri kuwa, pamoja na kwamba tunategemeana ,jukumu la maisha yako ni lako mwenyewe kwa 100%  hivyo, pambana.

4.   KUKOSA MUDA (LACK OF TIME).

Point hii ilitakiwa iwe ya kwanza kabisa, sema ni vile tu nimeamua kuiweka hapa lakini umuhimu wake ni mkubwa sana. watu wengi wamekuwa wakilalamika kukosa muda wa kutosha katika kufanyia kazi mipango na mikakati yao. Lakini, cha ajabu wana muda wa kutosha kuangalia mpira kushinda vijiweni, kupiga umbea, kushinda mtandaoni. Kwa namna hii huwezi kupata muda wa kutosha wa kufanyia kazi ndoto yako ni ngumu sana. Halafu pia, tambua kuwa hakuna muda wa kutosha kufanya kila kitu ila, kuna muda wa kutosha kufanyia kazi ndoto yako. Hivyo, ukisubiri muda utoshe ndiyo uanze utapata tabu sana. Ndugu, muda haujawahi kutosha hivyo  anza sasa kupambania ndoto yako inawezekana.

5.   KUKOSA RAHA/FURAHA (LACK OF ENJOYMENT).

Kwasababu ya hamasa ya nje watu wengi hutamani kuwa kama baadhi ya watu maarufu hapa duniani. Wanatarajia kuwa na furaha siku zote za maisha yao hasa, katika suala la kutimiza mipango na mikakati waliyojiwekea. kitu hiki ni kinyume na uhalisia na haiwezekani kabisa. Kwani, kwenye maisha kuna nyakati za furaha , huzuni, kukata tamaa, kushindwa, kukosa msaada na kutaka kuonewa huruma na mengine mengi. Hivyo, kama utategemea kupata raha na furaha wakati wote na usitake kuukubali uhalisia utashindwa kusonga mbele. Kunamsemo mmoja naupenda sana na mwandishi kauzungumzia ambao  unasema “if you don’t enjoy your fitness plan change it” kwa tafsiri isiyo rasimi ni kwamba “kama haifurahii program yako ya kujiimarisha ibadilishe”. Hapa tunajifunza kuwa usifanye kitu ambacho hukipendi fanya kitu ambacho kinakupa raha, unakipenda na unakifurahia. 

Rafiki natambua kuwa una ndoto kubwa sana, mipango na mikakati lukuki ya kuitimiza hiyo ndoto, hilo ni jambo la kwanza na zuri sana. Lakini, kama hautaamua kuchukua hatua ya kuanza na kusonga mbele utabaki nayo mwenyewe ndani yako hivyo, amua kuifanyia kazi ndoto yako bila kujali wengine wanasemaji, watakuonaje au kutaka kuwapendeza wengine. Ndugu tumia hamasa ya nje kuichochea  hamasa ya nje matokeo utayapata naamini utanipenda. 

Ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu rafiki!

na kama unachangamoto katika hili pengine njinsi ya kuigundua ndoto yako wasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu wa Saikolojia, uchumi na maisha.  Mwanzilishi na Mwendeshaji wa   mtandao wa addvaluetz  karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Sim na Whatsapp >>+255783327456 / +255767653697.

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu,niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe


Popular posts from this blog

PANDE ZA MAFANIKIO

MAAJABU YA AKIBA

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.