HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26.

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 26. Ilipoishia.......... Alipomgeuza tu alishangaa kuona sura ya yule binti ni ya mbuzi. Aliogopa na kudondoka chini kwa kelele kuu alilia 'maaamaaaaaaa!!!!" Alijiokotaokota huku akiangukaanguka mpaka kwenye gari yake. Alipanda ndani ya gari na kuwasha gari. Alikimbiza gari mpaka akafika karibu na geti la nyumba ya Elvine, lakini kabla hajafika getini alishangaa kuona anaguswa mabegani ndani ya gari lake. Alitoa macho kwa uoga na mshtuko mkubwa mpaka akakosea njia na kwenda kugonga mti... Kusoma sehemu ya 25 bonyeza hapa. Sasa inaendelea......, Aligonga mti kwa nguvu mpaka naye akajipigiza kichwa kwenye usukani wa gari na gari ikaharibika sana upande wa mbele, alipona kwa neema tu kwa namna gari ilivyokuwa mwendo kasi angeweza hata kupoteza maisha lakini haikuwa hivyo. Alijikaza na kushuka kwenye gari akakimbia kuelekea kwenye nyumba ya Elvine,  njiani alikumbwa na kimbunga cha ajabu sana. Baada ya kile kimbunga kumpitia na kumzingazinga kwa muda

KUWA KIELELEZO (BE A REFERENCE)!



KUWA KIELELEZO (BE A REFERENCE).

Tunaishi kwenye dunia ambayo kila mtu anataka kuwa maarufu,tajiri na mtu muhimu sana katika Dunia hii.Na wengine wanajitahidi kufanya kila linalowezekana ili tu kufikia lengo hilo la kuwa maarufu  ulimwenguni,Kubwa Zaidi watu wanasahau kuwa  kuna gharama za kuufikia umaarufu na kuwa mtu muhimu duniani.

Mwalimu wangu wa shule ya Msingi aliwahi kunambia ukitaka kuwa maarufu na kujulikana sehemu yeyote ile basi inakupasa ufanye kitu kizuri au kibaya sana tena ufanye kwa bidii na utofauti .Nikamuuliza kivipi? Akasema ukifanya kitu kizuri cha kujenga na kuisaidia jamii watu watakufahamu tu tena watakufahamu kwa mazuri mfano, kutengeneza labda ndege,kuelimisha jamii,kuwa kiongozi bora n.k,mchango wako katika jamii utafahamika.Lakini pia ukifanya jambo baya la aibu katika jamii mfano, kama kuiba,kujiingiza kwenye makundi ya ugaidi,umalaya n.k watu watakufahamu tu tena watakufahamu kwa mabaya hayo.

Hapa ndipo nikaja kugundua kuwa kumbe hata ufanye jambo zuri au baya watu watafahamu tu kuhusu wewe hata kama ufanye kwa siri.Nakumbuka mama mmoja alikuwa rafiki yangu sana mwaka 2020 siku moja nilikua napiga naye stori ,mama huyu alikuwa na watoto wanne ambao hawa kuwa wakubwa bado.Alinambia na kusema kuwa natamani sana watoto wangu waje wawe kama watoto wa Fulani  au hata wote wakiwa kama familia ya mtu Fulani nitafurahi sana.Nikauliza kwanini?, akasema kwa namna ambavyo familia hiyo wanajiheshimu ,wanafanya kazi kwa bidii,wanautii lakini pia ni watu ambao karibia kila mtu katika jamii anawafahamu kwa wema wao.Mama huyu alichomekea na kusema tena kijana wa kiume akitaka kuoa namshauri akaoe katika familia hiyo hahaha.Kwa uelewa wangu mdogo kwa kipindi kile nilimjibu na kusema mtoto umleavyo ndivyo akuavyo  kwa hiyo kama unataka wawe kama hiyo familia nenda kajifunze kwamba familia hiyo inafanya vipi na imewezaje kuwa mfano wa kuigwa ,kisha amua kufanyia kazi njia hizo.

Lakini ukijiuliza tena kwa upande mwingine utakuja kuona kuna watu au familia ambazo ni pasua kichwa mtaani kila mmoja anaelewa kasheshe lake .Na wakati mwingine utakuja kuta watu hawa wanalifahamu hilo au hawalitambui kabisa kuwa wao ni pasua kichwa mtaani.

Rafiki ninachotaka uone ni kwamba ukiamua kufanya mema au mabaya hayohayo ndiyo yatakutambulisha na watu watakujua kwayo,yaani ukiwa mlevi  wa kupindukia watu watakujua kwa ulevi huo huo,ukiwa Malaya au tapeli watu watakujua kwa namna hiyo hiyo,ukiwa mwema watakujua kwa wema huo huo,ukiwa mwalimu na mshauri mzuri watu watakujua kwa namna hiyohiyo,hali kadharika kwa uongo,umbea,wizi, n.k

Tambua kwamba mtu kuwa kielelezo chema au kibaya ni suala la yeye kuchagua awe kielelezo kwa mambo mazuri au kielelzo kwa mambo mabaya,na haya yote yanaonekana katika jamii hata kama utaamua kuyafanya kwa siri watu watafahamu tu.hapa kuna msemo mmoja unasema “Even if no one is watching you, you have to be sure that everyone is watching you”.kwa tafsiri isiyo rasmi ni kwamba “hata kama hakuna anayekuona uwe na uhakika kuwa kila mtu anakuona”.kwa lolote unalolifanya tambua kuwa watu wanakutazama na amua kuwa kielelezo chema katika hilo.

Hivi ulisha wahi kuona kila mtu katika eneo lake mfano kwa wachezaji wa mpira wanatamani kuwa kama messi na lonaldo,kwa waandishi wanatamani kuwa kama kiyosaki,Robin shama,Robert Green,Brian Tracy n.k, wanamziki, wakulima, waalimu, washauri kadharika katika maeneo yao.Hii ni kwa namna ambavyo watu hawa walichagua kuwa kielelezo chema na mfano wa kuigwa katika jamii pengine hata wao hawakujua kuwa itakuwa kieleleza kwa kuchagua kufanya mema.Sina hakika kama na waliokuwa kielelezo kwa mambo mabaya kama walijua kuwa siku moja watakuwa mfano wa tabia na watenda mabaya.

Goja nikuibie siri hii kidogo,pengine hauifahamu nayo ni “kwa maisha hayo hayo unayoishi kunawatu wengi sana wanayatamani na ni ndoto yao siku moja kuishi maisha kama unayoishi wewe saivi”.Lakini ajabu nikwamba unayadharau sana na kuona hayana maana,unakuwa mtu wa kunung’unika,kulalamika kila kukicha  hali hii siyo nzuri kabisa tafuta furaha ya maisha yako. 

Ndugu tambua kuwa kuna watu wanakufuatilia katika maisha yako, wanajifunza kwako wengine wanajivunia kukufahamu na wengine wanakuita Role model wao cha ajabu ni kwamba mwenyewe huwafahamu ,hivyo usikate tamaa wala kurudi nyuma kwani utawakatisha tamaa na kuwarudisha nyuma watu wengi sana .Ndiyo maana utakuta mtu anasema kama Fulani kafanya hivi mimi ni nani nisifanye?.Binafsi watu wengi sana wamekuwa wakinipigia simu na wengine kunifuata ana kwa ana na kunishukuru na wakisema “ninajifunza vitu vingi sana kutoka kwako nilikuwa sian hili wala lile lakini umenifanya nimekuwa na 1,2,3…  Mungu akubariki sana”.Cha ajabu wengine hata siwafahamu kabisa.kusema haya si kwamba najisifia sana hapana nachotaka uone ni namna gani watu wengi wanafuatiria maisha yako na kujifunza kwako.

Rafiki kuna vitu muhimu sana viwili yakupasa kuvifahamu navyo ni REPUTATION NA CHARACTER..Reputation hiki ni kitu au sifa ambayo watu wengine wanasema kuhusu wewe wakati wewe haupo.Mfano hivi nikitaja John pombe Magufuli unafahamu nini,nikitaja Joel Nanauka je,vip kuhusu Osama,Diamond je?.Binafsi nimeshiriki sana kwenye vikao vya kuchagua kamati,sasa kunakitu nilikuja kujifunza katika hili kwani kuna majina yalikuwa yakitajwa kila mtu anaguna na kupinga kabisa.Lakini baadhi ya majina yakitajwa kila mtu anakubali tena kwa kuongeza na maelezo juu yake.

Wakati Character kile kitu unacho kifanya kwa siri pale ambapo hakuna  mtu  anakuona.Hiki kitu ndiyo wewe sasa. Hata kama ukienda nje au ukiwa na watu wanakusifia sana lakini kama unafanya mambo ya kijinga siri ambapo watu hawakuoni amini kuwa ipo siku watu watakudharau na kukupuuza sana.Kwa sababu character ndiyo imebeba tabia na sifa za mtu halisi na hizi watu wengi huzifanya kwa siri sana,na zinaweza kuwa ni nzuri au mbaya lakini wakija nje wanaigiza maisha na kuishi nje ya uhalisia wao huku nako wanajulikana kwa sifa nyingine tofauti na character yao. Na watu watakapo jua character yake wataivunja reputation haraka sana, hivyo character ina nguvu kuliko reputation na inaweza kuivunja reputation aliyo ijenga mtu.

Ulishawahi kuona mtu mhimu sana mtaani anayeaminika na anajina lake kalijenga mtaani chukulia labda ni mchungaji ,mara inagundulika kafumaniwa na mke wa mtu  reputation yake itavunjika mara moja kwasababu ya character (uzinzi) aliyo kuwa anaifanya kwa siri sana.Hata katika mwizi au tapeli aliyekuwa anaaminika sana katika jamii ni hivyo hivyo akigundulika na character yake.

Ndugu nimalize kwa kusema achana na maisha ya kuigiza ishi maisha yako halisi usije kuangukia pua watu wakizijua siri zako.Iwe ndani au nje popote utakapo kuwa fanya vitu ambavyo vitakutafsiri vyema kwasababu watu wanakuona hata kama huonekani,watu wanajifunza kwako hata kama hujawafundisha.kuwa kielelezo chema na cha kuigwa katika jamiii,ifananine ile familia ambayo yule mama rafiki yangu alikuwa anaitamani.

Afu ukiwa kielelezo ni rahisi sana kuacha alama katika jamii yako ujue.

rafiki! ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine namna gani ya kuwa kielelezo wasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia,Uchumi na Maisha.Mwanzilishi na Mwendeshaji wa   Mtandao wa addvaluetz.Karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu,niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe  


Popular posts from this blog

GHARAMA 5 ZA KUUFIKIA UKUU UNAOUTAKA.

USIKUBALI KUAJIRIWA KABLA HUJASOMA HAPA.

SIRI ILIYOPO NYUMA YA TABASAMU.