HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31

Image
  HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31 Ilipoishia………. Elvine alipoteza amani kuliko hata mkewe maana kila alipomtazama mkewe basi moyo wake ni kama ulikuwa unachomwa na mwiba uliojishikiza huko kwenye mishipa ya moyo. Nafsi yake ilitaabika na ndipo alipoamua kutafuta muda mzuri, baada ya chakula cha jioni, azungumze na mkewe, maana ule ukimya wa siku mbili ulikuwa adhabu kubwa sana kwake. Kusoma sehemu ya 30 bonyeza hapa Sasa inaendelea………. Elimina mamy naomba kujua kwanini hutaki kuniuliza kuhusu sababu ya haya yote? Maana najua unajua kuwa kuna mahali mimi nilikosea, sasa unapokaa kimya hivyo… kiukweli unazidi kunichanganya maana ni kama hutaki kujua, sasa unadhani mimi roho yangu itatulia kweli?. Hata kama ungekuwa wewe lazima usingepata amani, ungekuwa hata unawaza hivi nakuwaziaje, nakuonaje na ninajisikiaje ninapokuona, sasa kwanini wewe umekaa kimya, sema neno tafadhali? (Elvine alikuwa akiongea bila kumtazama mkewe usoni maana moyo wake haukuwa katika hali ya utulivu). Pamoja na ...

JE MAARIFA YANAKUIMARISHA AU YANAKUHARIBU?



JE MAARIFA YANA KUIMARISHA AU YANA KUHARIBU?

“Learning makes a wise wiser and a fool more foolish”. Huu ni moja kati ya semi ninazozipenda sana, sababu umebeba uhalisia fulani hivi kwa namna ambavyo dunia ya sasa inaenenda. Hebu ngoja tuone maana yake kwanza ambayo ni kwamba “kujifunza kunamfanya mtu mwenye hekima kuwa na hekima Zaidi na mjinga kuwa mjinga Zaidi”. Ukweli huu nauunga mkono kwa 100% kabisa nadhani hata wewe utakuja kuungana na mimi katika hili hapo baadaye. Na Mara, utakapo maliza kusoma andiko hili hutabaki kama ulivyo.

Hivi ulishawahi kuona mtu wa namna hii? Kwamba kabla ya kwenda shule tuseme labda sekondari au chuo alikuwa na nidhamu, heshima, maadili, utii, kufanya kazi kwa bidii, uzalendao, tabia njema na alikuwa mfano wa kuigwa katika jamii. Lakini mara baada tu! Ya kwenda shule au chuo mambo yanabadilika kabisa na kuwa tofauti na vile alivyokuwa mwanzo, utashangaa anaanza kuwa mkaidi, tabia mbaya kama vile uraibu wa pombe, umalaya , anapoteza uaminifu n.k. yaani anabadilika nakuwa tofauti kabisa na vile jamii ilikuwa ikimtarajia kuwa. Kwa maana hiyo, unakuja kujiuliza mtu kama huyo alikwenda shuleni au chuoni kuongeza maarifa ili kujiboresha au alikwenda kujiharibu na kujibomoa? Hebu twende pamoja kunakitu nataka nikuoneshe.

Hali hii imewafanya baadhi ya wazazi huko kijijini na mijini kuwa na vigugumizi vingi kuwapeleka watoto wao shuleni au Vyuoni wakijua ni wale wale tu kasoro mavazi. Juzi juzi tu hapa nilikuwa naongea na mtu mmoja wa huko kijijini nikamuuliza kuhusu habari ya kusoma kwa watoto wake. Ndugu huyo alikana wazi wazi na kusema kwamba hawezi kufanya ujinga kama huo, huku akijua anafanya ujinga ingekuwa bora angekuwa hafahamu kama anafanya ujinga. kama kawaida yangu nilitamani kujua sana juu ya msimamo wake aliokuwa ameusimamia nilimdadsi kwa kina.

Na hoja yake kubwa ilikuwa ni kwamba watoto wakienda shule wanakuwa na tabia mbaya, wanajiinua, wanakuwa wabishi, wavivu, wanaangukia kwenye, ushoga, umalaya na kupata magonjwa, wanaleta mimba na kuzaa watoto kabla ya ndoa, wanaongeza idadi ya watoto ombaomba na machokoraa mitaa wanaharibu maadili ya jamii  na wanashusha maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla. Sasa ukijiuliza tunapeleka kusomesha au kuharibu watoto wetu ? Akaendelea kwa kutolea na mifano ya baadhi ya watu pale kijijini ambao wamesoma lakini hao ndiyo wamekuwa wa kwanza kukimbilia na kutetea maovu,sasa tunakwenda wapi na mimi sipo tayari kwenda kuharibu watoto wangu bora nikapambana nao tu hapa hapa kijijini nitawafundisha mwenyewe, afu mbona babu zetu walifanya hivyo na maisha yalikuwa safi tu? Jamaa alihoji. Hallo! kwamifano mingi aliyonipa huyo mtu niliona kama kunauhalisia na ukweli katika hoja yake.Niseme tu ukweli nilitumia nguvu kubwa na muda mwingi sana kumwondosha katika mtazamo huo. Lakini Mungu ni mwema katika yote. huyo mtu alikubali kusikiliza, akauliza maswali akaelewa, akawa mpole, akajifunza na akaahidi kuufanyia kazi ushauri huo na kwamba amebadili mtazamo wake.

Pamoja na hayo ukija upande mwingine utakutana na watu ambao pengine hapo kabla ya shule au chuo walikuwa mbumbu, ziro, gesi, hawakuwa wanajiamini, waongo, tabia mbaya, waoga na mengine mengi ya kufanana na hayo. Lakini baada ya kwenda shule walibadilika kabisa na kuwa watu wa kutegemewa, kuaminika na kuwa mifano mizuri ya kuigwa katika jamii. Baada ya shule walifanyika kuwa watu tofauti na zamani sasa ni watu wema na wenye msaada katika jamii na taifa kwa ujumla.

Ndugu hapa ukubali au ukatae kunawatu wanaenda shuleni na vyuoni wanapotelea hukohuko juu kwa juu huku wengine wakibadilishwa na kuwa watu wema na muhimu sana katika jamii zetu na taifa letu. Na hapa ndipo penye uhalisia wa ule usemi wetu hapo juu “Learning makes a wise wiser and a fool more foolish”, Na hii, si katika shule na vyuo tu. Bali ni katika Nyanja zote za maisha mfano katika biashara, jeshi, kanisa na sehemu nyingine lukuki.Yaani kwa lugha rahisi ni kwamba, maarifa yanawaimarisha wenye heshima  na kuwaharibu kabisa wajinga, hapa ndio maana biblia ilisema mwenye nacho ataongezewa na asiyenacho hata alichonacho atanyang'anywa. Hii ni Kali asee!

Mfano mtu anasoma na kufundishwa biblia vizuri kabisa lakini baadaye utasikia mtu huyohuyo anaipinga na kusema imekosewa ooh mara imepitwa na wakati, kisha anaasi na kuacha iman. Lakini wengine wanaimarishwa na kufanywa upya kila siku kupitia biblia hiyo hiyo.

Mwingine anafundishwa mafunzo ya jesha na kuwa mzalendo na raia mwema lakini kuna mwingine anakengeuka na kuwa jangili tishio la usalama, kama hutaki kuamini kamuulize Iddy Amini mjukuu wa Dadaa.

Utakuta mwingine mitandao ya kijamii imemuharibu kabisa, imempotezea muda na kupoteza malengo yake haswa yaani anakuwa ni yeye na wassap na mitandao mingine ya kijamii anachati na kufuatilia kila kitu asubuhi hadi jioni. Lakini wengine wanaitumia hiyo hiyo mitandao kujifunza vitu vipya, kufanya biashara, kujifunza kwa wengine ili kujiimarisha, kuelimisha jamii na kuzalisha kipato cha kuendesha maisha yao.

Nachotaka ujue ni kwamba, tunaishi kwenye kipindi cha ulimwengu wa taarifa na maarifa ni tofauti kabisa na vipindi vingine vilivyo wahi kupita huko nyuma. Kulikuwa na vipindi vya kutumia nguvu na mabavu ambapo mataifa na watu wenye nguvu waliweza kuushinda ulimwengu huo  na kuwa watawala,watu muhimu na maarufu sana kipindi hicho.Vivyo hivyo katika kipindi hiki watu wenye wingi wa maarifa na taarifa wanautawala ulimwengu wa sasa na kuishi kama wafalme.

Nasema hivi tupo katika utandawazi, taarifa, habari na maarifa. Watu wengi wanapo haribikiwa wanaanza kuulaumu utandawazi na wingi wa maarifa kuwa vinawachanganya. Ndugu tambua kuwa pamoja na kwamba hivi vitu vina faida na hasara, hivi vipo vimesimama tu havina upande wowote.Yaani ukiamua kuvitumia kwa faida vitakufaidisha sana tena zaidi ya unavyofikiria. Na ukiaamua kuvichukua kama hasara kwa kweli vitakuharibu na kukufilisi kabisa. Hapo ndipo utabaki kuulaumu utandawazi pamoja na sayansi na teknolojia.

Nimalize kwa kusema utandawazi upo, maendeleo ya technolojia yapo kabisa na kama ilivyo katika uhalisia kuwa hakuna kitu kisicho na faida na hasara, hivyo hata hivi vina hasara na faida yake. Wale wote wanaoharibiwa kutokana na  kujifunza teknolojia, taarifa na utandawazi wanachukulia upande wa madhara  ya hivi vitu, ndiyo maana badala ya kuboreshwa wanabomorewa na kuharibiwa kabisa.

Na wale ambao wananufaika na kufaidika ni wale ambao wameaamua kutumia kwa upande wa faida na wamenufaika na kufanikiwa sana katika Mipango na Malengo yao. Kwa hiyo uamuzi na uchaguzi wa mtu hujulisha kuwa ataharibiwa au atafanikiwa . Ndugu chagua na amua kutumia kwa faida huu utandawazi na wingi wa maarifa tuliyo nayo katika ulimwengu wa sasa pia, amua kupuuzia katika upande wa harasa.  Maamuzi! maamuzi! Maamuzi! ni yako mwenyewe. 

Les Brown mwanahamasa huko marekani amewahi kusema, “Hatima inaanza kujengwa katika kipindi cha kufanya maamuzi” hivyo jenga hatima yako kwa kufanya maamuzi sahihi usiendeshwe na mihemuko na mikumbo ya watu wengine. Fanya kitu kitakacho kunufaisha na kukusukuma kuitimiza ndoto yako katika kila unacho taka kukifanya jiulize kwamba hiki kitu kitaniongezea hamasa ya kufanyia kazi ndoto yangu au hapana ? Kama ni ndiyo basi kifanye tena kwa bidii na ubora na kama sivyo kipuuzie mara moja.

Amua sasa inawezekana kupambania malengo na ndoto yako kuwa mtu wa kuigwa na wa faida kwa familia, jamii na taifa kwa ujumla. Pia chagua kufanya mema kwani watu wengi wanakufatilia na kujifunza kwako kimya kimya pasipo hata wewe kujua,hivyo usiwaangushe asee!

rafiki! ni matumaini yangu kuwa umejifunza kitu.

na kama unachangamoto katika hili pengine jinsi yakufanya maamuzi ya kutumia kujifunza kwa faida yako wasiliana na mimi moja kwa moja kupitia mawasiliano hapo chini naamini utasaidika.

GeT tO ThE nExT lEvEl!

Makala hii imeandaliwa na kuandikwa na MIGONGO ELIAS Mshauri & Mwalimu Wa Saikolojia,Uchumi na Maisha.  Mwanzilishi na Mwendeshaji wa   mtandao wa addvaluetz  karibu sana ujiongezee thamani yako. 

Kwa mawasiliano;

Whatsapp & Sim >>+255767653697 /+255783327456

Email>> eliasmigongo120@gmail.com.

Facebook>> MIGONGO ELIAS.

LinkedIn>>Migongoe. 

Pinterest>>eliasmigongo.

Kama umejifunza kitu,niachie maoni yako nitafurahi kujifunza pamoja nawe


Popular posts from this blog

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 29

UCHAMBUZI WA KINA HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 27.

HATIMA YA KIMUNGU SEHEMU YA 31